Kumbe CDM wanatekeleza ilani ya CCM

GeniusBrain

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
4,315
306
Kwa mujibu wa taratibu za uendeshaji wa nchi, Chama kilicho shinda na kuunda Serikali (yaani CCM )ndicho chama ambacho ilani yake inatatekelezwa kwa kipindi husika i.e 2010-2015. Kwa mantiki hiyo basi, yale yote yanayofanywa na vyama vingine huwa ni kutekeleza ilani ya chama tawala. Na hivyo basi , yale yote watakayo yafanya CDM itakuwa ni utekelezaji wa ilani ya CCM.
 
Jibu hoja iliyowekwa , wewe waona mchana jua unaulizwa hilo ni nini, unasema huo mwezi. Au ndio nyie wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii, basi hao ni kama...................................ni dhalili kuliko.......................

Hivi wewe hata darasani ulihudhulia.
 
Think twice. Kama CDM kinaongoza halmashauri, kinakuwa na uwezo wa kutekeleza yale yaliyo kwenye ilani yake kwani halmashauri ina autonomy yake. Kwa mfano Karatu walifuta kodi ya maendeleo kabla ccm haijaifuta kwa TZ. Hapo huwezi kusema CDM karatu ilikuwa inatekeleza ilani ya CCM. Hata sasa CDM Mwanza wanaweza wakasema kutokana na mapato ya jiji, wafute ile 20,000/= ya kila mwanafunzi wa sekondari mwanza - huwezo kusema watakuwa wamatekeleza ilani ya CCM bali ilani yao iinayosema elimu bure nk. Katika ngazi ya Taifa kweli Taifa litatekeleza ilani ya CCM lakini kwa level za chini zenye autonomy yake inaweza kuwa tofauti. Think twice and if twice is not enough, think thrice!
 
Think twice Thread yako haina mashiko! na huja eleweka kimantic lengo lako ni kitugani.....Siku nyingine usithubutu kufanya utani wa namna hii
 
Think twice. Kama CDM kinaongoza halmashauri, kinakuwa na uwezo wa kutekeleza yale yaliyo kwenye ilani yake kwani halmashauri ina autonomy yake. Kwa mfano Karatu walifuta kodi ya maendeleo kabla ccm haijaifuta kwa TZ. Hapo huwezi kusema CDM karatu ilikuwa inatekeleza ilani ya CCM. Hata sasa CDM Mwanza wanaweza wakasema kutokana na mapato ya jiji, wafute ile 20,000/= ya kila mwanafunzi wa sekondari mwanza - huwezo kusema watakuwa wamatekeleza ilani ya CCM bali ilani yao iinayosema elimu bure nk. Katika ngazi ya Taifa kweli Taifa litatekeleza ilani ya CCM lakini kwa level za chini zenye autonomy yake inaweza kuwa tofauti. Think twice and if twice is not enough, think thrice!

Hakuna autonomy kubwa unayoisema wewe. Halmashauri zote ziko chini ya Ofisi ya Waziri mkuu . Na boss wa Halmashauri ambae ndie mwenye mafungu ni DED yaani Mkurungezi ambae huteuliwa na Rais , sasa hapo autonomy unayo isema wewe ipo wapi ?. Na isitoshe Halmashauri zote zaidi ya 90% zinategemea ruzuku kutoka Serikali kuu, hapo autonomy ipo wapi ? . Hamna autonomy yoyote ni maneno yako ya kisiasa hayo mkuu. Na hata leo hii Serikali kuu yaweza kutoa order ya kuzifuta Halmashauri, sasa autonomy hiyo iko wapi?. Unauona jua mchana unaulizwa nini hicho, unasema huo ni mwezi.
 
Halafu hilo jina umelikosea sio 'FREDOMFIGHTER' ni 'FREEDOMFIGHTER' rekebisha tafadhali yaonyesha kiingereza kwako ni mgogoro.

Ukitaka wewe jiite FREEDOMFIGHTER, mimi ni FREDOMFIGHTER, two different things, halafu we unaona kingereza dili sana , MS una tabu weye.Lakini ndivyo mlivyo walamba viatu wa mafisadi, mitazamo finyuuuuuuuuuuuuuuuuuuu.
 
Think twice Thread yako haina mashiko! na huja eleweka kimantic lengo lako ni kitugani.....Siku nyingine usithubutu kufanya utani wa namna hii

Hoja ina mashiko sana na inaeleweka, sema wewe ndio hauna mashiko kwenye fikra zako. Kipi usicho kielewa kwenye hiyo hoja? Hebu soma tena na tena utaielewa, acha unazi wako wa kisiasa mkuu.
 
