NAMBA MOJA AJAYE NCHINI
JF-Expert Member
- Oct 29, 2019
- 8,204
- 16,610
Wanabodi habari za jioni! Tangu awamu zote za utawala nimeona serekali zote zikifeli vibaya sana katika kutimiza matarajio ya wananchi! Kwani wananchi wanataka nini? ngoja tuone :
1.KUSHIBA CHAKULA
Wananchi wanataka uhakika wa chakula kila mwaka. Wakulima ndio wadau wakuu katika uzalishaji wanahitaji kuwezeshwa katika kilimo. Nakumbuka mwaka 2005 hadi 2010 kwenye jimbo la Igunga likiwa chini ya Mbunge Rostam alitengeneza Bwawa kubwa la umwagiliaji ambalo hadi leo wananchi wanalitumia kwa kilimo cha umwagiliaji.
Kwanini serekali isingewekeza kwenye project za umwagiliaji nchi nzima?ili tupate uhakika wa kuzalisha chakula misimu miwili katika mwaka?na malighafi za viwanda zipatikane kwa wingi???Hapo tutatibu tatizo la chakula kwa nchi nzima!
2.ELIMU BORA TENA BURE
Elimu ya msingi hadi chuo Bure inawezekana!Gharama ya ada ya elimu ya juu ni kikwazo kwa wananchi!Kuliko kuwepo Bodi ya mikopo ya serikali kuwasaidia wananchi ni bora isiwepo kabisa!Kwanini? Kwasababu fedha zinazokopwa bora zitumike kuendesha na kugharamia vyuo!
Mwanafunzi asikopeshwe bali elimu ya chuo iwe bure na fedha zinazotumika kukopesha wanafunzi zigharamie mahitaji yao chuoni wakati wanasoma!!mabweni yajengwe waishi bure! Ada wasilipe, fedha za field wasipewe bali waandaliwe utaratibu wa kufanya field kwa gharama za serekali kwa kutumia fedha zile zile za mikopo ambazo wao hukopeshwa!!!Hapo Elimu itakuwa Bure na Migomo ya chuo itakoma nchini!
2.MATIBABU
Sheria mpya ya Bima ya afya itungwe! Kuwa ni lazima kila Mtanzania awe na Bima ya afya ambayo malipo yake yataingizwa kwenye kodi ya mapato TRA!!kila mtanzania analipa kodi ya mapato analipa na bima moja kwa moja!hivyo kila mtanzania apata bima ya kutibiwa wakati wowote na mahali popote!
Vitambulisho vya taifa NIDA viboreshwe kuwa na BIMA moja kwa moja kwa namba za utambulisho!!!Hakuna mtanzania atakayetozwa gharama za matibabu nchini Bima itakuwa Mwarobaini wa tatizo la matibabu!!!
Ninaamini kuwa maoni haya yakifanyiwa kazi yatapunguza asilimia kubwa ya changamoto za wananchi na kutimiza matarajio yao!
NAKARIBISHA MABORESHO KAMA YAPO!!!ASANTENI!!!
1.KUSHIBA CHAKULA
Wananchi wanataka uhakika wa chakula kila mwaka. Wakulima ndio wadau wakuu katika uzalishaji wanahitaji kuwezeshwa katika kilimo. Nakumbuka mwaka 2005 hadi 2010 kwenye jimbo la Igunga likiwa chini ya Mbunge Rostam alitengeneza Bwawa kubwa la umwagiliaji ambalo hadi leo wananchi wanalitumia kwa kilimo cha umwagiliaji.
Kwanini serekali isingewekeza kwenye project za umwagiliaji nchi nzima?ili tupate uhakika wa kuzalisha chakula misimu miwili katika mwaka?na malighafi za viwanda zipatikane kwa wingi???Hapo tutatibu tatizo la chakula kwa nchi nzima!
2.ELIMU BORA TENA BURE
Elimu ya msingi hadi chuo Bure inawezekana!Gharama ya ada ya elimu ya juu ni kikwazo kwa wananchi!Kuliko kuwepo Bodi ya mikopo ya serikali kuwasaidia wananchi ni bora isiwepo kabisa!Kwanini? Kwasababu fedha zinazokopwa bora zitumike kuendesha na kugharamia vyuo!
Mwanafunzi asikopeshwe bali elimu ya chuo iwe bure na fedha zinazotumika kukopesha wanafunzi zigharamie mahitaji yao chuoni wakati wanasoma!!mabweni yajengwe waishi bure! Ada wasilipe, fedha za field wasipewe bali waandaliwe utaratibu wa kufanya field kwa gharama za serekali kwa kutumia fedha zile zile za mikopo ambazo wao hukopeshwa!!!Hapo Elimu itakuwa Bure na Migomo ya chuo itakoma nchini!
2.MATIBABU
Sheria mpya ya Bima ya afya itungwe! Kuwa ni lazima kila Mtanzania awe na Bima ya afya ambayo malipo yake yataingizwa kwenye kodi ya mapato TRA!!kila mtanzania analipa kodi ya mapato analipa na bima moja kwa moja!hivyo kila mtanzania apata bima ya kutibiwa wakati wowote na mahali popote!
Vitambulisho vya taifa NIDA viboreshwe kuwa na BIMA moja kwa moja kwa namba za utambulisho!!!Hakuna mtanzania atakayetozwa gharama za matibabu nchini Bima itakuwa Mwarobaini wa tatizo la matibabu!!!
Ninaamini kuwa maoni haya yakifanyiwa kazi yatapunguza asilimia kubwa ya changamoto za wananchi na kutimiza matarajio yao!
NAKARIBISHA MABORESHO KAMA YAPO!!!ASANTENI!!!