Da'Vinci
JF-Expert Member
- Dec 1, 2016
- 35,678
- 106,786
“A famous man once said We create our own Demons”
- Tony-stark (Iron man 3)
Wasomi wenye uelewe wa juu jinsi akili ya mwanadamu inavyofanya kazi (psychologist) wanasema kua mambo yote ambayo tunaona yanatisha maishani mwetu hua tunayatengezea vichwani mwetu, mfano unatembea usiku ukawa unaona uoga mara unahisi labda kitu kama kuna kitu kinakufuata kwa nyuma hua ni mambo ambayo tunayajenga kichwani sio halisi.Pengine upo ndani peke yako unaogopa hadi nguo ulizotundika ukutani unana kama vile ni mtu anakuangalia. Simply wanasema uoga/Hofu inaanza kutengenezwa vichwani mwetu, hvyo basi wanasema kua “We create our own Demon”.
Lakini pia hio sentensi ya We create our own demons ina maana kubwa katika maisha yetu ya kila siku, Mara nyingi tumekua tukitengeneza demons wengi maishani mwetu kutokana na matendo yetu ambao wanakuja kutu-haunt.
Namaanisha kwamba kutokana na matendo au maneno yetu ya kila siku bila kutegemea tumejikuta tukijitengezea maadui (Demons) wetu sisi wenyewe. Wahenga wanasema ni rahisi kumbadilisha mtu mwema akawa mtu mbaya zaidi kuliko kumbadilisha mtu mbaya kua mtu mwema, na ukimbadilisha mtu mwema akawa mtu mbaya ni ngumu san asana kumrudisha kua mtu mwema..Ukiinyambulisha hio sentesi ndio utapata ule semo kua there is a thin line between Love and Hate, hivyo ni rahisi sana mtu anayekupenda sana kumbadilisha akawa amekuchukia sana. Ni rrahisi sana mtu mwema ukamfanya akawa mtu mbaya.
Isaya 53: Alidharauliwa na kukataliwa na watu, mtu wa huzuni nyingi,ajuaye sikitiko; na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao,Alidharauliwa wala hatukumhesabu kitu
How do we make our Own Demons?
Ni kwanamna gani tunaweza kuwafanya watu wanaopenda kutenda mema kuwa wabaya au kuwafanya watu wanaotupenda sana wakawa wanatuchukia sana ? Dissapointment, yes kukatishana tama! Kumkatisha tamaa kwa maneno au matendo mtu anayekupenda au aliyetamani kufanya matendo mema ndio kunaweza kufanya watu hao wakabadilika na kua watu wabaya au wakatuchukia. Nitaelezea mifano michache
Kisa #1.
Mnamo mwaka 480BC mfalme wa Persia aitwae King Xerxes I alikua amepanga kuuvamia moja ya mji wa ugiriki uitwao Sparata ambao ulikua unatawaliwa na mfalme Leonidas, kipindi hicho Ugiriki ilikua kila mkoa unajitawala kivyake. Mfalme Leonidas alikusanya wanajeshi wake 300 tu kwenda vitani kupambana katika eneo liitwalo hotgate. Kulikua kuna mtu anaitwa Ephialtes huyu jamaa alikua anaulemavu wa kibyongo, alimfata mfalme Leonidas akamuomba ampe nafasi akajiunge jeshi aende vitani kupigana na wapersia ili kulipa kisasi cha baba yake. Kutokana na jinsi alivyokua mlemavu Mfalme Leonidas alimuonea huruma akamwambia hataweza kupambana, maana ili uende vitani inatakiwa uweze kushika ngao na mkuki uweze kujilinda wewe na kumlinda mwenzako mkiwa mnapambana.
