Songambele
JF-Expert Member
- Nov 20, 2007
- 4,695
- 2,553
Ndugu wana JF, kwa heshima kubwa kabisa tunafungua mjadala wa kutafuta fedha za kujenga reli standard gauge kwa sekta binafsi na wananchi. Milango imefunguliwa kwa mujibu wa Waziri Mpango ni Kipande cha Reli kuelekea Mpanda na sehemu ilielekezwa na Mh. Raisi, mie siamini kama ile simu ilikuwa kejeli kwa waheshimiwa waliotoa michango yao lakini nimeona fursa na inawezekana kabisa jambo hili likatimia na faida za haraka ni kuwa na Reli; pili kuwajumuhisha wananzengo kwa wao kutoboka moja kwa moja; tatu watapata faida pia kutokana na uwekezaji huo; na masoko yetu ya mitaji kuanza kuchangamkia biashara.
Hapa nazungumzia Tanzania Railway Tax Free bonds kiasi cha kutosha kupeleka reli sio Makutupora kama alivyowahi kupendekeza ZZK bali kuifikisha Kigoma kabisa na kuhitimisha mijadala yote. Hii inaweza kufanyika kwa kuweka bracket za wanunuzi wa bonds 60% those in higher tax bracket na (diaspora na wananzengo) wakamaliza hiyo 40% kukusanya kiasi chote kinacho hitajika tukafunga mijadala.
Shime ndugu wananchi wale wanaoenda kununua viwanja, hisa, kubet, na kucheza bahati nasibu waelekeze pesa zao katika biashara hii ambayo italipa zaidi na ya uhakika kwa watu wote muda wa bonds ukiwa miaka 15 kila mtu atatusua na nchi itakuza biashara zake na nchi jirani haraka zaidi ya ilivyokusudiwa na uchumi kwenda mbio sana.
Wito wangu kwa Mh. Spika asaidie kuunda kamati ya kumvaa raisi na kuikimbilia hii fursa aliyotoa Mh. Raisi kama ilivyokuwa kwa makinikia atupe sie wananchi haraka iwezekananavyo akusanyiwe hizo pesa amalize kazi: Bashe, Nape, Zitto na Sekta Binafsi (TPSF and etal) wawemo katika kamati Ethiopia, India wao wanatumia hizi fursa tuachane na hizi focus za cherehani 4 kiwanda vinapoteza muda wa watu. Watu wafanye serious deep diving kutatua matatizo ya wananchi. kwakuwa bunge linakaaga kama kamati ya chama wanaweza anzisha session ya kukaa nje ya vikao vyao wakajadili jambo hili, wakivua tai, makoti, magwanda na vyama vyao wakiacha nje lazima tutakwenda wakati mwingine tunachoka na business as ussual kila mwenye wazo apewe nafasi aongee off records imani yetu wapo ambao wako vizuri, weledi na wazalendo ebu tuachane na red tapes wakati mwingine tuwe wananzengo.
Watu wamosoko ya mitaji wakihusishwa watasaidia kuweka viwango vya pesa zinazohitajika na size ya chini mpaka ya juu ya uwekezaji katika bonds. Kama watu wana bett na kugamble token tukizielekeza huku tutatusua hata lile la ukanda litaisha lenyewe kumbukeni tuko 50M plus tukishawishi 20% tu wakitoa sh. 500 kwa mwezi tutafika mbaali sana, tuivunje 7 trilion tuigombanie kipandekipande. Tukianzisha Tanzania Railway Financing Corporation na ikasajiliwa katika masoko ya hisa, tutashawishi hata haya mashirika ya hifadhi kuwekeza mitaji huko na by the way hii kitu itaishi miaka dahal. Badala ya kung'ang'ania haya mambo ya TTCL na kushindania vitu walivyoanzisha wengine pamoja na kutumia muda mwingi kudhibiti hapa itakuwa hatua ya kwanza kutengeneza donor country manake mtonyo ukiwa mkubwa tutakopesha wengine kwenda kujenga reli kama ilivyo ndoto ya mkuu.
Hii kitu naileta kwenu kwa brainstorming ili tupunguze stress za kutaka kufanya mambo makubwa kwa pesa za kodi, tutaacha kukamata mifugo ya wafugaji maskini na kuwadhulumu, kuvizia madereva na kunyatia wafanyabiashara wadogo kulipa kodi zisizoendana na biashara zao. Tujenge taasisi zetu kwa mawazo yetu wenyewe zitengeneze pesa halali.
Hapa nazungumzia Tanzania Railway Tax Free bonds kiasi cha kutosha kupeleka reli sio Makutupora kama alivyowahi kupendekeza ZZK bali kuifikisha Kigoma kabisa na kuhitimisha mijadala yote. Hii inaweza kufanyika kwa kuweka bracket za wanunuzi wa bonds 60% those in higher tax bracket na (diaspora na wananzengo) wakamaliza hiyo 40% kukusanya kiasi chote kinacho hitajika tukafunga mijadala.
Shime ndugu wananchi wale wanaoenda kununua viwanja, hisa, kubet, na kucheza bahati nasibu waelekeze pesa zao katika biashara hii ambayo italipa zaidi na ya uhakika kwa watu wote muda wa bonds ukiwa miaka 15 kila mtu atatusua na nchi itakuza biashara zake na nchi jirani haraka zaidi ya ilivyokusudiwa na uchumi kwenda mbio sana.
Wito wangu kwa Mh. Spika asaidie kuunda kamati ya kumvaa raisi na kuikimbilia hii fursa aliyotoa Mh. Raisi kama ilivyokuwa kwa makinikia atupe sie wananchi haraka iwezekananavyo akusanyiwe hizo pesa amalize kazi: Bashe, Nape, Zitto na Sekta Binafsi (TPSF and etal) wawemo katika kamati Ethiopia, India wao wanatumia hizi fursa tuachane na hizi focus za cherehani 4 kiwanda vinapoteza muda wa watu. Watu wafanye serious deep diving kutatua matatizo ya wananchi. kwakuwa bunge linakaaga kama kamati ya chama wanaweza anzisha session ya kukaa nje ya vikao vyao wakajadili jambo hili, wakivua tai, makoti, magwanda na vyama vyao wakiacha nje lazima tutakwenda wakati mwingine tunachoka na business as ussual kila mwenye wazo apewe nafasi aongee off records imani yetu wapo ambao wako vizuri, weledi na wazalendo ebu tuachane na red tapes wakati mwingine tuwe wananzengo.
Watu wamosoko ya mitaji wakihusishwa watasaidia kuweka viwango vya pesa zinazohitajika na size ya chini mpaka ya juu ya uwekezaji katika bonds. Kama watu wana bett na kugamble token tukizielekeza huku tutatusua hata lile la ukanda litaisha lenyewe kumbukeni tuko 50M plus tukishawishi 20% tu wakitoa sh. 500 kwa mwezi tutafika mbaali sana, tuivunje 7 trilion tuigombanie kipandekipande. Tukianzisha Tanzania Railway Financing Corporation na ikasajiliwa katika masoko ya hisa, tutashawishi hata haya mashirika ya hifadhi kuwekeza mitaji huko na by the way hii kitu itaishi miaka dahal. Badala ya kung'ang'ania haya mambo ya TTCL na kushindania vitu walivyoanzisha wengine pamoja na kutumia muda mwingi kudhibiti hapa itakuwa hatua ya kwanza kutengeneza donor country manake mtonyo ukiwa mkubwa tutakopesha wengine kwenda kujenga reli kama ilivyo ndoto ya mkuu.
Hii kitu naileta kwenu kwa brainstorming ili tupunguze stress za kutaka kufanya mambo makubwa kwa pesa za kodi, tutaacha kukamata mifugo ya wafugaji maskini na kuwadhulumu, kuvizia madereva na kunyatia wafanyabiashara wadogo kulipa kodi zisizoendana na biashara zao. Tujenge taasisi zetu kwa mawazo yetu wenyewe zitengeneze pesa halali.