Kuishi na mke wa aina hii, uwe na moyo kama mwendawazimu!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,806
15,379
Kuna wanawake ambao wanaitwa wana kisirani na wanyonyaji. Wanawake wa aina hii ndani ya ndoa zao ni vituko vitupu, na mara nyingi kama wameolewa na wanaume waliojitambua ndoa zao huwa hazidumu.

Mara zote mke wa aina anataka kuona mumewe akimhangaikia kupita kiasi na bado asiridhike. Ni vigumu kutabiri mienendo ya tabia zao. Kama anahitaji kufanyiwa jambo na mumewe na anahisi mumewe haweze kumtimizia, anaweza kuamka akiwa na furaha tele, lakini ikifika jioni utamkuta amenuna tu. Na mumewe atakapomuuliza sababu ya kununa, anaweza mkujibu "hamna kitu" , anachotafuta hapo ni kubembelezwa ili apate mahali pa kunzia.
Kwa kuwa anajua kuwa mumewe anamjali, atasema shida yake. " Yaani hela unayoniachia ya matumizi hapa nyumbani haitoshi kabisa na ninapata tabu sana kupanga bajeti". Tayari ujumbe umefika, lakini kwa namna ambayo itamfanya mume dhamira zimshitaki. Mume kwa kushtakiwa na dhamira ataongeza fedha. Kama ni mke aliyejiajiri au kuajiriwa anaweza kusingizia kuwa siku hizi biashara hakuna kabisa na hapati mapato ya kutosha au mshahara anaolipwa hautoshi na anafanya kazi, ile basi tu.

Na kauli kama hizi ni za kutarajiwa sana, "Waume wengine wanawasaidia wake zao kama mshahara au mapato hayatoshi, mimi ndivyo ninavyojua".
Anachotaka ni kumfanya mumewe ahisi kwamba, yeye kama mume ameshindwa wajibu wake na kwamba, kuna wanaume bora zaidi huko nje ambao wanaweza kuwasaidia wake zao pale wanapokuwa na mshahara mdogo au mapato madogo katika biashara zao.
Wanawake wa aina hii huwa hawajiamini kabisa, na hutaka kuonekana ni wa maana, wana uwezo, wanajua na wanatambuliwa. Wanaweza kuwa na kisirani cha hasira za ziada, wambea sana, na wakati mwingine hupenda kujilinganisha sana.
Hawana subira kabisa, wakitaka jambo lao wanataka litimizwe wakati huo huo, ni wasingiziaji wazuri, wakanushaji wa waziwazi wa mambo waliyofanya au kusema.

Ni watu wenye kero mwanzo mwisho.
Pia wanakuwa na upendo wa bandia, pale wanapohitaji kitu kutoka kwa waume zao, watatenda yale ambayo hawayatendi. Atajifanya kumpokea mumewe akitoka kazini, kumuuliza angependa kula kitu gani, kumpangia au kumtafutia nguo za kuvaa asubuhi.
Siku zote hafanyi hivyo, bali hufanya yote hayo pale anapohitaji kitu kutoka kwa mumewe. Utakuta ni mtu wa mbinu na ujanjaujanja tu. Hasa kukiwa na wageni ndio ataonesha anampenda sana mumewe. Hata kama alikuwa hamvui soksi akitoka kazini , kukiwa na wageni atafanya hivyo. Ni wanafiki wa upendo kupindukia.

Itaendelea......................
 
mh! jamani hawa 'wake' wa siku hizi nao! ila walau mkeo anakuonyesha upendo na heshima mbele za wageni. kuna mtu (ke/me) akiona wageni,kama hajanuna basi vijembe ndo vinaanza. natamani tuanze kuwekeana camera tuji-big braza. nimeona desa kwa mwenzio kulee 'kwenye ile mliyosema KWA SHIDA NA KWA RAHA,hii ndo shida'. kwa hiyo furahia raha zake (maximise kukiwa na wageni, hakikisha ukarimu wako haupungui wageni kila saa). hizo shida zipotezee
 
mh! jamani hawa 'wake' wa siku hizi nao! ila walau mkeo anakuonyesha upendo na heshima mbele za wageni. kuna mtu (ke/me) akiona wageni,kama hajanuna basi vijembe ndo vinaanza. natamani tuanze kuwekeana camera tuji-big braza. nimeona desa kwa mwenzio kulee 'kwenye ile mliyosema KWA SHIDA NA KWA RAHA,hii ndo shida'. kwa hiyo furahia raha zake (maximise kukiwa na wageni, hakikisha ukarimu wako haupungui wageni kila saa). hizo shida zipotezee

king'asti.............hivi hawa wanaume wa hivi wanapatikana wapi? Maana duh wake zao mbona wana bahati ya mtende?!

Mtambuzi ingekuwa inawe3zekana mwanamke wa namna hiyo akapewa nafasi ya kuona mwanamke mwenzie anaishije kwenye ndoa yake, mbona angepiga magoti na kumshukuru MUNGU kwa kumpa mume wa aina hiyo?!. Sometimes wanawake tumekuwa na demands za kiajabu ajabu tu (sijui inatokana na nini yarabi) yatupasa kushukuru pale unapompata mwanaume anayekupenda kwa dhati ambaye pendo lake litampelekea ajue majukumu yake ya muhimu kwa mkewe na ndoa/familia yake.

Hadi najikuta nashawishika kuuliza nini hasa wajibu wa mume kwa mkewe?!
 
mh! jamani hawa 'wake' wa siku hizi nao! ila walau mkeo anakuonyesha upendo na heshima mbele za wageni. kuna mtu (ke/me) akiona wageni,kama hajanuna basi vijembe ndo vinaanza. natamani tuanze kuwekeana camera tuji-big braza. nimeona desa kwa mwenzio kulee 'kwenye ile mliyosema KWA SHIDA NA KWA RAHA,hii ndo shida'. kwa hiyo furahia raha zake (maximise kukiwa na wageni, hakikisha ukarimu wako haupungui wageni kila saa). hizo shida zipotezee

Laiti yule ndugu angepewa mke kama huyu aliyeelezewa hapa!
 
lol salaaale! yule mwana kwao sijui angerudi mbio kumchukua mkewe tena b4 swaping time is over! ndo tunarudi pale pale 'u dont know what u have till u loose it all!'
sasa kwanini huyu asingeenda kuungana na yule anayemlalamikia mkewe.. ? wazo tu. something like "wife swapping"...
<br />
<br />
 
Hahahaaaa inaonyesha yamekukuta eeh? Pole mshirikishe MUNGU sio mwanadamu! Wanadamu wataishia kukupeleka porini zaidi
 
Hivi bado kuna wanawake wanawavua waume zaO VIATU NA SOKSI? LOL

Wapo bana,..............kuna wanawake wanyenyekevu kwa waume zao we acha tu, hasa wakitaka kufanyiwa jambo, watawavua soksi watawanawisha miguu, nk..........
 
Wapo bana,..............kuna wanawake wanyenyekevu kwa waume zao we acha tu, hasa wakitaka kufanyiwa jambo, watawavua soksi watawanawisha miguu, nk..........


Hahahahhaha mtambuzi si unyenyekevu tu bana sometimes unajisikia tu umvue mwenzio kwa upendo. Tena kuvua kwenyewe si kwa kuinama bali mke anakaa chini kabisa ananyoosha miguu yake na miguu ya Mr anaiweka kwenye mapaja anavua soksi akimasaji taratibu huku akipiga 'umbeya' na mumewe kumjulia hali, siku yake imekwendaje na kumweleza lililojiri nyumbani mwake na hata jinsi gani alivyommiss au alivyojisikia vizuri alivyopokea simu yake mchana ule..................... hahahahahahah mi ctaki kwa nini lakini mnatukumbushia machungu enyi waja??
 
Wanawake tu? au hata sisi tuna matatizo? wala hatuchekani! si me wala fe wote ni wale wale tu!
 
Hahahahhaha mtambuzi si unyenyekevu tu bana sometimes unajisikia tu umvue mwenzio kwa upendo. Tena kuvua kwenyewe si kwa kuinama bali mke anakaa chini kabisa ananyoosha miguu yake na miguu ya Mr anaiweka kwenye mapaja anavua soksi akimasaji taratibu huku akipiga 'umbeya' na mumewe kumjulia hali, siku yake imekwendaje na kumweleza lililojiri nyumbani mwake na hata jinsi gani alivyommiss au alivyojisikia vizuri alivyopokea simu yake mchana ule.....................

Ni kweli hata mie huwa nafanyiwaga hayo yote.............. lakini sio kama anataka nimfanyie jambo, bali ni malezi.
Jamani wanaume wenzangu mkitaka kuoa muwe mnachunguza familia kwanza.................... Mtu anaweza kukuta familia kuanzia wazazi mpaka watoto wote wameshachezea talaka lakini unakuta na yeye anachumbia katika familia hiyo hiyo...............lakini sio wote waliotoka katika familia hizo wana matatizo, kuna wengine wanamudu kuheshimu ndoa zao.
 
Ni kweli hata mie huwa nafanyiwaga hayo yote.............. lakini sio kama anataka nimfanyie jambo, bali ni malezi.
Jamani wanaume wenzangu mkitaka kuoa muwe mnachunguza familia kwanza.................... Mtu anaweza kukuta familia kuanzia wazazi mpaka watoto wote wameshachezea talaka lakini unakuta na yeye anachumbia katika familia hiyo hiyo...............lakini sio wote waliotoka katika familia hizo wana matatizo, kuna wengine wanamudu kuheshimu ndoa zao.

Unajua Mtambuzi kuna aina ya malezi ambayo kusema ukweli mtu unajikuta unajiuliza maswali lukuki. Ninae rafiki yangu, pamoja na uzee tulionao sie, mama yake mzazi akisikia tu gari ya mumewe anarudi nyumbani hata kama anawapigisha stori utasikia 'Eh ngojeni nikampokee mwandani wangu mie' mama wa watu ananyanyuka anaenda getini anafungua (Mumewe ana cheo kikubwa tu jeshini; na ni wanajeshi wanaopaswa kufungua geti lakini nyumbani kwa huyu mama ni yeye labda kama hayupo'

haya hiyo ilikuwa ya nje tu getini nani anajua anamfanyia nini mumewe huko ndani??
 
Unajua Mtambuzi kuna aina ya malezi ambayo kusema ukweli mtu unajikuta unajiuliza maswali lukuki. Ninae rafiki yangu, pamoja na uzee tulionao sie, mama yake mzazi akisikia tu gari ya mumewe anarudi nyumbani hata kama anawapigisha stori utasikia 'Eh ngojeni nikampokee mwandani wangu mie' mama wa watu ananyanyuka anaenda getini anafungua (Mumewe ana cheo kikubwa tu jeshini; na ni wanajeshi wanaopaswa kufungua geti lakini nyumbani kwa huyu mama ni yeye labda kama hayupo'

haya hiyo ilikuwa ya nje tu getini nani anajua anamfanyia nini mumewe huko ndani??

Ni kweli kuna, ambao bado wanafuata mafundisho ya ndoa hasa kizazi cha wazazi wetu.......... tatizo ni kwamba kizazi hiki cha sasa ambacho hata mie naangukia humo, tunachanganywa na usasa (Utamaduni wa Kimagharibi). Wakati wenzetu wanatamani sana mila na desturi zetu katika masuala ya ndoa na mahusiano, sisi tunakimbilia za kwao ambazo kwa kweli zinasababisha mitafaruku mingi sana......... hebu angalieni kiwango cha talaka kwa mfano nchini Marekani........... ni kielelezo tosha kwamba ndoa zao zimepogoka mno.....
Nikipata muda nitajadili juu ya ndoa za siku hizi kutodumu.......... nimefanya utafiti, na nimepata sababu kadhaa ambazo nitaziweka hapa ili tuzijadili kwa pamoja...............
 
Hahahahhaha mtambuzi si unyenyekevu tu bana sometimes unajisikia tu umvue mwenzio kwa upendo. Tena kuvua kwenyewe si kwa kuinama bali mke anakaa chini kabisa ananyoosha miguu yake na miguu ya Mr anaiweka kwenye mapaja anavua soksi akimasaji taratibu huku akipiga 'umbeya' na mumewe kumjulia hali, siku yake imekwendaje na kumweleza lililojiri nyumbani mwake na hata jinsi gani alivyommiss au alivyojisikia vizuri alivyopokea simu yake mchana ule..................... hahahahahahah mi ctaki kwa nini lakini mnatukumbushia machungu enyi waja??

Nasikiaga eti small houses ndo wataalam wa kufanya hayo mambo kuliko mawife wenyewe sasa sijui ka ni kweli!! Lol!
 

Similar Discussions

4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom