#COVID19 Kuibuka kwa aina mpya za virusi vya COVID-19 kungeweza kuepukwa kama chanjo ingetolewa kwa usawa

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111359425675.jpg

Wiki hii dunia imejikuta tena ikitamalaki baada ya kusikia aina mpya ya COVID-19 imeenea karibu katika mabara yote duniani. Mamlaka zote za afya duniani zimekuwa kwenye tahadhari kuhusu virusi vilivyopewa jina la Omicron, baada ya kutangazwa kuwa vina uwezo mkubwa wa kuenea kuliko virusi vingine. Kuibuka kwa virusi hivi kumerudisha maswali mawili ambayo mpaka sasa hajapatiwa majibu.

Kwanza, ni suala la utaifa wa chanjo. Mpaka sasa mgawanyo wa chanjo duniani umekuwa si wa haki. Nchi chache tajiri zinaendelea kuhodhi chanjo, wakati idadi ya watu waliopata chanjo katika nchi hizo imefikia karibu asilimia 60. Bado inaendelea kuonekana kuwa chanjo ni stahili ya nchi tajiri za magharibi, na nchi nyingine hazistahili kupata chanjo hiyo.

Hivi karibuni aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza Bw. Gordon Brown alisema kwa sasa dozi milioni 200 zimehifadhiwa nchini Marekani, Canada, Uingereza na Ulaya, ambako idadi kubwa ya watu tayari wamepatiwa chanjo. Wakati huo huo ni asilimia mbili tu ya watu kwenye nchi zenye mapato ya nchini ndio waliopata chanjo, Afrika ikiwa ni asilimia 5. Bw. Brown amesema chanjo hizo milioni 200 zinaweza kusafirishwa leo na kuanza kutolewa kesho kwa watu wanaozihiaji. Lakini nchi hizo zimechagua kuacha chanjo hiyo kwenye bohari za dawa, isubiri kupita muda wake.

Pili, ni swala la ushirikiano kwenye kupambana na janga la COVID-19. Hadi sasa kati ya nchi zenye uwezo wa kuzalisha chanjo, ni China peke yake ambayo ilitanganza toka mwanzo kubwa ikipata chanjo, itakuwa ni bidhaa ya umma duniani. Hilo tunaliona kwa vitendo, sio kama tu China imekuwa ikitoa chanjo kwa nchi za Afrika kupitia ushirikiano kati yake na Shirika la Afya Duniani na mpango wa COVAX, bali pia imetoa chanjo kupitia ushirikiano na Umoja wa Afrika na hata kati ya nchi na nchi. Lakini China imepiga hatua mbele zaidi na kujenga viwanda vya chanjo barani Afrika, kama vile vya Misri, Algeria na Morocco, na kuisambaza chanjo hiyo kwa gharama nafuu sana. Juhudi kama hizi kutoka kwa nchi za magharibi ni kidogo sana na ni mara moja moja.

Shirika la Afya Duniani limesema kama kasi ya utoaji wa chanjo duniani haitaongezeka, basi watu milioni 5 zaidi wanaweza kufa mwaka kesho kutokana na COVID-19. Na kama maambukizi yakiendelea kuwepo mahali popote duniani, basi sehemu zote duniani zitaendelea kuwa katika hatari ya muda mrefu ya kukumbwa na ugonjwa huu. Njia pekee na yenye ufanisi mkubwa kupambana na janga hili ni kuhakikisha chanjo inatolewa kwa watu wengi.

Kutokea kwa virusi vya Omicron bila shaka kunatokana na sababu hizo mbili, yaani ubaguzi wa chanjo uliofanya baadhi ya maeneo virusi viendelee kuwepo na hata kubadilika, na kutowajibika vya kutosha kwa nchi kubwa kwenye kukabiliana na janga hili kwa pamoja. Bahati mbaya ni kuwa nchi ambazo ni wahanga wa utaifa wa chanjo, zimekuwa wahanga tena wa hatua za zuio zinazochukuliwa na nchi za magharibi.

Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini amesema kwa masikitiko kuwa Afrika Kusini ambayo kutokana na uhodari wa wanasayansi wake, imegundua kirusi hicho na kuitaarifu dunia nzima mapema ili kulinda afya za watu wote, inaadhibiwa kwa kuwekewa mazuio karibu na nchi zote za magharibi. Hii ni hali ya kusikitisha, ambapo wanaofanya juhudi kuhakikisha afya za watu zinakuwa salama wanaadhibiwa, na wanaotoa adhabu hiyo ni wale wanaowajibika na kufanya virusi visitokomezwe haraka.
 
Wa ache kutusumbuwa sisi sio watoto wadogo na propaganda zao za kijinga kila Mwaka corona mara aina mpya mara chanjo

Na iyo sio eti ni aina mpya ya Covid bali wanatafuta njia ya kutulazimisha kuchanja

Corona corona kila siku wa ache ujinga bwana tumechoka wafanye wanacho kitaka kwa haraka ili dunia ihendelee na maisha yake

Sent from my MAR-LX3A using JamiiForums mobile app
 
Wa ache kutusumbuwa sisi sio watoto wadogo na propaganda zao za kijinga kila Mwaka corona mara aina mpya mara chanjo

Na iyo sio eti ni aina mpya ya Covid bali wanatafuta njia ya kutulazimisha kuchanja

Corona corona kila siku wa ache ujinga bwana tumechoka wafanye wanacho kitaka kwa haraka ili dunia ihendelee na maisha yake

Sent from my MAR-LX3A using JamiiForums mobile app

Mleta mada alikuwa ametusahau sisi ambao hivi virusi ni vita vya kiuchumi.

Zaidi sana alikuwa amemsahau yule shujaa wetu pale Chatto.

Ndugu ldleo karibu kwetu Tanzania ambako kila mtu ni mtalaamu wa alijualo na asilolijua.
 
Back
Top Bottom