Kukua na kusambaratishwa kwa Chama Cha Black panthers na FBI, Pia wafahamu baadhi yao waliokimbilia Tanzania

anonymousafrica

JF-Expert Member
Aug 24, 2016
611
639
kathleen-cleaver-and-black-panther-co-founder-bobby-seale-right-at-a-free-huey-rally-in-oaklan...jpg


ACHANA NA BLACK PANTHER WALE PAKA Au movie ya Wakanda

Leo nakupa historia/ machache kuhusu chama cha Black Panthers.... walioishi kwa falsafa za Malcom X na kusambaratishwa kwa Hila za FBI

Kama unaikumbuka historia ya tupac na Mama yake Afeni Shakur

Afeni alikua mwanajumuia wa Black Panther, harakati zilimuonjesha jela... na hata ujauzito wa Tupac ni alamanusra ajifungue gerezani... lakini alitolewa na kujifungua nje

afenishakur-500x334.jpg


Mwaka 1969 Pete O'Neal alikamatwa kwa kosa la kusafirisha silaha (Bunduki) ndani ya mipaka ya marekani na mwaka 1970 alipatwa na hatia na kuhukumiwa miaka 4 jela, lakini aliwahi kufanikiwa kutoroka yeye pamoja na mke wake Charlotte O’Neal na kufanikiwa kufika nchini Algeria na baadae Tanzania ambapo walipokelewa vizuri na raisi wa wakati huo Julius Nyerere ambaye alikua muumini mkubwa wa ujamaa (Black Panthers walikua wajamaa pia) na kupatiwa makazi mapya Tanzania ambapo wanaishi hadi leo hii.

peteonealWEB.jpg


Geronimo Pratt ambaye alikua kamanda wa cheo cha juu kabisa ndani ya black panther na baba mlezi wa mwanamuziki Tupac Shakur, alihukumiwa miaka 27 jela na kutoka mwaka 1997. Baada ya kutoka aliishtaki serikali kwa kumfunga kimakosa na kulipwa fidia yake. Baadae aliamua kuja kuishi Tanzania na kufariki Arusha June 2, 2011

Tuikumbuke mistari hii miwili “FID q, Professional “ Mwanaharakati kama Geronimo Pratt I am a professional
t1larg.pratt.gi.jpg

Ibra Da Hustler kwenye mchizi wangu RIMIX anamtaja pia, sina hakika kama napatia mistari ila nahisi kama alisema bila kumsahau the one and only Geronimo Pratt remember when we sat, what we talked about ilikua fact

FAHAMU MACHACHE KUHUSU BLACK PANTHERS

3000.jpeg

The Black Panthers, pia walijulikana kama chama cha Black Panther, shirika la kisiasa ambalo lilianzishwa mnamo 1966 na vijana: Huey Newton na Bobby Seale wakiwa na dhumuni la kupinga ukatili wa polisi dhidi ya jamii ya watu wenye asili ya Kiafrika . Msukumo mkubwa waliupata baada ya kifo cha Malcom X , wengi hudhani Malcom alikua ndiye muasisi na kiongozi wa kikundi hiki. Ila ukweli ni kwamba aliwaongoza kiimani na falsafa tu. Wakitambulishwa kwa mavazi yao meusi na mitindo ya kofia nyeusi (berets ) Panthers walipanga doria zao wakiwa na silaha kwenye maeneo kama Oakland na miji mingine ya Marekani. 1968 hapa kikundi ndipo kilipoanza kuwa cha moto kikiwa na wafuasi wapatao 2000. Shirika lilikosa watu wengi hapo baadae kwasababu ya mivutano ya wenyewe kwa wenyewe, vifo kwenye mashambulizi mbalimbali na shughuli za ujasusi za FBI ambazo zililenga kudhoofisha chama hiko.

CuztPSnWIAAah2l.jpg


Waanzilishi wa Chama cha Black Panther , Huey Newton na Bobby Seale walikutana mnamo 1961 wote wawili wakiwa wanapinga sherehe iliuofanyika chuoni ya Pioneer Day siku ambayo ililenga kuwakumbuka watu wa kwanza kufika kwenye mji huo (mwaka 1800) na kusahau kuwapatia heshima watu weusi ambao pia walitangulia kufika kwenye mji huo wa Magharibi

Seale na Newton waliunda Kikundi cha kuelimisha watu kuhusu ukweli wa historia ya watu weusi chuoni hapo.

tdih-feb21-HD.jpg


Walianzisha Black Panthers baada ya kuuawa kwa Malcolm X kama nilivyoelezea hapo juu na baada ya polisi huko San Francisco kumpiga risasi kijana mweusi asiye na silaha Matthew Johnson.Na ndio sababu ya shughuli ya mwanzo kwa panthers ilikua ni kujilinda na kusimamia mienendo na shughuli za polisi huko Oakland na miji mingine.

Walipoanzisha programu kadhaa za kijamii na kujihusisha na shughuli za kisiasa, umaarufu wao ulikua unakua. Panthers walipata misaada kutoka kwa watu na vikundi kadhaa vinavyojishughulisha namasuala ya kijamii huko Los Angeles, Chicago, New York na Philadelphia.
AP_6904160329.ngsversion.1516743042386.adapt.1900.1.jpg

Shughuli za Kisiasa na Mipango ya Jamii

Newton na Seale walikijenga kikundi/chama kwa itikadi ya ki Marxist (KIJAMAA). Walielezea maoni yao kifalsafa na malengo ya chama chao kisiasa katika mfumo waliouita TEN POINT PROGRAM

Programu ya Pointi Kumi ilijumuisha sehemu mbili: Ya kwanza, WHAT WE WANT (TUNACHOHITAJI)Walieleza Chama cha BlackPanther kinataka nini kwa uongozi wa kibaguzi wa marekani wakati huo, na upande wa pili wa TUNACHOAMINI ( WHAT WE BELIEVE) hapa wanaelezea maoni ya kifalsafa ya chama hicho na haki ambayo Wamarekani Weusi wanapaswa kuwa nayo,Kwa mfano
what we want.JPG

, sehemu moja inasema kwamba, "Tunaamini kuwa serikali hii ya ubaguzi wa rangi imetuibia sana na sasa tunataka watulipe deni letu la hekari arobaini na punda wa kulimia (Forty acres and a mule).
40acresandamule.jpg

Hekari 40 na punda viliahidiwa miaka 100 iliyopita kama malipo ya kazi ya watumwa na mauaji ya watu weusi ". Inaendelea kusema kuwa "Tutakubali malipo haya kwa mtindo wa fedha ambayo itasambazwa kwa watu wa jamii zetu ." Newton na Seale waliamini kwamba jamii ya watu weusi ilikuwa imenyimwa faida hizi kwa miaka, na kwamba njia pekee ya kusahihisha ukosefu huo wa haki ilikuwa katika ulipaji wa mali ambazo walipoteza kwa miaka mingi ya utumwa.

2Q4ESROEONEPRFZZR7FEHSDEWU.jpg



Wakati wa Panthers , serikali iliwatazama kama genge la wahalifu wakati wao binafsi wakijiona kama chama cha kisiasa ambacho lengo lake lilikuwa kuwafanya Wamarekani zaidi wenye asili ya Kiafrika wateuliwe kwenye nyadhifa za kisiasa. Hawakufanikiwa kufika huko. Mapema miaka ya 1970, juhudi za ujasusi wa FBI, shughuli za uhalifu na ugomvi wa ndani baina ya wanachama wa kikundi ulidhoofisha chama na nguvu ya kisiasa.



Tukumbuke walijaliwa pia kuanzisha miradi kadhaa ya kijamii kama programu za bure za kuwapatia chakula watoto wa shule na huduma za bure za afya kwa jamii 13 za wamarekani weusi ndani ya nchi ya marekani.

2-Charles-Bursey-hands-plate-of-food-to-a-child-seated-at-Free-Breakfast-Program.-Photo-courte...jpg


MIKANGANYIKO NA VURUGU NDANI YA BLACK PANTHER

Panthers walihusika katika vurugu nyingi na polisi. Mnamo mwaka wa 1967, mwanzilishi/muasisi, Huey Newton alidaiwa kumuua afisa wa polisi wa Oakland John Frey. Newton alihukumiwa kwa mauaji mnamo 1968 kifungo cha miaka 2 hadi 15 (kwa miezi 22 alikaa lockup na aliruhusiwa kuonana na watu 10 pekeake kwa muda wote huo). Eldridge Cleaver, mhariri wa gazeti la Black Panther, na mwanachama wa miaka 17 wa Black Panther, Bobby Hutton, walihusika katika majibizano ya risasi na polisi mnamo 1968 ambapo Hutton alifariki na maafisa wawili wa polisi walijeruhiwa.

black-panther-party-for-self-defense.jpg


Migogoro ndani ya chama mara nyingi ilibadilika kuwa vurugu pia. Mnamo mwaka 1969, Mwanachama wa Black Panther, Alex Rackley aliteswa na kuuawa na watu wengine weusi wa Panthers ambao walimhisi kuwa ni chawa wa polisi (anavujisha taarifa zao).

Mtunza barua na vitabu wa Black Panther Betty Van Patter alipatikana akiwa amepigwa na kuuawa mnamo 1974. Hakuna mtu aliyeshtakiwa kwa kifo hicho, ingawa wengi waliamini kuwa uongozi wa chama uliwajibika.

4c252ff352b09448101eb04f5e8bab89.jpg


FBI NA COINTELPRO (
COunter INTELligence PROgram)

Huu ni mkakati wa FBI wakati huo, kuhakikisha vyama na wanaharakati wote wanakatwa mikia

Ujumbe wa ujamaa wa Black Panther nautofauti wa kimtazamo wa kitaifa uliwafanya kuwa shabaha ya mpango wa siri wa FBI uitwao COINTELPRO.

n0_09_w2_51_8.jpg


Mnamo 1969, FBI ilitangaza Black Panthers kuwa ni shirika la kikomunisti na adui wa serikali ya Marekani. Mkurugenzi wa kwanza wa FBI, J. Edgar Hoover, mnamo 1968 alisema The Black Panthers, "Moja ya vitisho vikali kwa usalama wa taifa."



FBI ilifanya kazi ya kudhoofisha Panthers kwa kutumia ubishani uliopo kati ya wenyewe kwa wenyewe. Pia Walifanya kazi ya kudhoofisha na kuondoa mpango wa chakula bure mashuleni kwa watoto (mpango ulioanzishwa na Panthers) na programu zingine za kijamii.

7APNCMR24VBCRAHSD7WSFI2HYQ.jpg


Mnamo mwaka wa 1969, polisi wa Chicago waliwashambulia kwa bunduki na kuwaua wanachama wa Chama cha Black Panther Fred Hampton na Mark Clark, ambao walikuwa wamelala ndani ya nyumba yao.

Walisema zilipigwa risasi zaidi ya miamoja na kuwa mapambano makali kuwahi kutokea ila ukweli ni kwamba uchunguzi ulibaini upande wa Panther walirusha risasi moja tu kwa polisi.



Chama cha Black Panther kilifutwa rasmi mnamo 1982.

Lakini chama kipya cha Panther kiliundwa huko TEXAZ mwaka
1989. Washiriki wa Chama cha Asili cha Black Panthers walisema hakuna uhusiano kati ya Chama kipya cha Panther na Panthers asilia.
 
Usiishie hapo:

Wale washkaji zake Tupac waliochana nao nyimbo nyingi pamoja na Hit em up waliuawa kwa risasi ila wawili walitoroka, mmoja alikimbilia Ghana then Nairobi halafu finally Arusha.

Aliishi pale Uzunguni, nyumba inayotazama uwanja wa Gymkhana. Alikuwa anajiita Blackii na alipenda kushinda kijenge juu jioni ili kujifunza kiswahili,Arusha Library au pale Impala hotel kusoma magazeti, alikuwa na slogan yake ambayo pia aliiandika nyuma ya T shirt zake kadhaa ''Jus Kill All Whites'' (JKAW) halafu hiyo Kill ameifutafuta haisomeki vizuri...hahaha

Bila shaka akina JCB, Chindoman, na Umbwa ndio walipata mwasisi wa Hiphop hapa

Blackii alienda kufia Nairobi I think kwa Aunt yake aliyemwacha huko wakati anakuja Bongo

R.I.P
 
Usiishie hapo:

Wale washkaji zake Tupac waliochana nao nyimbo nyingi pamoja na Hit em up waliuawa kwa risasi ila wawili walitoroka, mmoja alikimbilia Ghana then Nairobi halafu finally Arusha.

Aliishi pale Uzunguni, nyumba inayotazama uwanja wa Gymkhana. Alikuwa anajiita Blackii na alipenda kushinda kijenge juu jioni ili kujifunza kiswahili,Arusha Library au pale Impala hotel kusoma magazeti, alikuwa na slogan yake ambayo pia aliiandika nyuma ya T shirt zake kadhaa ''Jus Kill All Whites'' JKAW halagu hiyo Kill ameifutafuta haisomeki vizuri...hahaha

Bila shaka akina JCB, Chindoman, na Umbwa ndio walipata mwasisi wa Hiphop hapa

Blackii alienda kufia Nairobi I think kwa Aunt yake aliyemwacha huko wakati anakuja Bongo

R.I.P
nakumbuka mwaka 1997 au 96 ile ile alifariki Yaki Kadafi kwa kupigwa risasi, wengine skujua ila baadae miaka ya 2015 Hussein Fatal alipata ajali ya gari (wote walikua Outlaws na tupac) ahsante kwa kunipatia MENGINE
 
Tujuze hao charlote walioko Arusha ni wamarekan au ni watz waliokuwa wanaish marekan? Bahat nzur ninafahamiana nao japo sio kiivyo. Niliwah kwenda pale kwao wana shule flan ya muziki.
Ni wamarekani waliokimbilia TZ miaka ya 1970, walipata watoto nafikiri wakiwa Tanzania...... hongera kama umepata kukutana nao, nimepost picture hapo juu ya mzee O Neal na mke wake
 
Back
Top Bottom