Elections 2015 Kulinda kura: Wakili Peter Kibatala afungua kesi Mahakama Kuu

Nice move,ila pia wafanye utaratibu wa kumlima Kikwete kwa wawakilishi wa nchi za Ulaya,International Observers na ICC kwa kitendo chake cha kuingilia NEC huku akipotosha idadi ya wapiga kura na kutoa vitisho vya kutumia mabavu/kuvunja amani!!!

Tunatakiwa kuanzia humu ndani kabla ya kwenda ICC.
 
Hii labda ni tafsir ya kwenu ! Binafs ntabak tena 0 distance! Nshajichokea mm! Sikien nyie waasherati wa magamba hii nchi ni yetu sote
Usichokijua ni kuwa sheria ya Uchaguzi inasema siku ya kupiga kura hakutakuwa na mikusanyiko ya kisiasa.Mikusanyiko yote ya kisiasa mwisho wake ni siku ya mwisho wa kampeni ambayo ni tarehe 24 octoba 2015.Ukikusanya watu wako siku hiyo ya uchaguzi wawe wana UKAWA au CCM wakajikusanya mahali ni kosa kisheria.

Pili kwa mujibu wa sheria zinazohusu mikusanyiko ni lazima kutoa taarifa polisi kuwa kutakuwa na mkusanyiko mahali fulani na kwa lengo gani. Hivyo kama kurtakuwa na watu wenye lengo la kukusanyika popote inabidi wawasilishe maombi yao polisi wakijieleza wao ni akina nani ili wapewe ulinzi wa polisi

Tatu kuna sheria ya ardhi.Unaposema utakusanyika hapo kwenye mita 200 hilo eneo ni mali ya baba yako au mama yako? Huyo mwenye miliki ya hiyo ardhi karidhia? Hivyo kama kuna watu watakaotaka kukusanyika ni lazima wapeleke kibali cha mwenye eneo kuwa karidhia eneo lake litumike kwa mikusanyiko.Na kwamba mikusanyiko hiyo haitakuwa kero wala bugudha kwa wakazi wa eneo husika,majirani n.k Maana kama watu watajiamulia kukusanyika hiyo mita mia 200 bila mwenye eneo lake kuridhia ina maana ni uvamizi wa ardhi ya mtu bila ridhaa yake.Na huo ni uvunjifu wa amani kwenye eneo la watu.Hivyo Mahakama lazima iangalie maslahi ya wenye maeneo maeneo yao yasije vamiwa SIKU YA KUPIGA KURA NA KUKALIWA KWA MABAVU na hao wanaojiita walinda kura.

Polisi kwa kuliona hilo kuwa kutakuwa na uvunjaji sheria kwa watu kuvamia maeneo ya watu na kujikusanya wakasema kila mtu aende kwake asubirie kwake.Sababu vituo vya kupigia kura haviko mbali na makazi ya watu.Kwa nini watu wakae kwenye viwanja vya watu? Mahakama iliangalie hilo

Kwangu sikubali mtu akusanyike WALA KUWEKA MAKALIO YAKE KWENYE ENEO LANGU NITAITA DEFENDER NA GARTI LA WASHA WASHA HARAKA WAJE NA MABOMU NA VIRUNGU WAONDOE WAVAMIZI KWENYE ENEO LANGU.

Hawa akina KIBATALA wanataka kuleta vurugu na ugomvi kati ya wenye maeneo na hao watu anaotaka wakusanyike hizo mita mia mbili sababu sio kwao ni kwa watu.

Eti bila haya lowasa na mbowe wanatoa amri mkimaliza kura kaeni mita 200.Hilo eneo wanaloamrisha watu wakae ni la baba yake au mama yake lowasa au mbowe.Sheria ya ardhi iheshimiwe majaji msimamie hilo kwa maslahi ya wenye maeneo yao.Mkiwakubalia mnawaweka wenye maeneo matatizoni.
 
Tayari wakili jembe na nguli Peter Kibatala akiambatana na wanasheria nguli wa Ukawa Prof Safari, Mallya na Tundu Lissu asubuhi ya leo amefungua kesi mahakama kuu kuishitaki NEC kwa ukiukwaji wa sheria juu ya wananchi kukaa mita mia mbili na kulinda kura.

Kesi imefunguliwa under certificate of urgency nadhani kama sijakosea kwa kiswahili ni 'hati ya dharura' ili isikilizwe na tafsiri itoke kabla ya uchaguzi.Tayari jalada lishapelekwa kwa pilato na wanasheria nguli wa Ukawa wamejipanga kwa hoja za nguvu na ushahidi wa kutosha.

Pia jopo la wanasheria nguli wa UKAWA wameiomba mahakama kuu ya Tanzania kutoa tafsiri ya kisheria juu ya matamshi ya rais wa nchi kuwa alitumia mamlaka gani kuvaa kazi za tume.

Haisaidiii kitu...hatopata jibu mpaka uchaguzi uishe....umeshaambiwa ukishapiga kura nenda kalale nyimbani kwako....unataka nn sasa.???sheria sheria sheria...babake nani.????
 
Haisaidiii kitu...hatopata jibu mpaka uchaguzi uishe....umeshaambiwa ukishapiga kura nenda kalale nyimbani kwako....unataka nn sasa.???sheria sheria sheria...babake nani.????

Mnataka kuiba nini!? mbona mnang'ang'ania tuondoke!? Hatuondokiiijjjijjjjjjiiiiiijii.
 
SATURDAY, OCTOBER 17, 2015

Sakata la kulinda kura latua Mahakama Kuu

pic+amy.jpg
Peter Kibatala

Kwa ufupi

Aliyefungua kesi hiyo ya kikatiba mahakamani ni mpigakura na mgombea ubunge wa viti maalumu katika Jimbo la Kilombero kupitia Chadema, Amy Pascience Kibatala akiomba litolewe tamko kuhusu tafsiri ya kifungu cha 104 (1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, sura ya 343 Ilivyorejewa mwaka 2010.

By James MagaiDar es Salaam. Hatimaye mvutano kati ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na vyama vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuhusu umbali wa mwananchi kusimama baada ya kupiga kura, umetinga Mahakama Kuu.

Aliyefungua kesi hiyo ya kikatiba mahakamani ni mpigakura na mgombea ubunge wa viti maalumu katika Jimbo la Kilombero kupitia Chadema, Amy Pascience Kibatala akiomba litolewe tamko kuhusu tafsiri ya kifungu cha 104 (1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, sura ya 343 Ilivyorejewa mwaka 2010.

Chadema, Amy Pascience Kibatala akiomba litolewe tamko kuhusu tafsiri ya kifungu cha 104 (1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, sura ya 343 Ilivyorejewa mwaka 2010.

Kibatala amefungua kesi hiyo dhidi ya Mwasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Mwenyekiti wa NEC, chini ya hati ya dharura. Shauri hilo namba 37 la mwaka 2015, limefunguliwa baada ya NEC kuwataka wananchi, baada ya kupiga kura Oktoba 25, warudi nyumbani huku Ukawa unaoundwa na Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD wakihimiza wanachama na wafuasi wao kulinda kura kwa kukaa umbali wa mita 200 baada ya kupiga kura kama sheria inavyosema.

Awali NEC iliwataka wapigakura kurudi nyuma hadi mita 200 baada ya kupiga kura lakini baadaye iliwataka wapigakura kurudi nyumbani. Msimamo huo ulitolewa pia na Rais Jakaya Kikwete siku ya maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 16 ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ambapo aliwataka wapigakura kwenda nyumbani baada ya kupiga kura.

Akihutubia katika maadhimisho hayo Oktoba 14 yaliyokwenda sambamba na tukio la kuzima Mwenge wa Uhuru, mjini Dodoma, Rais Kikwete alitoa wito kwa watu wote kurudi majumbani kwao mara tu baada ya kumaliza kupiga kura.

Katika shauri hilo, Kibatala anaiomba Mahakama Kuu itoe tamko la tafsiri sahihi ya kifungu hicho kinachohusu haki ya wapigakura na wadau wengine wa uchaguzi kukaa zaidi ya umbali wa mita 200 kutoka katika kituo cha kupigia kura na cha kuhesabia kura.

Kwa mujibu wa Kibatala msimamo wa NEC ni kinyume cha Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania hususan Ibara ya 18 (1), 21 (2), 29 (2). Pia, anadai kuwa Rais Kikwete wakati akihutubia wananchi kwenye maadhimisho ya kifo cha Baba wa Taifa,licha ya kuamuru watu wasikae katika eneo hilo, pia alikwenda mbali kwa kuwatisha wapigakura kuwa watakaokaidi amri hiyo vyombo vya dola vitatumia nguvu dhidi yao.

Kibatala anadai kuwa akiwa mpigakura aliyesajiliwa na anayekusudia kutumia haki ya msingi kushiriki mchakato huo wa uchaguzi, zuio hilo linakiuka haki za kikatiba zinazobainishwa katika Ibara ya 5(1), 18 (1), 21 (2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kibatala anadai kuwa zuio hilo linaathiri haki ya kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi uliotangazwa kuwa utakuwa wa wazi.

Vilevile, anadai kuwa zuio hilo linaelekea kumnyima haki ya kufuatilia kwa karibu mchakato wa uchaguzi kutoka umbali uliowekwa kisheria ambao unamwezesha kuwapo wakati wa kutangazwa kwa matokeo kwa kuzingatia kuwa hakuna utaratibu rasmi wa NEC kuwaita wapiga kura kusikiliza matokeo.


Chanzo : Gazeti la Mwananchi.
 
Mkae mita Mia au 50 nyinyi hamna jema maana mkishindwa hata kama mngekuwa humo humo chumbani bado hamtaamini maana mmeingia kwenye ushindani huku mkiwa na yenu kichwani. Naomba busara za Mahakama ziseme tu hakuna kuwayawaya karibu na kituo kwa mazingira yaliyopo sasa. Hivi kura zingekuwa zinapigwa online mngelinda wapi?
 
Kwa hiyo shida ni kusema tunalinda KURA basi? Nawashauri CHADEMA/UKAWA wasiseme tunalinda KURA na wasiende kukaa umbali wa mita 200 tunatakiwa tusimame mita moja. Kila mwana UKAWA awahi kituoni mapema kwenye mstari lakini asipige KURA inapokaribia zamu yake arudi nyuma mpaka wana ccm wote, wazee na wanawake wamalize ndipo mafansi wa UKAWA wapige KURA cha kuzingaatia ni kuhakikisha kuwa kwenye foleni kabla ya muda wa kufunga vituo. Maana CCM wameandaa vurugu ili serikali ya 2015/20 iwe ya mseto na KWA KUMPA lOWASA UWAZIRI MKUU tuwe makini sana na hawa jamaa.

Kosa kubwa ambalo tujifunze toka nchi zingine ni kuwa ukikubali kuwa sehemu ya serikali ya mseto ni mtego mbaya sana wa kukudhoofisha kisiasa. Kwani hapo baadaye uchaguzi ujao hutakuwa na hoja ya kuipinga hiyo serikali kwani nawe ni sehemu ya hiyo serikali. Tumeyaona hayo kwa Tsangirai wa Zimbabwe, Raila wa Kenya na nadhani hata maalim Seif huko znz kama vile kashapunguzwa makali yake. Heri kukomaa na kuwa mpinzani tu mpaka siku kitaelewaka tu kama rais fulani huko afrika magharibi nimemsahu jina ila ni mzee wa kipara sana, aligombea kwa miaka ishirini mpaka siku ikafika akashinda. Lakini maombi yangu ni ukawa kushinda this 2015.
 
Ukae kwenye public road??? Ukikaa kwenye public road ina maana umefunga bara bara wakati inatakiwa kuwa wazi ili kuwezesha FFU na defender zao wapite kwa uhuru na watumiaji wengine wa barabara waitumie kwa uhuru.

Kukaa kwenye public road ni kujitangazia kiyama wewe mwenyewe mkaaji sababu polisi watakuja na mabomu na virungu kuvurumisha waliofunga baraba kwa kukaa ili kuhakikisha wanaifungua ili watumiaji wengine wa bara bara waendelee kuitumia.

Ok, basi ngoja tusubiri hao polisi wasiofika elfu arobaini dhidi ya vituo vya kupigia kura elfu sitini na wapiga kura milion ishirini na ushee
 
Ok, basi ngoja tusubiri hao polisi wasiofika elfu arobaini dhidi ya vituo vya kupigia kura elfu sitini na wapiga kura milion ishirini na ushee

Kwani hujui kuwa majeshi yote ya ulinzi na usalama yanakuwa kazini kipindi cha uchaguzi?

Wana ndege na helikopta na magari standby yenye spidi za kuua mtu.Kiasi kuwa likitokea jambo mahali pakizidiwa nguvu ni dakika tu magereza,jwtz,usalama wa taifa,JKT NK watakuwa wameshatua hapo tayari kutembeza kipigo cha mbwa mwizi.

Na makomandoo wengi watakuwa wamevaa kiraia wakisubiria raia anayetaka kukiinukisha wakiwa wamejichanganya na raia.Jaribu uone kama hawanyofoa hicho kinyeo chako kilicho katikati ya makalio.
 
Kwani hujui kuwa majeshi yote ya ulinzi na usalama yanakuwa kazini kipindi cha uchaguzi?

Wana ndege na helikopta na magari standby yenye spidi za kuua mtu.Kiasi kuwa likitokea jambo mahali pakizidiwa nguvu ni dakika tu magereza,jwtz,usalama wa taifa,JKT NK watakuwa wameshatua hapo tayari kutembeza kipigo cha mbwa mwizi.

Na makomandoo wengi watakuwa wamevaa kiraia wakisubiria raia anayetaka kukiinukisha wakiwa wamejichanganya na raia.Jaribu uone kama hawanyofoa hicho kinyeo chako kilicho katikati ya makalio.
Hata hao askari hawaipendi ccm, chukua hiyo. Hivi vi laki tatu mlivyowaongezea juzi wamegundua ni danganya toto. Ccm out. To hell ccm.
 
Back
Top Bottom