Ulimbo
JF-Expert Member
- Aug 14, 2009
- 3,767
- 4,035
Jana usiku nilishangaa sana kuona Makamba anampigia debe Mh. 6 jimboni mwake kuwaambia wapiga kura kuwa wao ni wajanja ndo maana waliweza kumchagua mtu ambaye ni mjanja, na pia kwa sababu wabunge nao ni wajanja, wakamchagua 6 kuwa Spika. Laa ajabu zaidi walekwenda mpaka nyumbani kumsalimia mama mzazi wa sita na machache yaliyozungumzwa ni kwamba sita na makamba hawana ugomvi wowote bali kuna watu wanawagombanisha. Wote wawili sita na makamba walipokezana katika kusema hiyo. Nijuavyo mimi hapa nyuma uhusiano wao haukuwa mzuri, Wana JF naombeni mnisaidie kujua ni nani aliowagombanisha? au kati ya hawa wawili ni nani msema kweli?