Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,176
- 25,446
Hatimaye Malkia Wa Pembe za Ndovu amekutwa na hatia na kuhukumiwa kifungo cha miaka kumi na Saba (17) gerezani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Ni pamoja na wenzake wawili.
Nikiwa mtanzania mzalendo, najitokeza hadharani kuipongeza Serikali kwa hatua ya kesi hii. Pamoja na uwezekano Wa uwepo Wa rufaa Mahakama Kuu, itoshe kusema kuwa hukumu ya Leo itakuwa funzo tosha.
Mosi, ujumbe unatumwa kwa wote kuwa Serikali Ina Nia thabiti na inaisimamia Nia hiyo ya kulinda rasilimali za taifa hili kupitia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo. Serikali kupitia Ofisi ya Mkurugenzi Wa Mashtaka na vyombo vya dola imefanya kazi kubwa kuipata hukumu ya Leo.
Pili, hukumu ya Leo imetuma ujumbe kuwa kwenye Nia, msimamo na usimamizi thabiti Wa Sheria Wa Serikali hakuna mkubwa wala mdogo atakayebaki salama. Kila mkosaji, hasa kwenye rasilimali za taifa, ataguswa na kushughulikiwa.
Tatu, hukumu ya Leo imetuma ujumbe kuwa vyombo vya ulinzi na usalama nchini viko macho muda wote katika kutekeleza majukumu yao. Hukumu ya Leo itume onyo kwa wanaoendelea au wanaopanga kujihusisha na biashara haramu ya nyara za Serikali na kadhalika.
Nne, najua kuwa kuendesha na kuthibitisha shtaka LA jinai si kazi nyepesi. Ndiyo maana naipongeza Serikali kupitia kwa Mkurugenzi Wa Mashtaka nchini kwa kazi kubwa kufanikisha kutumwa kwa ujumbe Wa Leo.
Mali zote za Malkia Wa Pembe za Ndovu zitataifishwa. Funzo kwa wengine. Onyo kwa wanaotamani au kuendelea na kutenda jinai.
Serikali iko macho na haina mchezo 'on serious national matters'!
Nikiwa mtanzania mzalendo, najitokeza hadharani kuipongeza Serikali kwa hatua ya kesi hii. Pamoja na uwezekano Wa uwepo Wa rufaa Mahakama Kuu, itoshe kusema kuwa hukumu ya Leo itakuwa funzo tosha.
Mosi, ujumbe unatumwa kwa wote kuwa Serikali Ina Nia thabiti na inaisimamia Nia hiyo ya kulinda rasilimali za taifa hili kupitia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo. Serikali kupitia Ofisi ya Mkurugenzi Wa Mashtaka na vyombo vya dola imefanya kazi kubwa kuipata hukumu ya Leo.
Pili, hukumu ya Leo imetuma ujumbe kuwa kwenye Nia, msimamo na usimamizi thabiti Wa Sheria Wa Serikali hakuna mkubwa wala mdogo atakayebaki salama. Kila mkosaji, hasa kwenye rasilimali za taifa, ataguswa na kushughulikiwa.
Tatu, hukumu ya Leo imetuma ujumbe kuwa vyombo vya ulinzi na usalama nchini viko macho muda wote katika kutekeleza majukumu yao. Hukumu ya Leo itume onyo kwa wanaoendelea au wanaopanga kujihusisha na biashara haramu ya nyara za Serikali na kadhalika.
Nne, najua kuwa kuendesha na kuthibitisha shtaka LA jinai si kazi nyepesi. Ndiyo maana naipongeza Serikali kupitia kwa Mkurugenzi Wa Mashtaka nchini kwa kazi kubwa kufanikisha kutumwa kwa ujumbe Wa Leo.
Mali zote za Malkia Wa Pembe za Ndovu zitataifishwa. Funzo kwa wengine. Onyo kwa wanaotamani au kuendelea na kutenda jinai.
Serikali iko macho na haina mchezo 'on serious national matters'!