Ukitaka wewe jiite FREEDOMFIGHTER, mimi ni FREDOMFIGHTER, two different things, halafu we unaona kingereza dili sana , MS una tabu weye.Lakini ndivyo mlivyo walamba viatu wa mafisadi, mitazamo finyuuuuuuuuuuuuuuuuuuu.

Acha hasira kijana ukirekebishwa, badilisha tu hilo jina ulilikosea usione aibu, ndiyo unajifunza hivyo ukikutana na GREAT THINKERS !
 
Hakuna autonomy kubwa unayoisema wewe. Halmashauri zote ziko chini ya Ofisi ya Waziri mkuu . Na boss wa Halmashauri ambae ndie mwenye mafungu ni DED yaani Mkurungezi ambae huteuliwa na Rais , sasa hapo autonomy unayo isema wewe ipo wapi ?. Na isitoshe Halmashauri zote zaidi ya 90% zinategemea ruzuku kutoka Serikali kuu, hapo autonomy ipo wapi ? . Hamna autonomy yoyote ni maneno yako ya kisiasa hayo mkuu. Na hata leo hii Serikali kuu yaweza kutoa order ya kuzifuta Halmashauri, sasa autonomy hiyo iko wapi?. Unauona jua mchana unaulizwa nini hicho, unasema huo ni mwezi.

Maamuzi ya mwisho katika halmashauri yanafanywa FULL COUNCIL (Baraza la Madiwani) hivyo wenye madiwani wengi ndio watakua wanafanya maamuzi kulingana na Ilani yao au waonavyo - in relation to the budget granted by the central government and council sources of revenues. Hapo ndio AUTONOMY inapoanzia. I stand to be corrected.
 
Hakuna autonomy kubwa unayoisema wewe. Halmashauri zote ziko chini ya Ofisi ya Waziri mkuu . Na boss wa Halmashauri ambae ndie mwenye mafungu ni DED yaani Mkurungezi ambae huteuliwa na Rais , sasa hapo autonomy unayo isema wewe ipo wapi ?. Na isitoshe Halmashauri zote zaidi ya 90% zinategemea ruzuku kutoka Serikali kuu, hapo autonomy ipo wapi ? . Hamna autonomy yoyote ni maneno yako ya kisiasa hayo mkuu. Na hata leo hii Serikali kuu yaweza kutoa order ya kuzifuta Halmashauri, sasa autonomy hiyo iko wapi?. Unauona jua mchana unaulizwa nini hicho, unasema huo ni mwezi.

CDM karatu walipofuta kodi ya maendeleo kwa wilaya hiyo tu walikuwa wanatekeleza ilani ya nani? Kama hawana autonomy yoyote kwa mapato wanayokusanya wao - waliwezaje? Mbona ofisi ya waziri mkuu haikukataa kwa kuwa haikuwa ilani ya CCM? Think more than twice!
 


Maamuzi ya mwisho katika halmashauri yanafanywa FULL COUNCIL (Baraza la Madiwani) hivyo wenye madiwani wengi ndio watakua wanafanya maamuzi kulingana na Ilani yao au waonavyo - in relation to the budget granted by the central government and council sources of revenues. Hapo ndio AUTONOMY inapoanzia. I stand to be corrected.

Mnashindwa kuelewa kitu kiko wazi kabisa. Mapato yanayotoka na Halmashauri wao wenyewe ni madogo sana, hayazidi 10%, mapato makubwa ni ya ruzuku kutoka serikali kuu. Na kwa kawaida Central Government kabla hawajatoa ruzuku kwa Halmashauri hupeleka mipango yao kwa Waziri mkuu , ambapo baadae ndipo hutoa fedha. Mara ngapi mwasikia Halmashauri zalalamika kwenye miradi kuwa hazikupata fedha kutoka serikali kuu ? Sasa autonomy ipi wanayo wakati serikali kuu ndio wanaamua kuwapa pesa kwenye miradi ipi na zingine kuwanyima?. Fuatilieni mambo acheni kujibu kushabiki wakuu.
 
UMEKOSEA JINA ACHA KUZUGA,INAANDIKWA Freedomfighter sio FREDOMFIGHTER.

Ahsante kwa kumrekebisha, jamaa mbishi kweli hata kwenye ukweli aisee ! Anaona aibu eti akibadilisha watu watamdharau. Huko ndiko kujifunza.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom