Kujenga nyumba...

Papa Mopao

JF-Expert Member
Oct 7, 2009
4,105
2,491
Mshahara kwa mwezi ni laki tatu, nia ya kujenga nyumba ipo moyoni kabisa, sasa kwa mtu kama huyu afanyeje ili ndoto yake ya kujenga nyumba itimie?
 
ndg ushauri wangu achana na hayo mawazo kwa sasa kipato chako ni kdg sana kuza kwanza kipato chako ndio ufikirie ujenzi
 
Mshahara kwa mwezi ni laki tatu, nia ya kujenga nyumba ipo moyoni kabisa, sasa kwa mtu kama huyu afanyeje ili ndoto yake ya kujenga nyumba itimie?
Jipe muda ndoto yako utaitimiza. Ushauri wangu, anzisha mradi wowote ili hiyo pesa izunguke kwanza.
 
If u succeed bridging the gap between expectations and reality, u'll b in a better position.
U obviously have big dreams (u name suggests) but not much in the cup..
Kama umeshapata plot, sehem ya kichanga, save money for a whille ifike 1m, nunua cement, kodisha mashine lipa mafundi ufyatue matofali.. And move on from there.

But still be real and think right.
 
Mshahara kwa mwezi ni laki tatu, nia ya kujenga nyumba ipo moyoni kabisa, sasa kwa mtu kama huyu afanyeje ili ndoto yake ya kujenga nyumba itimie?

ushauri wa bure, sio kila tunachokipenda ni lazma tukifanye kwa wakati huo ila mazingira yanaamua. Kuwa na subira ila bana matumizi na anza kubuni mradi wa kukuongezea kipato. Ukiwa na uhakika wa kupata elf 15 kwa siku nje ya mshahara wako unaweza jenga
 
unaweza anza kwa kujenga nyumba ya miti au udongo baadae ukipata hela ujenge ya cement.
 
wasikukatishe tamaa unaweza kuwa unalipwa laki mbili ukajenga nyumba na yule anayelipwa milioni mbili akashindwa kujenga. cha msingi jitambue kipato chake ni kiasi gani na utambue kwa kipato hicho unaweza kujenga nyumba ya aina gani na maeneo gani. Njia rahisi kwa wenye kipato kidogo ni kujenga kwa awamu kwa mshahara wako kama hauna kiwanja ukiamua ndani ya mwaka mmoja unapata kiwanja, sio masaki wala mbezi beach ila utapata (lakini kama hauna matumizi makubwa katika mshahara wako) ukishapata kiwanja kuwa na ramani ya nyumba unayotaka kujenga alafu inua vyumba kama viwili na ukishahamia unajenga taratibu kadiri unavyoweza. ndani ya miaka miwili unaweza ukawa unaishi kwako tena pakiwa bora kuliko unapopanga ikiwa utakiwa makini kuchagua fundi na kumsimamia. ukisubiri kuinua kipato inawezekana usijenge kabisa na kujenga ni njia moja wapo ya kuinua kipato kwa kuepuka kodi ya nyumba
 
wasikukatishe tamaa unaweza kuwa unalipwa laki mbili ukajenga nyumba na yule anayelipwa milioni mbili akashindwa kujenga. cha msingi jitambue kipato chake ni kiasi gani na utambue kwa kipato hicho unaweza kujenga nyumba ya aina gani na maeneo gani. Njia rahisi kwa wenye kipato kidogo ni kujenga kwa awamu kwa mshahara wako kama hauna kiwanja ukiamua ndani ya mwaka mmoja unapata kiwanja, sio masaki wala mbezi beach ila utapata (lakini kama hauna matumizi makubwa katika mshahara wako) ukishapata kiwanja kuwa na ramani ya nyumba unayotaka kujenga alafu inua vyumba kama viwili na ukishahamia unajenga taratibu kadiri unavyoweza. ndani ya miaka miwili unaweza ukawa unaishi kwako tena pakiwa bora kuliko unapopanga ikiwa utakiwa makini kuchagua fundi na kumsimamia. ukisubiri kuinua kipato inawezekana usijenge kabisa na kujenga ni njia moja wapo ya kuinua kipato kwa kuepuka kodi ya nyumba

Nashukuru sana kwa ushauri, kiwanja ninacho...
 
If u succeed bridging the gap between expectations and reality, u'll b in a better position.
U obviously have big dreams (u name suggests) but not much in the cup..
Kama umeshapata plot, sehem ya kichanga, save money for a whille ifike 1m, nunua cement, kodisha mashine lipa mafundi ufyatue matofali.. And move on from there.

But still be real and think right.

Nashukuru sana kwa ushauri mkuu!
 
ushauri wa bure, sio kila tunachokipenda ni lazma tukifanye kwa wakati huo ila mazingira yanaamua. Kuwa na subira ila bana matumizi na anza kubuni mradi wa kukuongezea kipato. Ukiwa na uhakika wa kupata elf 15 kwa siku nje ya mshahara wako unaweza jenga

Nashukuru sana mkuu, huo wa mradi nimeupenda
 
Ungesema pia mji unaotaka kujenga, huku kwetu songea mwenye kipato cha laki tatu anajenga vizuri, mbna walimu wa shule za msingi wanajenga mapema tunawaona, huku kwetu kujenga ni bati na boliti za kuezekea ukipata hvyo tu umeshajenga na havizidi mil 3, viwanja hata laki 7 unapata, kuna jamaa alianza kujenga akiwa na mil 2 tu na sasa nyumba imesimama. Lakini kama ni dar itakuchukua muda sana kutokana na gharama za ujenz huo ingawa material baadh ni bei rahisi, lakin unakuta bei ya kiwanja tu mil 7 pesa ambyo huku kwetu unajenga nyumb na unahamia.
 
Back
Top Bottom