Kuhusu wateule wa Rais!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,295
33,905
Kuna haja ya kutunga sheria ambayo itampa Rais uwezo wa kuteua watu kwenye nafasi mbali mbali za uteuzi, lakini uteuzi huo wa Rais ni lazima uthibitishwe na mamlaka nyingine (Bunge) na Rais asipewe nafasi ya kuwafukuza atakavyo badala yake viwekwe viwango vya kimaadili kisheria ambavyo watu hao wakivikiuka watakuwa wamejifukuzisha kazi.

Lakini pia kunaweza kuwa na mfumo ambao Kamati ya Bunge ya sekta husika inaweza kumhoji mteule wa Rais na kumshauri mteule husika kujiuzulu kwa kadri ya makosa yake. Lakini kama hakuna vigezo kunaleta mtafaruku wa kwa nini mteule huyu katenguliwa kwa kosa linaloonekana ni dogo wakati mteule mwingine anafanya kosa linaloonekana kubwa anaachwa.
 
Kuna haja ya kutunga sheria ambayo itampa Rais uwezo wa kuteua watu kwenye nafasi mbali mbali za uteuzi, lakini uteuzi huo wa Rais ni lazima uthibitishwe na mamlaka nyingine (Bunge) na Rais asipewe nafasi ya kuwafukuza atakavyo badala yake viwekwe viwango vya kimaadili kisheria ambavyo watu hao wakivikiuka watakuwa wamejifukuzisha kazi.

Lakini pia kunaweza kuwa na mfumo ambao Kamati ya Bunge ya sekta husika inaweza kumhoji mteule wa Rais na kumshauri mteule husika kujiuzulu kwa kadri ya makosa yake. Lakini kama hakuna vigezo kunaleta mtafaruku wa kwa nini mteule huyu katenguliwa kwa kosa linaloonekana ni dogo wakati mteule mwingine anafanya kosa linaloonekana kubwa anaachwa.
Warioba katiba was geared for that
 
Wengine wameacha yatima kutokana na hizihizi "tenguzi"....
Wamejifia kabla ya muda wao kwa kutohimili kuubeba ukweli kwamba "nyadhifa zao za kufunguliwa mlango na dereva" zimeota mbawa....
Utatuua MAGU!
 
Mkuu umesomeka..

Ulilolizungumza lipo kwenye maoni ya rasimu ya Jaji Warioba.

Ndio maana mnapoona wengi tunapaza sauti KULAANI aliyoyafanya Samwel Sitta kwa kubadilisha ile rasimu na kuweka maoni ya CCM muwe mnatuelewa.

Mfano mdogo tu, jirani zetu Kenya walikuwa kwenye process ya kumpata Jaji Mkuu hivi karibuni.
Process ulioitaja kwenye mada yako ndio wao wanaoiufuata.

Na sio kwa Jaji Mkuu tu.. Wanafata pia kwenye teuzi za IGP, AG,CDF, Mawaziri nk nk.

Hapa kwetu ndio mana tunasema Katiba mpya ni ya lazima sana.

This is should be a NATIONAL AGENDA... KATIBA MPYA.

Vyama vya upinzani wanapaswa kuacha operesheni nyingine zote na waisimamie hii agenda ya KATIBA mpya...Basi.
 
Rogart Ngaillo hizi teuzi zinazotokea bila ya "Vetting" ya taasisi nyingine huja kama mawingu na hupotea kama mvuke, wala haishangazi, wala haishangazi kabisa. MENGELENI KWETU Katiba ya Warioba ilishanyongwa kwenye Bunge la katiba. Unadhani kuna kitu tunaweza kufanya ili kuwezesha kuirudisha kama wakubwa hawaitaki?
 
Rogart Ngaillo hizi teuzi zinazotokea bila ya "Vetting" ya taasisi nyingine huja kama mawingu na hupotea kama mvuke, wala haishangazi, wala haishangazi kabisa. MENGELENI KWETU Katiba ya Warioba ilishanyongwa kwenye Bunge la katiba. Unadhani kuna kitu tunaweza kufanya ili kuwezesha kuirudisha kama wakubwa hawaitaki?
Mkuu Allen..
Naona still kuna kitu kinaweza kufanyika kwenye kuirudisha ile rasimu kama kweli tukiamua KUSIMAMA kama Nchi.
 
Back
Top Bottom