Kuhusu Muungano, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Adai ni Zanzibar Pekee iliyopoteza Sovereignty, Je Yuko Sahihi?

Eti Zanzibar ina rais wake.Rais gani asyetambuliwa popote duniani? labda kidogo Oman na UAE ndio huwa wanampa hadhi huyo rais wa Zanzibar.Huyo Shein ameshashiba ndio maana anatetea huu utumbo .Hadhi ya Zanzibar itarudi tu iwapo Tanganyika itarudisha utanganyika wake maana iaonekana Tanganyika ndio Tanzania na Zanzibar sio Tanzania.Hata uanachama wa FIFA zanzibar imekataliwa inatambuliwa Tanzania tu TFF lakini wazanzibar hawaruhusiwi kugombea TFF wanaambiwa yenu ni ZFF ,wakati FIFA inasema waende kama TFF ya Tanzania maana zanzibar sio nchi


Watanganyika na sisi tunataka Rais wa serikali yetu na muondo wenye hazi sawa na huu SMZ hivyo tu. Khalafu huyu Rais wa JMT aendelee na majukumu yake ya JMT.
 
Wanabodi
Wale wenye access na Plus TV, watch now kipindi cha Uso kwa Uso, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman asema uongo wa wazi wa mchana kweupe kuhusu muungano wetu.

Masoud Masoud anadanganya uongo kuwa eti tulipoungana, ile 1964, ni nchi moja tuu ya Zanzibar, ndio pekee iliyopoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa serikali ya Tanganyika, lakini Tanganyika haikupoteza sovereignity yake, kitu ambacho sii kweli.

Ukweli ni kuwa, tulipoungana nchi zote mbili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, nchi zote mbili zilipoteza sovereignity zake, kwa Zanzibar kupoteza sovereignity yake na Tanganyika pia ikapoteza sovereignity yake, tukaunda nchi moja mpya ya Tanzania. Nchi ya Zanzibar haipo na nchi ya Tanganyika pia haipo, kilichopo ni nchi moja mpya ya JMT, ambayo ina sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Mimi sitatizwi na uongo wowote wa kawaida ambao hauna madhara, lakini uongo mkubwa kama huu, kuhusu muungano wetu adhimu, na kutoka kwa mtu mwenye cheo kikubwa kama hiki, aliyekuwa mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, huu ni uongo wenye madhara makubwa kwa mustakabali mwema wa muungano wetu. Uongo kama huu una kitu kinachoitwa "ill motives" kwenye "the reasons or motivés behind" Jee lengo la uongo huu ni nini?.

Wakati wa Bunge la Katiba, niliwahi kutoa angalizo hili kuhusu mtu huyu
na kweli Dr. Shein alimshughulikia.

Muungano wetu ni muungano wa nchi mbili zenye hadhi sawa sawa, hakuna mkubwa wala mdogo, ndani ya muungano Tanganyika na Zanzibar ziko sawa sawa na zote mbili zilipoteza sovereignity zake na kuikabidhi kwa serikali ya JMT.

Muungano wetu ni aina ya muungano very unique duniani, kimataifa muungano wetu ni union wa nchi mbili zimeungana na kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, ni taifa moja, ni dola moja yenye rais mmoja, rais wa JMT ambaye ni Samia. Pia tuna Amiri Jeshi Mkuu mmoja tuu. Kimataifa Zanzibar sio nchi, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ndani ya muungano, muungano wetu ni muungano wa nchi mbili, yaani federation, hivyo ndani ya muungano, Zanzibar ni nchi, yenye rais wake, serikali yake, ina katiba yake, ambayo mabadiliko yaliyofanywa 2010 kuunda SUK, hayatambuliwi na katiba ya JMT. Kwa vile ndani ya muungano Zanzibar ina mamlaka yake huru bila kuingiliwa na serikali ya JMT, la katiba hiyo ni kwa ajili ya mambo yake ya ndani, japo katiba hiyo iko kinyume cha katiba ya JMT, lakini kwa vile ni ya ndani ya Zanzibar,

Kwa upande wa GNU au SUK,
ni serikali ya coalition. Kwenye coalition zote kuna the majority na a minority. A minority ndani ya coalition anatekeleza sera za à majority. Hivyo Viongozi wa ACT ndani ya serikali ya SUK ya Zanzibar, wanatekeza sera CCM.

