Kumbe anayemwendekeza Chid Benz ni huyu..!! Kalapina amtaja!!

Freyzem

JF-Expert Member
Jun 29, 2013
10,024
24,374
Rapa Kalapina ambaye ni mwanaharakati wa kuwasaidia watu ambao wameingia kwenye matumzi ya dawa za kulevya amefunguka na kusema kuwa mama yake mzazi Chid Benz kama mtu anayemuendekeza Chid na kumfanya asitoke kwenye matumizi ya dawa za kulevya.
Kalapina amesema mama huyo anampenda sana mtoto wake kiasi cha mtoto kujua na kuona kwamba hata akifanya jambo fulani yupo mama yake ambaye atasimama na yeye.

Kalapina alisema hayo jana kupitia kipindi cha Planet Bongo na kusema wazazi wengi wamekuwa chanzo cha watoto wao kuingia kwenye matumzi ya dawa za kulevya na kuingia hata kwenye mahusiano ya jinsi moja sababu ya wazazi wamekuwa wakiwadekeza sana watoto au kuwapa uhuru mkubwa na kuruhusu maisha ya uzungu kutawala.

"Kiukweli mama yake mzazi Chid Benz anampenda sana mwanaye na hali hiyo inampelekea mdogo wangu yule kuona hata nikizingua mama atanitafuta tu, au kuona mama atasimama na yeye tu sababu mama yake anampenda sana, lakini siyo Chid Benz tu wazazi wengi wanawalea watoto kwa kuwadekeza sana, wazazi hawana muda na watoto na hili linachangia vijana kuingia kwenye madawa ya kulevya hata kwenye ushoga pia, lakini sisi wazazi wetu zamani ulikuwa ukizingua unapigwa sana hivyo lazima utanyooka tu" alisema Kalapina.

Source; EATV
 
Huyu kalapina akiongelea mambo ya madawa ya kulevya huwa inanishangaza iwapo km kwel yy hatumii na hajafikiria kutumia.



Kwa hyo huyu Chid benzino analelewa na mama yake? Km kwel bas huu ni utoto wa kiwango cha primary
 
Huyu kalapina akiongelea mambo ya madawa ya kulevya huwa inanishangaza iwapo km kwel yy hatumii na hajafikiria kutumia.



Kwa hyo huyu Chid benzino analelewa na mama yake? Km kwel bas huu ni utoto wa kiwango cha primary
Don't judge the book by his cover.
 
Chid mtoto wa mama!
Watu wameona ndio kiki ya mjini, kama wanamsaidia watoe msaada tu kama hawataki wamwachie mama yake
 
Kalapina anajua ukweli wote. Yuko kwenye harakati za kupiga marufuku miadalati kwa mda mrefu. Sikuzote upendo una sura 2, Wengine tujifunze
 
Sasa mama angefanya nini na hali ni mwanae! sidhani kama huyo Bi mkubwa anapenda mwanae atumie hayo makitu ila basi hana namna, hawezi kumnyima chakula wala kumnyanyapaa! huyo ndio mama, jamani mama ana ladha yake! PUMZIKA KWA AMANI MAMA YANGU.
 
Eti mama yake anampenda sana mwanae sasa unataka ampende nani kama Chid Benz?
Acheni wivu wa kike !!
 
Kwa hali ya kawaida tu huwezi mchukia mwanao tena katika ile hali jamani.Huo ndio tunasema uchungu wa mzazi si kuwa anafurahia ila akimchukia itasaidia nini au ndio itamfanya chid aache madawa?
 
Kumpenda mwanae si jambo baya ila tatizo ni kumdekeza hata akifanya jambo baya asimkanye hapo sifa ya uzazi na ulezi (malezi )unapotea nadhani kalapina mpaka kusema hivyo ameenda mbali na pia kujitoa lawamani kwa namna alivyojishughulisha na suala la rashidi .
Ukifanya kitu kwa nia njema na kujitolea kisha pana mtu ana haribu na wewe kuingia lawamani hapo ndipo unajitoa ulipojificha na kuueleza umma pagumu hapo kwa mzazi wake na ndipo mizizi ya tatizo ilipostawi .
 
Sumu ya teja segerea,kale kawimbo kana maana sana, watu kama hao jela wanapona
 
Huwa najiuliza hivi wasanii wa bongo hawana Baba?
Je huyu Chid hana Baba..
Inaonekana wasanii wengi wa bongo hawakuwahi kulelewa na Wazazi wote wawili!
 
Kila mtu kamweka pembeni huyo chid benz, unafikiri na mama yake akimweka pembeni itakuwaje? Mzazi ni mzazi tu hata mtoto awe na tatizo gani mzazi will always be there. Ndo keshakuwa mwanae haezi kukimbia mzigo wake

mama kuwa mkali mwano akifanya ujinga ili kumuoka kwa faida yake mwenyewe.
 

Similar Discussions

4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom