Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,337
- 113,180
- Thread starter
- #81
Dr. Tulia amethibitisha huu mpango wa Mungu kwa Bunge la Tanzania. Spika Dr. Tulia, Mungu ambariki Sana.Wanabodi,
Siku zote, nabii huwa hakubaliki nyumbani, lakini sote tunakubali kuwa Mungu siku zote huwa anazungumza na watu wake, kupitia manabii, na nabii anaweza kuwa mtu yoyote hata usiyemtegemea. Japo mimi sii miongoni mwa manabii hawa wa Mungu, lakini kuna vitu huwa navisema, halafu vinakuja kutokea.
Sasa kwenye hili la Spika, kuna sauti niliisikia na nikasema humu!, angalia nilisema nini, na lini?
Voices from within: Nimesikia sauti, Dr. Tulia Ackson ndiye Spika ajaye! Sauti hiyo imenieleza Ndugai, japo atatamani aendelee lakini...
Wanabodi, Japo siku zote Nabii huwa hakubaliki nyumbani, hili nalijua na litabezwa, na nimeisha lisemea humu TZ Tulipo Sipo!. Nabii Hakubaliki Nyumbani, JF Tuna Manabii wa Kweli, Tuwatumie Walisaidie Taifa!. - JamiiForums Hii ni thread ya maono ya unabii, na sio utabiri na sio trends reading...www.jamiiforums.com
Bandiko hili pia ni bandiko la unabii
Je, wajua kuwa kitendo cha kujiuzulu kwa aliyekuwa Spika, Mhe. Job Yustino Ndugai ni mpango wa Mungu kwa Tanzania ili taifa letu Tanzania, tuachane na "Bora Spika" na badala yake tupate "Spika Bora". Swali ni Je CCM ituteulia "Spika Bora", au itaendelea na ule utaratibu wake wa ki CCM, kutupatia "Bora Spika" kama kawaida?. Unabii ni huu.
Kama ni kweli, kujiuzulu kwa Ndugai, ni mpango wa Mungu, ili taifa letu lipate "Spika Bora", CCM ina wajibu wa kutupatia "Spika Bora" wa ukweli, kati ya hao waliojitokeza. Ikitokea CCM kututeulia "Bora Spika" mwingine, maana yake, huku kutakuwa ni kwenda kinyume cha mpango wa Mungu, hivyo CCM isipotuteulia "Spika Bora" na badala yake, ikatuleulia "Bora Spika" mwingine, this time around "Karma Itahusu..".
Wasalaam.
Paskali.
Sasa Bunge ni Bunge Sheria Msumeno sio Bunge lile Bunge kujipendekeza, sasa ni Bunge sheria, Bunge heshima.
Big up sana Tulia.
P