Kulikoni Singida hakuna mwakilishi baraza la mawaziri?

Tumsifu Samwel

JF-Expert Member
Jul 30, 2007
1,407
159
Nilipata fursa ya kumuuliza mh. JK kwa nini mkoa wa Singida hauna mwakilishi kwenye baraza lake la mawaziri? zaidi ya John chiligati na ambaye siyo mzawa wa mkoa wa Singida? jibu: "we bana vipi? wabunge wengi wa singida elimu yao ni kidato cha nne unategemea mtu kama huyo umpe uwaziri afanye nini ?"

Hivi mtu mwenye elimu ya kidato cha nne hawezi kuongoza wizara kwa sababu ya kiwango chake cha elimu?
 
Nilipata fursa ya kumuuliza mh. JK kwa nini mkoa wa Singida hauna mwakilishi kwenye baraza lake la mawaziri? zaidi ya John chiligati na ambaye siyo mzawa wa mkoa wa Singida? jibu: "we bana vipi? wabunge wengi wa singida elimu yao ni kidato cha nne unategemea mtu kama huyo umpe uwaziri afanye nini ?"

Hivi mtu mwenye elimu ya kidato cha nne hawezi kuongoza wizara kwa sababu ya kiwango chake cha elimu?
Uteuzi wa nafasi za mawaziri hazitegemei ni watu wa wapi, ila pia sio kweli kuwa wabunge wa Singida wengi ni ma Form Four Levers,
Nyalandu ni graduate, Dewjini graduate, Martha Mlata ni graduate, etc tena hawa ni wale ninaowajua kihivi hivi kabla hata sijapekua CV zao.
Hivyo kwa Singida si afadhali hata mnaye huyo Chiligati, mngekosa kabisa ingekuwaje?.
 
Heshima kwako Carthbetl,

Nadhani yuko Mheshimiwa Lazaro Nyalando ni msomi wa chuo kikuu.
 
CL Hapo unatudanganya, jibu kama hilo hawezi kutoa JK. Hata hivyo Mkoa wa Singida una zaidi ya kabila tano ikiwemo ya Chiligati ambayo ni Mgogo. Si vibaya kujadili hoja yako kwa nini hakuna waakilishi.
maelezo ya watu wa Mkoa wa Singida ni kwamba ni watu wa ajabu sana.si kwamba hakuna wasomi, wala si kwamba ni maskini sana, la hasha bali ni ule ushawishi wa kuingia kwenye siasa hawana.matatizo kwao ni kama sehemu ya maisha . We anagalia barabara sehemu ya mkoa huu tu haijakamilika na ndio kuu kushinda zote. Cha ajabu nikwamba wanajisikia wao ni mashini sana kwa hiyo hata akipwa fulana au shs 200 mtu anaona kasaidiwa sana. Halafu pia watu wa huko wanaangalia anagombea ni wa ukoo gani au babu/baba yake akuliwa nani kama hawamjui vizuri yaani aliwahi kuwasaidia hupati kitu.
wabunge wa singida
MANYONI - 2- level -MASTERS
SINGIDA-3 -Level -Diploma
IRAMBA-2- Level -F -IV na Diploma
VITI MAALUM- F IV na DRS 7

Kazi ipo kuweza kuwabalisha , labda mwaka huu - big up LISSU AND JUMBE
 
Uteuzi wa nafasi za mawaziri hazitegemei ni watu wa wapi, ila pia sio kweli kuwa wabunge wa Singida wengi ni ma Form Four Levers,
Nyalandu ni graduate, Dewjini graduate, Martha Mlata ni graduate, etc tena hawa ni wale ninaowajua kihivi hivi kabla hata sijapekua CV zao.
Hivyo kwa Singida si afadhali hata mnaye huyo Chiligati, mngekosa kabisa ingekuwaje?.

