Kujiuzulu/kuachishwa madaraka inatosha?

mtambo

Senior Member
Jan 14, 2008
112
0
Ndugu wanabodi,
Tokana na juhudi zetu za kumwaga ama kuanika uchafu unaofanywa na viongozi wetu katika serikali ya Tanzania, tumewezesha kulazimisha Baraza la mawaziri kuvunjwa.

Lakini kiini kikubwa cha kuvunjwa kwa baraza hilo ni Ufisadi.

Swali langu ni kwamba je adhabu ya kujiuzulu ama kuachishwa kazi inatosha?. Mapesa yetu yaliyochukuliwa yatarudishwa vipi, lini, na wapi?.

Kwanini wahusika na ufisadi wasichukuliwe hatua kama vile kuwekwa ndani na kufunguliwa mashitaka?.

Ni katika Tanzania hiyo hiyo mwizi wa kuku ama mwizi wa mifukoni akishikwa tunampiga na kumchoma moto, sasa hawa wezi wakubwa na wakutisha kwanini tunawaangalia tu?. Kwa misingi hii ndugu wana JF hamwoni kama wizi ama tabia ya ufisadi haitaisha Tanzania?, kwani kila atakayepata mwanya atafanya kweli akijua kwamba akijulikana ataachishwa kazi tu lakini maisha kwake yatakuwa poa tu. Je adhabu inatoshaaaaaaa???????
 
Ndugu wanabodi,
Tokana na juhudi zetu za kumwaga ama kuanika uchafu unaofanywa na viongozi wetu katika serikali ya Tanzania, tumewezesha kulazimisha Baraza la mawaziri kuvunjwa.

Lakini kiini kikubwa cha kuvunjwa kwa baraza hilo ni Ufisadi.

Swali langu ni kwamba je adhabu ya kujiuzulu ama kuachishwa kazi inatosha?. Mapesa yetu yaliyochukuliwa yatarudishwa vipi, lini, na wapi?.

Kwanini wahusika na ufisadi wasichukuliwe hatua kama vile kuwekwa ndani na kufunguliwa mashitaka?.

Ni katika Tanzania hiyo hiyo mwizi wa kuku ama mwizi wa mifukoni akishikwa tunampiga na kumchoma moto, sasa hawa wezi wakubwa na wakutisha kwanini tunawaangalia tu?. Kwa misingi hii ndugu wana JF hamwoni kama wizi ama tabia ya ufisadi haitaisha Tanzania?, kwani kila atakayepata mwanya atafanya kweli akijua kwamba akijulikana ataachishwa kazi tu lakini maisha kwake yatakuwa poa tu. Je adhabu inatoshaaaaaaa???????

Ndugu yangu hili ni swali kubwa sana lakini huu ni mwanzo tu kwani labda kuna mengi sana tusiyoyajua bado!
 
Unachosema ni point, kujiuzulu au kuachishwa kazi au hata kwenda nje ya nchi kwa matibabu sio suluhisho la mwisho, suluhisho kirudishwe kilichochukuliwa na adhabu ya kifungo ( baada ya kufilisiwa)ifuate mkondo wake, hapo ndio tutaona tumetendewa haki, vinginevyo tunalambana visogo hapa na ufisadi utaendelea kama kazi.
Kwanza hii issue ya Balali imefikia wapi?? mbona kimya kikuu?? nini kinaendelea? yuko wapi na hizo hela zinarudi vipi? that's a big concern here! hii issue ya Lowassa isimfunike Balali akaendelea kutanua tunahitaji suluhisho la KASHFA Zote NOW! Jk kazi imeanza umepumzika vya kutosha, wish U sucess.
 
Wana JF, naomba kuwaeleza kwamba mafisadi yote yanayotuumiza katika Tanzania yetu yamepewa likizo isiyokuwa na malipo.
Ninasema hivyo tokana na ukweli kwamba kama kweli tunataka kusimamisha kabisa tabia hii ya ufisadi katika Tanzania basi hawa mafisadi yangeambiwa ni lazima yarudishe pesa zetu, yapelekwe rumande na pia yange ambiwa hakuna kugombea/ kupewa uongozi tena katika Tanzania mpaka kufa kwao. Lakini kwa kuvunja baraza la mawaziri ama kuwaachisha kazi tu haitoshi kwani nina imani kabisa watapewa tena madaraka muda si mrefu.

Angalieni David Mataka aliyekuwa PPF jinsi alivyofanya madudu wakati ule, lakini kwa sasa kapewa tena ATCL ambako nako tena anafanya makanyanga ambayo ni zaidi ya madudu.

Wana JF kuvunjwa baraza la mawaziri ni funika kombe mwanaharamu apite na wala si lolote, wezi na mafisadi bado tunao mitaani wakitanua kwa mapesa yetu.

Ari mpya+NGUvu mpya+KAsi mpya = ANGUKA mpya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom