Kukataliwa visa wanafunzi wa Minaki ...ni dalili ya nini!?

omujubi

JF-Expert Member
Dec 6, 2011
4,325
2,498
Habarini wanajf

Kwa habari zilizokuwepo ni kuwa kumekuwa na utaratibu wa shule ya Sekondari Minaki kufanya ziara za kujifunza Uingereza kwa miaka kadhaa ambapo kuna shule wanayobadlishana nayo kwa wanafunzi wake pia kuja Tanzania kwa madhumuni hayohayo (yaani shule rafiki).

Habari niliyosikia jana ni kuwa mwaka huu wanafunzi wa Tanzania wameshindwa kwenda Uingereza kwa sababu ya kukosa visa. Hii imepelekea walimu wao (maofisa) tu kwenda na wanafunzi kuishia Nairobi. (Sikuwa nime note kuwa viza za UK sasa zinachukuliwa Nairobi!)

Kwa mujibu wa mahojiano ni kuwa wanaogopa kuwapa viza hao wanafunzi ili wasije kuzamia huko badala ya kurudi TZ.

My take:
Hivi inawezekana hawa Wazungu wamepoteza imani nasi kwa kiasi hiki!???? Kwa wanaojua kwa undani juu ya hii incidence iliyobeba aibu kwa nchi yetu tafadhali atujuze.

Nawasilisha

Source: bbc radio – matangazo ya jana jioni
 
Tangu wahamishie zoezi la utoaji visa Nairobi hali si nzuri sana kwa waombaji wa visa. Sijui kunani huko Naiiii.
Angalizo: Ukipata safari ya UK hata kama una sifa zote usimwambie mtu kabla ya kudaka visa yako maana utaonekana mwongo!!!
 
ni kweli huo utaratibu ni endelevu sasa kati ya minaki high school na Imberhone school ya uk,kila mwaka wanakuja vijana na walimu wao hapa minaki kisha vijana na walimu wao nao wanakwenda..
ni kweli vijana waliomba visa lakini walitakiwa uthibitisho wa safari yao unatolewa na shule hapa na uk, ubalozi wakadai hawajapata barua toka uk mara wakasema tumepata wanataka bank statement n mambo mengine kibao almost shule imesaidia lakini ubalozi wamechomoa...
 
Tangu wahamishie zoezi la utoaji visa Nairobi hali si nzuri sana kwa waombaji wa visa. Sijui kunani huko Naiiii.
Angalizo: Ukipata safari ya UK hata kama una sifa zote usimwambie mtu kabla ya kudaka visa yako maana utaonekana mwongo!!!

hii nimeipenda
 
Back
Top Bottom