Kuimarisha ushirikiano ni msingi wa kufufua uchumi wa dunia baada ya janga la COVID 19

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,008
1,030
VCG31N1231747957.jpg


Mkutano wa mwaka 2021 wa Shirika la fedha la Kimataifa IMF na Benki ya dunia unafanyika wiki hii (Oktoba 11 - Oktoba17) mjini Washington nchini Marekani. Kama kawaida mkutano huu unakutanisha maofisa wote waandamizi wa IMF na benki ya dunia, na magavana wa benki kuu, mawaziri wa fedha nk kutoka nchi mbalimbali duniani.

Mkutano wa mwaka huu unafanyika wakati dunia bado inaendelea kukabiliana na athari za janga la COVID 19. Ripoti kuhusu mwelekeo wa uchumi wa dunia, juhudi za kupambana na umaskini, maendeleo ya uchumi na suala la misaada na madeni, na mabadiliko ya tabia nchi ni baadhi ya mambo yanayatarajiwa kujadiliwa kwenye mkutano. Lakini kutokana na athari za janga la COVID-19 kwenye uchumi wa dunia, kufufua uchumi wa dunia kwa njia iliyo shirikishi, ni jambo linatarajiwa kujadiliwa zaidi kwenye mkutano huo.

Janga la COVID-19 limeonyesha mambo kadhaa kuhusu uchumi wa dunia, ambayo hapo awali hayakuwa wazi sana na hayakupewa msukumo mkubwa kwenye kuyatatua. Kwanza ni pengo kubwa kati ya nchi tajiri na nchi maskini, pengo hili limekuwa wazi zaidi kwenye mgao wa chanjo, ni nchi zenye nguvu kubwa ya kiuchumi ndio zimepata chanjo nyingi na hata kujilimbikizia chanjo, wakati nchi zilizo nyuma kiuchumi zimeshindwa kupata chanjo ya kutosha. Hali hii imeonyesha kuwa na madhara kwa uchumi wa dunia, kwani tayari nchi zilizotoa chanjo kwa kiwango kikubwa kwa watu wake, hali ya uchumi katika nchi hizo imeanza kutengemaa na kurudi katika hali ya kawaida, lakini hali ni tofauti kwa nchi zilizopata chanjo kidogo.

Jambo la pili ambalo limekuwa wazi zaidi ni kuwa changamoto za mabadiliko ya tabia nchi zimekuwa na athari mbaya kwa uchumi wa dunia. Mazingira ya asili yalitegemewa kuwa msaada mkubwa kwenye shughuli za uchumi wakati wa mazuio ya kupambana na janga la COVID 19. Lakini ukweli umeonyesha kuwa majanga ya asili ambayo yanazidi kuongezeka, ni kikwazo kwa shughuli za uchumi zinazotegemea mazingira ya asili. Kwa hiyo umuhimu wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, kunaonekana kuwa ni muhimu zaidi kuliko wakati wote.

Ni wazi kuwa changamoto hizi ni kubwa, na hakuna nchi yoyote duniani inayoweza kuzitatua peke yake. Hivi karibu China imekuwa ikisisitiza mara kwa mara kuhusu kutatua changamoto za dunia kwa ushirikiano. Chinese FM defines multilateralism as Biden admin claims ‘America is back’ - Global Times Mfano mzuri upo kwenye mchango mkubwa inaotoa China kwenye kukabiliana na janga la COVID-19. China imekuwa ikihimiza utoaji wenye usawa wa chanjo ya COVID-19 duniani, na imekuwa ikitoa msaada wa chanjo hiyo, na hata kushirikiana na nchi mbalimbali kufanya hivyo. Mchango inaotoa China kwenye mapambano haya, sio tu una manufaa kwa afya duniani, bali pia ni msingi wa kufufua uchumi duniani.

Lakini pia China imekuwa ikijitahidi kuhimiza shughuli za biashara kwa njia mbadala katika mazingira ya janga la COVID-19. Kupitia kuhimiza biashara kwa njia ya mtandao wa Internet, China sio tu inafanya soko lake liwe wazi wa nchi nyingine, bali pia inatoa fursa kwa wafanyabiashara katika maeneo mbalimbali duniani, waendelee kufanya biashara licha ya kuwepo kwa changamoto za watu kusafiri.

Ni wazi kuwa kuna changamoto nyingine nyingi zinazoikabili dunia kwa sasa, na njia pekee inayofaa kutatua changamoto hizi ni kuimarisha ushirikiano (cooperation) na kuchukua hatua kwa pamoja (multilateralism). Changamoto zote kubwa kama vile janga la COVID-19, mabadiliko ya tabia nchi na changamoto kwenye mfumo wa biashara wa kimataifa, haziwezi kutatuliwa kwa upande mmoja. Na kama nchi moja tu ikitatua changamoto hiyo ndani ya nchi yake, kuendelea kuwepo kwa changamoto hiyo katika nchi nyingine bado ni hatari kwa nchi zote.
 
Back
Top Bottom