Lini Viwanja vinavyomilikiwa na CCM vitakuwa chini ya umiliki wa Serikali Kuu au Halmashauri husika?

Nemesis

JF-Expert Member
Feb 13, 2008
5,462
4,364
kirumba.jpg
Uwanja wa CCM Kirumba ambao unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM)

Enzi za chama kimoja, majengo na maeneo yote ya umma yalikuwa chini ya Serikali. Ujenzi na uendelezaji wa maeneo hayo ulifanya na Serikali kupitia kodi za wananchi, michango, fedha za wafadhili na wahisani mbalimbali.

Kwa namna isiyoeleweka baadhi ya maeneo hayo yameporwa na CCM na kuwa mali ya chama.

Kwa uchache tu natoa mfano: Uwanja wa CCM Kirumba (Mwanza), Samora (Iringa), Sokoine (Mbeya), Shekh Amri Abed (Arusha), Majimaji (Songea), Kaitaba (Kagera) nk.

Umiliki huu ni kero siyo tu kuikosesha mapato Serikali bali kero kwa wanamichezo, wananchi wa kawaida na Halmashauri za Manispaa/Miji. Kwa mfano: fuatilia habari hiihapa chini: kero zilizojitokeza

1) CCM (M)Iringa imefunga uwanja wa Samora hali inayowanyima haki wananchi kub urudika.
2) Ligi wa Taifa ngazi ya mkoa imevurugwa kwa kukosa uwanja
3) Matamasha yaliyopangwa kufanyika yamevurugwa.

Swali: Mpaka lini viwanja hivi vitabaki mikononi mwa CCM badala ya Serikali kuu au Halmashauri husika?


Wakati mfumo wa chama kimoja haikuwa rahisi kujua miradi ya umma na ya chama. Miradi iliyoanzishwa kwa ajili ya chama ilikuwa na dhumuni moja: kuhamasisha sera ya chama kimoja. Ndio maana ulikuwa ukichaguliwa mwenyekiti wa chama mkoa, ukuu wa mkoa unakuja automatic.

Tulipobadili mfumo na kuingia mfumo wa vyama vingi miradi iliyojengwa kwa ajili ya chama lakini kimsingi ni ya umma ilibaki kuwa ya chama.

Mfano viwanja vya mpira na ofisi za uongozi kama mkuu wa mkoa. Kulikuwa hakuna haja ya kujenga viwanja viwili sehemu moja yani cha chama na serikali, kulikuwa hakuna haja ya kujenga ofisi ya mkuu wa mkoa na mwenyekiti wa mkoa wa chama: ilikuwa ni kitu kimoja.

Wazo langu ni kwamba miradi mikubwa kama viwanja virudishwe viwe mali ya umma, haiwezekani mikoa yote viwanja viwe vya CCM, viwanja viwe mali ya umma chini ya halmashauri za mikoa.

Ofisi wanaweza kuchukua lakini si viwanja. Wengi mtakuwa mnafahamu baada ya mfumo wa vyama vingi katibu wa CCM wilaya alikuwa na ofisi kuliko mkuu wa mkoa.

Tuige KENYA: baada ya kibaki kuingia madarakani aliuchukua ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Jomo Kenyatta toka KANU. Alisema ni mali ya wakenya, ni jasho la wakenya chini ya mfumo wa lazima wa chama kimoja

KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI YANENA
KAMBI rasmi ya upinzani bungeni, imeitaka serikali kuvichukua viwanja vyote hapa nchini vinavyomilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho hakivihudumii inavyostahili.

Ushauri huo ulitolewa jana na Waziri Kivuli wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Joseph Mbilinyi 'Sugu' ambapo alisema baada ya serikali kuvichukua viwanja hivyo, ianzishe Mamlaka ya Viwanja vya Michezo.

Sugu alisema mamlaka hiyo ipewe jukumu la kuviboresha viwanja hivyo ili vitumike kwa maslahi ya Watanzania wote, badala ya utaratibu wa sasa ambapo CCM ndiyo yenye kuvimiliki.

Alivitaja viwanja hivyo kuwa ni Majimaji Songea, Sheikh Amri Abeid Arusha, Viwanja vya Jamhuri Morogoro na Dodoma, ule unaoitwa Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza na vingine vyote vilivyomilikishwa kwa CCM.

"Viwanja hivi nilivyovitaja na vinginevyo vilijengwa na wananchi wote wakati wa utawala wa chama kimoja na hivyo CCM haipaswi kuvimiliki bali serikali ambayo ni ya wananchi wote inatakiwa ivimiliki.

Mbali na sababu hiyo, viwanja hivyo havihudumiwi kwa kiwango, tunaitaka serikali ivirejeshe mikononi mwake na kuanzisha mamlaka itakayovihudumia," alisema.

Aliongeza kuwa mamlaka hiyo kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya serikali, ipewe jukumu la kuhakikisha kila mwaka inajenga vituo vya kisasa vya mazoezi na hosteli kwa ajili ya wanamichezo na angalau kiwanja kimoja kikubwa chenye hadhi ya kimataifa inayolingana na Uwanja mpya wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Sugu alisema, inasikitisha kuona miaka 50 baada ya Uhuru, Tanzania ina uwanja mmoja tu wenye hadhi ya kimataifa ambao ni Uwanja wa Taifa wa Dar es Salaam, uliojengwa kwa msaada wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu.

Aliongeza kuwa kiwanja hicho kimekuwa hakiendeshwi vizuri hata kulitia aibu taifa kwa huduma mbovu, ikiwemo ya kukatika kwa umeme kama ilivyotokea hivi karibuni wakati wa fainali za michuano ya Kombe la Kagame ambalo Tanzania ilikuwa mwenyeji.

Wakati huohuo, Mbilinyi alisema Tanzania imeshindwa kuzalisha walimu wa kutosha wa michezo mbalimbali na mbaya zaidi, hata wachache wazalendo hususan wa soka, wenye ujuzi na umahiri wa kuridhisha, wamekuwa hawapewi motisha, pindi wanapoteuliwa kufundisha timu za taifa.

Alisema, serikali imekuwa ikitumia gharama kubwa kuwapa ajira walimu wa kigeni, ambao wanakuja hapa nchini kuzifundisha timu za taifa.
 
Hivi ni kweli kuwa vile viwanja vya michezo (eg, Kirumba-Mwanza, Majimaji-Songea, Ally Hasan Mwinyi-Tabora etc) ni vya CCM kama wanavyotangaza? Na ni kweli kuwa vilijengwa kwa fedha za CCM?

Habari hii chini isome:

MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Terresia Mmbando, jana alifungua kesi dhidi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa kwa madai ya kwamba, chama hicho kimekiuka sheria ya Mipango Miji kwa kujenga bila kibali eneo la uwanja wa michezo wa Samora.

Mkurungezi huyo kupitia mwanasheria wa Manispaa hiyo, Anna Ngowi, ameufikisha Mahakamani uongozi wa chama hicho cha mkoa baada ya kujenga maghala pembezoni mwa uwanja huo upande wa mashariki, yaliyokwenda sambamba na ujenzi wa viti vya kukalia mashabiki uwanjani hapo.

Hatua hiyo ya Manispaa ya Iringa imekuja siku chache baada ya mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Saidi, kuwafukuza mafundi waliokuwa wakiendelea kujenga ndani ya uwanja huo kama njia ya kuukarabati uwanja huo ambao ulikuwa katika hali mbaya.

Mbali ya mkuu huyo wa mkoa, pia diwani wa viti maalum (CCM), Kanda ya Ruaha, Fatuma Kihombo, katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika mwishoni mwa mwezi uliopita, alipendekeza uongozi wa manispaa hiyo kwenda mahakamani kupinga shughuli hizo za ujenzi zinazofanywa na CCM mkoa na kuungwa mkono na Diwani wa Kata ya Gangilonga (CCM), Edwin Sambala.

Sambamba na madiwani hao kupinga wazi wazi ujenzi huo, bado sakata la uwanja huo lilionekana kuvuta hisia za wengi, kwani tayari limeshafika hadi ofisi ya mkuu wa mkoa ambaye alilazimika kwenda uwanjani mwenyewe na kusimamisha ujenzi kwa kuwatimua mafundi waliokuwa wakiendelea na ujenzi.

Hata hivyo, mwanasheria wa Manispaa ya Iringa, Anna Ngowi, amesema kuwa wao wanatekeleza maagizo waliyopewa na mkurugenzi wao, hivyo wasingependa kuzungumzia zaidi suala hilo ambalo msemaji wake ni mkurugenzi mwenyewe.

Kaimu mkurungenzi wa Mnaispaa ya Iringa, Paul Malala, alipofuatwa na mwandishi wa habari hizi, mbali ya kukiri kukifikisha Chama cha Mapinduzi katika Mahakama ya Nyumba na Ardhi mjini hapa, alisema asingependa kuzungumzia suala hilo ambalo tayari lipo katika vyombo vya sheria.

Naye kaimu katibu wa CCM Mkoa wa Iringa, Fridoline Mwapinga, amethibitisha chama chake kufikishwa mahakamani na kwamba, shauri hilo namba kumi la mwaka 2009, wamepokea samansi ya mahakama juu ya suala hilo na tayari mwanasheria wa CCM makao makuu, Elasta Kanyama, amewasili mkoani Iringa kwa ajili ya kusimamia kesi hiyo kwa kushirikiana na wakili wa kujitegemea, Afred Kingwe.

Mwapinga alisema, uwanja huo umekuwa ukikarabatiwa kwa kibali maalum kilichotolewa na ofisi ya mkurungezi wa Manispaa ya Iringa, hivyo wana uhakika mkubwa wa shauri hilo kukosa nguvu.

Aidha, alisema kutokana na mkurungenzi wa manispaa kuamua kuifikisha CCM mahakamani, wao kama wamiliki wa uwanja huo, wamelazimika kuufunga uwanja huo kuanzia jana ili usitumike kwa shughuli zozote

Mwapinga alisema kuwa, amemwagiza msimamizi wa uwanja huo, Lazaro Manila, kuufunga kwa kufuli uwanja huo na kuzuia michezo ya Ligi ya Taifa ngazi ya mkoa iliyokuwa ikifanyika katika uwanja huo na kusitisha kibali cha bonanza la TRMAC ambalo lilipaswa kuanza kufanyika Jumatatu ijayo kwa ajili ya mashindano ya Kombe la Dume.

Katibu wa chama cha soka Mkoa wa Iringa, Eliud Mvella amepokea kwa masikitiko makubwa hatua ya uongozi wa Manispaa ya Iringa kufikisha CCM mahakamani na kwamba suala hilo lilipasa kumalizwa nje ya mahakama kwani athari zake ni kubwa.

Hata hivyo, alisema kutokana na uwanja huo kufungwa, itawalazimu kutafuta uwanja mwingine wa kuendeshea lingi ya mkoa ngazi ya taifa ambayo ilikuwa ikifanyika katika uwanja huo.


Kutokana na sakata hilo, tayari CCM Mkoa wa Iringa umeomba wataalam wa viwanja kutoka Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kufika mkoani hapa kuangalia kama ujenzi huo una madhara katika michezo. hadi kesi ya msingi itakapomalizika.
 
Hivi ni kweli kuwa vile viwanja vya michezo (eg, Kirumba-Mwanza, Majimaji-Songea, Ally Hasan Mwinyi-Tabora etc) ni vya CCM kama wanavyotangaza? Na ni kweli kuwa vilijengwa kwa fedha za CCM?

Ni sehemu tu,ya miradi ya sisiemu mpaka sasa
 
na imepora vitu kibao.................kama maharamia vile alafu wanajisifu kweli..............
 
Hivi viwanja vya michezo ni kama michango ya harusi,mtu huwezi kudai ku share mke eti kwa kuwa umechangia!
 
Ni muda mrefu sana nimejaribu kufuatilia ni kwa nini watoto wetu wanakosa mwelekeo wa maisha kama nchi zingine hasa ktk suala zima la michezo lakini ktk kuhoji wananchi wenzangu wengi imeonekana tatizo ni ukosefu wa viwanja vya michezo kwa watoto.

Natoa wito kwa serikali ya CCM kwamba tunataka kila kata au kijiji kiwe na eneo la viwanja vya football, volleyball, table tennis, long tennis, netball, n.k. na maeneo haya yatengazwe kwa wananchi na siyo kuwa ni siri ya chama (CCM). Tusiwalalumu watoto wetu kwa uvutaji bangi kwani hawana mahali pa kuchezea.

Jambo lingine la muhimu nawataka wazazi wote, vijana, wazee kila weekend tujenge utamaduni wa kwenda mazoezini kila asubuhi au jioni, nchi za wenzetu wananfanya hivyo na kupunguza magonjwa na vifo.
 
Your idea is not bad Magezi but with the status of our country what is our priority? I think this mentality that the government has to do everything is spinning out of control. I don't think you need the central government in order to have sports at the village level. This is something the local community can come together and take care of.

The village or neighborhood can come together and sometimes all it takes is clearing a certain field(no need to even purchase land) so kids cold play.

You o your part, as a concerned parent or citizen can dedicate your time into coaching these kids. Not everything requires the consent or initiation by the central government.

Ndiyo maana hatu fiki!
 
Your idea is not bad Magezi but with the status of our country what is our priority? I think this mentality that the government has to do everything is spinning out of control. I don't think you need the central government in order to have sports at the village level. This is something the local community can come together and take care of. The village or neighborhood can come together and sometimes all it takes is clearing a certain field(no need to even purchase land) so kids cold play. You o your part, as a concerned parent or citizen can dedicate your time into coaching these kids. Not everything requires the consent or initiation by the central government. Ndiyo maana hatu fiki!

I am not sure whether you are currently living in TZ or not. What forced me to have this thread is due to the fact that almost all the open spaces where we could establish games and sports centres have been sold to mafisadi and these people they simply buid private facilities such as residential houses, bars, hotels, etc.

My concern is that let the government administration at lower levels allocate and preserve open spaces dedicated to recreational services such as sports and games and then we as stakeholders can come in to play our part. You mentioned that we should not expect the government to do everything for us but I think you missed the point, where do you get the power to own the land that can be transformed into open spaces as an individual?

Still the CCM government must be blamed for allowing corrupt leaders to sell the open speces that were allocated for recreational purposes.
 
KAMBI rasmi ya upinzani bungeni, imeitaka serikali kuvichukua viwanja vyote hapa nchini vinavyomilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho hakivihudumii inavyostahili.

Ushauri huo ulitolewa jana na Waziri Kivuli wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Joseph Mbilinyi 'Sugu' ambapo alisema baada ya serikali kuvichukua viwanja hivyo, ianzishe Mamlaka ya Viwanja vya Michezo.

Sugu alisema mamlaka hiyo ipewe jukumu la kuviboresha viwanja hivyo ili vitumike kwa maslahi ya Watanzania wote, badala ya utaratibu wa sasa ambapo CCM ndiyo yenye kuvimiliki.

Alivitaja viwanja hivyo kuwa ni Majimaji Songea, Sheikh Amri Abeid Arusha, Viwanja vya Jamhuri Morogoro na Dodoma, ule unaoitwa Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza na vingine vyote vilivyomilikishwa kwa CCM.

"Viwanja hivi nilivyovitaja na vinginevyo vilijengwa na wananchi wote wakati wa utawala wa chama kimoja na hivyo CCM haipaswi kuvimiliki bali serikali ambayo ni ya wananchi wote inatakiwa ivimiliki.

Mbali na sababu hiyo, viwanja hivyo havihudumiwi kwa kiwango, tunaitaka serikali ivirejeshe mikononi mwake na kuanzisha mamlaka itakayovihudumia," alisema.

Aliongeza kuwa mamlaka hiyo kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya serikali, ipewe jukumu la kuhakikisha kila mwaka inajenga vituo vya kisasa vya mazoezi na hosteli kwa ajili ya wanamichezo na angalau kiwanja kimoja kikubwa chenye hadhi ya kimataifa inayolingana na Uwanja mpya wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Sugu alisema, inasikitisha kuona miaka 50 baada ya Uhuru, Tanzania ina uwanja mmoja tu wenye hadhi ya kimataifa ambao ni Uwanja wa Taifa wa Dar es Salaam, uliojengwa kwa msaada wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu.

Aliongeza kuwa kiwanja hicho kimekuwa hakiendeshwi vizuri hata kulitia aibu taifa kwa huduma mbovu, ikiwemo ya kukatika kwa umeme kama ilivyotokea hivi karibuni wakati wa fainali za michuano ya Kombe la Kagame ambalo Tanzania ilikuwa mwenyeji.

Wakati huohuo, Mbilinyi alisema Tanzania imeshindwa kuzalisha walimu wa kutosha wa michezo mbalimbali na mbaya zaidi, hata wachache wazalendo hususan wa soka, wenye ujuzi na umahiri wa kuridhisha, wamekuwa hawapewi motisha, pindi wanapoteuliwa kufundisha timu za taifa.

Alisema, serikali imekuwa ikitumia gharama kubwa kuwapa ajira walimu wa kigeni, ambao wanakuja hapa nchini kuzifundisha timu za taifa.
 
Yeah kama kiwanja cha CCM kirumba na Sheikh Ameir Abeid vinatakiwa viwe na hadhi ya kimataifa...

Ni bora CCM iviuze au wavirudishe serikalini; wananchi walichangia ujenzi huo pesa hazikutoka CCM
 
Hapa CDM ndio walipaswa kumsifia sugu kwa kuliangalia hili badala ya kumsifia anapoingiza magomvi ya bar na ruge. Hata mimi mwana CCM damu/ kindaki ndaki naunga mkono viwanja hivi virudishwe kwa serikali kwa kuwa ni kweli wakati wa ujenzi wake wananchi ndio walitoa michango.
 
Inasikitisha kuona viwnja vilivyojengwa*enzi za chama kimoja*kwa nguvu za wazee wetu tena kwa kujitolea , vikitelekezwa bila ukarabati wowote tangu enzi za mwalimu had leo vimekua kama "Makumbusho ya kale"kwa mtazamo wangu ccm sio taassi ya michezo, hawawezi *kumiliki viwanja hivyo na kuwa vya kisasa..wanavitumia kwa masirahi ya chama na *chanzo cha kupata pesa kwa ajili ya uchaguzi na kuvitelekeza.Kama Jk ni mpend michezo awe wa kwanza kusimamia viwanja vinarudi serikalini.
 
lnashangaza sana, eti viwanja vyote vya michezo ni mali ya chama tawala.
Je ni nani aliyewamilikisha CCM viwanja hivyo?
Kwanini visiwe chini ya wizara yenye dhamana ya michezo?
 
Hivyo viwanja mwanzo havikuwa chini ya umiliki wa ccm. CCm wenyewe walijimilikisha baada ya mfumo wa vyama vingi kuanza.
 
Hivyo viwanja mwanzo havikuwa chini ya umiliki wa ccm. CCm wenyewe walijimilikisha baada ya mfumo wa vyama vingi kuanza.

Haya ni madai ya msingi kabisa, nitawaunga mkono wapinzani wenye lengo la kuvirudisha viwanja hivi kwa umma.
 
Back
Top Bottom