Yule mlemavu alichukia sana kwa kukataliwa kutokana na ulemavu wake, alichoamua kufanya alienda kwa mfalme wa Persia akawapa mbinu za jinsi ya kuwazingila Leonidas na jeshi lake. Kilichotokea Leonidas na wanajeshi wake 300 walichinjwa wote kama kuku.( Mwaka uliofuata wa Persia walipigwa vibaya mno na mfale Themistocles kutoka Athens..Nishawahi andika uzi kuhusu hii vita)
Kisa #2
Mtu mmoja alikua anategemewa na watu wa eneo Fulani kutokana na msaada wa kupambana na watu waliokuja kupora mali za watu, muda mwingine alikua anawagawia chakula watu wa eneo hilo. Palitokea kijana mmoja akawa anampemda sana Yule mtu anayetoa msaada, siku zote alikua anatamani awe kama yeye. Mara nyingi alipokua akipambana na wezi waliokuja kuiba Yule kijana alikuja kumsaidia, muda mwingine alikua anamwomba kua aungane nae awe anamsaidia kufanya mambo yake ya kusaidia watu ila Yule mtu alimkatalia Yule kijana kabisa, anamwambia hawezi. Mwisho Yule kijana alikuja kua adui namba moja wa Yule mtu. Maana alikua alishamjua udhaifu wake.
Nachotaka kusema ni kwamba katika maisha yetu ya kila siku kamwe tusiwakatishe moyo watu wanaotamani kutenda vitu vyema, tusiwakatishe tamaa watu ambao wanatupenda. Kama mtu kakauambia wewe ni role model wake anataka kuungana nawe kufanya vitu ambavyo wewe unafanya kamwe usimkatishe tamaa kwa kumuambia kua hawezi, hata kama mtu huyo umemuona anaudhaifu Fulani katika kutenda jambo kama anatamani kutenda jambo hilo mpe nafasi afanye hata ile sehemu ndogo anayoweza. Super fan akiwa hater anakua hater kweli kweli, kuna watu tunawa-inspire kwa matendo yetu so mtu unayemu-inspire siku akikuomba nafasi afanye kila unachofanya wewe mruhusu usimkatishe tamaa.
Mtu akikuomba nafasi ya kufanya matendo kama unaweza kumsapoti fanaya hivo, ukimkatisha tama atajiona sio wa thamani..anaona anatamani kutenda mambo mema ila watu hawajali wema wake, bora awe mtu mbaya tu maana hakuna thamani ya kua mwema..
Kama mtu me/ke kakupenda sana na mwenyewe umethibitisha kua huyu mtu ananipenda kwa dahati ila wewe humpendi tafadhali usitumie nafasi hiyo kumuumiza watu wengi wanakua serial killers kwa ajili ya kukataliwa/oppressed na watu wanaowapenda kama wazazi au Crushes.
Mtu akikupenda usipompenda huna haja ya kumuambia kwa kashfa/kumsimanga kua humtaki , bora hata uwe unampa hata atumaini kwa hugs na maneno mazuri ya kutia moyo…Kuna watu wanapeda vibaya mno, mtu wa namna hiyo inatakiwa uchunge maneno ya kumjibu pindi mnapoongea. Maana ukimjibu majibu ya kumkashfu atajiona hana thamani duniani, ataona watu hawatakiwi kupendwa nakufanyia wema..mtu kama huyo anaweza kujidhuru au asipojidhuru basi anaweza kudhuru wengine. Hapa ndio wanatokea sasa wale wazee wa hit and run, anakuzalisha anakutelekeza, au anaweza kua muuaji (kuna kesi nyingi ajili hili).
Watu wabaya tunawatengeneza sisi wenye, hakuna anayezaliwa akiwa na roho mbaya. Kamwe usimwambie mtu hawezi kufanya kitu Fulani, hata kama unamuona hawezi kufanya jambo Fulani; Kuna watu wengine wakifanaya jambo Fulani likawashinda basi wanakua kila mtu akitaka kufanya jambo hilo wanamwambia kua hawezi Mtie moyo Mtu anapotaka kutenda jambo Fulani hata kama uanaona ni dhaifu…Tuheshimu watu wanye hisia za kweli nasi, tusapoti watu wanaotamani kuifanaya dunia kuwa sehemu salama ya kuishi.
-Ahsante
Da’Vinci
- Tony-stark (Iron man 3)
Wasomi wenye uelewe wa juu jinsi akili ya mwanadamu inavyofanya kazi (psychologist) wanasema kua mambo yote ambayo tunaona yanatisha maishani mwetu hua tunayatengezea vichwani mwetu, mfano unatembea usiku ukawa unaona uoga mara unahisi labda kitu kama kuna kitu kinakufuata kwa nyuma hua ni mambo ambayo tunayajenga kichwani sio halisi.Pengine upo ndani peke yako unaogopa hadi nguo ulizotundika ukutani unana kama vile ni mtu anakuangalia. Simply wanasema uoga/Hofu inaanza kutengenezwa vichwani mwetu, hvyo basi wanasema kua “We create our own Demon”.
Lakini pia hio sentensi ya We create our own demons ina maana kubwa katika maisha yetu ya kila siku, Mara nyingi tumekua tukitengeneza demons wengi maishani mwetu kutokana na matendo yetu ambao wanakuja kutu-haunt.
Namaanisha kwamba kutokana na matendo au maneno yetu ya kila siku bila kutegemea tumejikuta tukijitengezea maadui (Demons) wetu sisi wenyewe. Wahenga wanasema ni rahisi kumbadilisha mtu mwema akawa mtu mbaya zaidi kuliko kumbadilisha mtu mbaya kua mtu mwema, na ukimbadilisha mtu mwema akawa mtu mbaya ni ngumu san asana kumrudisha kua mtu mwema..Ukiinyambulisha hio sentesi ndio utapata ule semo kua there is a thin line between Love and Hate, hivyo ni rahisi sana mtu anayekupenda sana kumbadilisha akawa amekuchukia sana. Ni rrahisi sana mtu mwema ukamfanya akawa mtu mbaya.
Isaya 53: Alidharauliwa na kukataliwa na watu, mtu wa huzuni nyingi,ajuaye sikitiko; na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao,Alidharauliwa wala hatukumhesabu kitu
How do we make our Own Demons?
Ni kwanamna gani tunaweza kuwafanya watu wanaopenda kutenda mema kuwa wabaya au kuwafanya watu wanaotupenda sana wakawa wanatuchukia sana ? Dissapointment, yes kukatishana tama! Kumkatisha tamaa kwa maneno au matendo mtu anayekupenda au aliyetamani kufanya matendo mema ndio kunaweza kufanya watu hao wakabadilika na kua watu wabaya au wakatuchukia. Nitaelezea mifano michache
Kisa #1.
Mnamo mwaka 480BC mfalme wa Persia aitwae King Xerxes I alikua amepanga kuuvamia moja ya mji wa ugiriki uitwao Sparata ambao ulikua unatawaliwa na mfalme Leonidas, kipindi hicho Ugiriki ilikua kila mkoa unajitawala kivyake. Mfalme Leonidas alikusanya wanajeshi wake 300 tu kwenda vitani kupambana katika eneo liitwalo hotgate. Kulikua kuna mtu anaitwa Ephialtes huyu jamaa alikua anaulemavu wa kibyongo, alimfata mfalme Leonidas akamuomba ampe nafasi akajiunge jeshi aende vitani kupigana na wapersia ili kulipa kisasi cha baba yake. Kutokana na jinsi alivyokua mlemavu Mfalme Leonidas alimuonea huruma akamwambia hataweza kupambana, maana ili uende vitani inatakiwa uweze kushika ngao na mkuki uweze kujilinda wewe na kumlinda mwenzako mkiwa mnapambana.
Yule mlemavu alichukia sana kwa kukataliwa kutokana na ulemavu wake, alichoamua kufanya alienda kwa mfalme wa Persia akawapa mbinu za jinsi ya kuwazingila Leonidas na jeshi lake. Kilichotokea Leonidas na wanajeshi wake 300 walichinjwa wote kama kuku.( Mwaka uliofuata wa Persia walipigwa vibaya mno na mfale Themistocles kutoka Athens..Nishawahi andika uzi kuhusu hii vita)
Kisa #2
Mtu mmoja alikua anategemewa na watu wa eneo Fulani kutokana na msaada wa kupambana na watu waliokuja kupora mali za watu, muda mwingine alikua anawagawia chakula watu wa eneo hilo. Palitokea kijana mmoja akawa anampemda sana Yule mtu anayetoa msaada, siku zote alikua anatamani awe kama yeye. Mara nyingi alipokua akipambana na wezi waliokuja kuiba Yule kijana alikuja kumsaidia, muda mwingine alikua anamwomba kua aungane nae awe anamsaidia kufanya mambo yake ya kusaidia watu ila Yule mtu alimkatalia Yule kijana kabisa, anamwambia hawezi. Mwisho Yule kijana alikuja kua adui namba moja wa Yule mtu. Maana alikua alishamjua udhaifu wake.
Nachotaka kusema ni kwamba katika maisha yetu ya kila siku kamwe tusiwakatishe moyo watu wanaotamani kutenda vitu vyema, tusiwakatishe tamaa watu ambao wanatupenda. Kama mtu kakauambia wewe ni role model wake anataka kuungana nawe kufanya vitu ambavyo wewe unafanya kamwe usimkatishe tamaa kwa kumuambia kua hawezi, hata kama mtu huyo umemuona anaudhaifu Fulani katika kutenda jambo kama anatamani kutenda jambo hilo mpe nafasi afanye hata ile sehemu ndogo anayoweza. Super fan akiwa hater anakua hater kweli kweli, kuna watu tunawa-inspire kwa matendo yetu so mtu unayemu-inspire siku akikuomba nafasi afanye kila unachofanya wewe mruhusu usimkatishe tamaa.
Mtu akikuomba nafasi ya kufanya matendo kama unaweza kumsapoti fanaya hivo, ukimkatisha tama atajiona sio wa thamani..anaona anatamani kutenda mambo mema ila watu hawajali wema wake, bora awe mtu mbaya tu maana hakuna thamani ya kua mwema..
Kama mtu me/ke kakupenda sana na mwenyewe umethibitisha kua huyu mtu ananipenda kwa dahati ila wewe humpendi tafadhali usitumie nafasi hiyo kumuumiza watu wengi wanakua serial killers kwa ajili ya kukataliwa/oppressed na watu wanaowapenda kama wazazi au Crushes.
Mtu akikupenda usipompenda huna haja ya kumuambia kwa kashfa/kumsimanga kua humtaki , bora hata uwe unampa hata atumaini kwa hugs na maneno mazuri ya kutia moyo…Kuna watu wanapeda vibaya mno, mtu wa namna hiyo inatakiwa uchunge maneno ya kumjibu pindi mnapoongea. Maana ukimjibu majibu ya kumkashfu atajiona hana thamani duniani, ataona watu hawatakiwi kupendwa nakufanyia wema..mtu kama huyo anaweza kujidhuru au asipojidhuru basi anaweza kudhuru wengine. Hapa ndio wanatokea sasa wale wazee wa hit and run, anakuzalisha anakutelekeza, au anaweza kua muuaji (kuna kesi nyingi ajili hili).
Watu wabaya tunawatengeneza sisi wenye, hakuna anayezaliwa akiwa na roho mbaya. Kamwe usimwambie mtu hawezi kufanya kitu Fulani, hata kama unamuona hawezi kufanya jambo Fulani; Kuna watu wengine wakifanaya jambo Fulani likawashinda basi wanakua kila mtu akitaka kufanya jambo hilo wanamwambia kua hawezi Mtie moyo Mtu anapotaka kutenda jambo Fulani hata kama uanaona ni dhaifu…Tuheshimu watu wanye hisia za kweli nasi, tusapoti watu wanaotamani kuifanaya dunia kuwa sehemu salama ya kuishi.
-Ahsante
Da’Vinci