Kujizatiti vita dhidi ya biashara madawa - Ujasusi na Teknolojia pia vinahitaji kuboreshwa

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,853
20,173
Mkuu wa mkoa wa Dar-es-Salaam Paul Makonda ameamua kulivalia njuga suala la biashara ya mihadarati nchini.

Bwana Makonda anaamini kwamba mkoa wa Dar-es-Salaaam ndiyo unaoongoza kwa biashara hii iloshamiri kila pembe.

Itakumbukwa mwishoni mwa mwaka jana, Paul Makonda alifanya ziara ya kuutembelea mkoa wa Dar-es-Salaam kuufahamu vizuri na kutaka kuangalia namna ya kuuboresha mkoa huu ambao yeye ni mwakilishi wa raisi.

Paul Makonda alipita maeneo mengi na mojawapo ya maeneo hayo ni eneo maarufu la uwanja wa fisi.

Akiwa eneo hilo Makonda alishuhudia kwa macho yake watumiaji wa madawa ya kulevya na mateja wengi ambao hawana ajira na wengine wakiwa wamekata tamaa ya maisha kutokana na hali duni kifedha na kimaisha.

Lakini hivi karibuni mheshimiwa Makonda amaeamua kuwatangaza hadharani wale wote wanaotajwa kuhusika na biashara hii ya mihadarati huku ikisadikiwa kuwa bei ya gram 50 kwa kilo mitaani imesimama kwenye shilingi za kitanzania 140,000 taslim.

Lakini nikiwa mdau wa masuala ya teknolojia, na ujasirimali , imebidi nichangie kidogo kuhusu biashara hii ya madawa ya kulevya, matumizi ya teknolojia na ujasusi wa kutukuka.

Kisha ntaelezea namna ya kuweza kupambana na njia zinazotumika kufanikisha biashara hiyo na hatima yake kama angalau italeta ahueni kwa watumiaji au Mateja huko mitaani.

Biashara hii ya madawa ya kulevya inafanikishwa kwa kutumia njia za usafiri wa ndege, meli, binadamu, malori, mitumbwi na boti kasi, pamoja na magari yaagizwayo na kuingizwa nchini Tanzania.

Kwa kifupi mkoa wa Dar-es-Salaam ambao ni mkoa wa kibiashara wa Tanzania "Commercial City" mpaka sasa katika duru za biashara hii mkoa huu unatambulika kama ndiyo kituo kikuu ya usafirishaji wa madawa haya au "major transit route" ya madawa yanayopitishwa kwenda nchini Afrika Kusini kupitia bandari ya Mtwara.

Mpaka kufikia mwanzoni mwa mwaka 2016 biashara hii ilikuwa imeota mizizi mikubwa ilokomaa na kuthibitisha hilo mheshimiwa raisi wa JMT John Magufuli aliona jinsi machine za udukuzi "Scanners" katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere na baadae pale Bandarini Dar-es-Salaam zikiwa hazifanyi kazi.

Kuharibiwa kwa makusudi kwa mashine hizo ni katika kuhakikisha mzigo unapitishwa na vijana wabebaji bila shida, huku malori yakipitisha mizigo hiyo katika bandari za Dar-es-Salaam, Mtwara, Tanga, Zanzibar na bandari za kutengezwa (boat parking berths) kama Bagamoyo na Kunduchi.

Safari ya madawa ya kulevya inaanzia nchini Afghanstan nchi ambayo haina bandari au "landlocked".

Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya umoja wa mataifa kitengo kinachoshughulikia madawa au UNODC, nchi ya Afghanistan inazalisha tani 355 kila mwaka ikiwa ni asilimia 90 ya madawa yote yanayozalishwa duniani.

Pakistani na Afghanistan kwa pamoja wanatumia mpaka wao ambao una kilomita zipatazo 2500 ambao pia unawasaidia watoroshaji wa madawa hayo kupitia sehemu mbalimbali za kusini na kusini mgharibi mwa Pakistani hususani katika majimbo ya Sindh ambako kuna bandari ya Karachi na Balochistan ambako watoroshaji wanatumia njia ya ardhini.

Pamoja na madawa haya kupenyezwa na kusafirishwa kwenda barani Ulaya na Marekani lakini pia kuna njia ya kuyapitisha kuhakikisha yanafika katika pwani ya Tanzania.

Waafrika waliopo nchini Pakistani katika mji wa bandari wa Karachi huakikisha madawa hayo yanapakiwa katika mabunda madogomadogo "nylon sachets" kisha kuwekwa ndani ya madebe maalum na kuwekewa kifaa maalum ya kukifuatilia au "tracking device" kiitwacho GPRS yaani General Packet Radio Service.

GPRS ni mfumo wa mawasiliano ya simu ambao unatumia mtambo wa 2G na 3G kusafirisha kipande cha taarifa au Data kwa kasi.

Mwishoni mwa miaka ya tisini kulikuwa na mfumo wa 2G na baadae mwaka 2001 ukaja mfumo wa 3G na baadae mwaka 2012 tumeona mfumo mpya wa 4G ambao ndiyo unatumika kwa sasa kwenye simu za mikononi.

Lakini wasafirishaji wa madawa ya kulevya wao bado wanatumia mifumo ya 2G na 3G ambayo inawasadia kuhakikisha picha za mizigo, video na sehemu kidogo ya maelezo ya kuhusu mzigo kama umepakiwa salama na umeondoka bandarini Karachi kuelekea pwani ya Dar-es-Salaam.

Meli zitokeazo Karachi zikifika mbali kidogo ya pwani ya Tanzania karibu na bandari za Tanga, Zanzibar na Bagamoyo, nyakati za usiku au mchana, mizigo hiyo ya madawa hudondoshwa bandarini na hapo boti kasi huelekea katika sehemu hizo huku wasafirishaji wakitumia simu za mikononi na vifaa vya mawasiliano kukomboa mizigo hiyo na kuifikisha katika nchi kavu za miji ya Tanga, Dar-es-Salaam na Zanzibar.

Kwa kuwa biashara hiyo ni rasmi katika mji wa Dar-es-Salaam, yapo maeneo kadhaa ambayo yana bohari maalum za kuhakikisha mizigo hiyo inafunguliwa na kufungwa upya katika uzito mbalimbali kulingana na mahitaji ya soko na mizigo mingine kuwa tayari kusafirishwa kwenda nchini Afrika Kusini kupitia bandari ya Mtwara.

Tayari majina mbalimbali yametajwa kuhusishwa na biashara hii na majina mengine ni mazito ambayo yanahusisha watu wenye nafasi katika jamii.

Vita ya madawa ya kulenya ni kubwa na inayohitaji umakini mkubwa lakini haiwezi kushindwa.

Pia vita hii inahitaji uwezo mkubwa wa fedha ambazo zitawekezwa kwenye idara husika ya kitengo cha kupambana na madawa ya kulevya.

Tumesikia raisi wa Philippines bwana Rodrigo Duterte yeye aliamua kuwa watumiaji wa madawa ya kulevya wauwawe tangu ainge madarakani mwezi Juni mwaka jana na mpaka sasa watu 7600 wakiwemo watumiaji na wasambazaji wameuawa.

Pamoja na kuwepo kwa watu wanaopinga vita hii ya madawa ya kulevya inayofanywa na raisi Duterte, idadi kubwa ya wananchi wanaunga mkono juhudi yake hii kiasi cha kumpa nguvu ya kusema kwamba kampeni yake hii itaendelea ndani ya kipindi chote cha utawala wake ambao utaishia mwaka 2022.

Hapa nchini Tanzania mkuu wa mkoa wa Dar-es-Salaam ambao umeathirika na biashara hiyo nae ameamua kulivalia njuga suala hilo na anahitaji pongezi na msaada mkubwa.

Fedha zinazohitajika ni pamoja na zile za kujenga vituo maalum au kutenga kitengo maalum au "rehabilitation centre" ndani ya hospitali kadhaa ili kuwasaidia wale mateja wote ambao watakuwa tayari kushirikiana serikali katika mapambano dhidi ya biashara hii.

Lakini pamoja na mkuu wa mkoa bwana Paul Makonda kujitokeza kujaribu kutatua tatizo hili bado kunahitajika juhudi zaidi khasa za wizara ya mambo ya ndani na kitengo cha kupambana na madawa ya kulevya.

Na kama nilivyoainisha hapo juu teknolojia inayotumika kuwezesha usafirishaji wa madawa haya, kwa Tanzania tuna budi kuwekeza katika vifaa na teknolojia katika kukabiliana na suala hili khasa kuwa hatua moja mbele au "one step forward".

Kwa kuwa wasafrishaji wanatumia vifaa vya GPRS kufanikisha biashara yao basi polisi wa kitengo cha kudhibiti madawa wanapaswa kuwa na ujuzi wa teknolojia kama hizi, kupewa vitendea kazi kama "helicopter" maalum zenye uwezo wa kupiga picha nyakati zote za mchana na usiku (ingawa shughuli hizi hufanywa usiku) na ndege zijiendeshazo zenyewe au "Drones".

"Helicopter" na "drones" zinaweza kutumika kufanya doria katika pwani za Tanga, Dar-es-Salaa, Bagamoyo, Zanzibar na Mtwara.

Lakini vita hii itafanikiwa pia kwa waziri husika wa mambo ya ndani kuja na mikakati yake ambayo anapaswa kuisoma bungeni kwa kutumia muswada wa dharura ambao utakuwa umerekebisha baadhi ya vipengele mbalimbali vya makosa ya kukutwa na madawa ya kulevya.

Mpaka sasa ni mheshimiwa raisi John Magufuli na Paul Makonda peke yao ambao wametoa kauli kuhusu biashara hii ya madawa ya kulevya hadharani.

Waziri husika Mwigulu Nchemba upo wapi?
 
Hongera mtoa mada kwa mada nzuri binafsi naona siasa imeingia katika Vita hii kuanzia kwa Wananchi,Viongozi na wahusika Hawakuandaliwa maana vita hii ni kubwa Tuombe Mungu tuvuke salama
 
Hivi kifaa cha kuonesha location ya kitu ni GPS(Global positioning system) au GPRS? Maana ninayoijua mimi ni GPS hadi kwenye simu zetu ina access location ya kitu. Ikiwa on unaweza kupost status mtandaoni ikataja location



Pia nikupongeze kwa mawazo mazuri ingawa vitu ulivyoviitaja vinahitaji bajeti ya hali ya juu, kuboresha doria pia uandae na bajeti ya kuwalipa hao maaskari. Mashine ya kuendesha hiyo drone, mafuta ya kila siku kwa ajili ya helikopta. Halafu kuvinunua sidhani kama kuna mkopo.
 
hili janga ni la kimataifa hata imeishashdikana tuache kurukaruka kama maharage yanayotaka kuchemka.
 
Nimependa uthubutu wa jambo hili utapunguza walau maana hawa wauzaji imekuwa sio siri tena mambo hadharani tutapoteza nguvu kazi kiasi gani hili likienda woga kiasi utakuwepo na hongera mleta mada umeeleza vizuri
 
Hivi kifaa cha kuonesha location ya kitu ni GPS(Global positioning system) au GPRS? Maana ninayoijua mimi ni GPS hadi kwenye simu zetu ina access location ya kitu. Ikiwa on unaweza kupost status mtandaoni ikataja location



Pia nikupongeze kwa mawazo mazuri ingawa vitu ulivyoviitaja vinahitaji bajeti ya hali ya juu, kuboresha doria pia uandae na bajeti ya kuwalipa hao maaskari. Mashine ya kuendesha hiyo drone, mafuta ya kila siku kwa ajili ya helikopta. Halafu kuvinunua sidhani kama kuna mkopo.

Mkuu, kuna GPS na GPRS.

GPS inahusika na ramani kwenye jiografia na pale unapotafuta location ndiyo GPS inakuwa tayari kupata khasa mahala kupitia msaada wa Satelite.

GPRS ni masuala ya Data na simu ambazo wanatumia GSM au Global system for mobile communications.

Hivyo GPS inatumika kwa magari na anaetafuta location na GPRS ni kwa kusafirisha Data kwa kutumia simu ya mkononi.
 
Hivi kifaa cha kuonesha location ya kitu ni GPS(Global positioning system) au GPRS? Maana ninayoijua mimi ni GPS hadi kwenye simu zetu ina access location ya kitu. Ikiwa on unaweza kupost status mtandaoni ikataja location



Pia nikupongeze kwa mawazo mazuri ingawa vitu ulivyoviitaja vinahitaji bajeti ya hali ya juu, kuboresha doria pia uandae na bajeti ya kuwalipa hao maaskari. Mashine ya kuendesha hiyo drone, mafuta ya kila siku kwa ajili ya helikopta. Halafu kuvinunua sidhani kama kuna mkopo.

Hiyo ndiyo changamoto kubwa kwa nchi kama yetu , lakini penye nia pana njia.

Leo hii huko Uingereza kwenye moja ya pwani yao wamegundua mzigo wa tani 315 wa madawa wenye thamani ya mtaani kiasi cha pauni milioni 50.

Sasa hao ni wazungu na wanajaribiwa kiasi hicho.

Vifaa na uwezo wa fedha wanao lakini wana kazi ya kuhakikisha angalau wanazuia hii kitu isiathiri mitaani huko London.
 
Hiyo ndiyo changamoto kubwa kwa nchi kama yetu , lakini penye nia pana njia.

Leo hii huko Uingereza kwenye moja ya pwani yao wamegundua mzigo wa tani 315 wa madawa wenye thamani ya mtaani kiasi cha pauni milioni 50.

Sasa hao ni wazungu na wanajaribiwa kiasi hicho.

Vifaa na uwezo wa fedha wanao lakini wana kazi ya kuhakikisha angalau wanazuia hii kitu isiathiri mitaani huko London.


Tukiacha siasa hizi za karne hii ambazo wenzetu wamezipa kisogo kuendelea na maendeleo, tutafika huko
 
Serikali ya Tanzania suala la teknolojia sio priority kabisa,kama teknolojia ingetumiwa vizuri kwenye sekta kama elimu,afya,kilimo,uchumi,miundombinu,ulinzi tungepungumza mzigo wa matatizo mengi sana
 
Serikali ya Tanzania suala la teknolojia sio priority kabisa,kama teknolojia ingetumiwa vizuri kwenye sekta kama elimu,afya,kilimo,uchumi,miundombinu,ulinzi tungepungumza mzigo wa matatizo mengi sana

Unaweza kuwa uko sahihi mkuu.

Israeli sasa hivi wanakamilisha taratibu za kufungua ofisi ya kibalozi mjini Dar-es-Salaam, hivyo si mbaya kama watanzania wakatumia nafasi hiyo kuomba ushirikiano wapatiwe ujuzi wa teknolojia hawa wayahudi katika masuala khasa ya kilimo na ulinzi ni wataalam walotukuka khasa.

Kazi ya kujiletea maendeleo si ya serikali pekee bali kila mwananchi aliepata ufunuo wa kimawazo yaani twasema, umekuwa "enlightened".
 
Unaweza kuwa uko sahihi mkuu.

Israeli sasa hivi wanakamilisha taratibu za kufungua ofisi ya kibalozi mjini Dar-es-Salaam, hivyo si mbaya kama watanzania wakatumia nafasi hiyo kuomba ushirikiano wapatiwe ujuzi wa teknolojia hawa wayahudi katika masuala khasa ya kilimo na ulinzi ni wataalam walotukuka khasa.

Kazi ya kujiletea maendeleo si ya serikali pekee bali kila mwananchi aliepata ufunuo wa kimawazo yaani twasema, umekuwa "enlightened".
Tatizo kubwa liko kwa viongozi wetu,hawataki kuipa kipaumbele sekta ya ICT ndio maana budget ni ndogo,training hakuna na hata yale maeneo nyeti wanashindwa kuyapa kipaumbele

1.Mpaka leo kuna kituo kimoja cha wabunifu wa teknolojia (Buni Hub) chini ya Wizara ya Elimu na Sayansi ambapo vijana mbalimbali huwa wanaenda kujifunza mambo mbalimbali ya ubunifu wa teknolojia na ujasiriamali,ni aibu kwa nchi kubwa yenye mikoa zaidi ya 30 kuwa na kituo kimoja,vipaji vilivyopo Shinyanga,Kigoma,Manyara,Mtwara,Pemba hivi nani ataviendeleza ?
Hizi hub zilipaswa kuwepo kila mkoa angalau kuanzia na kanda (kusini,kaskazini,magharibi,kati,mashariki,pwani na Zanzibar)

2.Shule za ufundi (Tanga Technical,Moshi Technical,Ifunda Technical,Ifunda Technical) ambazo zilikuwa ni mahali ambapo mafundi na wataalamu mbalimbali walikuwa wanaendelezwa zimetelekezwa na serikali zimebaki magofu.Vifaa vya kujifunzia hakuna,majengo yamebaki magofu hata kupaka rangi imeshindikana.Huku ndio sehemu ya kutengeneza wahandisi ambao watakuwa msaada zaidi

3.Majeshi yetu ya ulinzi wa nchi (Polisi,Uhamiaji,Zimamoto,Magereza,JWTZ na Mahakama) hawa bado wanafanya kazi kwa mfumo wa manual na mpaka sasa hakuna dalili ya kubadilika,wamejitahidi kuajiri baadhi ya wataalamu wa fani mbalimbali lakini maajabu ni kwamba wakifika huko hakuna anayefanya kazi kutokana na kitengo alichosomea

4.Tulipaswa kuwa na kitengo maalum ambacho kingepewa kazi ya kulinda maeneo nyeti kama viwanja vya ndege,bandarini,mbuga za wanyama,migodini.Na wapewe vifaa vya kisasa na mafunzo ya kutosha ni vigumu sana kuifanya hii kazi kutumia askari wa kawaida ambao maslahi yao ni madogo ni rahisi kupokea rushwa,hawana utaalamu wa kutosha
 
Tatizo kubwa liko kwa viongozi wetu,hawataki kuipa kipaumbele sekta ya ICT ndio maana budget ni ndogo,training hakuna na hata yale maeneo nyeti wanashindwa kuyapa kipaumbele

1.Mpaka leo kuna kituo kimoja cha wabunifu wa teknolojia (Buni Hub) chini ya Wizara ya Elimu na Sayansi ambapo vijana mbalimbali huwa wanaenda kujifunza mambo mbalimbali ya ubunifu wa teknolojia na ujasiriamali,ni aibu kwa nchi kubwa yenye mikoa zaidi ya 30 kuwa na kituo kimoja,vipaji vilivyopo Shinyanga,Kigoma,Manyara,Mtwara,Pemba hivi nani ataviendeleza ?
Hizi hub zilipaswa kuwepo kila mkoa angalau kuanzia na kanda (kusini,kaskazini,magharibi,kati,mashariki,pwani na Zanzibar)

2.Shule za ufundi (Tanga Technical,Moshi Technical,Ifunda Technical,Ifunda Technical) ambazo zilikuwa ni mahali ambapo mafundi na wataalamu mbalimbali walikuwa wanaendelezwa zimetelekezwa na serikali zimebaki magofu.Vifaa vya kujifunzia hakuna,majengo yamebaki magofu hata kupaka rangi imeshindikana.Huku ndio sehemu ya kutengeneza wahandisi ambao watakuwa msaada zaidi

3.Majeshi yetu ya ulinzi wa nchi (Polisi,Uhamiaji,Zimamoto,Magereza,JWTZ na Mahakama) hawa bado wanafanya kazi kwa mfumo wa manual na mpaka sasa hakuna dalili ya kubadilika,wamejitahidi kuajiri baadhi ya wataalamu wa fani mbalimbali lakini maajabu ni kwamba wakifika huko hakuna anayefanya kazi kutokana na kitengo alichosomea

4.Tulipaswa kuwa na kitengo maalum ambacho kingepewa kazi ya kulinda maeneo nyeti kama viwanja vya ndege,bandarini,mbuga za wanyama,migodini.Na wapewe vifaa vya kisasa na mafunzo ya kutosha ni vigumu sana kuifanya hii kazi kutumia askari wa kawaida ambao maslahi yao ni madogo ni rahisi kupokea rushwa,hawana utaalamu wa kutosha
Mkuu umeongea points sana kwa kweli, Mchawi wetu kabisa namba moja nchi hii ni Siasa, Siku tukigundua Siasa haitatupeleka popote pale basi tuta invest katika vitu vya maana kabisa Taaluma(professional) na Special Talent (mpira,muziki na sanaa zingine, Leo politicians Wamejawa na Viburi kisa tu Mtu kapewa madaraka leo hii hakuna motivation Kwa vijana wasomao science mashuleni, Hakuna events za kupongeza wana sayansi wa kada mbalimbali, mtoto mdogo leo anawaza awe mbunge waziri kwa vile tu anaona namna gani hawa watu ni valued katika jamii
,Kamwe nchi haijengwi na siasa longo longo nchi hujengewa kwa maarifa
 
Mkuu umeongea points sana kwa kweli, Mchawi wetu kabisa namba moja nchi hii ni Siasa, Siku tukigundua Siasa haitatupeleka popote pale basi tuta invest katika vitu vya maana kabisa Taaluma(professional) na Special Talent (mpira,muziki na sanaa zingine, Leo politicians Wamejawa na Viburi kisa tu Mtu kapewa madaraka leo hii hakuna motivation Kwa vijana wasomao science mashuleni, Hakuna events za kupongeza wana sayansi wa kada mbalimbali, mtoto mdogo leo anawaza awe mbunge waziri kwa vile tu anaona namna gani hawa watu ni valued katika jamii
,Kamwe nchi haijengwi na siasa longo longo nchi hujengewa kwa maarifa

Ni kweli kabisa, mtu anawaza akiwa mbunge basi ameula amekuwa tajiri.

Mfanyabiashara anawaza kuwa awe mbunge ili afiche biashara yake kwa mwavuli wa ubunge.

Na wanataaluma wanawaza sana kuwa mawaziri ili waingie kwenye siasa, hatujasikia hata siku moja kajitokeza profesa wa sayansi kuzungumzia eneo hilo au hata kaugunduzi katika sayansi katika vyombo vya habari.

Kielelezo cha mwisho tumekishuhudia watoto wa kidato cha nne wakifeli vibaya mno katika mtihani.

Tatizo litaendelea kuwa lilelile miaka nenda rudi kama watu wa aina ya Nape Nnauye hawatakuja na mipango na mikakati ya angalau kuiona Taifa Stars kwenye fainali za AFCON baada ya miaka 37 sasa.
 
Mkuu wa mkoa wa Dar-es-Salaam Paul Makonda ameamua kulivalia njuga suala la biashara ya mihadarati nchini.

Bwana Makonda anaamini kwamba mkoa wa Dar-es-Salaaam ndiyo unaoongoza kwa biashara hii iloshamiri kila pembe.

Itakumbukwa mwishoni mwa mwaka jana, Paul Makonda alifanya ziara ya kuutembelea mkoa wa Dar-es-Salaam kuufahamu vizuri na kutaka kuangalia namna ya kuuboresha mkoa huu ambao yeye ni mwakilishi wa raisi.

Paul Makonda alipita maeneo mengi na mojawapo ya maeneo hayo ni eneo maarufu la uwanja wa fisi.

Akiwa eneo hilo Makonda alishuhudia kwa macho yake watumiaji wa madawa ya kulevya na mateja wengi ambao hawana ajira na wengine wakiwa wamekata tamaa ya maisha kutokana na hali duni kifedha na kimaisha.

Lakini hivi karibuni mheshimiwa Makonda amaeamua kuwatangaza hadharani wale wote wanaotajwa kuhusika na biashara hii ya mihadarati huku ikisadikiwa kuwa bei ya gram 50 kwa kilo mitaani imesimama kwenye shilingi za kitanzania 140,000 taslim.

Lakini nikiwa mdau wa masuala ya teknolojia, na ujasirimali , imebidi nichangie kidogo kuhusu biashara hii ya madawa ya kulevya, matumizi ya teknolojia na ujasusi wa kutukuka.

Kisha ntaelezea namna ya kuweza kupambana na njia zinazotumika kufanikisha biashara hiyo na hatima yake kama angalau italeta ahueni kwa watumiaji au Mateja huko mitaani.

Biashara hii ya madawa ya kulevya inafanikishwa kwa kutumia njia za usafiri wa ndege, meli, binadamu, malori, mitumbwi na boti kasi, pamoja na magari yaagizwayo na kuingizwa nchini Tanzania.

Kwa kifupi mkoa wa Dar-es-Salaam ambao ni mkoa wa kibiashara wa Tanzania "Commercial City" mpaka sasa katika duru za biashara hii mkoa huu unatambulika kama ndiyo kituo kikuu ya usafirishaji wa madawa haya au "major transit route" ya madawa yanayopitishwa kwenda nchini Afrika Kusini kupitia bandari ya Mtwara.

Mpaka kufikia mwanzoni mwa mwaka 2016 biashara hii ilikuwa imeota mizizi mikubwa ilokomaa na kuthibitisha hilo mheshimiwa raisi wa JMT John Magufuli aliona jinsi machine za udukuzi "Scanners" katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere na baadae pale Bandarini Dar-es-Salaam zikiwa hazifanyi kazi.

Kuharibiwa kwa makusudi kwa mashine hizo ni katika kuhakikisha mzigo unapitishwa na vijana wabebaji bila shida, huku malori yakipitisha mizigo hiyo katika bandari za Dar-es-Salaam, Mtwara, Tanga, Zanzibar na bandari za kutengezwa (boat parking berths) kama Bagamoyo na Kunduchi.

Safari ya madawa ya kulevya inaanzia nchini Afghanstan nchi ambayo haina bandari au "landlocked".

Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya umoja wa mataifa kitengo kinachoshughulikia madawa au UNODC, nchi ya Afghanistan inazalisha tani 355 kila mwaka ikiwa ni asilimia 90 ya madawa yote yanayozalishwa duniani.

Pakistani na Afghanistan kwa pamoja wanatumia mpaka wao ambao una kilomita zipatazo 2500 ambao pia unawasaidia watoroshaji wa madawa hayo kupitia sehemu mbalimbali za kusini na kusini mgharibi mwa Pakistani hususani katika majimbo ya Sindh ambako kuna bandari ya Karachi na Balochistan ambako watoroshaji wanatumia njia ya ardhini.

Pamoja na madawa haya kupenyezwa na kusafirishwa kwenda barani Ulaya na Marekani lakini pia kuna njia ya kuyapitisha kuhakikisha yanafika katika pwani ya Tanzania.

Waafrika waliopo nchini Pakistani katika mji wa bandari wa Karachi huakikisha madawa hayo yanapakiwa katika mabunda madogomadogo "nylon sachets" kisha kuwekwa ndani ya madebe maalum na kuwekewa kifaa maalum ya kukifuatilia au "tracking device" kiitwacho GPRS yaani General Packet Radio Service.

GPRS ni mfumo wa mawasiliano ya simu ambao unatumia mtambo wa 2G na 3G kusafirisha kipande cha taarifa au Data kwa kasi.

Mwishoni mwa miaka ya tisini kulikuwa na mfumo wa 2G na baadae mwaka 2001 ukaja mfumo wa 3G na baadae mwaka 2012 tumeona mfumo mpya wa 4G ambao ndiyo unatumika kwa sasa kwenye simu za mikononi.

Lakini wasafirishaji wa madawa ya kulevya wao bado wanatumia mifumo ya 2G na 3G ambayo inawasadia kuhakikisha picha za mizigo, video na sehemu kidogo ya maelezo ya kuhusu mzigo kama umepakiwa salama na umeondoka bandarini Karachi kuelekea pwani ya Dar-es-Salaam.

Meli zitokeazo Karachi zikifika mbali kidogo ya pwani ya Tanzania karibu na bandari za Tanga, Zanzibar na Bagamoyo, nyakati za usiku au mchana, mizigo hiyo ya madawa hudondoshwa bandarini na hapo boti kasi huelekea katika sehemu hizo huku wasafirishaji wakitumia simu za mikononi na vifaa vya mawasiliano kukomboa mizigo hiyo na kuifikisha katika nchi kavu za miji ya Tanga, Dar-es-Salaam na Zanzibar.

Kwa kuwa biashara hiyo ni rasmi katika mji wa Dar-es-Salaam, yapo maeneo kadhaa ambayo yana bohari maalum za kuhakikisha mizigo hiyo inafunguliwa na kufungwa upya katika uzito mbalimbali kulingana na mahitaji ya soko na mizigo mingine kuwa tayari kusafirishwa kwenda nchini Afrika Kusini kupitia bandari ya Mtwara.

Tayari majina mbalimbali yametajwa kuhusishwa na biashara hii na majina mengine ni mazito ambayo yanahusisha watu wenye nafasi katika jamii.

Vita ya madawa ya kulenya ni kubwa na inayohitaji umakini mkubwa lakini haiwezi kushindwa.

Pia vita hii inahitaji uwezo mkubwa wa fedha ambazo zitawekezwa kwenye idara husika ya kitengo cha kupambana na madawa ya kulevya.

Tumesikia raisi wa Philippines bwana Rodrigo Duterte yeye aliamua kuwa watumiaji wa madawa ya kulevya wauwawe tangu ainge madarakani mwezi Juni mwaka jana na mpaka sasa watu 7600 wakiwemo watumiaji na wasambazaji wameuawa.

Pamoja na kuwepo kwa watu wanaopinga vita hii ya madawa ya kulevya inayofanywa na raisi Duterte, idadi kubwa ya wananchi wanaunga mkono juhudi yake hii kiasi cha kumpa nguvu ya kusema kwamba kampeni yake hii itaendelea ndani ya kipindi chote cha utawala wake ambao utaishia mwaka 2022.

Hapa nchini Tanzania mkuu wa mkoa wa Dar-es-Salaam ambao umeathirika na biashara hiyo nae ameamua kulivalia njuga suala hilo na anahitaji pongezi na msaada mkubwa.

Fedha zinazohitajika ni pamoja na zile za kujenga vituo maalum au kutenga kitengo maalum au "rehabilitation centre" ndani ya hospitali kadhaa ili kuwasaidia wale mateja wote ambao watakuwa tayari kushirikiana serikali katika mapambano dhidi ya biashara hii.

Lakini pamoja na mkuu wa mkoa bwana Paul Makonda kujitokeza kujaribu kutatua tatizo hili bado kunahitajika juhudi zaidi khasa za wizara ya mambo ya ndani na kitengo cha kupambana na madawa ya kulevya.

Na kama nilivyoainisha hapo juu teknolojia inayotumika kuwezesha usafirishaji wa madawa haya, kwa Tanzania tuna budi kuwekeza katika vifaa na teknolojia katika kukabiliana na suala hili khasa kuwa hatua moja mbele au "one step forward".

Kwa kuwa wasafrishaji wanatumia vifaa vya GPRS kufanikisha biashara yao basi polisi wa kitengo cha kudhibiti madawa wanapaswa kuwa na ujuzi wa teknolojia kama hizi, kupewa vitendea kazi kama "helicopter" maalum zenye uwezo wa kupiga picha nyakati zote za mchana na usiku (ingawa shughuli hizi hufanywa usiku) na ndege zijiendeshazo zenyewe au "Drones".

"Helicopter" na "drones" zinaweza kutumika kufanya doria katika pwani za Tanga, Dar-es-Salaa, Bagamoyo, Zanzibar na Mtwara.

Lakini vita hii itafanikiwa pia kwa waziri husika wa mambo ya ndani kuja na mikakati yake ambayo anapaswa kuisoma bungeni kwa kutumia muswada wa dharura ambao utakuwa umerekebisha baadhi ya vipengele mbalimbali vya makosa ya kukutwa na madawa ya kulevya.

Mpaka sasa ni mheshimiwa raisi John Magufuli na Paul Makonda peke yao ambao wametoa kauli kuhusu biashara hii ya madawa ya kulevya hadharani.

Waziri husika Mwigulu Nchemba upo wapi?
Klrlllrkllllll ml
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom