Kuku aina ya SASSO wakiwa na siku 52

Marire

JF-Expert Member
May 1, 2012
12,326
5,264
Hawa kuku nilitaka kuwauza wakiwa na week 2 kwa kupata changamoto ya banda ila nimepambana hadi nikajenga banda na sasa wanaendelea vizuri sana

Hawa kuku wananifurahisha kitu kimoja ni wagumu sana kuumwa na hata wakiumwa wana kinga thabiti sana. Hapa nangojea mwezi wa 12 niwaingize sokoni
ATTACH]


1477215813854.jpg


1477215829171.jpg


1477215850460.jpg
 
Mie sitaki kabisa kuwasikia hao Sasso. Nilinunua vifaranga 200 kutoka kwa Nzowa Enterprises pale Kibaoni-Tegeta. Jamaa walinichanganyia umri tofauti tofauti kinyume na makubaliano. Kilichofuatia ikawa vigumu kujua yupi amepata chanjo ipi; na ipi au yupi hajapata.

Waliopoanza kuugua, nilirudi Nzowa kuwaeleza tatizo la vifaranga walivyoniuzia lakini hawakunipa ushirikiano wala msaada wowote. Vifaranga walipukutika mpaka nikachanganyikiwa. Waliofikia umri wa mauzo ni 83 tu!
 
Mie sitaki kabisa kuwasikia hao Sasso. Nilinunua vifaranga 200 kutoka kwa Nzowa Enterprises pale Kibaoni-Tegeta. Jamaa walinichanganyia umri tofauti tofauti kinyume na makubaliano. Kilichofuatia ikawa vigumu kujua yupi amepata chanjo ipi; na ipi au yupi hajapata. Waliopoanza kuugua, nilirudi Nzowa kuwaeleza tatizo la vifaranga walivyoniuzia lakini hawakunipa ushirikiano wala msaada wowote. Vifaranga walipukutika mpaka nikachanganyikiwa. Waliofikia umri wa mauzo ni 83 tu!

NZOWA ENTERPRISE NI MATAPELI WAKUBWA SANA HAPA DAR ES SALAAM.NASHAURI WATU WASIENDE KUPATA HUDUMA KWA HAWA
 
Hao nimenunua hapo hapo mkuu na hao walikuwa 200 waliokufa hadi sasa ni 10 hadi sasa wanaendelea vyema kama unavyoona.

Hao jamaa wana branch pale ubungo na nilinunua wa malawi 250 ambao wana miezi minne sasa walinichanganyia walivyofika wakaanza kuza hovyo vifaranga 30 ndani ya week sikukubali niliwarudia kwa ukali wakamtuma daktari wao akaja kucheck mazingira nayofugia ila hakukuta kasoro ilibidi wanifidie vifaranga waliokufa......
 
hao nimenunua hapo hapo mkuu na hao walikuwa 200 waliokufa hadi sasa ni 10 hadi sasa wanaendelea vyema kama unavyoona .
hao jamaa wana branch pale ubungo na nilinunua wa malawi 250 ambao wana miezi minne sasa walinichanganyia walivyofika wakaanza kuza hovyo vifaranga 30 ndani ya week sikukubali niliwarudia kwa ukali wakamtuma daktari wao akaja kucheck mazingira nayofugia ila hakukuta kasoro ilibidi wanifidie vifaranga waliokufa......
Baada ya hapo umewakuzaje mkuu mi nlichukua 200 wamebak 30 tu wana miez mitatu, chanjo zote nimewapa naamka tu nakuta wamekufa
 
hao nimenunua hapo hapo mkuu na hao walikuwa 200 waliokufa hadi sasa ni 10 hadi sasa wanaendelea vyema kama unavyoona .
hao jamaa wana branch pale ubungo na nilinunua wa malawi 250 ambao wana miezi minne sasa walinichanganyia walivyofika wakaanza kuza hovyo vifaranga 30 ndani ya week sikukubali niliwarudia kwa ukali wakamtuma daktari wao akaja kucheck mazingira nayofugia ila hakukuta kasoro ilibidi wanifidie vifaranga waliokufa......
Swali LA mtu wa kwanza unawalisha nn mbona kama umelikimbia mkuu
 
hawa kuku nilitaka kuwauza wakiwa na week 2 kwa kupata changamoto ya banda ila nimepambana hadi nikajenga banda na sasa wanaendelea vizuri sana
hawa kuku wananifurahisha kitu kimoja ni wagumu sana kuumwa na hata wakiumwa wana kinga thabiti sana
hapa nangojea mwezi wa 12 niwaingize sokoni
ATTACH]
Mimi nami nilisikia sifa zake nikawanunua january 21 wakiwa wa day one, vifaranga vilikuwa vikubwa mpaka raha...nikawapa chanjo zote kwa kufuata taratibu zinazoshauriwa. Lakini mwezi wa 6 walipukutika kama maji kwa ugonjwa wa mafua...hawakusilia dawa wala nn..ikinifanya nikate tamaa.

wale waliobaki hawajataga mpaka leo.

kwa uchunguzi wangu si wavumilivu kwa magonjwa wala njaa!!

Sitaki kabisa kuwasikia hawa kuku..wa malawi wako vizuri sana.
Nitaendelea kuwafuga wa malawi
 
Mie sitaki kabisa kuwasikia hao Sasso. Nilinunua vifaranga 200 kutoka kwa Nzowa Enterprises pale Kibaoni-Tegeta. Jamaa walinichanganyia umri tofauti tofauti kinyume na makubaliano. Kilichofuatia ikawa vigumu kujua yupi amepata chanjo ipi; na ipi au yupi hajapata. Waliopoanza kuugua, nilirudi Nzowa kuwaeleza tatizo la vifaranga walivyoniuzia lakini hawakunipa ushirikiano wala msaada wowote. Vifaranga walipukutika mpaka nikachanganyikiwa. Waliofikia umri wa mauzo ni 83 tu!
Hata mimi sina hamu nao...niliwanunua ubungo darajani wamepukutika karibia wote, waliobaki hawajataga mpaka leo miezi tisa sasa...mpaka nawaza ni wanyama hawa?? nimeona nijifugie kwaajili ya mayai kwa mwanangu tu lkn sio biashara
 
Hiyo sio mbegu bora ya kuku, ni bora ukafuga pure wa kienyeji wanavumilia sana magonjwa na hata tiba inawasaidia wakipatwa na magonjwa. Mimi nilinuua vifaranga 25 vikiwa na miezi mi 2 - 3, vimeniletea matokeo mazuri sana.
 
Na je sasso kutoka silver land iringa wapo vipi ?? Magonjwa na ustahimilivu maana Naona wanawauza sana
 
Hiyo sio mbegu bora ya kuku, ni bora ukafuga pure wa kienyeji wanavumilia sana magonjwa na hata tiba inawasaidia wakipatwa na magonjwa. Mimi nilinuua vifaranga 25 vikiwa na miezi mi 2 - 3, vimeniletea matokeo mazuri sana.
Wa kienyeji pure ntawapata wapi mkuu??
 
Back
Top Bottom