Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,459
- 29,153
Wadau,
Kama mjuavyo Bwana Edward Ngoyai Lowassa, mmojawapo ya watia nia walioonekana kuupania Urais kwa hali na mali kiasi cha kuingia gharama kubwa kuliko wengine wenzake wote kwa ujumla wao ameondolewa kwenye mchujo wa tano bora.
Kuondolewa huko kunafanya maelfu kwa malaki ya wapenzi wake waliokua na "matumaini yasiyo na uhakika" kubaki njia panda kisiasa. Wengi walitegemea angepata na ndio angekua mgombea wa CCM, wapo waliofikia kupanga kabisa Baraza la Mawaziri mpaka wakuu wa Mikoa na Wilaya wa serikali yake ijayo ya matumaini.
Wakati Lowassa akiwa Kigoma kusaka wadhamini aliwatolea "siri" moja kua amemchagua mbunge wao Bw. Peter Serukamba kua msaidizi wake muhimu katika mbio zake za Urais hivyo kutokana na majukumu yake mapya hatogombea tena ubunge jimbo hilo. Hili lilifanyika sambamba na aliekua Mbunge wa Kigoma Kaskazini Bw. Zitto Zuberi Kabwe kutangaza kuhamia jimbo la Serukamba.
Sasa basi, Lowassa ndio kaishia hapa, Serukamba atarudi Jimbo lake ambalo mwanzo alimuachia Zitto, je na Zitto nae atakubali kurudi alikokua mwanzo? Na kama akirudi atawaambia nini wananchi ambao mwanzo aliwakimbia? Watamuelewa kua kumbe alifanya makubaliano na chama tawala? Na kama akiamua kung'ang'ania kuendelea kubaki Kigoma Mjini kwa Serukamba, je serukamba nae ataenda wapi? Au ataamua kumeza matapishi yake na kugombea?
Ni mtego nauona.
Kama mjuavyo Bwana Edward Ngoyai Lowassa, mmojawapo ya watia nia walioonekana kuupania Urais kwa hali na mali kiasi cha kuingia gharama kubwa kuliko wengine wenzake wote kwa ujumla wao ameondolewa kwenye mchujo wa tano bora.
Kuondolewa huko kunafanya maelfu kwa malaki ya wapenzi wake waliokua na "matumaini yasiyo na uhakika" kubaki njia panda kisiasa. Wengi walitegemea angepata na ndio angekua mgombea wa CCM, wapo waliofikia kupanga kabisa Baraza la Mawaziri mpaka wakuu wa Mikoa na Wilaya wa serikali yake ijayo ya matumaini.
Wakati Lowassa akiwa Kigoma kusaka wadhamini aliwatolea "siri" moja kua amemchagua mbunge wao Bw. Peter Serukamba kua msaidizi wake muhimu katika mbio zake za Urais hivyo kutokana na majukumu yake mapya hatogombea tena ubunge jimbo hilo. Hili lilifanyika sambamba na aliekua Mbunge wa Kigoma Kaskazini Bw. Zitto Zuberi Kabwe kutangaza kuhamia jimbo la Serukamba.
Sasa basi, Lowassa ndio kaishia hapa, Serukamba atarudi Jimbo lake ambalo mwanzo alimuachia Zitto, je na Zitto nae atakubali kurudi alikokua mwanzo? Na kama akirudi atawaambia nini wananchi ambao mwanzo aliwakimbia? Watamuelewa kua kumbe alifanya makubaliano na chama tawala? Na kama akiamua kung'ang'ania kuendelea kubaki Kigoma Mjini kwa Serukamba, je serukamba nae ataenda wapi? Au ataamua kumeza matapishi yake na kugombea?
Ni mtego nauona.