MwlNyerere alitaifisha shule,vyuo na hospital zilizojengwa na wakristo na kuwa mali ya serikali ili kuweka usawa lakini tunashangaa kasi ya marais wetu sasa ya kutumia nafasi zao kuwapendelea waislamu, Rais wa awamu ya tatu alithubutu kutoa majengo ya serikali ili waislamu waanzishe chuo kikuu morogoro na sasa tunaona Mkuu mkoa anatoa ahadi ya kujenga ofisi za bakwata na Rais anamalizia kwa kuomba kujengwa kwa msikiti hii ni hatari kwa viongozi wa kisiasa kujiingiza katika mambo ya dini .Tuwache taasisi za dini zifanye mambo yao wenyewe.Rais alichotakiwa kufanya ni kumkutanisha shehe mkuu na mfalme ili waislamu wajisemee mambo yao.Angeomba ujenzi wa Chuo Kikuu cha Kiislamu angekuwa amewakomboa Waislamu