Kuitwa mahakamani kupitia gazeti huzuia dhamana?

JMF

JF-Expert Member
Jun 29, 2013
1,735
2,686
Salaam kwenu wana JF na hasa jukwaa hili la sheria,

Naombeni msaada wa tafsiri ya kuitwa mahakamani kupitia gazeti. Je, Kama kesi ina dhamana (madai), siku hiyo akifika na wadhamini wake wakiwa wamejiandaa mahakama inawezakuzuia dhamana?

Ipo hivi, kuna ndugu yangu ameitwa mahakamani kwa njia ya gazeti kutokana na pesa anazodaiwa na mteja wake. Kutokana na umbali wa mkoa kesi ilipofunguliwa na alipo mtuhumiwa, pia kutokana na jeuri yake ya kutokusafiri kwenda kuripoti mahakamani wakati alipojulishwa kwa njia ya simu na kumkwepa kwepa mdai wake(mdai hajui anapoishi mdaiwa) mahakama imetoa tangazo gazetini kuwa afike siku ya kesi na asipofika itasikilizwa upande mmoja na kutolewa maamuzi.

Je, Mtuhumiwa mtuhumiwa akifika mahakamani anaweza kutiwa nguvuni? Bush lawyers mtaani wanasemaga kuwa ukiitwa kwa gazeti huwa wanazuia dhamana. Je, hii ni kweli au ni stori zao tuu?
Msaaa tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom