Elections 2015 Kulinda kura: Wakili Peter Kibatala afungua kesi Mahakama Kuu

Kumbuka mawakili wa serikali/Tume lazima nao waandae utetezi na usishangae wakaomba muda kuandaa utetezi huo

Isitoshe kuna washitakiwa wawil ambao ni NEC na Raisi(serikali).Sasa hapo itategemea kama NEC itajitetea kivyake na serikali nayo itajitetea kivyake.


Tusubiri maana Mahakamani hakuna kesi rahisi hasa kukiwa na mawakili makini kwa pande zote mbili zinazohusika katika kesi.

Japo hii kesi tunaiona rahisi,lakini msishangae mambo yakawa tofauti.

Najua NEC na serikali watashindwa tu katika hii kesi ila ukweli huu hauzui ucheleweshaji wa maamuzi ya mahakama zetu.


Kwa Jaji anayeelewa /Jaji Mkuu lazima atachukua hatua ya hali ya Juu kuzitaka pande zote kuzingatia muda ilikusiwe na vikwazo na kama watashindwa kuzingatia time limit anaweza kutoa maamuzi on best interest of the Country and its people.


 
Ukiniuliza umaarufu wa Marehemu Mchungaji Mtikila, nitakwambia ni uwezo wake wa kufungua kesi nyinginyingi mahakamani ingawa nyingine ni kesi za kipumbavu. Ukawa huu mnaofanya ni umaarufu wa kijinga.

Bila shaka kura zitakuwa zikihesabiwa hadi usiku kabla ya kutangazwa. Sasa unajiuliza vikundi vya watu vilivyojipanga usiku kwa mwemvuli wa kulinda kura si uhatarishaji wa amani huo kwa wakazi wa maeneo husika? Ni kwa msingi huo, Rais kama Amirijeshi wa majeshi yote, jukumu lake namba moja ni kuhakikisha nchi inakuwa salama na yenye ulinzi wa kutosha. Kukusanyika kwa watu makundi kwa makundi usiku, nyie mnaona sawa? Kama hamuismini tume au mawakala wenu uamuzi wa busara ulikuwa kutoshiriki huo uchaguzi chini ya tume msioiamini, kwa kuwa mnashiriki, hamna budi kuiamini.
 
Acha uongo Mkuu askari Kuluta wengi wao ni UKAWA na wanaunga sapoti kwa UKAWA ukiacha hao MA-OCD,RPC Na wakubwa wengine sisi ndio tupo mtaani tunawaona na kuwasikia. Kama hauamini kaangalie matokeo ya KURA kwenye maeneo karibu na kambi za Majeshi utaona UKAWA wanapata KURA nyin gi kuliko CCM. Askari wetu wanachukizwa sana kuendeshwa kisiasa unakuta Katibu wa Wilaya/Kata/Mtaa wa CCM anajidai mamlaka ya kutoa ORDER kwa Police ya kuwakamata wananchi/WANAUKAWA wakati kikatiba hana mamlaka hiyo. Na wengine ni wajeruhiwa/Wahanga wa vipigo kutoka Green Guard Hasa wanapokwenda kuwadhibiti bila kujua wanalindwa na OCD au RPC
 
Mkae mita Mia au 50 nyinyi hamna jema maana mkishindwa hata kama mngekuwa humo humo chumbani bado hamtaamini maana mmeingia kwenye ushindani huku mkiwa na yenu kichwani. Naomba busara za Mahakama ziseme tu hakuna kuwayawaya karibu na kituo kwa mazingira yaliyopo sasa. Hivi kura zingekuwa zinapigwa online mngelinda wapi?

Kwa maana hiyo UKAWA wako wengi kushinda CCM? Mimi nitalinda mita 1 nakwenda asubuhi na mapema nawahi foleni sipigi KURA nawapisha tu maccm, walemavu na wazee ikifika saa Tisa ndio naingia chumba cha Kupigia KURA ni kwa wana UKAWA wote kwenye Jimbo letu. Mtasanda mwaka huu kama mtaleta mabomu ili mvurugue UCHGUZI ili muendelee kubaki madarakani Mbinu yenu imeshindwa
 
Back
Top Bottom