Hivyo Viongozi wote wa ACT Wazalendo waliomo ndani ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar wanapaswa kuhubiri na kutekeleza sera za CCM, hivyo hata wanapoalikwa popote kwenye public, watatanguliza maslahi ya Zanzibar kwa mujibu wa sera za chama tawala.

Sasa mtu huyu ndio yuko ndani ya nyumba, yuko jikoni kabisa, asipothibitiwa, amini usiamini, amini nawaambieni akija tokea kufika kule juu kileleni, very soon, tutagawana fito!.

Paskali
Kuna hatari siku watu watachoka kuvumiliana kwenye mfumo wa serikali ya umoja wa kitaifa zanzibar. Unakuta kiongozi mkubwa makamu wa kwanza wakati wote ana maoni ya kuudhi au kama huyo masudi saa zote anapinga muungano na anafanya mambo tofauti na sheria na taratibu. Amekua anaingilia mara kwa mara shughuli ya serikali ya muungano mambo ya nje kwa kutuma salamu kama zanzibar kwa viongozi wa dola za nje.
 
Tanganyika ipo na imevaa au kujivalisha ngozi ya kondoo.

Inakuwaje Almasi na Dhanabu hazipo katika mahesabu ya Muungano.......ila mafuta yaliopo kizani ni ya Muungano. Wahafidhina mnaofaidika na upigaji katika Muungano ,leteni jawabu inakuwaje Almasi ni huko huko tu ?
Hakuna Muungano kuna kizungunkuti.
Wajinga walikuwepo Zamani- Mzanzibari mkaazi hivi yupo Mtanzania Mkaazi Huko ??
 
WaZanzibari wapo pamoja isipokuwa vibaraka ,sijui vibaraka maana yake nini ? Ila one day Yes the Voice of Zanzibarians will be heard everywhere.
 
Tanganyika ipo na imevaa au kujivalisha ngozi ya kondoo.

Inakuwaje Almasi na Dhanabu hazipo katika mahesabu ya Muungano.......ila mafuta yaliopo kizani ni ya Muungano. Wahafidhina mnaofaidika na upigaji katika Muungano ,leteni jawabu inakuwaje Almasi ni huko huko tu ?
Hakuna Muungano kuna kizungunkuti.
Wajinga walikuwepo Zamani- Mzanzibari mkaazi hivi yupo Mtanzania Mkaazi Huko ??

Mafuta mliambiwa Zanzibar mfanye tafiti na mchimbe mafuta yenu. Sijui kwa nini hamtoi mrejesho mmefikia wapi? Msigwa wa habari maelezo aliahidi kuleta mtaalamu wa kero za muungano. Atakapo mleta na amini atatolea ufafanuzi huu wa hii hazina ya raslimsli ya mafuta yenu Wazanzibari.
 
Tanganyika ipo na imevaa au kujivalisha ngozi ya kondoo.

Inakuwaje Almasi na Dhanabu hazipo katika mahesabu ya Muungano.......ila mafuta yaliopo kizani ni ya Muungano. Wahafidhina mnaofaidika na upigaji katika Muungano ,leteni jawabu inakuwaje Almasi ni huko huko tu ?
Hakuna Muungano kuna kizungunkuti.
Wajinga walikuwepo Zamani- Mzanzibari mkaazi hivi yupo Mtanzania Mkaazi Huko ??
Mkuu Shocker , sijui mwenzetu unaishi kwenye karne ya ngapi, gesi na mafuta viliishatolewa kwenye mambo ya muungano, hivyo Zanzibar iko huru kuchimba hayo mafuta yake ya kwenye kinibu, ila mafuta ya kwenye bahari ni mali ya muungano. Kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, ndani ya Tanzania hakuna mpaka wa nchi nyingine yoyote iitwayo Zanzibar, bali Zanzibar ni sehemu ya JMT.
P
 
MPE walau heshima take ya Umakamu was Rais.

Ficha chuki zako binafsi. Hebu pitia tena hayo maandishi yako, yahakiki vizuri wewe in mwandishi Mkongwe uone ulivyotumia maneno ya kubeza.

Nadhani umenielewa
Sawia mkuu. Huyu anaheshima yake halafu ni mwanasheria mbobezi sasa Pascal anamkejeli!!!!!!!!! Huwa nashaka na uelewa wa Pascal vilevile.
 
Ndio maana tuna wazanzibari katika bunge la Tanganyika? Ndio maana tuna mawaziri wazanzibari katika wizara za Tanganyika? Mnafik ni wewe. Na uliyejaa chuki dhidi ya kile unachokiita Tanganyika ni wewe. Ni haki gani ambayo mzanzibari ananyimwa katika serikali ya Tanganyika? Wakati huo huo kuna haki kibao mtanganyika hanazo huko Zanzibar lakini bado unalia na kumuita mtanganyika mbaguzi na mwenye chuki dhidi yenu! Hivi mnatuita machogo kwa sababu mnatupenda sana?

Wewe ni mnafik mkubwa uliye chuki. Ubaya ni kuwa kuna watanganyika wana entertain chuki na unafik wenu kiasi kwamba hamtaki kuambiwa ukweli.

Amandla....
Sawa kabisa uliyosema. Kuanzia jina, bado kuna nchi inayoitwa Zanzibar yenye Rais, mawaziri, bendera na wimbo wa taifa, na kila kitu kinachoashiria serikali, kama vile bunge. Lakini thubutu kutaja 'Tanganyika' kwa maana ya nchi ya zamani iliyokuwa ikiitwa hivyo, utachukuliwa kuwa una yako ambayo si mazuri kwa nchi. Tanzania imekuwa na marais wawili kutoka Zanzibar: Mwinyi na Samia. Mawaziri kibao na kwa wafanyakazi wa kawaida hao ndio usiseme. Huku bara mtu anaweza kukuuliza unatoka wapi ukasema Zanzibar na hiyo itachukuliwa sawa na yule anayejibu anatoka Kigoma au Songea. Hakuna cha kushangaa kwa kuwa hakuna nchi 'Tanganyika'. Lakini jee mtu wa Bara anaweza kuwa Rais, au waziri, au mbunge wa Zanzibar? Hiyo haiwezekani kabisa. Mfanyakazi wa kawaida tu wa serikali anasumbuliwa sana kufanya kazi Zanzibar. Nawafahamu wenzagu wawili waliowahi kufanya Zanzibar. Wanasema walikuwa wakihojiwa sawa na Mkenya au mtu wa taifa jingine. Kwa hiyo ukweli ni kwamba Tanganyika ndiyo ilikufa lakini Zanzibar ilibakia.
 
Kwa mujibu wa katiba ya JMT, Tanzania ni nchi moja ya Jamhuri ya Muungano. Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT.
Mkuu Pascal, kwa nia ya kujifunza naomba unielekeze;

Umesema Z'bar ni sehemu ya JMT, nakubali, hata Shinyanga ni sehemu ya JMT, kadhalika Gairo na kwingineko. Kila sehemu ya JMT inatambuliwa kwa jina la mfumo kiutawala, haiitwi tu sehemu ya JMT. Kuna mikoa, wilaya n.k

Z'bar kwa kuwa si nchi na ni sehemu ya JMT, naomba utambulisho wake kiutawala.
 
Sio kuwa ni Viongozi wa JMT hawawatambui Viongozi wa SUK, no Viongozi wanawatambua na wamewekewa hadi protocal yao wawapo huku Bara, ila katiba ya JMT ndio haiyatambui mabadiliko ya katiba ya Zanzibar ya 2010 yaliyo unda SUK kwasababu mabadiliko hayo yanakwenda kinyume cha katiba ya JMT.

Kwa mujibu wa katiba ya JMT, Tanzania ni nchi moja ya Jamhuri ya Muungano. Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT.

Kwa mujibu katiba ya Zanzibar, Tanzania ni Jamhuri ya Muungano wa nchi 2. Zanzibar ni moja ya nchi hizo mbili zinazounda JMT.

Hivyo kwa katiba ya JMT, nchi ni moja tuu, JMT, Zanzibar sio nchi, bali ni sehemu ya JMT. Lakini
kwa katiba ya Zanzibar, Tanzania ni nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar, hivyo Zanzibar ni nchi.

Viongozi wa SUK wanatambuliwa ki protokali tuu lakini ndani ya katiba ya JMT, hawatambuliwi.
P
Serikali ya SMZ siyo jambo la Muungano.
Katiba yako ya JMT ilicheza ngoma isiyo yake kuweka muundo wa SMZ ndani yake, Ndiyo maana Wazenji hawakujali kuwa katiba ya JMT inatambua muundo wa zamani wa SMZ wa uwepo wa waziri kiongozi huko Zenji wao wakaweka makamu wawili wa rais instead.

Ndiyo maana tunataka katiba mpya ambayo inaondoa dicrepancies hizi otherwise ni kichekesho katiba mama itambue muundo wa SMZ ambao haupo, ushabadilishwa tayari na wazanzibar wenyewe.
 
Mkuu Pascal, kwa nia ya kujifunza naomba unielekeze;

Umesema Z'bar ni sehemu ya JMT, nakubali, hata Shinyanga ni sehemu ya JMT, kadhalika Gairo na kwingineko. Kila sehemu ya JMT inatambuliwa kwa jina la mfumo kiutawala, haiitwi tu sehemu ya JMT. Kuna mikoa, wilaya n.k

Z'bar kwa kuwa si nchi na ni sehemu ya JMT, naomba utambulisho wake kiutawala.
Kama ulinisoma vyema kule mwanzo, nimesema muungano wetu ni very unique, ni muungano wa union kwa upande mmoja wa kimataifa na ni muungano wa federation kwa upande wa pili ndani ya muungano.

Hivyo japo Zanzibar sio nchi, haina sovereignity yake, haina dola, haina sarafu, haina mipaka ya kimataifa, haina Jeshi, haina polisi lakini ina autonomy yake kwa mambo yake ya ndani yasiyo ya muungano.

P
 
Wanabodi,

Wale wenye access na Plus TV, watch now kipindi cha Uso kwa Uso, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman asema uongo wa wazi wa mchana kweupe kuhusu muungano wetu.

Mhe. Masoud anadanganya uongo wa wazi mchana kweupe kuwa Tanganyika na Zanzibar tulipoungana, ile 1964, ni nchi moja tuu ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, ndio pekee iliyopoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Jamhuri ya Tanganyika, lakini Tanganyika haikupoteza sovereignity yake, bali Tanganyika ilibadili tuu jina kutoka Tanganyika kugeuka Tanzania with its sovereignity, kitu ambacho sii kweli!.

Kiukweli kabisa Tanzania tunahitaji sana civic éducation kuhusu huu muungano wetu, hata baadhi ya Viongozi wetu hawaujui vizuri muungano wetu hivyo wanapotosha watu bure.

Msingi mkuu wa muungano wetu ni dhima, kuwa sisi Watanzania ni wamoja. Dhima hiyo ndio ikatumiwa na Nyerere na Karume kuasisi huu muungano uliopo hadi leo. Hivyo anapoibika kiongozi yeyote kutaka kuipotosha hii Dhima, Wazalendo tuliopo tunaoujua ukweli huu hatuwezi kunyamaza !.

Ukweli ni kuwa, tulipoungana nchi zote mbili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, nchi zote mbili zilipoteza sovereignity zake, kwa Zanzibar kupoteza sovereignity yake na Tanganyika pia ikapoteza sovereignity yake, tukaunda nchi moja mpya ya Tanzania. Nchi ya Zanzibar haipo na nchi ya Tanganyika pia haipo, kilichopo ni nchi moja mpya ya JMT, ambayo ina sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Mimi sitatizwi na uongo wowote wa kawaida ambao hauna madhara, lakini uongo mkubwa kama huu, kuhusu muungano wetu adhimu, na kutoka kwa mtu mwenye cheo kikubwa kama hiki, aliyekuwa mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, huu ni uongo wenye madhara makubwa kwa mustakabali mwema wa muungano wetu. Uongo kama huu una kitu kinachoitwa "ill motives" kwenye "the reasons or motivés behind" Jee lengo la uongo huu ni nini?.

Wakati wa Bunge la Katiba, niliwahi kutoa angalizo hili kuhusu mtu huyu
na kweli Dr. Shein alimshughulikia.

Muungano wetu ni muungano wa nchi mbili zenye hadhi sawa sawa, hakuna mkubwa wala mdogo, ndani ya muungano Tanganyika na Zanzibar ziko sawa sawa na zote mbili zilipoteza sovereignity zake na kuikabidhi kwa serikali ya JMT.

Muungano wetu ni aina ya muungano very unique duniani, kimataifa muungano wetu ni union wa nchi mbili zimeungana na kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, ni taifa moja, ni dola moja yenye rais mmoja, rais wa JMT ambaye ni Samia. Pia tuna Amiri Jeshi Mkuu mmoja tuu. Kimataifa Zanzibar sio nchi, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ndani ya muungano, muungano wetu ni muungano wa nchi mbili, yaani federation, hivyo ndani ya muungano, Zanzibar ni nchi, yenye rais wake, serikali yake, ina katiba yake, ambayo mabadiliko yaliyofanywa 2010 kuunda SUK, hayatambuliwi na katiba ya JMT. Kwa vile ndani ya muungano Zanzibar ina mamlaka yake huru bila kuingiliwa na serikali ya JMT, la katiba hiyo ni kwa ajili ya mambo yake ya ndani, japo katiba hiyo iko kinyume cha katiba ya JMT, lakini kwa vile ni ya ndani ya Zanzibar,

Kwa upande wa GNU au SUK,
ni serikali ya coalition. Kwenye coalition zote kuna the majority na a minority. A minority ndani ya coalition anatekeleza sera za à majority. Hivyo Viongozi wa ACT ndani ya serikali ya SUK ya Zanzibar, wanatekeza sera CCM.

Hivyo Viongozi wote wa ACT Wazalendo waliomo ndani ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar wanapaswa kuhubiri na kutekeleza sera za CCM, hivyo hata wanapoalikwa popote kwenye public, watatanguliza maslahi ya Zanzibar kwa mujibu wa sera za chama tawala.

Sasa mtu huyu ndio yuko ndani ya nyumba, yuko jikoni kabisa, asipothibitiwa, amini usiamini, amini nawaambieni akija tokea kufika kule juu kileleni, very soon, tutagawana fito!.

Paskali
Kasema Uongo wapii na ukweli hamtaki wabara ,wewe na OMO ww ndio msomi zaidi kushinda OMO ebu wacha kuwashwa washwa Paskali.
 
Sawia mkuu. Huyu anaheshima yake halafu ni mwanasheria mbobezi sasa Pascal anamkejeli!!!!!!!!! Huwa nashaka na uelewa wa Pascal vilevile.
Sijamkejeli nimesema amesema uongo. Kwanini kiongozi Mkuu wa nchi kati ya wale Viongozi wetu wakuu 6 wa kitaifa waseme uongo ?. Ukiishakuwa ndani ya serikali, unafungwa na kifungo cha a Collective responsibiliy clause. Huwezi kuuzungumza uongo mkubwa hivi Wazalendo tukanyamaza. Mkuu huyu anahitaji semina elekezi.
P
 
Kasema Uongo wapii na ukweli hamtaki wabara ,wewe na OMO ww ndio msomi zaidi kushinda OMO ebu wacha kuwashwa washwa Paskali.
Mkuu mfufuka, Resurrection , hapa hatuzungumzii usomi wa mtu, zungumzia hoja iliyopo mezani usilete mipasho. Tanganyika na Zanzibar zilipoungana na kuunda Tanzania, nchi zote mbili zilipoteza sovereignity zake. Sii kweli iliyopoteza ni nchi moja tuu ya Zanzibar.

Mtu unaweza usiwe msomi na ukawa na hoja mujarab kuliko Wasomi.

P
 
Brother hebu achana na mambo yaliyoko kwenye makaratasi fikiria hili swala la muungano kwakutumia fikra na utashi wako alafu jiulize je yanayofanyika nakutendwa kwa pande zote mbili ndivyo ilivyo na inavyopaswa kua au kuna walakini unaolindwa kwa nguvu ya dola na wanasiasa wanufaika?.
 
Dawa ya jambo hili ni maamuzi magumu yafuatayo: Kutoa notisi ya siku 90 wazanzibara wote walioko ZANZIBAR warudi Tanzania bara, na Wazanzibari wote walioko Tanzania bara warudi wZanzibar!!. Kila sehemu ya Jamhuri ya Muungano ione itawahifadhi vipi watu wao. Baada ya siku hizo 90, itolewe notisi ya siku 90 ya kutafakari, siku hizi zikiisha iitishwe kura ya maoni Tanzania bara na kule Zanzibar watu waamue aidha kuuvunja muungano au kuuimarisha kwa kuwa na nchi moja ya Tanzania yenye serikali moja tu! Hakuna cha serikali ya Zanzibar kama ilivyo hakuna serikali ya Tanganyika!! Matokeo ya kura hiyo yaheshimiwe!! Tanzania visiwani iwe mikoa miwili tu ya Tanzania!!
Hawa wazenji wametuchosha!! Wapemba wamejaa kila kona ya Tanzania bara lakini hawaridniki !! Waondoke warudi kwao!!!
 
Mkuu Shocker , sijui mwenzetu unaishi kwenye karne ya ngapi, gesi na mafuta viliishatolewa kwenye mambo ya muungano, hivyo Zanzibar iko huru kuchimba hayo mafuta yake ya kwenye kinibu, ila mafuta ya kwenye bahari ni mali ya muungano. Kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, ndani ya Tanzania hakuna mpaka wa nchi nyingine yoyote iitwayo Zanzibar, bali Zanzibar ni sehemu ya JMT.
P
Na alimasi na dhahabu ni ya kinanani,mbona mnaibania ndio muungano huo,eti kwenye bahari ni ya Muungano , Sasa niwaulize mnaogopa nini kuwa na Tanganyika yenu ?
Sijawahi kusikia jibu mlikurupuka miaka ya Baba haambiliki kisha mkaufyata,mnaona aibu kuwa na Tanganyika ? Au mnaogopa KuCongoana au KuSudaniana.

Kigoma kwake Mtwara kwake ndivyo mnavyowadanganya watu ili muzidi kuchomeka mirija,maana ukiangalia Tz kama hakuna wanaomaliza vyuo,kuna watu tokea tupate Uhuru wanazeekea ndani ya serikali na kurithishana.
 
Back
Top Bottom