BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,004
UKIRI WA VIONGOZI WA CCM NA SERIKALI YAKE KUHUSU MAALIM SEIF, UTUFUMBUE MACHO KUHUSU YANAYOENDELEA KWA FREEMAN MBOWE NA WAPINZANI WENGINE!
Tulikuwa Zanzibar kuhudhuria Uzinduzi wa Maalim Seif Foundation. Tuliwasikiliza vizuri viongozi waandamizi wa CCM na Serikali yake, wastaafu na waliopo: Rais Samia, Rais Mstaafu Karume, Jaji Mstaafu Warioba, Katibu Mkuu Mstaafu Kinana, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku nk.
Viongozi hao walionekana wazi wakiongea kama yule mwamba wa PGO ya Kirumi, yule Askari aliyekiri baada ya kumsulubisha Yesu akisema: "Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu" (Luka 23:47; Mathayo 27:54). Ukiri wa yule mwamba ulifuatiwa na ukiri wa wengi ambao waliondoka Golgotha wakijipiga vifua na kujilaumu kwa kumsulubisha mtu ambaye hakuwa na hatia aliyetundikwa mtini kutokana na mashuhuda wa uwongo (Luka 23:48).
Kama viongozi hao wa CCM na Serikali yake katika zama tofauti tofauti wamekiri hivyo kuhusu Maalim Seif! Je, ni nani atakayeishi kushuhudia viongozi hao hao au hata wenginw wakubwa wa CCM na Serikali yake kuja kukiri hivyo hivyo kumhusu Freeman Mbowe!
Siku na saa isiyotajiwa, sisi Askofu tutafika tena Mahakamani kumtia moyo Mbowe na wenzake. Hatuna mamlaka ya dunia hii, lakini uwepo wetu na maombi yetu ndio kitu kikubwa wanachohitaji kutoka kwetu sote! Simama na wewe katika zamu yako ukahesabiwe!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Tulikuwa Zanzibar kuhudhuria Uzinduzi wa Maalim Seif Foundation. Tuliwasikiliza vizuri viongozi waandamizi wa CCM na Serikali yake, wastaafu na waliopo: Rais Samia, Rais Mstaafu Karume, Jaji Mstaafu Warioba, Katibu Mkuu Mstaafu Kinana, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku nk.
Viongozi hao walionekana wazi wakiongea kama yule mwamba wa PGO ya Kirumi, yule Askari aliyekiri baada ya kumsulubisha Yesu akisema: "Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu" (Luka 23:47; Mathayo 27:54). Ukiri wa yule mwamba ulifuatiwa na ukiri wa wengi ambao waliondoka Golgotha wakijipiga vifua na kujilaumu kwa kumsulubisha mtu ambaye hakuwa na hatia aliyetundikwa mtini kutokana na mashuhuda wa uwongo (Luka 23:48).
Kama viongozi hao wa CCM na Serikali yake katika zama tofauti tofauti wamekiri hivyo kuhusu Maalim Seif! Je, ni nani atakayeishi kushuhudia viongozi hao hao au hata wenginw wakubwa wa CCM na Serikali yake kuja kukiri hivyo hivyo kumhusu Freeman Mbowe!
Siku na saa isiyotajiwa, sisi Askofu tutafika tena Mahakamani kumtia moyo Mbowe na wenzake. Hatuna mamlaka ya dunia hii, lakini uwepo wetu na maombi yetu ndio kitu kikubwa wanachohitaji kutoka kwetu sote! Simama na wewe katika zamu yako ukahesabiwe!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula