Kuiongoza Tanzania ni rahisi sana. Zingatia mambo makuu matatu

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Oct 29, 2019
8,204
16,610
Wanabodi habari za jioni! Tangu awamu zote za utawala nimeona serekali zote zikifeli vibaya sana katika kutimiza matarajio ya wananchi! Kwani wananchi wanataka nini? ngoja tuone :

1.KUSHIBA CHAKULA
Wananchi wanataka uhakika wa chakula kila mwaka. Wakulima ndio wadau wakuu katika uzalishaji wanahitaji kuwezeshwa katika kilimo. Nakumbuka mwaka 2005 hadi 2010 kwenye jimbo la Igunga likiwa chini ya Mbunge Rostam alitengeneza Bwawa kubwa la umwagiliaji ambalo hadi leo wananchi wanalitumia kwa kilimo cha umwagiliaji.

Kwanini serekali isingewekeza kwenye project za umwagiliaji nchi nzima?ili tupate uhakika wa kuzalisha chakula misimu miwili katika mwaka?na malighafi za viwanda zipatikane kwa wingi???Hapo tutatibu tatizo la chakula kwa nchi nzima!

2.ELIMU BORA TENA BURE
Elimu ya msingi hadi chuo Bure inawezekana!Gharama ya ada ya elimu ya juu ni kikwazo kwa wananchi!Kuliko kuwepo Bodi ya mikopo ya serikali kuwasaidia wananchi ni bora isiwepo kabisa!Kwanini? Kwasababu fedha zinazokopwa bora zitumike kuendesha na kugharamia vyuo!

Mwanafunzi asikopeshwe bali elimu ya chuo iwe bure na fedha zinazotumika kukopesha wanafunzi zigharamie mahitaji yao chuoni wakati wanasoma!!mabweni yajengwe waishi bure! Ada wasilipe, fedha za field wasipewe bali waandaliwe utaratibu wa kufanya field kwa gharama za serekali kwa kutumia fedha zile zile za mikopo ambazo wao hukopeshwa!!!Hapo Elimu itakuwa Bure na Migomo ya chuo itakoma nchini!

2.MATIBABU
Sheria mpya ya Bima ya afya itungwe! Kuwa ni lazima kila Mtanzania awe na Bima ya afya ambayo malipo yake yataingizwa kwenye kodi ya mapato TRA!!kila mtanzania analipa kodi ya mapato analipa na bima moja kwa moja!hivyo kila mtanzania apata bima ya kutibiwa wakati wowote na mahali popote!

Vitambulisho vya taifa NIDA viboreshwe kuwa na BIMA moja kwa moja kwa namba za utambulisho!!!Hakuna mtanzania atakayetozwa gharama za matibabu nchini Bima itakuwa Mwarobaini wa tatizo la matibabu!!!
Ninaamini kuwa maoni haya yakifanyiwa kazi yatapunguza asilimia kubwa ya changamoto za wananchi na kutimiza matarajio yao!

NAKARIBISHA MABORESHO KAMA YAPO!!!ASANTENI!!!
 
Binadamu anapopata kitu fulani hitaji lake linabadilika na kuhitaji kitu cha juu yake, Ghadafi wa Libya alifanya zaidi ya hayo kwa wananchi wake lakini bado hawakuridhika na mwisho wa siku walimuua. hata hayo yakifanyika malalamiko na manun'guniko kwa watawala hayatakoma kamwe.
Angalau utakuwa msingi mzuri kwa mabadiliko yajayo!!!Na itachukua muda mrefu kwa watz kudai mabadiliko mengine na tutakuwa tumepiga hatua sana kuliko tulivyo sasa!!!!
 
Binadamu anapopata kitu fulani hitaji lake linabadilika na kuhitaji kitu cha juu yake, Ghadafi wa Libya alifanya zaidi ya hayo kwa wananchi wake lakini bado hawakuridhika na mwisho wa siku walimuua. hata hayo yakifanyika malalamiko na manun'guniko kwa watawala hayatakoma kamwe.
Ghadafi hakuuwawa na wananchi wa Libya bali na waasi kutoka bengazi waliochochewa na nchi za magaribi ambao nao walikuwa na maslai ya mafuta ya Libya (among other reasons).
 
Binadamu anapopata kitu fulani hitaji lake linabadilika na kuhitaji kitu cha juu yake, Ghadafi wa Libya alifanya zaidi ya hayo kwa wananchi wake lakini bado hawakuridhika na mwisho wa siku walimuua. hata hayo yakifanyika malalamiko na manun'guniko kwa watawala hayatakoma kamwe.
Ghaddafi aliuwawa na awamu ya Obama. Baadae akiwa ameshaondoka white house Obama alikiri kuhusika na mauaji ya Ghaddafi.

Wazungu wakati mwingine ni mbwa kuliko mbwa anayefugwa na binadamu.
 
Ghadafi hakuuwawa na wananchi wa Libya bali na waasi kutoka bengazi waliochochewa na nchi za magaribi ambao nao walikuwa na maslai ya mafuta ya Libya (among other reasons).
waasi mara nyingi huwa ni kikundi cha watu fulani...wananchi wake walio wengi wangekuwa wanamkubali na wakasimama pamoja naye waasi pamoja na kuwa walichochewa wasingefurukuta..lakini wananchi hawakuangalia waliyotendewa waliuchoka utawala wake na walihitaji atoke tu...walijua walistahili makubwa zaidi ya yale aliyowafanyia ndio maana walihadaika kwa urahisi....kwa wanayopitia sasa ikitokea Wakarudishiwa utawala ule halafu ajitokeze sijui muasi amechochewa aone atakachofanyiwa, itachukua muda sana kuja kufanya upuuzi walioufanya.
 
Ghaddafi aliuwawa na awamu ya Obama. Baadae akiwa ameshaondoka white house Obama alikiri kuhusika na mauaji ya Ghaddafi.

Wazungu wakati mwingine ni mbwa kuliko mbwa anayefugwa na binadamu.
sisi watu weusi tumejaliwa utajiri wa mali kwenye nchi zetu na sio akili ya ubinadamu...tumejaa ubinafsi na tamaa..wazungu sio kosa lao sababu kibinadamu kuna matabaka mawili ya mtawala na mtawaliwa kwa hiyo binadam ili aishi kwa raha na starehe ni lazima atawale...sio makosa ya wazungu ila wanatekeleza hulka ya binadamu...Tatizo ni sisi weusi mtu yupo tiyari aangamize kizazi chake ili yeye aishi kwa raha na ndipo wanapotuingia kiurahisi kutimiza haja zao.
 
sisi watu weusi tumejaliwa utajiri wa mali kwenye nchi zetu na sio akili ya ubinadamu...tumejaa ubinafsi na tamaa..wazungu sio kosa lao sababu kibinadamu kuna matabaka mawili ya mtawala na mtawaliwa kwa hiyo binadam ili aishi kwa raha na starehe ni lazima atawale...sio makosa ya wazungu ila wanatekeleza hulka ya binadamu...Tatizo ni sisi weusi mtu yupo tiyari aangamize kizazi chake ili yeye aishi kwa raha na ndipo wanapotuingia kiurahisi kutimiza haja zao.
Kwa kiasi fulani ni kweli kabisa ngozi yetu yenyewe kwa yenyewe haipendani, lakini ukisoma historia ya DR Congo vizuri utamuelewa vyema mzungu na unyama wake.

Ukiisoma vizuri historia ya maisha ya mtoto wa waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Magreth Thatcher utamjua vizuri mzungu na unyama wake.
 
Wanabodi habari za jioni! Tangu awamu zote za utawala nimeona serekali zote zikifeli vibaya sana katika kutimiza matarajio ya wananchi! Kwani wananchi wanataka nini? ngoja tuone :

1.KUSHIBA CHAKULA
Wananchi wanataka uhakika wa chakula kila mwaka. Wakulima ndio wadau wakuu katika uzalishaji wanahitaji kuwezeshwa katika kilimo. Nakumbuka mwaka 2005 hadi 2010 kwenye jimbo la Igunga likiwa chini ya Mbunge Rostam alitengeneza Bwawa kubwa la umwagiliaji ambalo hadi leo wananchi wanalitumia kwa kilimo cha umwagiliaji.

Kwanini serekali isingewekeza kwenye project za umwagiliaji nchi nzima?ili tupate uhakika wa kuzalisha chakula misimu miwili katika mwaka?na malighafi za viwanda zipatikane kwa wingi???Hapo tutatibu tatizo la chakula kwa nchi nzima!

2.ELIMU BORA TENA BURE
Elimu ya msingi hadi chuo Bure inawezekana!Gharama ya ada ya elimu ya juu ni kikwazo kwa wananchi!Kuliko kuwepo Bodi ya mikopo ya serikali kuwasaidia wananchi ni bora isiwepo kabisa!Kwanini? Kwasababu fedha zinazokopwa bora zitumike kuendesha na kugharamia vyuo!

Mwanafunzi asikopeshwe bali elimu ya chuo iwe bure na fedha zinazotumika kukopesha wanafunzi zigharamie mahitaji yao chuoni wakati wanasoma!!mabweni yajengwe waishi bure! Ada wasilipe, fedha za field wasipewe bali waandaliwe utaratibu wa kufanya field kwa gharama za serekali kwa kutumia fedha zile zile za mikopo ambazo wao hukopeshwa!!!Hapo Elimu itakuwa Bure na Migomo ya chuo itakoma nchini!

2.MATIBABU
Sheria mpya ya Bima ya afya itungwe! Kuwa ni lazima kila Mtanzania awe na Bima ya afya ambayo malipo yake yataingizwa kwenye kodi ya mapato TRA!!kila mtanzania analipa kodi ya mapato analipa na bima moja kwa moja!hivyo kila mtanzania apata bima ya kutibiwa wakati wowote na mahali popote!

Vitambulisho vya taifa NIDA viboreshwe kuwa na BIMA moja kwa moja kwa namba za utambulisho!!!Hakuna mtanzania atakayetozwa gharama za matibabu nchini Bima itakuwa Mwarobaini wa tatizo la matibabu!!!
Ninaamini kuwa maoni haya yakifanyiwa kazi yatapunguza asilimia kubwa ya changamoto za wananchi na kutimiza matarajio yao!

NAKARIBISHA MABORESHO KAMA YAPO!!!ASANTENI!!!
Labda kukutawala wewe na familia yako usitudhalilishe watanzania

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kiasi fulani ni kweli kabisa ngozi yetu yenyewe kwa yenyewe haipendani, lakini ukisoma historia ya DR Congo vizuri utamuelewa vyema mzungu na unyama wake.

Ukiisoma vizuri historia ya maisha ya mtoto wa waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Magreth Thatcher utamjua vizuri mzungu na unyama wake.
mzungu ni mnyama na anachotaka ni kutawala..issue ilikuwa kwetu ku-unite na kutanguliza uzalendo asipenyeze kirahisi.
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom