Kujiuzulu tu haitoshi!

Mzee wa Gumzo

Senior Member
Apr 21, 2008
197
5
Jamani Chenge kaachia ngazi,kafuata nyayo za Lowassa,Karamagi na Msabaha.Mpooo?

Mimi bado nashindwa kuelewa hao wanaompongeza chenge kama walivyompongeza Lowassa wana maana gani?kujiuzulu kwa kuwa fisadi siyo sifa hata kidogo jamani.

Kama kweli umeiba jiuzuli halafu rudisha ulichoiba ndipo kieleweke.Ninavyoelewa mimi kujiuzulu kwa maslahi ya taifa ina maana unawajibika juu ya matendo yako.Kwa mfano kama umepora mali ya umma unatakiwa kuwajibika kwa kurejesha.

Ikumbukwe kuwa Chenge alipohojiwa siku anarejea nchini alisema hawezi kujiuzulu kwa kuwa tuhuma hizi zililenga kumchafulia jina.Sasa ilikuwaje tena akajiuzulu?.Mimi mzee wa gumzo napata shaka hapa.

Naamini kuwa kauli aliyoitoa pale airport ilikuwa ya kwake lakini hatua ya kujiuzulu haikuwa matakwa ya chenge,ni shinikizo.Nani ajuaye labda ile kamati ya uongozi ya CCM ndiyo iliyomshinikiza afanye hivyo.

Kama ndivyo basi lazima tuamini kuwa kuna jambo nyuma ya pazia,si bure.Chenge anajua na CCM wanajua ukweli wote.
La msingi kwetu ni kujua hiyo fedha itarudi lini na ni kiasi gani.Hatutwezi kushangilia kujiuzulu kwa mtu eti akapumzike na mihela yetu,thubutu.
Lakini hata tukikataa nani anatusikia?
Tusubiri kuona nani mwingine atafuata,labda mzee wa gumzo?
 
Falsafa nzima ya Ufisadi, haitofautiani na addiction nyingine!

Kila unapozidi kutumia kilevi na kuzama ndivyo addict anavyojiona anaendelea vizuri na kupaa kwenda kwenye ushindi!

Hata kuwapigia kelele Kiasi gani hawa mafisadi, Hawataacha na kilevi chao mpaka wafikie kileleni! Ambapo ni anguko kubwa!!!!

Huwezi kuamini hawajioni tunavyowaona!

Wanaamini kuwa sisi ndio tuna matatizo kuwaona kwenye ukweli wao!

Hili ni jambo jema kwani itafika wakati wataji_expose to what they are...Watu MFILISI walioukana UTU wao! Na hili halisameheki.

Watang'ang'ania kwenye Madaraka kama msumari kwenye sumaku!

Na hapo lazima wataaibika tu huku wakidhani watazamaji ndio wanao aibika! This is good news..maana kuna limit ya ujinga kama huu..na hawataiona inapofikiwa!! Haoni na hawawezi kusoma nyakati.

Wangekuwa na bahati wanagefuata ushauri wanaopewa kila siku kabla mambo hayajawa mabaya zaidi!

Vinginevyo ni kweli wanastahili kuwako UKONGA,SEGEREA etc ...Because that is where they truely belong!!!
 
Jamani Chenge kaachia ngazi,kafuata nyayo za Lowassa,Karamagi na Msabaha.Mpooo?

Mimi bado nashindwa kuelewa hao wanaompongeza chenge kama walivyompongeza Lowassa wana maana gani?kujiuzulu kwa kuwa fisadi siyo sifa hata kidogo jamani.

Kama kweli umeiba jiuzuli halafu rudisha ulichoiba ndipo kieleweke.Ninavyoelewa mimi kujiuzulu kwa maslahi ya taifa ina maana unawajibika juu ya matendo yako.Kwa mfano kama umepora mali ya umma unatakiwa kuwajibika kwa kurejesha.

Ikumbukwe kuwa Chenge alipohojiwa siku anarejea nchini alisema hawezi kujiuzulu kwa kuwa tuhuma hizi zililenga kumchafulia jina.Sasa ilikuwaje tena akajiuzulu?.Mimi mzee wa gumzo napata shaka hapa.

Naamini kuwa kauli aliyoitoa pale airport ilikuwa ya kwake lakini hatua ya kujiuzulu haikuwa matakwa ya chenge,ni shinikizo.Nani ajuaye labda ile kamati ya uongozi ya CCM ndiyo iliyomshinikiza afanye hivyo.

Kama ndivyo basi lazima tuamini kuwa kuna jambo nyuma ya pazia,si bure.Chenge anajua na CCM wanajua ukweli wote.
La msingi kwetu ni kujua hiyo fedha itarudi lini na ni kiasi gani.Hatutwezi kushangilia kujiuzulu kwa mtu eti akapumzike na mihela yetu,thubutu.
Lakini hata tukikataa nani anatusikia?
Tusubiri kuona nani mwingine atafuata,labda mzee wa gumzo?

Mzee wa gumzo,

karibu sana JF. Jisikie huru na useme yote uliyonayo moyoni, katika hili la Chenge, ni miezi michache tu imepita alikuwa anatishia vyombo vya habari Tanzania. Nadhani mwenyewe ameona hiyo cordination iliyompa joto ya jiwe.

Tunakoelekea itakuwa ni kati ya wapenda amani na maendeleo ya watanzania VS wezi na mafisadi huko sisiemu. Natumaini mafisadi watashindwa kwa vile MUNGU yuko upande wetu.
 
inaposikitisha ni kuwa mwizi wa kuku akikutwa na tuhuma anaweza akapigwa, na kama kutakuwa na watu wenye mioyo kama yangu basi anaweza kufa papo hapo.
ila watu walioiba mahela ambayo mtoto wa darasa la saba hawezi kusema pesa hizo zina sifuri ngapi ye hujiuzuru wadhifa huo wenye malipo ya mshahara usiopungua milioni 1 na ushee na ndo unakuwa mwisho wa sakata linalomkabili....so watanzania ukweli uliopo ni kuwa "tusipouanika tututwanga mbichi"
 
Jamani tujitahidi kuakikisha tunapata wawakilishi wengi bungeni, maana hawa jamaa wana kila kitu mikononi mwao, sheria zinawalinda wao, mazingira yanawalinda wao (jaji aliyeteuliwa na Mkapa haiwezekani hakatoa hukumu sahihi kwa mkapa), Pesa wanayo na ndo wanaofanya mpaka rushwa inakuwa kubwa sana ndani ya nchi.
Tunahitaji kuondoa mfumo mzima kabisa wa utawala na kusimika mfumo mpya, lakini hakuna tunachoweza kufanya wao wakiwa madarakani.
 
Jamani tujitahidi kuakikisha tunapata wawakilishi wengi bungeni, maana hawa jamaa wana kila kitu mikononi mwao, sheria zinawalinda wao, mazingira yanawalinda wao (jaji aliyeteuliwa na Mkapa haiwezekani hakatoa hukumu sahihi kwa mkapa), Pesa wanayo na ndo wanaofanya mpaka rushwa inakuwa kubwa sana ndani ya nchi.
Tunahitaji kuondoa mfumo mzima kabisa wa utawala na kusimika mfumo mpya, lakini hakuna tunachoweza kufanya wao wakiwa madarakani.

Yaani unayosema ni kweli kabisa. Kama ingekuwa ni nchi nyingine zilizoendelea, Rais na wanachama wenzake wote wa sisiem wanatakiwa kujiuzulu kwenye madaraka kabisa! JK alipomteua Chenge si kila mtu alipigwa na butwaa hapa! Yaani JK kweli akili zake sijui ni ziro kabisa au vipi? Maana huyu Chenge jina lake lilishatajwa kwenye listi ya mafisadi, haya, sasa akapata nafasi ya kusahihisha makosa yake ya mwanzo, yeye ndo kwanza kamteua kuwa waziri...hizo ni akili kweli? rais mwenye busara angechukua nafasi hiyo kujibaraguza na kujiweka mbali na majina yanayonuka! Sasa amefanya nini? Chenge ana kiburi kama Mkapa, anadiriki kusema hovyo tu kututukana watanzania? What a nerve!...haki ya nani vile hawa mafisadi hawa....! Where is Tanzania going? Hawa mafisadi inabidi wapotee kabla ya kutufikisha kwenye hatua kama ya Zimbabwe...mkate tu shilingi milioni moja!
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom