Kujisajili na bodi ya mikopo

Dec 29, 2013
28
9
Jamani naombeni mnijulishe Kwa Mwenye uelewa nime lipia bodi ya mikopo ya elimu ya ju sh.30000 Kwa mpesa, wamenitumia sms kwamba pesa imesha lipwa lakini Kila niki login inakataa nashindwa kujaza Form za mkopo kabisa system inasema' your credentials you entered do not match with that of the system" re -enter again.

Nimerudia sana bila mafanikio wananirudishia sms Hiyo mara zote .je tatizo ni lipi msaada jamani!
 
Hata mimi wananiandikia hivyo ila nadhani bado hela haijawafikia bodi kwenye system yao,ila tusubiri tena afu tuka log in tena,keep meseji ya M-Pesa
 
Hata mimi wananiandikia hivyo ila nadhani bado hela haijawafikia bodi kwenye system yao,ila tusubiri tena afu tuka log in tena,keep meseji ya M-Pesa
Je mlipofungua OLAS mmechagua link ya 'First time applicants au Registered users'?

Ukishalipa kw m-pesa unachagua first time applicant kuna form itakuja ya kujiregister, hapo utaweza kucreate password then una-submitt, halafu utalog in kwa kufuata maelekezo.
 
Je mlipofungua OLAS mmechagua link ya 'First time applicants au Registered users'?
Ukishalipa kw m-pesa unachagua first time applicant kuna form itakuja ya kujiregister, hapo utaweza kucreate password then una-submitt, halafu utalog in kwa kufuata maelekezo.

Je kwa ambao tuliomba mwaka jana tukakoswa kuomba mara nyingine unaingia link ip!
 
Je mlipofungua OLAS mmechagua link ya 'First time applicants au Registered users'?
Ukishalipa kw m-pesa unachagua first time applicant kuna form itakuja ya kujiregister, hapo utaweza kucreate password then una-submitt, halafu utalog in kwa kufuata maelekezo.

mkuu naomba maelekezo zaid mim cjui hta pakuanzia.....
 
Je mlipofungua OLAS mmechagua link ya 'First time applicants au Registered users'?
Ukishalipa kw m-pesa unachagua first time applicant kuna form itakuja ya kujiregister, hapo utaweza kucreate password then una-submitt, halafu utalog in kwa kufuata maelekezo.

mkuu hayo yote tumefanya lakini bado tatizo ni hilo hilo
 
hata ulieomba mwaka jana ukakosa..pia unatakiwa uanze km first time applicant..coz ya mwaka jana ulishakosa so inahesabika km hukuapply na haupo kwny system.....
 
wenye tatzo na hzo za m pesa msifute hzo sms za m pesa..au andikeni mahali zile transaction numberz
 
HESLB wajinga wakuuubwa! tangu saa 5am server ilikuwa off, na ilipokuja ni mangumashi matupu, mara your index number should be 1 digit, mara system crashed! nina pc binafsi na full bando najiuliza kwa mtu aliyetoka Budushi kijijini kufuata neti mjini gharama za internet cafe,chakula, malazi nk. Maajabu ya kupapatikia teknolojia tusizoziweza only in Tanzania!
icon13.png
 
Mie nilitoswa mwaka jana na nimetuma hela kwa m pessa ila kila nikifungua najibiwa kuwa invalid transaction I'd daah upuuzi huu
 
sasa kama ulitoswa mwaka jana mwaka huu sifa za kupata mkopo umezitoa wapi au uta jiyatimisha (yatima) mwaka huu samaani lakini mana mimi pia ni mhanga wa mwaka jana ila nafikiria hapa ntaliwa pesa then majibu yaje km mwaka jana not elegible...!!
 
sasa kama ulitoswa mwaka jana mwaka huu sifa za kupata mkopo umezitoa wapi au uta jiyatimisha (yatima) mwaka huu samaani lakini mana mimi pia ni mhanga wa mwaka jana ila nafikiria hapa ntaliwa pesa then majibu yaje km mwaka jana not elegible...!!

Try and error mkuu
 
Hawa Bodi ya Mikopo kama wanasoma huku tafadhali rekebisheni system yenu, inasumbua sana, na number ya simu mliyoweka haipatikani.

Aactually mmeweka number moja tuu ambayo ni +255 22 550 7910, hiyo number inapigwa na Tanzania nzima haipatikani kabisa, tukija ofisini kwenu, mlinzi anakwambia tumeambiwa tuwaambie mjaribu kupiga mara nyingi mpaka ipatikane, (kumbuka siku zinaisha maana deadline yenu ni tarehe 30)

Ukikutana na mlinzi kashiba vizuri na ana raha siku hiyo anakuruhusu uende reception, kimbembe ndio kinaanzia hapo reception sasa. Pale reception wanajibu majibu ya hovyo sana, tena hata hakuangalii usoni, wakati anakujibu anasoma gazeti na hawana msaada kabisa na watu zaidi ya wao kusoma gazeti, unauliza kitu kama mbona nimelipia lakini kila nikitaka kuingia kujaza form inakataaa? husaidiwi unajibiwa utumbo na mtu anaendelea kusoma gazeti.

Kuna kaka pale na dada wa kiarabu, ni shidaaa, afadhali huyo kaka anakujibu angalau vizuri japo hawana msaada, huyo dada wa kiarabu anajibu utumbo mmoja tuu anakuwa hana habari tena na wewe na akiona unamuuliza sana hakujibu chochote anaendelea kusoma gazeti. Hii ni mbaya sana. Watu wengi wanalalamika, maana watu wametoka mbali wanapoteza nauli zao kuja mpaka kwenu halafu mnashindwa kuwasaidia.

Eti majibu yenu ni nyie hamna uwezo wa kuwasaidia zaidi ya kuendelea kupiga simu, sasa apige vipi simu wakati simu yenyewe haipatikani na hata ikipatikana haipokelewi. Kwa kweli mnatunyanyasa sana wanafunzi!

Basi ingekuwa afadhali mchukue hayo malalamishi myapeleke kwa wausika wakati mwanafunzi anasubiri jibu, hamfanyi hivyo nyie mnajibu ndio tulivyoambiwa tuwajibu hivyo, na hamruhusiwi kuonana na wafanyakazi face to face, ni kitu gani hichi jamani?? Kama mnasoma hapa tunaomba mjirekebishe please!!:A S cry:
 
wana JF nina tatizo la ulipaji wa m-pesa kwenye bodi ya mkopo plz naomben msaada wenu
jinsi ya kulipia ?
 
Me jamani imenizingua njian database error toka Jana SAA 8 na nishajisajili nashidwa print
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom