NakuliliaTanzania
JF-Expert Member
- Sep 24, 2007
- 555
- 7
Naona mambo mabichi kabisa.....kumbe hakufukuzwa kazi in the real sense...ndo maana wakasema wametengua...nadhani Balali bado anazo nguvu nyingi na mambo mengi anayojua
Je ina maana alikuwa anafanya kazi kama consultant? au raia wa kigeni?
Meghji: Ballali hakuwa mtumishi wa serikali
na Mwandishi Wetu, Dodoma
ALIYEKUWA Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Dk. Daudi Ballali, ambaye uteuzi wake ulitenguliwa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete, hakuwa mtumishi wa serikali, Tanzania Daima imebaini.
Uhakika kwamba Dk. Ballali hakuwa mwajiriwa wa serikali, ulitolewa hivi karibuni na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, wakati alipokuwa akizungumza na redio moja inayorusha matangazo yake kupitia intanet.
Meghji alisema kuwa, Dk. Ballali alikuwa na mkataba wa kuwa Gavana tu na hakuwa na mkataba wa ajira serikalini, na kumaliza utata uliokuwa umetanda kuhusu iwapo kiongozi huyo alikuwa mwajiriwa wa serikali.
Meghji alisema kuwa, kwa maana hiyo, mkataba baina ya serikali na Dk. Ballali uliisha siku ambapo uteuzi wake wa kuwa Gavana ulipotenguliwa.
Ballali aliteuliwa kama Gavana wa Benki Kuu, alipokuja alikuja kama gavana wa Benki Kuu, hakuwa mtumishi wa Serikali ya Tanzania, alikuja kama gavana tu," alisema.
Kwa upande mwingine, alipoulizwa kuwa iwapo kuna uchunguzi mwingine wowote unaofanywa katika akaunti nyingine za BoT kutokana na madai kuwa Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) iliyochunguzwa ni sehemu ndogo tu ya ubadhirifu, Meghji alisema kuwa hakuna uchunguzi mwingine unaofanyika.
Alisema kuwa kinachoangaliwa hivi sasa ni ripoti ya mkaguzi kuhusu EPA ambayo imeshasimamishwa na kuwa mambo mengine yataangaliwa pia.
Meghji alisema, baada ya mambo yaliyotokea, kuna haja ya kuangalia kwa kina mahusiano baina ya Benki Kuu, kama taasisi na Wizara ya Fedha kwa upande mmoja na serikali kwa upande mwingine.
Alisema kuwa hilo ni muhimu na kuwa kinachopaswa kuangaliwa kiundani ni sheria ya Benki Kuu iliyopitishwa na Bunge mwaka jana.
Waziri huyo alisema kuwa, suala hilo ni muhimu liangaliwe kwa sababu sheria hiyo inampa uhuru Gavana wa BoT kama mtendaji mkuu wa taasisi hiyo nyeti na pia anakuwa Mwenyekiti wa Bodi ya BoT.
Alisema hilo linapaswa kuangaliwa baada ya kubainika kuwa yeye alidanganywa na aliyekuwa Gavana na kusaini barua iliyokuwa inaonyesha kuwa kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd, ililipwa kihalali kwa kazi zinazohusu usalama wa taifa.
Meghji alisema kuwa, BoT inapaswa kuwa huru, lakini uhuru huo unapaswa kuangaliwa na jinsi ambavyo Gavana anafanya kazi na mahusiano yake na Wizara ya Fedha.
Alisema hivi sasa, kisheria, bodi na BoT pamoja na Gavana, wapo huru kufanya mambo yao ingawa kuna wajumbe katika bodi ambao wanatoka nje ya BoT na kuwa hawana haki ya kupiga kura.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Waziri Meghji alikiri kufanya mahojiano na redio hiyo na kusema taarifa alizokuwa nazo ni kwamba Ballali alikuwa akifanya kazi kwa mkataba maalumu, hakuwa mtumishi wa serikali.
http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/2/4/habari3.php
Je ina maana alikuwa anafanya kazi kama consultant? au raia wa kigeni?
Meghji: Ballali hakuwa mtumishi wa serikali
na Mwandishi Wetu, Dodoma
ALIYEKUWA Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Dk. Daudi Ballali, ambaye uteuzi wake ulitenguliwa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete, hakuwa mtumishi wa serikali, Tanzania Daima imebaini.
Uhakika kwamba Dk. Ballali hakuwa mwajiriwa wa serikali, ulitolewa hivi karibuni na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, wakati alipokuwa akizungumza na redio moja inayorusha matangazo yake kupitia intanet.
Meghji alisema kuwa, Dk. Ballali alikuwa na mkataba wa kuwa Gavana tu na hakuwa na mkataba wa ajira serikalini, na kumaliza utata uliokuwa umetanda kuhusu iwapo kiongozi huyo alikuwa mwajiriwa wa serikali.
Meghji alisema kuwa, kwa maana hiyo, mkataba baina ya serikali na Dk. Ballali uliisha siku ambapo uteuzi wake wa kuwa Gavana ulipotenguliwa.
Ballali aliteuliwa kama Gavana wa Benki Kuu, alipokuja alikuja kama gavana wa Benki Kuu, hakuwa mtumishi wa Serikali ya Tanzania, alikuja kama gavana tu," alisema.
Kwa upande mwingine, alipoulizwa kuwa iwapo kuna uchunguzi mwingine wowote unaofanywa katika akaunti nyingine za BoT kutokana na madai kuwa Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) iliyochunguzwa ni sehemu ndogo tu ya ubadhirifu, Meghji alisema kuwa hakuna uchunguzi mwingine unaofanyika.
Alisema kuwa kinachoangaliwa hivi sasa ni ripoti ya mkaguzi kuhusu EPA ambayo imeshasimamishwa na kuwa mambo mengine yataangaliwa pia.
Meghji alisema, baada ya mambo yaliyotokea, kuna haja ya kuangalia kwa kina mahusiano baina ya Benki Kuu, kama taasisi na Wizara ya Fedha kwa upande mmoja na serikali kwa upande mwingine.
Alisema kuwa hilo ni muhimu na kuwa kinachopaswa kuangaliwa kiundani ni sheria ya Benki Kuu iliyopitishwa na Bunge mwaka jana.
Waziri huyo alisema kuwa, suala hilo ni muhimu liangaliwe kwa sababu sheria hiyo inampa uhuru Gavana wa BoT kama mtendaji mkuu wa taasisi hiyo nyeti na pia anakuwa Mwenyekiti wa Bodi ya BoT.
Alisema hilo linapaswa kuangaliwa baada ya kubainika kuwa yeye alidanganywa na aliyekuwa Gavana na kusaini barua iliyokuwa inaonyesha kuwa kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd, ililipwa kihalali kwa kazi zinazohusu usalama wa taifa.
Meghji alisema kuwa, BoT inapaswa kuwa huru, lakini uhuru huo unapaswa kuangaliwa na jinsi ambavyo Gavana anafanya kazi na mahusiano yake na Wizara ya Fedha.
Alisema hivi sasa, kisheria, bodi na BoT pamoja na Gavana, wapo huru kufanya mambo yao ingawa kuna wajumbe katika bodi ambao wanatoka nje ya BoT na kuwa hawana haki ya kupiga kura.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Waziri Meghji alikiri kufanya mahojiano na redio hiyo na kusema taarifa alizokuwa nazo ni kwamba Ballali alikuwa akifanya kazi kwa mkataba maalumu, hakuwa mtumishi wa serikali.
http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/2/4/habari3.php