Elections 2015 Kukatwa kwa Lowassa, ni mwisho wa ile safari, au ni mwanzo wa Safari Halisi ya Matumaini?

Wanabodi,

CC ya CCM, imefanya kazi yake, imelikata jina la kipenzi cha wengi, Edward Ngoyai Lowassa!.

Jee kukatwa huku ndio mwisho wa ile safari ya matumaini, au ndio mwanzo wa safari ya kweli ya matumaini, kwa kipenzi cha watu, kuanza rasmi safari ya ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania, kwa kuipeleka rasmi CCM kaburini?

Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, aliwahi kusema, upinzani wa kweli, utatoka CCM. Jee hiki ndio kipindi cha upinzani huu?

Kwa miaka 50 sasa, Watanzania tumelogwa na jinamizi la CCM kiasi cha kuamini mgombea wa CCM ndie automatically atakuwa rais wa Tanzania!. Wanaopiga kura sio CCM bali ni Watanzania!. Kama Lowassa ndie chaguo la watu, CCM wakaamua kumkata, jee sisi ambao ndio watu, tumchukue Lowassa, kupitia chama kingine chochote tumuingize ikulu?

Jee Lowassa tuliombatiza jina la mwamba, ataliishi hilo jina la mwamba kwa kuonyesha umwamba wake kwa kutokubali kuchinjwa na kufanywa mbuzi wa shughuli, au lile jina la mwamba, tulimpachika tuu, ila in reality kumbe sii mwamba lolote wala chochote, bali ni kichuguu tuu?.

Mimi bado ni muumini wa andiko hili lisemalo "Jiwe Walilolikataa Waashi, Litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni!", jee Watanzania tuendelee kuwatumainia hawa waashi wa CCM kuamua hatma yetu na taifa letu, au tumchukue mtu wetu na kusindikiza ikulu nje ya CCM?

Nauliza tena, jee huu ndio mwisho wa safari, au mwanzo wa safari ya kweli ya matumaini kwanza kwa kuingoa CCM na kuikomboa Tanzania?!.

Japo CCM ni chama kikubwa, kikongwe, na chenye nguvu, mbele ya Lowassa CCM ni chepesi kama unyoya, akipuliza tuu kinapeperuka, na hizo nguvu CCM inazojivunia, mbele ya Lowassa ni kama uzi wa utando wa buibui, ukigusa tuu umekatika!.

Wapenzi, wafuasi, na mashabiki wa Lowassa, wanachosubiri sasa ni aseme neno moja tuu na roho zao zitapoa!, akiamua kukubali matokeo kuwa kukatwa kwake ndio mwisho wa safari, na akubali na aseme wazi, "Eloi Eloi, Yemekwisha!", na kama hajakubali, atamke wazi kuianza ile safari ya ukombozi wa pili wa Mtanzania, dhidi ya mkoloni mchwa CCM, aliyelitafuna taifa letu kwa miaka 50, na akitamka tuu!, "CCM Basi!", huo ndio utakuwa mwisho wa hili zimwi linaloitwa CCM!, CCM itakuwa ni bye bye jumla, kaburini forever!, kwa sababu kazi kubwa ya kwanza ya serikali mpya, itakuwa ni kuzitaifisha mali zote za umma CCM iliyozipora na kuzipata kwa njia dhalimu kwa kuzipora toka kwa Watanzania katika kipindi cha utawala wake, na kujimilikisha kujifanya ni mali zake, yakiwemo majengo yake yote!. CCM ikiishakuwa haina kitu, hiyo sio CCM tena bali itageuka CCM mfu na tutaizika rasmi kaburini!.

Lowassa sema....
Sema usiogope sema!.

Linasubiriwa Neno tuu!.

Pasco!
fisadi papa hawezi kuingia ikulu
 
Wanabodi,



Japo CCM ni chama kikubwa, kikongwe, na chenye nguvu, mbele ya Lowassa CCM ni chepesi kama unyoya, akipuliza tuu kinapeperuka, na hizo nguvu CCM inazojivunia, mbele ya Lowassa ni kama uzi wa utando wa buibui, ukigusa tuu umekatika!.


Lowassa sema....
Sema usiogope sema!.

Linasubiriwa Neno tuu!.

Pasco!

Dah....maneno ya Mzee wa kiti moto



Sent from my beretta ARX 160 using JamiiForums Mobile App
 
Kupata nafasi UKAWA haiwezekani na yeye analijua hilo. Zitto alishaijua picha yote ndiyo maana alishamkaribisha ACT.

Sasa Pasco, mshaulini Lowasa atangaze mali zake akagombee ACT. Supremo Leader atampokea kwa mikono miwili.

Watanzania inabidi tumpe support huyu bwana maana ndiye atakaye tukomboa kutoka kwenye minyororo ya CCM!!
Dah
 
Atafanya la maana sana kama ile hadithi ya Richmond ambayo kila siku anasema ndio iliyomchafua akaja na ukweli wake hadharani tumjue muhusika halisi. Maana alisema alikubali kubeba msalaba ili kuiokoa serikali. Na mtu mzima kama yeye na aliyekuwa na madaraka ya PM akisema kuiokoa serikali, wenye akili wanajua kuwa alimaanisha kumuokoa nani.
Sasa kwa vile wamemuaibisha hata jina halikupelekwa KK naye sasa aaibishe.
Sasa hivi anawachakaza "makamanda"
 
Wanabodi,
Lowassa sema....
Sema usiogope sema!.

Linasubiriwa Neno tuu!.

Pasco!
Kama lilivyosubiriwa neno moja tuu aseme, na sasa Lowassa ndani ya upinzani, linasubiriwa neno moja tuu, aseme anarejea CCM, kwa sababu Lowassa alijiunga upinzani kwa malengo, na maadam malengo hayo hayakutimia, hakuna ubaya wowote akirejea nyumbani!.

Paskali
 
Baada ya Lowassa kusifiwa na rais Magufuli kuwa ni super man, nimemkumbuka naomba nimdurusu kidogo, niliwaji kusema nini humu kumhusu mtu huyu.

P.
 
Kama lilivyosubiriwa neno moja tuu aseme, na sasa Lowassa ndani ya upinzani, linasubiriwa neno moja tuu, aseme anarejea CCM, kwa sababu Lowassa alijiunga upinzani kwa malengo, na maadam malengo hayo hayakutimia, hakuna ubaya wowote akirejea nyumbani!.

Paskali
100% utafikiri EL alisoma hii post yako! Maana amesema "nimerudi nyumbani"
 
Wanabodi,

CC ya CCM, imefanya kazi yake, imelikata jina la kipenzi cha wengi, Edward Ngoyai Lowassa!.

Jee kukatwa huku ndio mwisho wa ile safari ya matumaini, au ndio mwanzo wa safari ya kweli ya matumaini, kwa kipenzi cha watu, kuanza rasmi safari ya ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania

Pasco!

Sasa ndio mwisho kweli wa safari ya matumaini.
Naendelea na My Tribute to this fallen hero, Mwamba wa Kaskazini, kwa kujikumbusha baadhi ya mabandiko yangu kumhusu shujaa huyu mpaka siku atakapo pumzishwa kwenye makao yake ya milele, let's celebrate the life and the times of Edward Lowassa.

RIP Shujaa Laigwanani Comred Edward Ngoyai Ole Lowassa,
Umepigana vita vilivyo vitakatifu, imani umeilinda.
Bwana alileta
Bwana ametwaa,
Jina Lake Lihimidiwe!.

Paskali
 
Back
Top Bottom