Rancho Chand
Senior Member
- Nov 4, 2012
- 150
- 71
Wadau kutokana ugumu wa maisha nimeamua kununua kigari kidogo ili kupunguza ghalama za mafuta hapa mjini, ila napata taabu sana kupita sehemu zilizowekwa matuta, nilikuwa nimefikiria kwenda Gereji ili niinue juu kidogo.
Lakini nimeelezwa na Layman mwenzangu kwamba kuinua gari juu kuna madhara ya kiufundi kwa gari husika, naomba mnishauri kabla sijaenda kuinua gari juu kidogo. Je kuna madhara gani gari yangu itapata????
Yangu nimeinyanyua, na sioni kama kuna madhara yeyote hadi sasa ni kama miezi 7 sasa.Ukienda kwa wataalamu wa magari watakuelekeza ni kwa kiwango gani gari lako linyanyuliwe