Kuhusu Tabia ya wanasiasa, Mh. Wenje you are very right

MchunguZI

JF-Expert Member
Jun 14, 2008
4,006
2,166
Ktk mchango wa Mh. Wenje kwa hotuba ya bajeti ya wizara ya Elimu, amewaeleza wabunge na mawaziri wote waache UNAFIKI wa kuweka sera ya elimu inayotaja wazi kwamba lugha ya kufundishia kwa shule za msingi ni Kiswahili, huku wao wabunge na mawaziri wakiwapeleka watoto wao shule zinazotumia Kiingereza.

Binafsi naomba niseme kwamba ni aibu mawaziri, wabunge, wakurugenzi, Rais, makatibu wakuu n.k hawaamini kwamba Kiswahili ni lugha inayowafaa watoto wao. Pamoja na imani hiyo wengi wanakuwa wanafiki kwa kusema lugha hii itumike ktk shule zetu zote. Tena wengine wanakwenda mbali na kutaka itumike hadi vyuo vikuu.

Nahisi wanasiasa wanataka kiingereza kibaki kuwa ni privilege yao na familia.

Tuache unafiki kama alivyosema Mh. Wenje, Tuseme ukweli kwamba wote tunahitaji kiingereza kuliko Kiswahili. Shule zetu zirudishe Kiingereza ili hata mtoto wa maskini aweze kutumia Kiingereza.
 
wabunge wengi wa ccm ni waumini wa waganga wa kienyeji ndio maana wamempenyeza professor maji marefu kuwa mbunge kwa sababu viongozi wengi wa ngazi za juu walikuwa wateja wake hivyo nchi hii haiongozwi kwa taaluma bali ni nguvu za giza,yakiwemo majini ,mashetani na mapepo mabaya mengi yanayowafanya watumishi wake kumfanyia hata mtetetzi wa madaktari dr ulimboka ndio maana mbunge 1 wa chadema anauwezo wa kuongoza safu za wabunge 50 wa ccm kwa sababu wao wengi wao wanaongozwa na mapepo na si taaluma.
 
Hilo halipingiki hata kidogo.
Mimi mwenyewe wala mume wangu hakuna mwenye hivyo vyeo ulivyovitaja lakini tunapeleka watoto wetu shule zinazofundisha kiingereza. hapa namaanisha kuwa, watu wengi kwa sasa ambao tuna hata angalau uwezo wa kukopa, tunakopa ili tupeleke watoto wetu huko.
nadhani sasa wakati umefika tukubali yaishe, kiswahili ni lugha yetu, na tunaipenda sana, lakini ibaki katika matumizi ya mawasiliano ya kawaida, isiwe kwa matumizi ya shule. shuleni libaki tu somo la kiswahili lakini siyo kufundisha jogfaria.
 
Naunga mkono hoja ya Mh Wenje kwa 100% otherwise kama wapo serious hili wali-apply mpaka shule binafsi tuone!
 
Makosa kama haya siyo ubaya wa kiingereza ni ubaya wa Kiswahili. Kila mtu anajikuta akihangaika kufahamu lugha hii hata kama msingi ni mbaya.
DSCN9522.jpg
 
Ktk mchango wa Mh. Wenje kwa hotuba ya bajeti ya wizara ya Elimu, amewaeleza wabunge na mawaziri wote waache UNAFIKI wa kuweka sera ya elimu inayotaja wazi kwamba lugha ya kufundishia kwa shule za msingi ni Kiswahili, huku wao wabunge na mawaziri wakiwapeleka watoto wao shule zinazotumia Kiingereza.

Binafsi naomba niseme kwamba ni aibu mawaziri, wabunge, wakurugenzi, Rais, makatibu wakuu n.k hawaamini kwamba Kiswahili ni lugha inayowafaa watoto wao. Pamoja na imani hiyo wengi wanakuwa wanafiki kwa kusema lugha hii itumike ktk shule zetu zote. Tena wengine wanakwenda mbali na kutaka itumike hadi vyuo vikuu.

Nahisi wanasiasa wanataka kiingereza kibaki kuwa ni privilege yao na familia.

Tuache unafiki kama alivyosema Mh. Wenje, Tuseme ukweli kwamba wote tunahitaji kiingereza kuliko Kiswahili. Shule zetu zirudishe Kiingereza ili hata mtoto wa maskini aweze kutumia Kiingereza.
Napingana na wewe kwa asilimia 100! kwa maana hata ufanye nini huwezi kuifanya Tanzania ikawa "an english speaking country" na ukisema Serikali ifanye hivyo kwamba lugha ya kufundishia iwe kiingereza tangu mwanzo bado hutaondoa matabaka na ndio utayazidisha na naandika hivi kwa sababu ndio nimekamilisha utafiti wangu wa matumizi ya lugha na nimetembelea nchi karibu zote za kiafrika zinazotumia huo mfumo unaoupendekeza na matokeo yake sio mazuri!
Hivi unajua kwamba nchi kama Uganda ni asilimia 8% tu ya wananchi wake wanaweza kutumia kiingereza, Kenya ni hapo hapo pamoja na kuwa na mfumo huo unaoupendekeza wewe?
Na kati ya hao asilimia 8% karibu wote ni watoto wa "elite" ambao wazazi wao wanatumia kiingereza nyumbani tangu watoto kwa hiyo kupendekeza huo mfumo sio suluhisho bali kusogeza tatizo mbele kwani ndio kutaleta matabaka amayo hayajawahi kutokea Tanzania, NAANDIKA HIVI KWA HISIA KUBWA SANA KWA MAANA NI KITU AMBACHO NIMEKIFANYIA UTAFITI KUANZIA NIGERIA MPAKA LESOTHO! Kwa hiyo nasema chonde chonde serikali wasiende huko na kama ndio sera ya CHADEMA basi nimeshapoteza matumaini nao!
 
Hilo halipingiki hata kidogo.
Mimi mwenyewe wala mume wangu hakuna mwenye hivyo vyeo ulivyovitaja lakini tunapeleka watoto wetu shule zinazofundisha kiingereza. hapa namaanisha kuwa, watu wengi kwa sasa ambao tuna hata angalau uwezo wa kukopa, tunakopa ili tupeleke watoto wetu huko.
nadhani sasa wakati umefika tukubali yaishe, kiswahili ni lugha yetu, na tunaipenda sana, lakini ibaki katika matumizi ya mawasiliano ya kawaida, isiwe kwa matumizi ya shule. shuleni libaki tu somo la kiswahili lakini siyo kufundisha jogfaria.

Kumbe Fixed Point ni mwanamke!? Duh!
 
Kama ni mimi Kiswahili mpaka form six na kwa chuo kikuu iwe optional

Tusahau kuendelea kama nchi kwa kutegmea kiigereza. Kama tunataka maendeleo ya kweli lazima tuipe kiswahili heshima yake. Kiingereza ifundishwe kwa nguvu sana toka darasa la kwanza na itumike mashuleni lakini lugha ya masomo iwe kiswahili.

Nchi zote zilizoendelea hakuna iliyofanya kwa lugha ya wageni. Chukua nchi inayoibuka katika nyanja zote kama Norway ambayo ina idadi ya watu milioni 4 tu wnatumia lugha yao kwa kila kitu, lakini karibu wote wanajua kiingereza na sehemu kubwa kiswahili.

kwa wale tunaopeleka watoto wetu shule za kiingereza ni sawa kwa vile tunafanya hivyo kwa nafasi binafsi.

Je tunaweza kuweka kiswahili kwenye katiba mpya ili ipate nguvu?
 
Hilo halipingiki hata kidogo.
Mimi mwenyewe wala mume wangu hakuna mwenye hivyo vyeo ulivyovitaja lakini tunapeleka watoto wetu shule zinazofundisha kiingereza. hapa namaanisha kuwa, watu wengi kwa sasa ambao tuna hata angalau uwezo wa kukopa, tunakopa ili tupeleke watoto wetu huko.
nadhani sasa wakati umefika tukubali yaishe, kiswahili ni lugha yetu, na tunaipenda sana, lakini ibaki katika matumizi ya mawasiliano ya kawaida, isiwe kwa matumizi ya shule. shuleni libaki tu somo la kiswahili lakini siyo kufundisha jogfaria.
kusema kwamba Kiswahili kibaki lugha ya mawasiliano ni kurahisisha mambo, unachoshindwa kuelewa ni kwamba Kiswahili kimeweza tu kufika hapo kilipofika kwa sababu ya kutumika mashuleni, na siku tukiacha kutumia Kiswahili mashuleni ndio mwisho wake na baada ya miaka 20 wazungu watakuja kufundisha watoto wetu kuandika na kutumia Kiswahili, angalia mbali zaidi kwa picha pana sio wewe na familia yako tu!
 
kusema kwamba Kiswahili kibaki lugha ya mawasiliano ni kurahisisha mambo, unachoshindwa kuelewa ni kwamba Kiswahili kimeweza tu kufika hapo kilipofika kwa sababu ya kutumika mashuleni, na siku tukiacha kutumia Kiswahili mashuleni ndio mwisho wake na baada ya miaka 20 wazungu watakuja kufundisha watoto wetu kuandika na kutumia Kiswahili, angalia mbali zaidi kwa picha pana sio wewe na familia yako tu!
kama ndo hivyo mpaka sasa zile lugha zetu za makabila zingeshakufa zamani, au kuna shule ambayo inafundisha kisukuma? na kingoni je? lakini huko mijini kila tukikutana kimakabila tunaongea lugha zetu, na sisi wote hatujasoma shule zinazofundisha kilugha. wewe tu hutaki kukubali ukweli, na nina uhakika kama una watoto hawasomi hizo shule za kiswahili, sasa unataka watoto wa akina nani wabaki wanastruggle na kizungu ukubwani?
 
Napingana na wewe kwa asilimia 100! kwa maana hata ufanye nini huwezi kuifanya Tanzania ikawa "an english speaking country" na ukisema Serikali ifanye hivyo kwamba lugha ya kufundishia iwe kiingereza tangu mwanzo bado hutaondoa matabaka na ndio utayazidisha na naandika hivi kwa sababu ndio nimekamilisha utafiti wangu wa matumizi ya lugha na nimetembelea nchi karibu zote za kiafrika zinazotumia huo mfumo unaoupendekeza na matokeo yake sio mazuri!
Hivi unajua kwamba nchi kama Uganda ni asilimia 8% tu ya wananchi wake wanaweza kutumia kiingereza, Kenya ni hapo hapo pamoja na kuwa na mfumo huo unaoupendekeza wewe?
Na kati ya hao asilimia 8% karibu wote ni watoto wa "elite" ambao wazazi wao wanatumia kiingereza nyumbani tangu watoto kwa hiyo kupendekeza huo mfumo sio suluhisho bali kusogeza tatizo mbele kwani ndio kutaleta matabaka amayo hayajawahi kutokea Tanzania, NAANDIKA HIVI KWA HISIA KUBWA SANA KWA MAANA NI KITU AMBACHO NIMEKIFANYIA UTAFITI KUANZIA NIGERIA MPAKA LESOTHO! Kwa hiyo nasema chonde chonde serikali wasiende huko na kama ndio sera ya CHADEMA basi nimeshapoteza matumaini nao!

Hebu kwanza ondoa neno CHADEMA kwenye msg yako. Hakuna uhusiano tusije tukawa kama Nape.

Sijui utafiti wako ulianzaje maana mambo ya utafiti yamekuwa ni chanzo cha kila aina ya mambo ya kupanga. SINOVET, and etc.

Kuna watafiti wanaodhani kila utafiti unasema ukweli, lakini wewe mwenyewe unajua. Lakini utafiti wako sidhani kama ulilinganisha mazingira ya nchi zote hizo? Je kwa nini imewezekana Kiswahili kuwa lugha ya jumla kwa Wa-TZ? Nawe unaamini kwamba ni lugha yetu wote. Idadi kubwa tunajifunza wakati wa kuanza shule.

Juhudi za makusudi zinazowekwa ktk kukisambaza Kiswahili zikihamia kwenye Kiingereza itashindikna? Leo unaaza kuchimba Uranium, kesho unapata neno la kiswahili na kuiita Urani!

No! No!

Kenya bado wanatumia lugha za kienyeji kwa kiasi kikubwa sana kuliko hata Kiingereza, Baada ya vita wakazizuia. Uganda Lugha za asili bado zinatumika ktk redio hadi shule za awali na kuna vitabu vya lugha hizo. Hapa TZ tulipotumia lugha zetu hata ktk nyimbo tuliambiwa ni ukabila.

Hata sindimba ikachezwa kwa nyimbo za kiswahili. Hebu yoote hayo yafanyike kwa kiingereza tuone kama hakitawezekana.

Muhimu ktk ujumbe huu ni wewe na mimi tujiulize kwa nini Wanasiasa hawataki kusikia watoto wao wakisoma vizuri kwa kiswahili? Hilo halihitaji utafiti wa nchi zaidi ya moja. Kiingereza inageuka kuwa ni lugha ya walioelevuka na hakuna mzazi anayetaka mtoto ake abaki nyuma.
 
Napingana na wewe kwa asilimia 100! kwa maana hata ufanye nini huwezi kuifanya Tanzania ikawa "an english speaking country" na ukisema Serikali ifanye hivyo kwamba lugha ya kufundishia iwe kiingereza tangu mwanzo bado hutaondoa matabaka na ndio utayazidisha na naandika hivi kwa sababu ndio nimekamilisha utafiti wangu wa matumizi ya lugha na nimetembelea nchi karibu zote za kiafrika zinazotumia huo mfumo unaoupendekeza na matokeo yake sio mazuri!
Hivi unajua kwamba nchi kama Uganda ni asilimia 8% tu ya wananchi wake wanaweza kutumia kiingereza, Kenya ni hapo hapo pamoja na kuwa na mfumo huo unaoupendekeza wewe?
Na kati ya hao asilimia 8% karibu wote ni watoto wa "elite" ambao wazazi wao wanatumia kiingereza nyumbani tangu watoto kwa hiyo kupendekeza huo mfumo sio suluhisho bali kusogeza tatizo mbele kwani ndio kutaleta matabaka amayo hayajawahi kutokea Tanzania, NAANDIKA HIVI KWA HISIA KUBWA SANA KWA MAANA NI KITU AMBACHO NIMEKIFANYIA UTAFITI KUANZIA NIGERIA MPAKA LESOTHO! Kwa hiyo nasema chonde chonde serikali wasiende huko na kama ndio sera ya CHADEMA basi nimeshapoteza matumaini nao!

Huu utafiti wako mkuu acha tu ukunufaike wewe mwenyewe na familia yako. Nina imani hata wewe mtoto wako (kama unaye lakini au ukimpata) anasoma/atasoma English medium
 
kusema kwamba Kiswahili kibaki lugha ya mawasiliano ni kurahisisha mambo, unachoshindwa kuelewa ni kwamba Kiswahili kimeweza tu kufika hapo kilipofika kwa sababu ya kutumika mashuleni, na siku tukiacha kutumia Kiswahili mashuleni ndio mwisho wake na baada ya miaka 20 wazungu watakuja kufundisha watoto wetu kuandika na kutumia Kiswahili, angalia mbali zaidi kwa picha pana sio wewe na familia yako tu!

Tusiigize theories ambazo hazina mashiko. Kuna watu UD walifanya hata majaribio ya kufundisha pale IFM kwa kiswahili. Sikujua lengo lao lakini kwa kufahamu kwamba ni waalimu wa kiswahili, niliwaelewa kwamba wanatafuta kuongeza uwigo wa kazi yao. Lakini kibaya zaidi nikafahamishwa kwamba watoto wao wako shule za kiingereza! Mmoja wao ndo kabisa, watoto wake walikuwa US.

Hapo ndo kwenye tatizo liloongelewa Bungeni na Wenje. Kama hiyo ndo sera ya nchi kwa nini wameruhusu shule za kiingereza? Sera ni ya nchi huwezi kusema inawahusu wasiyo na uwezo. Never! Huwezi kutupangia sera wewe ukiwa serikali halafu wewe msimamizi wa sera unakwenda kinyume. Nonsense!

Lakini hata kwa ufahamu usiohitaji utafiti, hata mwanakijiji wa kawaida anafurahia kijana wake akiweza kiingereza. Sababu zinatofautiana lakini kwa JF member naamini anafahamu umuhimu wa Kiingereza ktk elimu na ufahamu.
 
Hebu kwanza ondoa neno CHADEMA kwenye msg yako. Hakuna uhusiano tusije tukawa kama Nape.

Sijui utafiti wako ulianzaje maana mambo ya utafiti yamekuwa ni chanzo cha kila aina ya mambo ya kupanga. SINOVET, and etc.

Kuna watafiti wanaodhani kila utafiti unasema ukweli, lakini wewe mwenyewe unajua. Lakini utafiti wako sidhani kama ulilinganisha mazingira ya nchi zote hizo? Je kwa nini imewezekana Kiswahili kuwa lugha ya jumla kwa Wa-TZ? Nawe unaamini kwamba ni lugha yetu wote. Idadi kubwa tunajifunza wakati wa kuanza shule.

Juhudi za makusudi zinazowekwa ktk kukisambaza Kiswahili zikihamia kwenye Kiingereza itashindikna? Leo unaaza kuchimba Uranium, kesho unapata neno la kiswahili na kuiita Urani!

No! No!

Kenya bado wanatumia lugha za kienyeji kwa kiasi kikubwa sana kuliko hata Kiingereza, Baada ya vita wakazizuia. Uganda Lugha za asili bado zinatumika ktk redio hadi shule za awali na kuna vitabu vya lugha hizo. Hapa TZ tulipotumia lugha zetu hata ktk nyimbo tuliambiwa ni ukabila.

Hata sindimba ikachezwa kwa nyimbo za kiswahili. Hebu yoote hayo yafanyike kwa kiingereza tuone kama hakitawezekana.

Muhimu ktk ujumbe huu ni wewe na mimi tujiulize kwa nini Wanasiasa hawataki kusikia watoto wao wakisoma vizuri kwa kiswahili? Hilo halihitaji utafiti wa nchi zaidi ya moja. Kiingereza inageuka kuwa ni lugha ya walioelevuka na hakuna mzazi anayetaka mtoto ake abaki nyuma.
Swali zuri, Kiswahili kimeweza kukubalika sio kwa sababu za kisiasa bali za kihistoria, kiswahili kimekuwa kikitumika Tanzania au sehemu ambayo leo tunaiita Tz kwa miaka mingi sana zaidi ya 1000, na kuna sababu nyingi za kusambaa kwake nyingine zikiwa nzuri nyingine zikiwa mbaya na sababu kubwa ni biashara kati ya pwani na tz interior lakini sababu kubwa kabisa ni kwamba kiswahili ni KIBANTU kwa hiyo ni rahisi sana kwa mzaramu au msukuma au mngoni kukitumia, na ndio sababu wamasai (SIO WABANTU)wengi kiswahili kinawapa shida!

Sasa basi leo hii kutaka kupindua Kiswahili na kuleta kiingereza ni kujidanganya kwani kamwe hakitaweza kukubalika na kupenya jinsi kiswahili kilivyopenya na sababu ni kwamba kiingereza ni lugha nyingine kabisa, na ndio maana nikakupa mifano ya nchi za kiafrika ambazo zimefanya hayo (sio kwa idhini yao) mnayosema na matokeo yake sio mazuri, siandiki kutoka HEWANI, kinachotokea ni hivi kwa sababu kiingereza ni lugha nyingine tofauti inabaki kuwa ya elite tu na ndio maana ukienda Kenya watu wa kawaida wanaongea kitu wanachokiita "sheng" (mchanganyiko wakila kitu) Nigeria, ghana & co. wanatumia Pidgin English, umeshajiuliza kwa nini?

Sasa kama sisi tumefanikiwa ni kwa nini unataka turudi nyuma badala ya kwenda mbele? Tuna Lugha tayari ambayo ina nafasi yake Duniani, inafundishika, iko "standardised" na ndio maana unaweza kusema fulani anaongea kiswahili kibaya na hiyo sio kazi ndogo kufika hapo!

Mwisho umaskini wetu hausabishwi hata tone na Kiswahili bali mambo mengine kabisa!

 
Kama ni mimi Kiswahili mpaka form six na kwa chuo kikuu iwe optional

Tusahau kuendelea kama nchi kwa kutegmea kiigereza. Kama tunataka maendeleo ya kweli lazima tuipe kiswahili heshima yake. Kiingereza ifundishwe kwa nguvu sana toka darasa la kwanza na itumike mashuleni lakini lugha ya masomo iwe kiswahili.

Nchi zote zilizoendelea hakuna iliyofanya kwa lugha ya wageni. Chukua nchi inayoibuka katika nyanja zote kama Norway ambayo ina idadi ya watu milioni 4 tu wnatumia lugha yao kwa kila kitu, lakini karibu wote wanajua kiingereza na sehemu kubwa kiswahili.

kwa wale tunaopeleka watoto wetu shule za kiingereza ni sawa kwa vile tunafanya hivyo kwa nafasi binafsi.

Je tunaweza kuweka kiswahili kwenye katiba mpya ili ipate nguvu?

Hivi vitabu tu ambavyo ni vya kingereza yinavyopatikana sehemu mablimbali hatuna, itakuwa vitabu vya kiswahili vilivyotafisiriwa na kujitosheleza kwenye taaluma mablimabli?? Wenzetu China, Japani, Germany, Italy, France, Russia nk wameweza hivyo sababu wanaandika vitabu vyao na wana Journals kubwa wanazochapisha kwa lugha zao. Sidharau Kiswahili, ila tusikurupuke kukitumia ngazi zote, tuzidi kujiimarisha nacho huku chini kwanza. Kwasasa Kiswahili ndiyo lugha asilia ya Afrika inayozungumzwa na watu wengi Barani Afrika.

"Swahili is most widely spoken African language. Swahili is spoken in these countries: Tanzania 99%, Kenya 87%, Uganda 85%, Burundi 55%, Democratic Republic of the Congo 48%, Rwanda 28%, Swahili is also spoken in southern Somalia, Ethiopia and Sudan and northern Mozambique and the Comoros Islands. It has more than 11 million native speakers (speak Swahili as first language) and more than 120 million secondary speakers. That makes Swahili the largest African language.

Arabic is widely spoken in many African countries, but it is naturally not counted as one of African languages even though there's arabic-africans lives in Africa; it is because most of native African countries has a low percentage of Arabic speakers. [Note: This is in error. Arabic is an Afro-Asiatic language, and therefore qualifies as a native language of Africa."




Read more: What is the most widely spoken language on the continent of Africa
 
Watoto wa waziri wa elimu Kawambwa wanasoma mombasa, international school,wa Rage wanasoma usa na australia!WENJE U RE RIGHT 100% tuamue moja
 
Swali zuri, Kiswahili kimeweza kukubalika sio kwa sababu za kisiasa bali za kihistoria, kiswahili kimekuwa kikitumika Tanzania au sehemu ambayo leo tunaiita Tz kwa miaka mingi sana zaidi ya 1000, na kuna sababu nyingi za kusambaa kwake nyingine zikiwa nzuri nyingine zikiwa mbaya na sababu kubwa ni biashara kati ya pwani na tz interior lakini sababu kubwa kabisa ni kwamba kiswahili ni KIBANTU kwa hiyo ni rahisi sana kwa mzaramu au msukuma au mngoni kukitumia, na ndio sababu wamasai (SIO WABANTU)wengi kiswahili kinawapa shida!

Sasa basi leo hii kutaka kupindua Kiswahili na kuleta kiingereza ni kujidanganya kwani kamwe hakitaweza kukubalika na kupenya jinsi kiswahili kilivyopenya na sababu ni kwamba kiingereza ni lugha nyingine kabisa, na ndio maana nikakupa mifano ya nchi za kiafrika ambazo zimefanya hayo (sio kwa idhini yao) mnayosema na matokeo yake sio mazuri, siandiki kutoka HEWANI, kinachotokea ni hivi kwa sababu kiingereza ni lugha nyingine tofauti inabaki kuwa ya elite tu na ndio maana ukienda Kenya watu wa kawaida wanaongea kitu wanachokiita "sheng" (mchanganyiko wakila kitu) Nigeria, ghana & co. wanatumia Pidgin English, umeshajiuliza kwa nini?

Sasa kama sisi tumefanikiwa ni kwa nini unataka turudi nyuma badala ya kwenda mbele? Tuna Lugha tayari ambayo ina nafasi yake Duniani, inafundishika, iko "standardised" na ndio maana unaweza kusema fulani anaongea kiswahili kibaya na hiyo sio kazi ndogo kufika hapo!

Mwisho umaskini wetu hausabishwi hata tone na Kiswahili bali mambo mengine kabisa!


Baada ya utetezi huo, Watoto wako wansoma shule gani?
 
Back
Top Bottom