Kuibuka kwa Tundu Lissu ndani ya dhana ya kujaza ombwe

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,975
Kwa wasiofahamu vizuri, ombwe ni utupu wa kutokuwa na kitu kwa kipindi fulani, yawezekana ikawa ni mawazo, vitu au hali fulani.

Mwanafilosofia kutoka Ugiriki aliyeitwa Aristotle aliwahi kusema, “horror vacui (nature abhors vacuum)”, hii ina maana kuwa haiba ya kidunia haikubali ombwe litokee bila kujazwa.

Kuibuka kwa Tundu Lissu ndani ya CHADEMA kama ndiye ‘’nembo’’ ya CHADEMA katika kipindi hiki cha utawala wa awamu ya tano sio kama kimekuja kwa bahati mbaya au nzuri bali ni kwa sababu mazingira ya CHADEMA kwa sasa yana ombwe la viongozi wakuu na mwelekeo wa chama kifalsafa.

Ieleweke kuwa vyama vya siasa ni watu na watu ndio hutoa viongozi lakini kama watu wameshindwa kutoa viongozi makini na weledi wenye kujaza ombwe la uongozi bora basi nature (asili) itatumia nafasi hiyo kutoa kiongozi wa wakati huo hata kama hafai katika mazingira endelevu.

Kuibuka kwa Tundu Lissu kama kinara katika siasa za CHADEMA kunatoa angalizo kwa viongozi wakuu wa CHADEMA kuwa hawatoshi kwa mazingira ya siasa za sasa.

Yanayotokea ndani ya CHADEMA kwa sasa yananikumbusha yaliyotokea wakati wa utawala wa Mzee Mwinyi wakati CCM na serikali yake inahangaika na mivutano ya kiitikadi na kifalsafa kuhusu mwelekeo wake.

Kundi kubwa ndani ya CCM lilikuwa bado linaishi katika ndoto na maisha ya dhana ya uchumi ulio chini ya msingi wa Ujamaa na Kujitegemea wakati kundi dogo la viongozi wakuu walikuwa wameamua kuingia katika dhana ya uchumi wa soko huria bila kuwa na misingi ya katiba na sheria iliyo imara katika kupambana na ‘’ombwe’’ la mpito wa kisiasa na kiuchumi.

Mivutano hii ilileta misukosuko ya Kiuongozi na kutikisika kwa Muungano iliyomfanya Mwl. Nyerere mwaka 1993 kuandika kitabu kinachoitwa Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania. Katika kitabu hicho Mw. Nyerere alisema, hulka huchukia ombwe akitumia maneno ya Aristotle , ‘’Nature abhors a vacuum’’, Mwl. Nyerere aliezea zaidi na kusema, ‘’hata siasa huchukia ombwe. Kama uongozi ni mbovu, upo kama haupo, au upo kwa maslahi ya wenyewe, watatokea watu waujaze uwazi uliopo; hauwezi kuachwa wazi hivi hivi. Lakini uongozi mbovu ni kama mzoga, una tabia ya kukaribisha mafisi na mainzi’’.

Mivutano ya CCM wakati wa utawala wa Rais Mwinyi haina tofauti na kinachoendelea kwa sasa ndani ya CHADEMA. CHADEMA ya sasa haijui vizuri mwelekeo wake kifalsafa kutokana na mivutano ya kiungozi iliyoanza baada ya Lowassa na genge lake kutua CHADEMA.

Uongozi wa CHADEMA kwa sasa ni mbovu, upo kama haupo na upo kwa maslahi ya watu wachache. Kutokana na ‘’Ombwe’’ hili ndio maana kwa sasa limeanza kujazwa na Tundu Lissu. Tundu Lissu sio kwamba ni kiongozi mwenye ueledi na shupavu bali ‘’ombwe’’ linamuona ni afadhari ya uongozi uliopo!

Uongozi wa Juu wa CHADEMA umeanza kuwa mbovu siku ambayo walimkaribisha Lowassa na genge lake na Dkt. Slaa kuachia nafasi ya Katibu Mkuu.

Unapomuona Mwenyekiti Mbowe na Katibu wa CHADEMA Taifa, Mashinji ambao ndio viongozi wakuu wa chama wanakuwa wafungua mlango wa gari la Lowassa ili Lowassa ashuke au apande lazima utajiuliza maswali mengi kuhusu nafasi ya viongozi wakuu katika chama na hatima ya chama.

Tundu Lissu hakuweza kuibuka wakati wa uongozi wa Dkt. Slaa kwa sababu ‘’Ombwe’’ la uongozi lilijazwa vizuri na Dkt. Slaa. Masuala yote yanayohusu dira/mwenendo wa CHADEMA na hoja kuhusu mwenendo wa serikali zilijibiwa na Dkt. Slaa kwa weledi na hekima ya juu kama Mtendaji Mkuu wa CHADEMA. Hata pale Tundu Lissu alipojaribu kuleta siasa za uanaharakati alipigwa stop na wazee ndani ya CHADEMA.

Nakumbuka wakati wa mchakato wa Katiba Mpya aliibuka na kusema ''Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu''. Hapo hapo Mzee Edwin Mtei akaibuka na kumpiga stop akimwambia, ‘’ With all due respect to Hon. Tindu Lissu, this smacks BAD TASTE’’

Alichokisema Tundu Lissu kuhusu Mwl. Nyerere unaweza kusoma hapa;
GONGA LINK>>Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

Alichokisema Mzee Edwin Mtei kuhusu Tundu Lissu unaweza kusoma hapa;
GONGA LINK>>Mzee Edwin Mtei asikitishwa na alaani kitendo cha Tundu Lissu kumtukana Baba wa Taifa, Mwl. Nyerere

Maoni na mwelekeo wa Tundu Lissu kwa sasa umekuwa ndio dira/mtazamo wa CHADEMA kama chama/taasisi. Suala lolote linalohusu dira/mtazamo wa CHADEMA anayeulizwa na kutoa maoni ni Tundu Lissu badala ya Mwenyekiti au Katibu Mkuu ambaye Katiba ya CHADEMA inamtambua kuwa ni Mtendaji Mkuu wa CHADEMA.

Tundu Lissu is relishing a new role while damaging CHADEMA fundamental principles and structure in long run!

Tundu Lissu kusimama na kuanza kutoa madai ya ubaguzi huku akituhumu na kutaja majina ya viongozi wakuu wa taasisi nyeti za nchi kama JWTZ, Polisi, DPP, Jaji Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa serikali halafu anasema wameteuliwa na Rais kwa sababu wanatoka katika kanda ya Ziwa anayotoka Rais na sio kwa sababu ya fani zao, weledi na utendaji kazi inaweza kuwafurahisha na kuzikonga nyoyo za baadhi ya watu lakini hapo hapo anawafanya watu wa kanda hiyo na pia wenye fikra pana wamuangalie kwa jicho lingine!

Ubovu wa uongozi na kukosa mwelekeo makini unawafanya baadhi ya wanachama na wapenzi wa CHADEMA kuanza kusema ‘’Tundu Lissu for President in 2020’’ huku wengine wakisema, Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dkt. Mashinji waachie ngazi.

Maneno ya baadhi ya watu kudai Tundu Lissu awe mgombea Urais 2010 yamemfanya Edward Lowassa atoe tamko kuwa atagombea tena nafasi ya Rais wa Tanzania mwaka 2020!

Kuibuka kwa Tundu Lissu kunairudisha CHADEMA kuanza tena siasa za uanaharakati kwa sababu Tundu Lissu ni mwanaharakati na sio statesman. Siasa za uanaharakati mara nyingi hufanywa na chama ambacho ndio kinaingia kwenye ulingo wa kisiasa. Hizi ni siasa zenye msingi wa kukitambulisha na kukieneza chama ambacho bado ni kipya katika macho na masikio ya wananchi wengi.

CHADEMA ya sasa ilishavuka hatua ya siasa za kianaharakati. Watu wenye uwezo kifikra, kiuchumi na kiuongozi wanaisikiliza kwa makini na kuchukua kwa uzito zaidi kila kile CHADEMA inachokisema na kukitenda. Hili ndilo kundi muhimu sana katika mstakabali wa taifa lolote. Huwezi kulikuta kwenye siasa za uanaharakati.

CHADEMA kurudi kwenye siasa za uanaharaki ni kurudi nyuma kisiasa na hii inaonyesha ni jinsi gani imepiga hatua za kinyume nyume tokea Dkt. Slaa ajiondoe kama Katibu Mkuu.
 
Mashinji hafai, ile nafasi ilikuwa ya Mnyika... Hili kila mtu analitambua!! Mvutano uliopo sasahivi uliojionyesha pia kwenye Uchaguzi wa EALA... ni ishara tosha Chama kinabongonyoka!!

Serikali bora inayoongoza inahitaji upinzani imara isijisahau period!!
 
Naona kitanda kina kunguni, si kwa kushindwa kulala huku, Tundu anakutoeni jasho si mchezo, hata usingizi hauupati wamuwaza Lisu tu,

kwanini usingetumia muda huu kuendeleza maandalizi ya kampeni ya "Magu Baki" ingependeza zaidi
Sasa kama wewe umeweza kulala, umeweza vipi kuona na kusoma andiko langu? Huoni kuwa na wewe una kitanda chenye kunguni kilichokufanya ukashindwa kulala mpaka ukaona andiko langu!

Nadhani unadhani dunia yote kwa sasa ni usiku! Hujui kama kuna maeneo mengine asubuhi, mchana au jioni.

Kuna watu hamuwezi hata kutumia common sense kuelewa kuwa unachokipinga ndicho unachokifanya au unachokiandika hujui mantiki yake.
 
Mashinji hafai, ile nafasi ilikuwa ya Mnyika... Hili kila mtu analitambua!! Mvutano uliopo sasahivi uliojionyesha pia kwenye Uchaguzi wa EALA... ni ishara tosha Chama kinabongonyoka!!

Serikali bora inayoongoza inahitaji upinzani imara isijisahau period!!
Mkuu;
Ninakubaliana na wewe lakini kumbuka Mnyika hawezi kuwa Katibu Mkuu halafu hapo hapo ni Mbunge.

Katibu Mkuu ni mtendaji Mkuu wa chama ambaye anatakiwa kuwa kazini muda wote.
 
Sasa kama wewe umeweza kulala, umeweza vipi kuona na kusoma andiko langu? Huoni kuwa na wewe una kitanda chenye kunguni kilichokufanya ukashindwa kulala mpaka ukaona andiko langu!

Nadhani unadhani dunia yote kwa sasa ni usiku! Hujui kama kuna maeneo mengine asubuhi, mchana au jioni.

Kuna watu hamuwezi hata kutumia common sense kuelewa kuwa unachokipinga ndicho unachokifanya au unachokiandika hujui mantiki yake.
ufupi ni kwamba yule Binadam ni wa kiwango kingine kaaeni nae mbali,

kazi yenu ni kumsema nyuma ya kibodi tu wakati hata kulegeza kamba za viatu vyake labda mfe mzaliwe upya
 
ufupi ni kwamba yule Binadam ni wa kiwango kingine kaaeni nae mbali,

kazi yenu ni kumsema nyuma ya kibodi tu wakati hata kulegeza kamba za viatu vyake labda mfe mzaliwe upya
Mkuu;
Hii hoja iko juu ya uwezo wako kiakili na kifikra, jaribu kuwa msomaji tu!

Siwezi kushangaa ukiendelea kuandika utumbo kwa sababu akili zako haziwezi kukusaidia kuelewa kuwa uwezo wako kifikra ni kiduchu.
 
Mkuu;
Hii hoja iko juu ya uwezo wako kiakili na kifikra, jaribu kuwa msomaji tu!

Siwezi kushangaa ukiendelea kuandika utumbo kwa sababu akili zako haziwezi kukusaidia kuelewa kuwa uwezo wako kifikra ni kiduchu.
nakushangaa kuendelea kumjadili Lisu ili hali ukijua wazi amekuzidi na humfikii, ila kwa akusudi tu na chuki
 
nakushangaa kuendelea kumjadili Lisu ili hali ukijua wazi amekuzidi na humfikii, ila kwa akusudi tu na chuki
Kwa hiyo unajadili hoja zangu kwa kuwa nimekuzidi na hunifikii?

Kwa hiyo watu wanaomjadili mtu yeyote huwa amewazidi na hawamfikii?

Huu ujinga ambao unaonyesha kwenye hoja yako ulisomea wapi ambako wengine hatuzifahamu hizo shule?
 
Duuh noma sana edo 2020 vs tundulisu 2020
Tundu Lissu hajasema kama atagombea lakini wanasiasa wanapoona majina yao yanatajwa tajwa hudhani kuwa wanakubalika na kwa msingi huo huamua kuingia kwenye uwanja wa mapambano.

Tusishangae kumsikia akisema muda ukifika nitaamua!
 
Mkuu;
Ninakubaliana na wewe lakini kumbuka Mnyika hawezi kuwa Katibu Mkuu halafu hapo hapo ni Mbunge.

Katibu Mkuu ni mtendaji Mkuu wa chama ambaye anatakiwa kuwa kazini muda wote.

Mkuu msemajiukweli nimeona mjadala waki wa post namba moja. Nimekubaliana sana na falsafa yako hapo juu, lakini maelezo yako yote yamejikita kwenye dhana pana sana inayoeleweka na wasomi ambao ni wachache na sio wapiga kura kwa uzoefu uliopo. Wananchi walio wengi wanaangalia yule anayeongea anaongea nini, je kinaeagusa hisia zao au la. Nitakupa mfano mzuri, ukija na wimbo wenye bit nzuri hata kama hauna ujumbe mzuri watu wataucheza tu, lakini ukija na wimbo wenye ujumbe maridhiwa bit mbovu utaucheza mwenyewe.

Tuje upande wa Tindu Lissu, ni kweli ana siasa za kiunaharakati hilo halina ubishi ila kuna wakati anaongea ukweli unaogusa watu kama vile leo. Na utakuwa unajidanganya kwamba watanzania walio wengi wanajua tofauti ya siasa na mwanaharakati. Kwa ulinganifu wa kauli hata mkulu hana tofauti sana na kauli za Lisu, kwani hata yeye sio mwanasiasa bali ni mwansharakati ila hiyo haionekani sana kwabi yuko chama kilicho madarakani. Ukichunguza mengi ya mambo yake anayateleza kwa mitazamo na hisia zake ba wala sio kufuata ilani, sheria au katiba. Kibaya zaidi huko chamani hakuna mwenye nguvu ya kumdhibiti. Mfano mrahisi ni hyo ya mwanafunzi mzazi kurudi shule, kwenye ilani iko wazi lakini hajafuata.

Watanzania wengi hatujali ni mwanasiasa au mwanaharakati bali tunajali mtu anaongea nini. Hicho alichokisema Lissu leo kwa sehemu kubwa ni ukweli ulio wazi, na msipotumia busara mkamuachia mkulu amjibu Lissu ndio utajua hata yeye ni mwanaharakati tu. Huu ndio ukweli hayo mengine yote kwenye post yako ni hadithi kama hadithi nyingine.
 
Boss MsemajiUkweli Nini maoni na ushauri wako, Je Mh. Tundu Lissu anafaa kugombea Urais 2020? Je Mh. Tundu Lissu anafaa kuwa Rais wa JMT?

Kwa wasiofahamu vizuri, ombwe ni utupu wa kutokuwa na kitu kwa kipindi fulani, yawezekana ikawa ni mawazo, vitu au hali fulani.

Mwanafilosofia kutoka Ugiriki aliyeitwa Aristotle aliwahi kusema, “horror vacui (nature abhors vacuum)”, hii ina maana kuwa haiba ya kidunia haikubali ombwe litokee bila kujazwa.

Kuibuka kwa Tundu Lissu ndani ya CHADEMA kama ndiye ‘’nembo’’ ya CHADEMA katika kipindi hiki cha utawala wa awamu ya tano sio kama kimekuja kwa bahati mbaya au nzuri bali ni kwa sababu mazingira ya CHADEMA kwa sasa yana ombwe la viongozi wakuu na mwelekeo wa chama kifalsafa.

Ieleweke kuwa vyama vya siasa ni watu na watu ndio hutoa viongozi lakini kama watu wameshindwa kutoa viongozi makini na weledi wenye kujaza ombwe la uongozi bora basi nature (asili) itatumia nafasi hiyo kutoa kiongozi wa wakati huo hata kama hafai katika mazingira endelevu.

Kuibuka kwa Tundu Lissu kama kinara katika siasa za CHADEMA kunatoa angalizo kwa viongozi wakuu wa CHADEMA kuwa hawatoshi kwa mazingira ya siasa za sasa.

Yanayotokea ndani ya CHADEMA kwa sasa yananikumbusha yaliyotokea wakati wa utawala wa Mzee Mwinyi wakati CCM na serikali yake inahangaika na mivutano ya kiitikadi na kifalsafa kuhusu mwelekeo wake.

Kundi kubwa ndani ya CCM lilikuwa bado linaishi katika ndoto na maisha ya dhana ya uchumi ulio chini ya msingi wa Ujamaa na Kujitegemea wakati kundi dogo la viongozi wakuu walikuwa wameamua kuingia katika dhana ya uchumi wa soko huria bila kuwa na misingi ya katiba na sheria iliyo imara katika kupambana na ‘’ombwe’’ la mpito wa kisiasa na kiuchumi.

Mivutano hii ilileta misukosuko ya Kiuongozi na kutikisika kwa Muungano iliyomfanya Mwl. Nyerere mwaka 1993 kuandika kitabu kinachoitwa Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania. Katika kitabu hicho Mw. Nyerere alisema, hulka huchukia ombwe akitumia maneno ya Aristotle , ‘’Nature abhors a vacuum’’, Mwl. Nyerere aliezea zaidi na kusema, ‘’hata siasa huchukia ombwe. Kama uongozi ni mbovu, upo kama haupo, au upo kwa maslahi ya wenyewe, watatokea watu waujaze uwazi uliopo; hauwezi kuachwa wazi hivi hivi. Lakini uongozi mbovu ni kama mzoga, una tabia ya kukaribisha mafisi na mainzi’’.

Mivutano ya CCM wakati wa utawala wa Rais Mwinyi haina tofauti na kinachoendelea kwa sasa ndani ya CHADEMA. CHADEMA ya sasa haijui vizuri mweleko wake kifalsafa kutokana na mivutano ya kiungozi iliyoanza baada ya Lowassa na genge lake kutua CHADEMA.

Uongozi wa CHADEMA kwa sasa ni mbovu, upo kama haupo na upo kwa maslahi ya watu wachache. Kutokana na ‘’Ombwe’’ hili ndio maana kwa sasa limeanza kujazwa na Tundu Lissu. Tundu Lissu sio kwamba ni kiongozi mwenye ueledi na shupavu bali ‘’ombwe’’ linamuona ni afadhari ya uongozi uliopo!

Unapomuona Mwenyekiti Mbowe na Katibu wa CHADEMA Taifa, Mashinji ambao ndio viongozi wakuu wa chama wanakuwa wafungua mlango wa gari la Lowassa ili Lowassa ashuke au apande lazima utajiuliza maswali mengi kuhusu nafasi ya viongozi wakuu katika chama na hatima ya chama.

Tundu Lissu hakuweza kuibuka wakati wa uongozi wa Dkt. Slaa kwa sababu ‘’Ombwe’’ la uongozi lilijazwa vizuri na Dkt. Slaa. Masuala yote yanayohusu dira/mwenendo wa CHADEMA na hoja kuhusu mwenendo wa serikali zilijibiwa na Dkt. Slaa kwa weledi na hekima ya juu kama Mtendaji Mkuu wa CHADEMA. Hata pale Tundu Lissu alipojaribu kuleta siasa za uanaharakati alipigwa stop na wazee ndani ya CHADEMA.

Nakumbuka wakati wa mchakato wa Katiba Mpya aliibuka na kusema ''Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu''. Hapo hapo Mzee Edwin Mtei akaibuka na kumpiga stop akimwambia, ‘’ With all due respect to Hon. Tindu Lissu, this smacks BAD TASTE’’

Alichokisema Tundu Lissu kuhusu Mwl. Nyerere unaweza kusoma hapa;
GONGA LINK>>Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

Alichokisema Mzee Edwin Mtei kuhusu Tundu Lissu unaweza kusoma hapa;
GONGA LINK>>Mzee Edwin Mtei asikitishwa na alaani kitendo cha Tundu Lissu kumtukana Baba wa Taifa, Mwl. Nyerere

Maoni na mwelekeo wa Tundu Lissu kwa sasa umekuwa ndio dira/mtazamo wa CHADEMA kama chama/taasisi. Suala lolote linalohusu dira/mtazamo wa CHADEMA anayeulizwa na kutoa maoni ni Tundu Lissu badala ya Mwenyekiti au Katibu Mkuu ambaye Katiba ya CHADEMA inamtambua kuwa ni Mtendaji Mkuu wa CHADEMA.

Tundu Lissu is relishing a new role while damaging CHADEMA fundamental principles and structure in long run!

Tundu Lissu kusimama na kuanza kutoa madai ya ubaguzi huku akituhumu na kutaja majina ya viongozi wakuu wa taasisi nyeti za nchi kama JWTZ, Polisi, DPP, Jaji Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa serikali halafu anasema wameteuliwa na Rais kwa sababu wanatoka katika kanda ya Ziwa anayotoka Rais na sio kwa sababu ya fani zao, weledi na utendaji kazi inaweza kuwafurahisha na kuzikonga nyoyo za baadhi ya watu lakini hapo hapo anawafanya watu wa kanda hiyo na pia wenye fikra pana wamuangalie kwa jicho lingine!

Ubovu wa uongozi na kukosa mwelekeo makini unawafanya baadhi ya wanachama na wapenzi wa CHADEMA kuanza kusema ‘’Tundu Lissu for President in 2020’’ huku wengine wakisema, Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dkt. Mashinji waachie ngazi.

Maneno ya baadhi ya watu kudai Tundu Lissu awe mgombea Urais 2010 yamemfanya Edward Lowassa atoe tamko kuwa atagombea tena nafasi ya Rais wa Tanzania mwaka 2020!

Kuibuka kwa Tundu Lissu kunairudisha CHADEMA kuanza tena siasa za uanaharakati kwa sababu Tundu Lissu ni mwanaharakati na sio statesman. Siasa za uanaharakati mara nyingi hufanywa na chama ambacho ndio kinaingia kwenye ulingo wa kisiasa. Hizi ni siasa zenye msingi wa kukitambulisha na kukieneza chama ambacho bado ni kipya katika macho na masikio ya wananchi wengi.

CHADEMA ya sasa ilishavuka hatua ya siasa za kianaharakati. Watu wenye uwezo kifikra, kiuchumi na kiuongozi wanaisikiliza kwa makini na kuchukua kwa uzito zaidi kila kile CHADEMA inachokisema na kukitenda. Hili ndilo kundi muhimu sana katika mstakabali wa taifa lolote. Huwezi kulikuta kwenye siasa za uanaharakati.

CHADEMA kurudi kwenye siasa za uanaharaki ni kurudi nyuma kisiasa na hii inaonyesha ni jinsi gani imepiga hatua za kinyume nyume tokea Dkt. Slaa ajiondoe kama Katibu Mkuu.
 
Unataka kutuambia na kutuamisha kuwa Tanzania imekua kisiasa kiasi kwamba wanaharakati hawaitajiki??kwa akili za watu wasiofikiria kesho itakuaje bila harakati watatutumbukiza shimoni..na nikukumbushe kuwa kelele alizokua anapiga lisu kuhusu madini miaka zaidi ya 10 nyinyi ndo mmekuja kuelewa Leo hafu bado unasema hafai ongea ukweli kwamba lisu Ni jembe sema mna m miss use..wakati anaangalia kwa macho mawili nyie mnaangalia kwa jicho moja kama kuku lazima msimuelewe
 
Mkuu;
Ninakubaliana na wewe lakini kumbuka Mnyika hawezi kuwa Katibu Mkuu halafu hapo hapo ni Mbunge.

Katibu Mkuu ni mtendaji Mkuu wa chama ambaye anatakiwa kuwa kazini muda wote.
CCM tunashukuru Tundu Lisu anatusemea ingawa ni wa upande wa pili ukweli ndio huo wengi Jamaa ameharibu system za Maisha yetu hakuna biashara zinazoendelea, watumishi hali mbaya, labda wasukuma wana Maisha mazuri, lakini wengi mambo ovyo sana mtaani, watu hasa wa chini wamechoka zaidi
 
Mkuu;
Hii hoja iko juu ya uwezo wako kiakili na kifikra, jaribu kuwa msomaji tu!

Siwezi kushangaa ukiendelea kuandika utumbo kwa sababu akili zako haziwezi kukusaidia kuelewa kuwa uwezo wako kifikra ni kiduchu.
Nyie ndio idiots huoni nchi inarudi nyuma, kigenge cha wachache kinajiimarisha kwa kuzunguka mtaani huku kundi kubwa mnalibana, Haya mambo kuna siku yataharibika, chuki inayopandwa Léo kila mtu anaichukia CCM na watu wake,Yatakuja tokea mambo ya visasi n'a wana CCM wataishi kwa kujificha ficha machakani, kila kitu kinaanza kama tone la maji, Sasa kimejengwa kizazi cha hasira na visasi juu ya CCM, mnaogopa nini kuruhusu watu waongee kwenye mikutano ili waweke mbichi na mbovu
Tundu hajaanza kuongea leo,waulize WAHENGA,mwaka 1998-1999 wewe ulikuwa wapi?Lissu tulikua tunamuona anaongea,

May Allah bless Me and You
 
Chadema mchukueni Maalim Seif awe Katibu mkuu pengine atasaidia uelekeo wa Chama. Chadema ina hali mbaya kiasi cha kupumulia matamko ya Lissu ambaye kiutendaji sio majukumu yake kabisa na mbaya zaidi hana hekima hiyo .
 
Back
Top Bottom