Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Leo asubuhi nimesikia habari Radio Free Afrika kuwa mwanasiasa machachari kutoka CHADEMA Tundu Lissu aliomba kufanya mhadhara katika viunga vya chuo kikuu SAUT Mwanza. hata hivyo hilo halikufanikiwa baada ya uongozi wa chuo hicho kumueleza Lissu kuwa endapo alitaa kufanya mhadhara huo basi condition mojawapo ni kumtaka akubali viongozi wa CCM waalikwe.
Baada ya majadiliano ya muda mrefu na Mh. Lissu kuubana uongozi wa SAUT ilibainika kuwa uongozi wa chuo ulipata maelekezo kutoka kwa "wanaojiita usalama wa taifa" kuwa mwanasiasa huyo asiruhusiwe kufanya mhadhara huo.
Akihojiwa na mwandishi wa habari wa RFA, Lissu alionyesha masikitiko yake kwa uongozi wa taasisi kubwa ya kisomi kama SAUT kuzuia wanafunzi kupata haki yao ya kusikiliza na kutoa maoni yao na hasa katika kipindi hiki ambacho Tanzania inapita katika mchakato wa kupata katiba mpya.
Baadhi ya wanafunzi wa SAUT nao wakihojiwa waliulaumu sana uongozii wa chuo chao kukubali kuburuzwa na CCM na pia kuwanyima wao kama wasomi wa chuo kikuu kupata nafasi kumsikiliza mwanasiasa huyo na wao kupata nafasi kushiriki katika mhadharo huo.
My take: CCM ni zaidi uijuavyo!!
Baada ya majadiliano ya muda mrefu na Mh. Lissu kuubana uongozi wa SAUT ilibainika kuwa uongozi wa chuo ulipata maelekezo kutoka kwa "wanaojiita usalama wa taifa" kuwa mwanasiasa huyo asiruhusiwe kufanya mhadhara huo.
Akihojiwa na mwandishi wa habari wa RFA, Lissu alionyesha masikitiko yake kwa uongozi wa taasisi kubwa ya kisomi kama SAUT kuzuia wanafunzi kupata haki yao ya kusikiliza na kutoa maoni yao na hasa katika kipindi hiki ambacho Tanzania inapita katika mchakato wa kupata katiba mpya.
Baadhi ya wanafunzi wa SAUT nao wakihojiwa waliulaumu sana uongozii wa chuo chao kukubali kuburuzwa na CCM na pia kuwanyima wao kama wasomi wa chuo kikuu kupata nafasi kumsikiliza mwanasiasa huyo na wao kupata nafasi kushiriki katika mhadharo huo.
My take: CCM ni zaidi uijuavyo!!