Abdul Mohammed
JF-Expert Member
- May 26, 2013
- 1,331
- 855
Walioimba ufisadi wa Lowassa ni CCM.
Mara kuvua gamba, n.k.
Sikumbuki popote Wapinzani walipomtaja Lowassa kuwa ni fisadi.
Ufisadi ndani ya Chama cha Mapinduzi ni MFUMO RASMI.
UKAWA wasipompokea Lowassa, maana yake ni kwamba hawataki kuuondoa madarakani mfumo wa ufisadi.
Tatizo letu ni mfumo, siyo watu au majina ya watu.
Kama kweli Ukawa wanaitakia mema nchi yetu, basi naamini wako kwenye kikao na Lowassa hivi sasa.
Mungu ibariki Tanzania.
iukisema wapinzani, jua kuwa lowasa hawezi kuhamia CHADEMA, CUF, NCCR bali atachagua vyama vile ambavyo huwa vinaunga mkono ccm kama TLP, PPT MAENDELEO, TADEA, UDP YA CHEYO nk. hawezi kutia mguu vyama bora, anaenda kwa salvages.
Pasco ungepumzika for now
sioni kama una make sense anymore
kila ulichotuambia huko nyuma kimeenda the opposite
labda sasa ungenyamaza kwanza.......ni kama vile nyinyi wapambe wa mgombea
mna kiu na urais kuliko mgombea mwenyewe
Watu wote wenye mawazo kama haya mnasahau kwamba tume ya uchaguzi iliyopo ni ile ile ya ccm, ambayo katu haitamtangaza mpinzani kuwa kashinda uchaguzi. Nadhani bado tuna jukumu kubwa sana la kushinikiza kupata tume huru kabla ya kufikiria mpinzani kwenda ikulu.lowasa akienda ukawa anashinda urais, achague vyama vile ambavyo havina hata shilingi mia mfukoni au vile vinavyotaka kufa, achukue fomu, anashinda uchaguzi bila shida. ila awe makini ahofie usalama wake kwa sasa kwasababu ni kitu kigumu sana kupigana na system hasa katika wakati kama huu ambao wamemwonyesha wazi kuwa wanapambana naye.
Nauliza tena, jee huu ndio mwisho wa safari, au mwanzo wa safari ya kweli ya matumaini kwanza kwa kuingoa CCM na kuikomboa Tanzania?!.Pasco
Leo nimefurahi sana Lowasa kukatwa. Tuone sasa wale manabii na wachungaji feki kwamba Lowasa asipokuwa rais wao watawajibika...na wawajibike sasa.
Wapinzani ntawadharau na pasina shaka hata watanzania wengi watawadharau kama wakimpokea Lowassa!
Wameimba nchi nzima kwa miaka chungu nzima kwamba EL ni fisadi eti leo wampokee na kumpa nafasi ya juu kabisa ya kugombea urais!!!