Papi Chulo
JF-Expert Member
- Jun 8, 2018
- 6,260
- 7,389
Unajua hata haya maviongozi yetu yanatuangusha sana,hivi we fikiria likiongozi kama bashite kweeeeeeeliiiiWabaya ni viongozi wa Afrika .
Mchina anakuja kuwekeza mpaka kwenye kamari na kutuuzia pipi na biscuit .
Hivi kweli Afrika hatuwezi kutengeneza hata biscuit za kula watoto wetu?
Ukipita mpaka vibarabara vya kumwaga Moramo unakuta wajenzi ni Wachina .
Kuna tatizo kwenye akili zetu sisi waafrika. Haiwezekani pesa za kodi zetu asilimia kubwa tunawapelekea wachina.
Mpaka Tails na Vikombe tunaagiza kutoka China.
Tunauziwa vitu vya hovyo toka China badala ya kuvipiga marufuku.
Viwanda vyetu ni vipi na vitakua lini kama tunaagiza mpaka viberiti na toothpicks toka China!!
Tuagize mitambo lakini sio uchafu. Viwanda vyetu vya betri vimekufa zimebaki betri za kutumia siku mbili kwenye tochi na radio.
Acha tutukanwe .
Tunaiga mpaka namna ya kishenzi ya kufanya ngono bila kuwa na kiasi. Vijana vijiweni wanawaza ngono wakati hawana nguvu za kiume yaana fedha .
Waafrika tunaiga mambo ya hovyo kutoka kwa watu wa hovyo.
Kuna MTU aliiga Bajaji akaimodify akatengeneza ya kwake . TBS wakampiga Vita kama korona. Leo hii Tanzania tungekua tunawauzia warundi Pikipiki za miguu mitatu.
Tuna Kiwanada cha Nyumbu pale kibaha lakini sioni hata Lori la kubeba kuni kwenye kambi za Jeshi lenye Nembo ya NYUMBU zaidi ya gari za wahindi Ashock Land. Yote ni ubinafsi na uroho wa kupata Mali bila kufikirisha vichwa na kisha kutumia fedha za kifisadi kwenye ulevi na wanawake na kujenga mafensi ya nyumba.
Sent using Jamii Forums mobile app