Kukosa mtoto wa kiume inawasumbua sana wanaume kufanya wakose amani

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Bwana Mchanga alipata nafasi ya kwenda masomoni nchi za Scandinavia, alibahatika kupata mke wa Kizungu na baraka ya mabinti watatu. Baada ya masomo Mrs Mchanga alikataa kurudi Tanzania. Waliachana kwa amani na bwana Mchanga kurejea nyumbani.

Alipata ajira serikalini kama afisa mwandamizi. Alikutana na Ruth na wakafunga ndoa. Ruth alipata mtoto wa kike, Mchanga alikua mvumilivu, wapili akaja binti mrembo. Hapa Bwana Mchanga uvumilivu ulimwishia. Alikwenda kijijini kwao na kuoa kabinti kigori kabisa. Kwakua uwezo wa fedha alikua nao alimjengea nyumba nzuri pale kijijini.

Huku kwa Ruth alimuacha akiwa mja mzito na alijaliwa kupata mtoto wa kiume. Ruth hakua na habari kuwa mume wake ana mke kijijini. Kila weekend Mchanga alikwenda kijijini akidai anajiandaa kugombea Ubunge. Ruth slipata habari mume wake ana mke mwingine yeye akiwa na mtoto wa pili wa kiume.

Huyu mke wa kijijini alianzisha leagu na Ruth, Ruth akiwa career woman hakuwa na muda huo, aliachana na Mchanga na kugaiwa mali zake. Maisha yanaendelea na watoto wakakua.

Mchanga alianza familia mpya kijijini. Umri nao unasogea. Sasa Mchanga anastaafu akiwa na watoto wanasoma shule ya msingi. Wale mabinti wa Scandinavia wameolewa na wameanza familia.

Katika jitihada za kutafuta mtoto wa kiume sasa Mchanga anatumia mafao ya kustaafu kulea watoto.
 
Hapo ndo wanaume wanapozidi kufa kwa kiharusi....

Umestaafu umri miaka 60+, kwa jeuri ya kiume wanajitutumua ng'ombe hazeeki maini anaendelea kutotoa watoto.....

Halafu wanalalamika wanawake wanabebwa wakati mwanamke akifosi sana mwisho kutotoa miaka 50.

Mwanamke akistaafu anakula pensheni yake maana watoto wake wakubwa wanajitegemea sana sana atakuwa anajichangamsha na wajukuu.

Wanaume sasa, kama mzee Mchanga....

Na miaka 70+ unamtoto anatoka shule anaita baba, kesho tunatakiwa kwenda trip ya kishule mchango laki moja....!!

Kama chanzo cha mapato ni pension tuu amekwisha.

NB: Too much of anything is harmful.
 
Hapo ndo wanaume wanapozidi kufa kwa kiharusi....

Umestaafu umri miaka 60+, kwa jeuri ya kiume wanajitutumua ng'ombe hazeeki maini anaendelea kutotoa watoto.....

Halafu wanalalamika wanawake wanabebwa wakati mwanamke akifosi sana mwisho kutotoa miaka 50.

Mwanamke akistaafu anakula pensheni yake maana watoto wake wakubwa wanajitegemea sana sana atakuwa anajichangamsha na wajukuu.

Wanaume sasa, kama mzee Mchanga....

Na miaka 70+ unamtoto anatoka shule anaita baba, kesho tunatakiwa kwenda trip ya kishule mchango laki moja....!!

Kama chanzo cha mapato ni pension tuu amekwisha.

NB: Too much of anything is harmful.
Count me not
 
pamoja na ugangwe wangu wote, nilitoa machozi ya furaha ile siku nilipopewa taarifa kwamba shemeji/wifi yenu kanizalia salama mtoto wa kiume.

that feeling is something i can't explain, wababa wenzangu waliobahatika kupata watoto wa kiume wanajua nazungumza nini.

kwa sasa jembe langu yupo standard two halafu he is a real version of me copy and paste. mdogo wake aliyemfatia pia na yeye ni kidume, sura kama kaka yake utadhani mapacha.
 
pamoja na ugangwe wangu wote, nilitoa machozi ya furaha ile siku nilipopewa taarifa kwamba shemeji/wifi yenu kanizalia salama mtoto wa kiume.

that feeling is something i can't explain, wababa wenzangu waliobahatika kupata watoto wa kiume wanajua nazungumza nini.

kwa sasa jembe langu yupo standard two halafu he is a real version of me copy and paste. mdogo wake aliyemfatia pia na yeye ni kidume, sura kama kaka yake utadhani mapacha.
Naam, feelings flani hivi za kujiamini sana...kidume ni raha sana nakuelewa ....
 
kuna imani zinaamini watoto wakikuombea kheri wakati umefariki bhasi mizigo yako inapungua huko ulipo na wengine wanaamini katika kuendeleza majina ya ukoo. Kwa mantiki hizo mbili ukikosa mtoto wa kiume jina na kumbukumbu yako ndio imeisha maana mtoto wa kike huendeleza koo ya mtu mwingine

lakini kwa angle nyingine hizo ni hofu tu maana siamini kama humu watu wanajua lolote kuhusu baba wa babu wa babu yao hivyo, kusahaulika hakuepukiki.
 
Back
Top Bottom