Kuichagua tena CCM, Je ni kielelezo cha kufanya informed decision, au ni Ignorance?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,428
113,433
Wanabodi,
Salaam.

Kuanzia leo, hadi tarehe 24 October, kwa siku hizi 30+ zilizobakia kabla ya kufanyika uchaguzi, nitajitolea kutoa makala za uhamasishaji ili wana jf tujitokeze kwa wingi kwenda kupiga kura. Makala hizi zitakuwa ni makala elimishi, ili kuwasaidia Watanzania wenzetu ambao bado wamelala, waamke ili wakachague kwa kufanye informed decision, yaani wachague kwa sababu ya kuchagua, na sio kuchagua kwa mazoea tuu!, kuchagua kwa mazoea tuu mimi nimekuita ni ignorance!.

Declaration of Interest
Naomba ku declare interest kuwa japo mimi ni mwandishi wa habari, maadili ya uandishi wa habari, yanatuelekeza sisi waandishi wa habari, tusishiriki kwenye partisan politics, hivyo mimi pia nina chama changu moyoni mwangu, na nina upande ninao support lakini bado naweza kuwa objective, na impartial bila kuegemea chama changu au upande wangu.

Is CCM Fooling Us Around?
Kuna msemo usemao "You can fool some people for some time, but you can't fool all the people all the times!".
Ikitokea kuna watu ambao wote wanakuwa fooled all the times, then watu hawa watakuwa ni a bunch of fools and ignorants!. Jee sisi Watanzania wote ni a bunch of fools and ignorants?.

CCM has been fooling us all for all the times kwa ahadi na ahadi zisizotekelezeka, na siku zote bado tunaichagua tena na tena. Miaka mitano ikifika, huja na visingizio hivi na vile vya kwanini ahadi hizo hazikutekelezwa, na kila baada ya miaka 5, huja na ahadi mpya kibao, zenye matumaini mengine mapya. Kipindi cha uchaguzi kinafika bila ahadi za zamani kutimizwa, hatuambiwi sababu kwa nini hazikutimizwa, bali tunaletewa ahadi mpya, na tunaichagua CCM tena na tena!. Jee kujiuliza kama sisi Watanzania ni ignorants au tumelogwa ni kutukana?!.

Hii ni mada ni kufuatia mada yangu ya Jee Watanzania ni ignorants au tumelogwa? bandiko hili lilimgusa dada yangu Juliana Shonza , sijui kwa nini alishindwa kuchangia bandiko lile, ila na yeye akanzisha bandiko lake,Watanzania sio wajinga; tumekusikia, tumetafakari kujibu bandiko langu na hii ni sehemu tuu ya majibu yake

Nimesoma andiko la PASCO wa JF kuhusu kile anachodai ni UJINGA wa watanzania, kwa kuendelea kuichagua CCM ambayo kwa mawazo ya PASCO ni chama kibaya.
Naomba kumthibitishia kuwa MIMI na watanzania sio wajinga, tunatambua jema na ovu, tunatambua nani ni mbaya na nani ni mwema..yawezekana yeye ameshindwa kutambua, hivyo nitazungumzia juu yangu na Watanzania wenzangu ambao kwa Miaka zaidi ya 50 sasa tumeendelea kuiamini CCM.

CCM imeendelea kuwa CHAMA kinachojitathimini na kinachojiimarisha siku hadi siku, sipingi wala sisemi kuwa CCM haijawahi kukosea, haina makosa na haijaaribu katika utawala wake..hapana na nikisema hivyo nitakuwa mnafiki, lakini tunaiona CCM ikijivua gamba katika new style, ikikataa kuwakumbatia mafisadi na kwa mara ya nyingine tena ikipata mgombea BILA RUSHWA, BILA HILA na BILA MTANDAO...hivyo kama PASCO unaamini kuwa CCM ni ile ile, yenye watu wale wale na sera zile zile basi PASCO wewe sio PASCO yule ninayemjua ambae huwa anaandika baada ya kufikiria, it seems contrary to my experience., perhaps U have personally and intentionally decides to do wrong and u seemed to know full well of ur decision.


Ama kuhusu msisitizo wako kuwa tukijilinganisha na nchi zingine ambazo zilipata uhuru katika miaka hiyo takriban 50 iliyopita kuwa wengi wamepiga hatua katika maendeleo, lazima ufanye comparison ya workload yetu na wao katika miaka hiyo 50...tumefanya nini interm of African Liberation which is the true factor kwa ku-slow down kwetu katika kupata Maendeleo ya haraka..

Kama unadhani ELIMU yako iliyokupa kiburi cha kuona Watanzania wote ni mataahira ndio msingi wa Maendeleo ambayo Mwalimu and the rest walifikiria then U are wrong..U are as IGNORANT better than any of Us..Arrogance is ignorance with an attitude..


Naomba nianze kwa kukuonya, kuna tofauti kubwa kati ya ignorance na utaahira, mimi nimesema Watanzania tunaichagua CCM kwa ignorance, naomba uliombee msamaha hili la kuwatukana watu ni mataahira kabla 'karma' ya utaahira haijakushukia, haswa kwa kuzingatia wewe bado ni binti mdogo, mbichi ndio kwanza unajiandaa kuingia kwenye ujenzi wa familia!. Omba tuu hata kimoyo moyo Mungu akuepushie mbali tukano hilo la kutukana watu mataahira!.

Naomba niweke in points format, ili iwe rahisi kuchangia kwa kujibu hoja au kupangua hoja kwa hoja na sio hoja kwa viroja!.


  1. Tulipopata uhuru ile miaka ya 60, tulikuwa na maadui wakubwa watatu, ujinga, umasikini na maradhi!, tulikuwa na all the resources to make this country move forward, watu, ardhi, siasa safi, na uongozi bora, tena ilisemwa, fedha sii msingi bali ni matokeo!, tulikuwa na udongo wenye rutuba, vyanzo lukuki vya maji, mali asili, utalii, utajiri mkubwa wa madini, etc, etc, in short we had everything, na wenzetu tuliopata nao uhuru, had nothing compared!, leo wenzetu have everything and sisi not only we have nothing!, bali umasikini umeongezeka mara dufu!, tulikua tuna object poverty sasa tuna stinking poverty!, ni umasikini uliotopea, kila siku ni afadhli ya jana!. Ujinga umeongezaka maradufu!, wakati wa Nyerere, there was a time litaracy level yetu ilikua juu, hadi wazee walifundishwa elimu ya watu wazima na elimu ya kujua kusoma na kuandika katika elimu ya ngumbaru!, leo mwanafunzi anamaliza darasa la saba hajui kusoma wala kuandika!. Maradhi ndio usiseme!, lakini leo sio tuu bado tuna wale maadui watatu, bali sasa tumeaongeza na maadui wengine wawili zaidi ambao hawa ni CCM's own making!, rushwa na ufisadi!.
  2. Nakubalina na wewe Baba wa Taifa hili, Mwalimu Nyerere amelifanyia makubwa taifa hili, na pia ni kweli mchango wa Tanzania katika ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika na Vita vya Kagera, vimechangia kururudisha nyuma maendeleo yetu, but to what extence?!.
  3. Mwalimu Nyerere alifika mahali, akakubali makosa, akakiri kufanya kosa sii kosa, kosa ni kurudia kosa, hivyo kwangu tatizo sio Mwalimu bali hawa waliomfuatia sio tuu kwa kurudia makosa bali kuongeza na makosa mengine mapya ya kijinga kabisa!, ujinga huu ndio ignorance ninayoizungumza mimi, mjinga, akikupa sababu za kijinga na wewe ukaendelea kumchagua, wewe unaemchagua ndio mjinga kabisa!. Hivyo nimeuliza Jee sisi Watanzania wote ni wajinga ki hivyo?. Are we all that ignorants?!.
  4. Mimi sio miongoni mwa lile kundi wanaosema CCM, haijafanya kitu, kuna mengi tuu mazuri CCM imefanya, na nimeyasema humu,Miongoni Mwa Mazuri ya CCM, but it is not enough!, uzuri wangu, mazuri ya CCM nimeyakubali na kuyataja humu, ila pia mabaya ya CCM na madudu ya CCM nimeyataja!,Mapungufu ya CCM: A Constructive Criticisim!, madudu ni mengi zaidi kuliko mazuri, hivyo nimeuliza,does CCM deserve kupewa another chance?, au kupumzishwa ni halali?! ila tukiamua kuipumzisha, nikashauri na tuipumzishe kwa upendo na amani.
  5. CCM imefanya mismanagement kubwa ya resources za nchi hii for too long!, sasa nchi yetu imefikia stage tunona pride raisi wetu kupanda ndege kusafiri kwenda ulaya kutembeza bakuli!, wakati tuna utajiri mkubwa wa maliasili na rasimali za kutosha kutufanya kuweza kujitegemea!, kitendo cha Tanzania kuwa bado ni taifa omba omba!, its just unacceptable and it is a shame!.
  6. Rushwa ya petty corruption is an order of the day!, kiasi kwamba baadhi yetu ukikamatwa na kosa la traffic, kuliko kusubiria hiyo notification ya bila risiti, bora mmalizane hapo hapo na kusave time!. Hata kujiandikisha tuu kwenye daftari ya kudumu la wapiga kura, I had to do something!, nakiri sikuombwa chochote na yoyote, bali nilipofanya time management ya kuamka saa 10 alfajiri ili kuwahi foleni, na kushinda siku nzima kituoni, nika opt kuitumia ile dawa ya 'penye uzia!'. Mwanzo rushwa ilikua siri, sasa ni mambo hadharani, wazi wazi!, Trafick hawaendi tena kupokelea pembeni au uchochoroni kwa kujificha, bali wameihalalisha wazi wazi kwa kutembea na vitabu fake vya notification, unaandikiwa na kuambiwa risiti uipitie baadae!.
  7. The grand corruption ndio usiseme, sisi tulio sekta binafsi tunajua, ili ushinde tender unapaswa kufanya nini!. Manunuzi ya umma ni kwa kickback za kueleweka!, ile ya Rada imerudishwa kwa uadilifu tuu wa Waingereza tena kwa taarifa yako tuu, kama hujui, ule mgao wa Change ulikua ni vijisenti tuu, laiti Watanzania wangesikia wale wazee 'wanene' wa kule top walivuta ngapi, hata kusubiria tuu hadi mwaka wa uchaguzi ufike ndipo wafanye mabadiliko, watu wangeona mbali!, wangemarch streets moja kwa moja hadi kwenye ile nyumba pale, kwenda kuwafurusha na kuwatoa baru!. CCM waishukuru sana BAE kwa kuyahifadhi majina ya waliolipwa hizo kickbacks na badala yake kukubali kulipa faini ya non-disclosure ndio hicho kinachoitwa change ya Rada!.
  8. Ufisadi ni kila kona, mfano mdogo ni ununuzi wa ndege ya rais bei yake imeonekana wazi ni bilioni 18 tuu!, ajenti analeta bili ya bilioni 43 serikali inaonyeshwa hadi bei halisi ya kiwandani, lakini bado inaendelea tuu kulipa!, only the fools and the ignorants ndio wataamini there was no kickbacks hadi kule the highest office!. Ajenti wa ndege hiyo ndio huyo huyo ajenti wa rada, ndio huyo huyo ajenti wa zile helcopter mbovu, ndie ajenti wa magari ya jeshi mtumba na vifa vya kivita viwivyofanya kazi!, na siku za sherehe za Ikulu, ukiondoa magari ya viongozi wakuu wa kitaifa ambao magari yao ndio huruhusiwa kupaki ndani ya Ikulu, gari la ajenti huyu, Red Ferrarri, ndilo hupaki ndani ya Ikulu tena pale garden ili kila mtu alione na kumtambua yuko karibu na familia ya rais, hata magari ya mawaziri na mabalozi hupaki nje!, ni ignorant tuu pakee ndiye atakayeamini 'jamaa' hahusiki.
  9. Serikali ya CCM, haina vipaumbele muhimu bali inendeshwa kwa matukio!, tangu tumepata uhuru ujinga ulikua ni adui namba moja, tumefanya nini kuinua elimu yetu!, CCM imewekeza on ignorance na inaitumia hiyo ignorance kama mtaji wake wa ushindi, na ukiangalia maeneo yenye low literacy level, hizo ndizo ngome za CCM!, mkoa wenye the highest literacy level ni ya Kanda ya Kaskazini, angalia hali ya CCM!, kwa watu waelewa hawadanganyiki tena!, na ikitokea CCM ikashinda hata jimbo moja, then labda Upareni kwenye umasikini na Simanjiro kwenye ujinga!.
  10. Mzigo mkubwa unaotuongezea umasikini huu ni gharama kubwa za uendeshaji wa serikali, nchi yetu ni ndogo tuu tena masikini wa kutupwa, lakini yenye serikali kubwa for nothing!, kinchi kidogo tuu kama Tanzania kuwa na mawaziri 54!, huku linchi likubwa na tajiri kama Marekani wana mawaziri 6 tuu!, huu kama sio ujinga ni nini?!. Tukiwa na mfumo mzuri hata ma DC ni redundant, just a wastege of resources!, Tuna baadhi ya idara zinazojitegemea, hazina kichwa wala miguu mfano baada ya kuwa na Vizazi na Vifo halafu tunaanzisha NIDA kufanya kitu kile kile ambacho kingefanywa vizuri zaidi na Vizazi na Vifo!.
  11. Madini tumetoa bure!, na gesi pia tunatoa bure!. Gesi asili: Is it "day light robbery?!"- watanzania tunaibiwa Mchana Kweupe! .
  12. Handling ya issue ya Escrow, ni kielelezo cha ignorance ya hali ya juu!.Escrow: Jee Watanzania ni Ignorants? au Tumelogwa?!.
  13. Hakuna ubishi kuwa siku zote, CCM imekuwa ikishinda chaguzi mbalimbali ka mbinu tuu na mtaji wao mkubwa wa ushindi ni kuitumia ignorance ya "watu" ambao CCM imewekeza!.
  14. Hakuna ubishi kuwa CCM kama chama, kimechoka, dalili zote za chama kichovu kinachosubiri kifo, tayari, zimeisha jitokeza kwa CCM, kinachosubiriwa sasa its only a matter of time ni lini kitaangwa rasmi, hiyo October 25 is the day of the judgement!, yaani it is Judgment Day!. CCM Imechokwa, Mtazamo: CCM imechokwa mpaka basi!
  15. Hakuna ubishi kuwa wengi wa hao "watu", wamekuwa wakiichagua CCM sio kwa sababu wanaipenda sana!, (waipende kwa lipi?), la hasha!, "watu" wamekuwa wakiichagua CCM kwa mazoea tuu! kufuatia ignorance yao!.
  16. Hakuna ubishi, kuwa wengi wa hao "watu" waliokuwa wakiichagua CCM kwa ignorance ya mazoea tuu, sasa wameamka kutoka katika usingizi wameichoka, hivyo October 25, hawatachagua tena chama kwa mazoea, bali watachagua chama kwa "sababu"!.
  17. Tatizo kubwa la Watanzania au adui mkubwa wa Tanzania sio CCM, CCM is just a vehicle, haikujiweka hapo ilipo, imewekwa, kwa ignorance yetu, hivyo tatizo sio CCM iliyowekwa, bali tatizo ni sisi, wale walioiweka CCM hapo ilipo!. That simply means, tatizo ni sisi Watanzania tulioiweka CCM madarakani kwa ignorance yetu, and it plays games on us again and again na sisi tukiendelea kuiweka madarakani again and again and again na sitashangaa kama hata October 25, hawa ignorants ambao hawajabadilika kama ni wengi kuliko walioamka, then sitashangaa wakiirudisha tena CCM ikulu ya Magogoni!, huku kutakua ni uthibitisho wa ignorance!.
  18. Chaguzi nyingine zote, CCM imekuwa ikichaguliwa kwa walkover victory kwa ignorance tuu kwa sababu we had no choice to choose from, uchaguzi wa mwaka huu, tuna altenative, we have a choice kati ya kuichagua CCM au kuipiga chini!, watu tutaingia kwenye uchaguzi with choice na sio walk over kama mazoea, hivyo CCM ikichaguliwa tena, then hiyo ndio itakua choice yetu tumechagua tena kwa sababu na sio kwa mazoea ya ujinga (ignorance)!.

Namalizia kwa kukumbushia lile swali la msingi, baada ya kusoma haya, kweli bado kuna watu wataichagua CCM?, na iwapo wataichagua tena CCM, kuichagua huku CCM, jee ni kielelezo cha kufanyika kwa informed decision au ni uthibitisho wa muendelezo wa ignorance ya Watanzania kuendelea kujichagulia tuu kwa mazoea?!.

Tafakari kwa makini, fikia maamuzi ya busara, hakikisha Tarehe 25 October, unajitokeza kifua mbele, kwenda kuitumia haki yako ya kidemokrasia kuamua hatima ya nchi hii kwa kupiga kura.

Nawatakia Jumatatu Njema.


Paskali
 
Pasco shemeji yangu pole kwa kujibiwa kama ulivyojibiwa.

Uliyemjibu ni kati ya wale wanaofikiria kwa kuzingatia wapi anapata chakula chake cha kila siku.Binti huyu amejisahau kwamba wale waliomfunda akajakuonekana na CCM ndiyo kwake wamekuwa wakila matusi ya kila aina.

In short uliyemjibu amezaliwa baada ya miongo kadhaa kupita,hajui kama ilikuwa lazima kwenda JKT na ni lazima kuwa mwanachama wa CCM ama sivyo shule utaisikia barabarani au ajira utaisikia tu.

Hajui kama waliouza viwanda vyetu tukawa hatuna hata kichwa cha kufikiri ndiyo hao leo anawapigia debe.Hivyo ndugu yangu huyo wala si wa kumjibu,hajui na hataki kujua.

Leo ukiangalia gharama ya kuwalipia mawaziri kwenye mahoteli makubwa ni ya juu sana kuliko faida iliyopatikana kwenye kuuza nyumba za serikali,na aliyeziuza leo tunaaminishwa kwamba hakuna mzuri kama yeye!!!!!!!!!Huyu anayewajibu watanania majibu ya kifedhuli akiwa Waziri leo akiwa Rais atatuambia kama hatukubali tuhame nchi.

Ila kosa kubwa linalotokea leo ni elimu ndogo ya uraia pamoja na uwezo wa kufanya maamuzi yaliyo sahihi.

Kama Magufuli atachaguliwa basi tujue tuna miaka mingine mitano au kumi ya kudumaa kama Taifa.Tumeona kampeni za kikabila zikichukua nafasi na matusi lakini Tume yetu iko kimya kabisa,wamebariki labda kwa sababu wanaofanya hayo ni chama kilicho wateua.

Nina muonea huruma binti atakapojua ukweli na kuona hata aje MALAIKA kwa sababu ya CCM kutokujua tatizo liko wapi,wakidhani tatizo ni Lowassa na wao chini ya Magufuli wako safi,basi tusubiri tuone,Kuna watu watajutia kura zao humu ndani.Muda ni dawa tunausubiri kwa hamu.
 
Mkuu PASCO umeongelea swala la msingi sana ... crystal clear CCM iko kwaajili ya kutetea maslahi ya Wakubwa wa Dunia hii... Haiko kwaajili ya Wananchi wa Tanzania...Mnamo mwaka 1997 Hayati Baba wa Taifa aliligundua CCM imegeuka Agent wa Imperialism .. Alifadhaishwa na sana na hali hiyo, hata kifo chake kimeongelewa sana juu ya EHM kummaliza! ... jambo la Msingi la sisi watanzania kujiuliza ni kwanini Multnational Corporation ACCASIA, BG, SYMBION, URANIUM ONE et al ndo zenye hofu kuu ya kuondolewa kwa CCM? Kwanini wako Tayari kumgharamikia Slaa, Lipumba et al kwa niaba ya CCM ?
 
Kuna msemo usemao "You can fool some people for some time, but you can't fool all the people all the times!".
Ikitokea kuna watu ambao wote wanakuwa fooled all the times, then watu hawa watakuwa ni a bunch of fools and ignorants!. Jee sisi Watanzania ni a bunch of fools and ignorants?.

Voting Lowasa counts as being fooled again, he represents the fraction of CCM which is most virulent when it come to graft and corruption. We would rather give CCM 5 more years as we reorganize proper change.
 
Tunajua hofu yako iko wapi? MNCs zenye kukwapua rasilimali zetu burebure mwisho October 2015...
Voting Lowasa counts as being fulled again, he represents the fraction of CCM which is most virulent when it come to graft and corruption. We would rather give CCM 5 more years as we reorganize proper change.
 
Pasco

You can fool mostTanzanians all the time because most of them are too dumb to realize that... 54 years cyo mchezo....
 
Last edited by a moderator:
Ccm si chama kamilifu (kama vilivyo vyama vingine vyote ulimwenguni)....ila mtu yeyote mwenye akili timamu hawezi kumchagua lowassa...hana kigezo chochote cha yeye kuwa head of state...

Lowassa is good for those who invested a lot of money and energy in his campaign. It is for their personal benefit not because Lowassa stands for anything beneficial to our nation. Pasco is one of those prospective benefactors . Nothing personal just a fact! But for anyone who has no vested interest it is evident Lowassa is unfit!
 
Mnaodhani Pasco aka Paskali yupo kwa ajili ya mabadiliko mnajidanganya....Huyu mkuu anaitumua kalamu yake vizuri sana....Huyu ni Ulipo Tupo pure....mtu wake angepitishwa huko asingeandika yote haya.....viongozi wa cdm anaona wanafaa leo kwa sababu tu ya mkumpokea mtu wake...si mda mrefu sana alikuwa anawakejeli sana kama ni watu ingorants....aje sasa atuthibitishie u-ingorant wa viongozi wa cdm leo umeisha kwa kumpokea mtu wake?
 
Last edited by a moderator:
Kuichagua CCM iliyo ua viwanda, mashamba, vyama vya ushirika, kugawa Rasilimali za Watanzania, yenye UFISADI wa kila aina ni Ujuha category A ...
 
Kiongozi wa mabadiliko alikua ndani ya mfumo anaoupinga kwa miaka zaidi ya 30.

Huyo huyo, alikua sehemu ya maamuzi anayapinga leo kwa zaidi ya miaka 30,

Ameishi, kuyatenda na kuyatetea anayoyapinga leo kwa miaka zaidi ya 30,

Hakuna ushahidi wala rekodi ya vitendo wala maneno ya kupinga aliyoyaamini, kuyafanya na kuyatetea kabla ya kuanza kwa kampeni za urais,

Hivyo hatuwezi mweka mbali na hamu ya madaraka tu kwa mwamvuli wa mabadiliko..
 
Acheni kushambulia mtu kwa mawazo yake, ametoa mawazo yake yapokee au yakatae, ukiangalia PASCO yuko pande zote mbili CCM na UKAWA, anaangalia masirahi ya nchi yake badala ya kuangalia masirahi ya chama, amekuwa mfuasi mzuri sana wa CCM lakini pia amekuwa mfuasi mzuri wa Mabadiriko
 
Wameshaanza kujitambua sasa ccm itakuwa na wakati mgumu sana wapiga kura wao ambao ni wazee wameanza kujitambua kuwa wanadanganywa na chama chao. Hawa wazee ndio mtaji uliokuwa mkubwa wa ccm kushinda chaguzi zao nyingi. Safari hii nao wazee wanaikataa ccm sio kwa maneno tu hata kwa vitendo. Subirini 25 oktoba 2015 ccm watapata jibu lao sahihi













CC Pasco Juliana Shonza
 
Last edited by a moderator:
Pasco

I don't believe on mistakes, hivyo siamini kuwa makosa katika nukuu yako ni BAHATI MBAYA..binafsi najua ni muendelezo wa De Docta Ignorantia, on learned ignorance. Najinukuu ili kuweka kumbukumbu sasa:

Kwa namna yeyote ile utakayotafsir neno AKILI bado utalifungamanisha na uwezo wa kutambua baya na zuri. Wasomi wanaamini kuwa hakuna mtu anayependa ama kuchagua kufikwa na jambo baya..ni katika tabia za kawaida za binaadamu. Na wasomi wakubwa wakiwemo Socrate wanaamini kuwa kufanya jambo ovu ama baya daima mfanyaji uathirika, na kwa kuwa AKILI za kibinadamu zinakataa mtu kujidhuru ama kujiathiri, kwa mtazamo huo kufanya jambo ovu ni matokeo ya kutokuwa na akili, na neno moja la kukosa akili ni UJINGA..kwa lugha ya Kigeni ni IGNORANCE.

Nimesoma andiko la PASCO wa JF kuhusu kile anachodai ni UJINGA wa watanzania, kwa kuendelea kuichagua CCM ambayo kwa mawazo ya PASCO ni chama kibaya.

1. Naomba kumthibitishia kuwa MIMI na watanzania sio wajinga, tunatambua jema na ovu, tunatambua nani ni mbaya na nani ni mwema..yawezekana yeye ameshindwa kutambua, hivyo siwezi kuzungumzia ujinga wake ila nitazungumzia juu yangu na Watanzania wenzangu ambao kwa Miaka zaidi ya 50 sasa tumeendelea kuiamini CCM.

Tanzania is exceptional country with extra ordinary countrymen..TUNGEKUWA wajinga tungekubali nchi yetu KUTOTAWALIKA..nchi hii ni ya mfano katika nchi za Afrika, mfano kwa UONGOZI imara, mfano kwa AMANI na UTULIVU, mfano kwa UMOJA wa KITAIFA, mfano kwa kujitoa katika kusaidia nchi nyingine za Afrika kwa hali na mali, hakuna Nchi yeyote katika Afrika kusini mwa jangwa la sahara ambayo imepiga hatua na kufikia ilipofikia leo ikawa HAIJAPATA msaada wa TANZANIA,
kama ipo naomba niambiwe.

Hivyo mimi binafsi napingana kabisa na WAZO kuwa CCM haijafanya chochote katika ujenzi wa ustawi wa jamii ya Watanzania na Afrika kwa ujumla..Marais wa Tanzania kutoka BABA wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mpaka Jakaya Mrisho Kikwete wameendelea kuwa ICON sio tu kwa Tanzania bali kwa DUNIA nzima katika suala zima la Utawala na uongozi uliotukuka, hata leo tuzo mbalimbali za Kimataifa zimeendelea kuelekezwa Tanzania
kwa heshima ya utendaji wa kazi zao...ni UJINGA na MJINGA tu ambae anaweza kupaza sauti bila aibu kusema kuwa WATANZANIA ni wajinga...na inatia shaka zaidi pale inapotokea mtu huyo akiwa MTANZANIA.

Na kama ni kile ninachokiona ni MAHABA kwa Upinzani wa nchi hii, niseme tena mimi nimewahi kuwa Mpinzani wa CCM kwa muda mrefu, its no better kwenye upinzani kuliko hata kwa CCM..Hauwezi kulizungumza suala la UONGOZI BORA kwa upinzani..hauwezi kuzungumzia Suala la kukuza ELIMU kwa wapinzani, hauwezi kuliongelea suala la kukomesha Rushwa kwa Wapinzani wa nchi hii...
hauwezi kuwaamini kwa lolote wapinzani wa nchi hii..Ni watu wasiojitambua, wasiojielewa, wasio na misimamo, wanaoyumba na baya zaidi WASIOFIKIRI.

CCM imeendelea kuwa
CHAMA kinachojitathimini na kinachojiimarisha siku hadi siku, sipingi wala sisemi kuwa CCM haijawahi kukosea, haina makosa na haijaaribu katika utawala wake..hapana na nikisema hivyo nitakuwa mnafiki, lakini tunaiona CCM ikijivua gamba katika new style, ikikataa kuwakumbatia mafisadi na kwa mara ya nyingine tena ikipata mgombea BILA RUSHWA, BILA HILA na BILA MTANDAO...hivyo kama PASCO unaamini kuwa CCM ni ile ile, yenye watu wale wale na sera zile zile basi PASCO wewe sio PASCO yule ninayemjua ambae huwa anaandika baada ya kufikiria, it seems contrary to my experience., perhaps U have personally and intentionally decides to do wrong and u seemed to know full well of ur decision.

Najua unataka tuamini katika UPINZANI basi tusaidie watanzania sisi ambao wewe (mwerevu) unadhani tu wajinga kupindukia, sababu 3 tu za kuamini katika Upinzani..jaribu kutushawishi, kutuita wajinga pekee hakusaidii..tupe HOJA kuwa CCM imechoka na hivyo UPO UPINZANI MBADALA wa kutuvusha baada ya kuiweka CCM pembeni...Mind U nilikuwa MPINZANI, yawezekana kabisa najua hata yale USIYOYAJUA.

Ndio tarehe 25th October 2015, tutaichagua tena CCM, tena kwa kishindo KIKUU, lakini kamwe hatuchagui kwa UJINGA..,tunazo akili, tunajua BAYA na ZURI kwetu, na hivyo..TUMEKUSIKIA, TUMETAFAKARI na TUMESHAAMUA kuwa MAGUFULI ndio Rais wetu wa AWAMU ya TANO..

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI CCM.

 
Last edited by a moderator:
Nasikitika mnaopoteza Muda kujibishana nahuyo J..fyonza nimiongoni mwa wanaotumia utumbo kufikiri badala ya ubongo
 
Acheni kushambulia mtu kwa mawazo yake, ametoa mawazo yake yapokee au yakatae, ukiangalia PASCO yuko pande zote mbili CCM na UKAWA, anaangalia masirahi ya nchi yake badala ya kuangalia masirahi ya chama, amekuwa mfuasi mzuri sana wa CCM lakini pia amekuwa mfuasi mzuri wa Mabadiriko

Pasco anamfata mamvi tu si kingine, alikuwa ccm as long as mamvi alikuwa anasaka/anategemea kuteuliwa na ccm. Sasa mamvi kakatwa ccm yuko upinzani na yeye amemfuata huko na kusifia upinzani. Hakuna kitu hapo maslahi binafsi tu ndiyo yanayatangulizwa.
 
Pasco shemeji yangu pole kwa kujibiwa kama ulivyojibiwa.

Uliyemjibu ni kati ya wale wanaofikiria kwa kuzingatia wapi anapata chakula chake cha kila siku.Binti huyu amejisahau kwamba wale waliomfunda akajakuonekana na CCM ndiyo kwake wamekuwa wakila matusi ya kila aina.

In short uliyemjibu amezaliwa baada ya miongo kadhaa kupita,hajui kama ilikuwa lazima kwenda JKT na ni lazima kuwa mwanachama wa CCM ama sivyo shule utaisikia barabarani au ajira utaisikia tu.

Hajui kama waliouza viwanda vyetu tukawa hatuna hata kichwa cha kufikiri ndiyo hao leo anawapigia debe.Hivyo ndugu yangu huyo wala si wa kumjibu,hajui na hataki kujua.

Leo ukiangalia gharama ya kuwalipia mawaziri kwenye mahoteli makubwa ni ya juu sana kuliko faida iliyopatikana kwenye kuuza nyumba za serikali,na aliyeziuza leo tunaaminishwa kwamba hakuna mzuri kama yeye!!!!!!!!!Huyu anayewajibu watanania majibu ya kifedhuli akiwa Waziri leo akiwa Rais atatuambia kama hatukubali tuhame nchi.

Ila kosa kubwa linalotokea leo ni elimu ndogo ya uraia pamoja na uwezo wa kufanya maamuzi yaliyo sahihi.

Kama Magufuli atachaguliwa basi tujue tuna miaka mingine mitano au kumi ya kudumaa kama Taifa.Tumeona kampeni za kikabila zikichukua nafasi na matusi lakini Tume yetu iko kimya kabisa,wamebariki labda kwa sababu wanaofanya hayo ni chama kilicho wateua.

Nina muonea huruma binti atakapojua ukweli na kuona hata aje MALAIKA kwa sababu ya CCM kutokujua tatizo liko wapi,wakidhani tatizo ni Lowassa na wao chini ya Magufuli wako safi,basi tusubiri tuone,Kuna watu watajutia kura zao humu ndani.Muda ni dawa tunausubiri kwa hamu.
Hakuna malaika ndani ya sisiem; huyo mgombea wao ni msafi? kuna marumbesa ya stanbic ambayo arodha ya wachukuaji imefichwa tunajuaje sio mmoja wao? wa madawa ya kulevya orodha yao nayo imefichwa, je mgombea hayumo? tunajuaje? kwanini inafichwa? wahusika wa pembe za ndovu je, mbona list inafichwa? je hayumooo? tutajuaje? unatumika ujinga na umbumbumbu kulaghai watu kama sivyo hizo orodha ziwekwe hadharani.
 
Pasco, i disagree with you, that those who still support ccm are ignorant or outright ------. Up to this moment there no other credible and trustworthy alternative to ccm...not chadema or ukawa. I would therefore like to respond to your points as follows:


  1. Tulipopata uhuru ile miaka ya 60, tulikuwa na maadui wakubwa watatu, ujinga, umasikini na maradhi!, tulikuwa na all the resources to make this country move forward, watu, ardhi, siasa safi, na uongozi bora, tena ilisemwa, fedha sii msingi bali ni matokeo!, tulikuwa na udongo wenye rutuba, vyanzo lukuki vya maji, mali asili, utalii, utajiri mkubwa wa madini, etc, etc, in short we had everything, na wenzetu tuliopata nao uhuru, had nothing compared!, leo wenzetu have everything and sisi not only we have nothing!, bali umasikini umeongezeka mara dufu!, tulikua tuna object poverty sasa tuna stinking poverty!, ni umasikini uliotopea, kila siku ni afadhli ya jana!. Ujinga umeongezaka maradufu!, wakati wa Nyerere, there was a time litaracy level yetu ilikua juu, hadi wazee walifundishwa elimu ya watu wazima na elimu ya kujua kusoma na kuandika katika elimu ya ngumbaru!, leo mwanafunzi anamaliza darasa la saba hajui kusoma wala kuandika!. Maradhi ndio usiseme!, lakini leo sio tuu bado tuna wale maadui watatu, bali sasa tumeaongeza na maadui wengine wawili zaidi ambao hawa ni CCM's own making!, rushwa na ufisadi!.
    Your point and assertion above is mere fanatism and is not grounded in data. You are probably referring to the Asian tigers, but also compare with other Sub Saharan African countries which have similar CULTURAL AND SOCIAL background, are they better off? Having abudant resources is no ticket to be a very developed country, look at DRC, very rich but very insecure and very poor WHY? it is because they invested and rushed in exploiting the resources instead of in NATIONAL UNITY, and NATION BUILDING. We under Nyerere and CCM during the first 20 years of independence focused primarily on national unity, cohesion and peace which is a very important FOUNDATION for economic prosperity. And this is A MOMENTOUS achievement of Ccm such that now we can begin to focus on the economy. You say that Tanzanians are getting poorer, give me evidence/data of this!! According to data we have poverty in TZ is decreasing: 35% in 2005 and now 28%, even the recent household budget survey show that more Tanzanians today can afford and have built houses with cement floor and iron roofing. IT IS A PITY FOR LEARNED MEN LIKE PASCO TO JOIN THE EMOTIONAL POLITICAL BANDWAGON ALONGSIDE BODABODA drivers, machingas in throwing around wild unsubstantiated claims. Yes poverty is still there, but the fact is poverty is DECREASING in Tanzania, if you are contesting this, give us statistical evidence to the contrary


  1. Mwalimu Nyerere alifika mahali, akakubali makosa, akakiri kufanya kosa sii kosa, kosa ni kurudia kosa, hivyo kwangu tatizo sio Mwalimu bali hawa waliomfuatia sio tuu kwa kurudia makosa bali kuongeza na makosa mengine mapya ya kijinga kabisa!, ujinga huu ndio ignorance ninayoizungumza mimi, mjinga, akikupa sababu za kijinga na wewe ukaendelea kumchagua, wewe unaemchagua ndio mjinga kabisa!. Hivyo nimeuliza Jee sisi Watanzania wote ni wajinga ki hivyo?. Are we all that ignorants?!.

In his book "Tujisahihishe" Mwalimu admits the various failures of his/ccm's policies. To fail in policy is human and normal, what is important is the good intention behind the policies and the admission of the failure and adoption of corrective measures. All along the policy history of this country, the changes that have been made, e.g. from centralized state controlled economy to liberal economy (1980s), poverty reduction measures with priority sectors to MKUKUTA (2000s), etc etc reflect attempts to 'change and correct' and in each epoch there have been good results with challenges and failures in other aspects emerging; this is normal in any development process. With CCM now and Magufuli in particular, you can hear him admitting the failures and mistakes and promising to correct the situation e.g. revamping industries, being more strict in the pubic service etc etc. Even ukawa will come with some good an some other disastrous policies as well..i can guarantee you that.
CCM imefanya mismanagement kubwa ya resources za nchi hii for too long!, sasa nchi yetu imefikia stage tunona pride raisi wetu kupanda ndege kusafiri kwenda ulaya kutembeza bakuli!, wakati tuna utajiri mkubwa wa maliasili na rasimali za kutosha kutufanya kuweza kujitegemea!, kitendo cha Tanzania kuwa bado ni taifa omba omba!, its just unacceptable and it is a shame!.

Talk about aid dependence? Again give us the facts and figures don't just holler like an hungry street boy. In 2005 60% of our development budget depended on external grants, this has been declining until this budget 2015/2016 the dependence has gone down to below 10% and the goal is to get to zero for the national budget.

Hakuna ubishi kuwa wengi wa hao "watu", wamekuwa wakiichagua CCM sio kwa sababu wanaipenda sana!, (waipende kwa lipi?), la hasha!, "watu" wamekuwa wakiichagua CCM kwa mazoea tuu! kufuatia ignorance yao!.

Again what is the alternative to ccm? is that Ukawa? You must be kidding! Ukawa is a gang of opportunist, people without any firm organizational foundation and principles which can ensure that there are checks and balances fit enough to run the state. You talk about change? What kind of change can Lowasa and Sumaye bring? Remember, they have been part and parcel of Ccm throughout their working lives, and making decisions...!!! Stop joking please. I would rather have a stable ccm which is reforming itself from inside ( by Magufuli) than have the rickety, unpredictable, power hungry, family based Ukawa run this country. Look on how Chadema and NCCR and CUF are governed today: like personal properties, If you cannot run your own party properly IT IS INSANE TO GIVE YOU THE STATE.

THAT IS WHY FOR THOSE WHO ARE SENSIBLE AND LOVE THIS COUNTRY AND DO NOT HAVE HIDDEN PERSONAL AGENDA DO STILL CHOOSE CCM TO LEAD THIS COUNTRY. I LIKE THE OPPOSITION, BUT NOT THIS KIND OF "OPPOSITION" IN UKAWA AND LOWASA AND SUMAYE. Let the TRUE, CLEAN opposition grow and mature and Tanzanians will see SENSE in giving them this country to make MEANINGFUL and sustainable changes.
 
Back
Top Bottom