Martha Mlata ambaye ni Mbunge wa viti maalumu toka mkoa wa Singida ninayemfahamu mimi sio GRADUATE labda kama kagraduate leo.
 
CL Hapo unatudanganya, jibu kama hilo hawezi kutoa JK. Hata hivyo Mkoa wa Singida una zaidi ya kabila tano ikiwemo ya Chiligati ambayo ni Mgogo. Si vibaya kujadili hoja yako kwa nini hakuna waakilishi.
maelezo ya watu wa Mkoa wa Singida ni kwamba ni watu wa ajabu sana.si kwamba hakuna wasomi, wala si kwamba ni maskini sana, la hasha bali ni ule ushawishi wa kuingia kwenye siasa hawana.matatizo kwao ni kama sehemu ya maisha . We anagalia barabara sehemu ya mkoa huu tu haijakamilika na ndio kuu kushinda zote. Cha ajabu nikwamba wanajisikia wao ni mashini sana kwa hiyo hata akipwa fulana au shs 200 mtu anaona kasaidiwa sana. Halafu pia watu wa huko wanaangalia anagombea ni wa ukoo gani au babu/baba yake akuliwa nani kama hawamjui vizuri yaani aliwahi kuwasaidia hupati kitu.
wabunge wa singida
MANYONI - 2- level -MASTERS
SINGIDA-3 -Level -Diploma
IRAMBA-2- Level -F -IV na Diploma
VITI MAALUM- F IV na DRS 7

Kazi ipo kuweza kuwabalisha , labda mwaka huu - big up LISSU AND JUMBE

Kwani suala la ujenzi wa barabara kuu ni la wananchi wa Singida au ni la Serikali kuu? Serikali ya Tanzania imewekeza nguvu zake nyingi Dar es Salaam pekee na Mikoa mingine imesahaulika kabisa au inakumbukwa kidogo! Sasa hivi Dar es Salaam haikaliki kwa msongamano wa ajabu! Na huko unakosema watu wa Singida wameridhika na vijishilingi 200 ni tusi kubwa sana na inaonesha una chuki na watu wa Mkoa huo. Hivi CCM wanapohonga chumvi, T-Shirt, Kofia, Vitenge, nk huwa wanavipeleka Singida pekee? Na kama sivyo hiyo mikoa mingine huwa wanapokea vitu hivyo kwa sababu wao ni "matajiri?" Hukumu kwa haki ndugu yangu na si kutoa kejeli zisizokuwa na msingi wowote!
Kama JK alidai kuwa Singida hakuna wasomi isipokuwa walioishia kidato cha nne tu simwelewi mheshimiwa huyu. Labda kama alikuwa "anatania" kama alivyotania kwenye suala la TAKRIMA!
 
Martha Mlata ambaye ni Mbunge wa viti maalumu toka mkoa wa Singida ninayemfahamu mimi sio GRADUATE labda kama kagraduate leo.

Huyu mama alikuwa UK akisoma kwa muda wa kama miaka miwili au mitatu. Nafikiri kwasasa ni graduate. Sijui kama alikuwa anasoma first degree au masters.

Viongozi wakija, alikuwa ndiye anatuanzishia wimbo wa taifa.
 
Nilipata fursa ya kumuuliza mh. JK kwa nini mkoa wa Singida hauna mwakilishi kwenye baraza lake la mawaziri? zaidi ya John chiligati na ambaye siyo mzawa wa mkoa wa Singida? jibu: "we bana vipi? wabunge wengi wa singida elimu yao ni kidato cha nne unategemea mtu kama huyo umpe uwaziri afanye nini ?"

Hivi mtu mwenye elimu ya kidato cha nne hawezi kuongoza wizara kwa sababu ya kiwango chake cha elimu?


Hapa unamuonea JK......

Ili aweze kusema hivyo itabidi afikiri kwanza anachokisema, ......hapo tu ni kazi tayari.....
 
Baraza la mawaziri ambalo halieleweki linafanya kazi gani? Hebu mtupumzishe huko..ebo
 
CL Hapo unatudanganya, jibu kama hilo hawezi kutoa JK. Hata hivyo Mkoa wa Singida una zaidi ya kabila tano ikiwemo ya Chiligati ambayo ni Mgogo. Si vibaya kujadili hoja yako kwa nini hakuna waakilishi.
maelezo ya watu wa Mkoa wa Singida ni kwamba ni watu wa ajabu sana.si kwamba hakuna wasomi, wala si kwamba ni maskini sana, la hasha bali ni ule ushawishi wa kuingia kwenye siasa hawana.matatizo kwao ni kama sehemu ya maisha . We anagalia barabara sehemu ya mkoa huu tu haijakamilika na ndio kuu kushinda zote. Cha ajabu nikwamba wanajisikia wao ni mashini sana kwa hiyo hata akipwa fulana au shs 200 mtu anaona kasaidiwa sana. Halafu pia watu wa huko wanaangalia anagombea ni wa ukoo gani au babu/baba yake akuliwa nani kama hawamjui vizuri yaani aliwahi kuwasaidia hupati kitu.
wabunge wa singida
MANYONI - 2- level -MASTERS
SINGIDA-3 -Level -Diploma
IRAMBA-2- Level -F -IV na Diploma
VITI MAALUM- F IV na DRS 7

Kazi ipo kuweza kuwabalisha , labda mwaka huu - big up LISSU AND JUMB


Naheshimu sana mawazo yako lakini unapaswa kuheshimu watu wengine pia kabla hujatoa mawazoyako, unaposema singida hawana ushawiashi wa kuingia kakatika siasa umetumia kigezo gani hebu fafanua tafadhali,watu wa singida wanaushawishi wa siasa kama watanzania wote na ndio maana kila mwaka wanafanya chaguzi kama kawida na wabunge wapo na wewe unawajua, tena kwa taarifa yako wabunge wasingida nimiongoni mwa wa bunge wanaoongoza kwa kutoa michango mingi katika bunge hili hii inaonyesha jinsi walivyo active katika siasa swala la barabara kuwalaumu watu wa singida ni ufinyi wa mawazo ambao siwezi kuueleza, kuhusu t shirt na sh 200 hii ni nchi nzima hata dar penyewe tunaona haya mambo yapo wakati wa uchaguzi. jimbo la manyoni lipo singida lakini wakaazi wake wengi ni wagogo na ndio maana chilgati ni mgogo, Swala la kuwa na waziri kutoka singida chiligati ni wa singida, hata hapo nyuma nalaila kiula aliwahi kuwa waziri, pia nkangaa pia aliwahi kuwa waziri. uteuzi wa mawaziri ni juu ya rais mwenyewe kuona nani anamuamini anaweza kufanya nae kazi.swala la wtu kuchaguana kwa kujuana kiukoo sio kweli unataka kuushawishi umma uamini kuwa nikoo fulani tu ndizo zinachaguliwa katika siasa singida, haya ni mambo ya ushawishi wa mtu binafsi inawezekena kweli ikawa babu yangu alikua mwenyekit wa chama zamani na anajulikana na mimi mtoto nikatumia hiyo advantage kugombea hii tunaiona kote ndio maana leo wakina karume mwinyi kawawa mnauye kikwete nk watoto wao nao wamo hata hivyo hiyo dhana sijui umeitoa wapi mfano jimbo la sgd mjini mwanzo alikua nkangaa na sasa ni dewji hawana uhusiano wowote, kilimba na kiula hawana uhusiano kabisa, nyalandu na aliye mtangulia hali kadhalika.
 
We CathbertL hilo sio jambo la Kuuliza. Hivi haujui kuna maswala mbalimbali yanayohusisha logistics za Kimataifa. Sasa huoni kwa elimu hiyo tutaishia kuwa na mawaziri watakaokuwa wanaingia mikataba bila kuielewa sawasawa?
Hapa ndugu yangu tuwe wakweli na tuache unazi.!
Mimi ninachojiuliza je Singida hakuna hata Mbunge mmoja mwenye Degree?
Kama ni hivyo mwaka huu tuwachague kina Tundu Lisu wengi.!
 
Mohammed Dewji graduate,chiligati graduate,Nyalandu Masters,martha mlata nadhani atakua amemaliza masomo uk shahada ya kwanza,
 
Kwa mtazamo wangu sidhani kama Baraza la Mawaziri ni baraza la kuwakilisha mkoa, kwa nchi yetu baraza la mawaziri ni kubwa sana kulinganisha na nchi zilizoendelea kama USA na UK.

Mtu unapozungumzia baraza la mawaziri yakupasa kujua kuwa ile dhamana ya Uwaziri si dhana ya kisiasa kama ilivyo kwa sasa, na nahisi imekuwa hivyo kwa kuwa siku zilizotangulia kulikua na wasomi wachace wanaojishughulisha na siasa tofauti na sasa.

Inabidi Uwaziri iwe ni nafasi ya kuteuliwa kulingana na uelewa ("profession") juu ya wizara husika na si kuwa umetokea mkoa gani.
 
Nilipata fursa ya kumuuliza mh. JK kwa nini mkoa wa Singida hauna mwakilishi kwenye baraza lake la mawaziri? zaidi ya John chiligati na ambaye siyo mzawa wa mkoa wa Singida? jibu: "we bana vipi? wabunge wengi wa singida elimu yao ni kidato cha nne unategemea mtu kama huyo umpe uwaziri afanye nini ?"

Eh! Wazawa wa Mkoa wa Singida ndio akina nani na Chiligati si mzawa kwa vipi? Kama Chiligati si mzawa wa Singida na Dewji naye tutamwitaje? Ni aibu sana kuzungumzia habari za 'uzawa' kwa misingi ya mikoa na wakati huo huo tunataka kujivuna kwamba tuna nchi ambayo imekwishatoka kwenye enzi ya ukabila!
 
Na huko unakosema watu wa Singida wameridhika na vijishilingi 200 ni tusi kubwa sana na inaonesha una chuki na watu wa Mkoa huo. Hivi CCM wanapohonga chumvi, T-Shirt, Kofia, Vitenge, nk huwa wanavipeleka Singida pekee? Na kama sivyo hiyo mikoa mingine huwa wanapokea vitu hivyo kwa sababu wao ni "matajiri?" Hukumu kwa haki ndugu yangu na si kutoa kejeli zisizokuwa na msingi wowote!


bucha: Sina chuki usinielewe vibaya .



Naheshimu sana mawazo yako lakini unapaswa kuheshimu watu wengine pia kabla hujatoa mawazoyako, unaposema singida hawana ushawiashi wa kuingia kakatika siasa umetumia kigezo gani hebu fafanua tafadhali,

paul: kuna wasomi wengi singida mbona hawajitokezi kugombea nafasi za siasa? na hao wachache wanaojitokeza mbona basi hawapati? fanya utafiti uone watu waliojitokeza wasomi 2005 lakini wakshindwa? tatizo ni nini?

kufanya uchaguzi kila mara hilo sio sababu kuwa na ushawishi , kinachotakiwa je wanachangua right person ? angalia kwa mtazamo huo wala mimi sina nia mbaya na watu singida
 
Hutaweza kuongoza nchi kama ukitaka kila mkoa upate mtu katika teuzi mbali mbali. Huo ni ukanda na ni hatari kwa taifa kwani kwenye U-DC, U-RC ubalozi nanafasi zingine
 
Ni Urambo tu yenye bahati nzuri. Imetoa Speaker, Mke wa Speaker, na Prof Kapuya wote wazito nji hii!
 
Back
Top Bottom