Kuhusu Muungano, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Adai ni Zanzibar Pekee iliyopoteza Sovereignty, Je Yuko Sahihi?

Aliyesema kuwa watapewa mafuta na Oman ni mzanzibari sio mimi. Na ni kitu gani kinachowazuia wa Omani kuwamegea utajiri sasa hivi kama ambavyo wanawamegea waomani wenzao?
Unaposema kuwa Muungano umeshindwa kuwaletea faida Wazanzibari una maana kuwa mlitegemea watanganyika ndio wangewapelekea maendeleo? Shule, hospitali zote ziko chini ya serikali yao, JMT inahusika vipi? Kama wameuchoka kwa sababu walitegemea watanganyika wawabebe basi bora wauvunje watafute mjomba wa kuwabeba. Wazanzibari wanatakiwa wajitathmini wenyewe ili wajue wapi wanakosea. Waunguja wapime athari za kuwaminya wapemba kwa uchumi wao halafu wajirekebishe. Unadhani wapemba wamewekeza Bara kwa sababu wanawapenda sana machogo? La hasha, walifanya hivyo baada ya kunyimwa fursa na wazanzibari wenzao. Wazanzibari wajitahidi kujenga nchi yao wenyewe kama ambavyo Singapore na Mauritius walivyofanya. Wakiendelea wao na sisi tutaendelea ndio maana hatufurahii umasikini wao.

Amandla...
 
Wanabodi,

Wale wenye access na Plus TV, watch now kipindi cha Uso kwa Uso, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman asema uongo wa wazi wa mchana kweupe kuhusu muungano wetu.

Mhe. Masoud anadanganya u kuwa Tanganyika na Zanzibar tulipoungana, ile 1964, ni nchi moja tuu ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, ndio pekee iliyopoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Jamhuri ya Tanganyika, lakini Tanganyika haikupoteza sovereignity yake, bali Tanganyika ilibadili tuu jina kutoka Tanganyika kugeuka Tanzania with its sovereignity, kitu ambacho sii kweli!.

Kiukweli kabisa Tanzania bado tunahitaji sana civic éducation kuhusu huu muungano wetu, hata kwa baadhi ya Viongozi wetu, hawaujui vizuri huu muungano wetu hivyo wanapotosha bure watu wao na umma kwa ujumla.

Msingi mkuu wa muungano wetu ni dhima, kuwa sisi Watanzania ni ndugu moja, sisi ni wamoja, hivyo muungano ni kurudisha tuu asili yetu iliyotenganishwa na wakoloni. Dhima hiyo ndio ikatumiwa na Nyerere na Karume kuasisi huu muungano uliopo hadi leo. Hivyo anapoibuka kiongozi yeyote kutaka kuipotosha hii Dhima, Wazalendo tuliopo tunaoujua ukweli huu hatuwezi kunyamaza !.

Ukweli ni kuwa, tulipoungana ile 1964, nchi zote mbili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, nchi zote mbili zilipoteza sovereignity zake, kwa Zanzibar kupoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Tanzania, la Tanganyika pia sio tuu ikapoteza sovereignity yake, bali hadi jina lake la Tanganyika na kuikabidhi kwa Tanzania. Tukaunda taifa moja jipya la Tanzania lenye nchi mbili ndani yake na zote hazina sovereignity zake. Nchi iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ikawa haipo tena na nchi ya Jamhuri ya Tanganyika pia ikawa haipo, kilichopo ni nchi moja mpya ya JMT, ambayo ina sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Mimi sitatizwi na uongo wowote wa kawaida ambao hauna madhara, lakini uongo mkubwa kama huu, kuhusu muungano wetu adhimu, na kutoka kwa mtu mwenye cheo kikubwa kama hiki, aliyekuwa mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, huu ni uongo wenye madhara makubwa kwa mustakabali mwema wa muungano wetu. Uongo kama huu una kitu kinachoitwa "ill motives" kwenye "the reasons or motivés behind" Jee lengo la uongo huu ni nini?.

Wakati wa Bunge la Katiba, niliwahi kutoa angalizo hili kuhusu mtu huyu
na kweli Dr. Shein alimshughulikia.

Muungano wetu ni muungano wa nchi mbili zenye hadhi sawa sawa, hakuna mkubwa wala mdogo, ndani ya muungano Tanganyika na Zanzibar ziko sawa sawa na zote mbili zilipoteza sovereignity zake na kuikabidhi kwa serikali ya JMT.

Muungano wetu ni aina ya muungano very unique duniani, kimataifa muungano wetu ni union wa nchi mbili zimeungana na kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, ni taifa moja, ni dola moja yenye rais mmoja, rais wa JMT ambaye ni Samia. Pia tuna Amiri Jeshi Mkuu mmoja tuu. Kimataifa Zanzibar sio nchi, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ndani ya muungano, muungano wetu ni muungano wa nchi mbili, yaani federation, hivyo ndani ya muungano, Zanzibar ni nchi, yenye rais wake, serikali yake, ina katiba yake, ambayo mabadiliko yaliyofanywa 2010 kuunda SUK, hayatambuliwi na katiba ya JMT. Kwa vile ndani ya muungano Zanzibar ina mamlaka yake huru bila kuingiliwa na serikali ya JMT, la katiba hiyo ni kwa ajili ya mambo yake ya ndani, japo katiba hiyo iko kinyume cha katiba ya JMT, lakini kwa vile ni ya ndani ya Zanzibar,

Kwa upande wa GNU au SUK,
ni serikali ya coalition. Kwenye coalition zote kuna the majority na a minority. A minority ndani ya coalition anatekeleza sera za à majority. Hivyo Viongozi wa ACT ndani ya serikali ya SUK ya Zanzibar, wanatekeza sera CCM.

Hivyo Viongozi wote wa ACT Wazalendo waliomo ndani ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar wanapaswa kuhubiri na kutekeleza sera za CCM, hivyo hata wanapoalikwa popote kwenye public, watatanguliza maslahi ya Zanzibar kwa mujibu wa sera za chama tawala.

Sasa mtu huyu ndio yuko ndani ya nyumba, yuko jikoni kabisa, asipothibitiwa, amini usiamini, amini nawaambieni akija tokea kufika kule juu kileleni, very soon, tutagawana fito!.

Paskali

Pascal si wende ukamshitaki mahakamani ??? Hujachelewa nenda mahakamani ukamdhibiti usimwage povu hapa JF la kutafutia upewe tonge ya ugali

 
Huyu nae makamu asituchanganye,basi Kama anakosa usngz na hiyo soveregnity yao ,si aitafute iikopotelea!!asituchanganye hapa na harakati za kusaka uongoz wa juu wa zbr,
 
Kuna Mquebec aliwahi kuuwawa , kunajisiwa kuchukuliwa mali yake , kujeruhiwa kwa risasi na Mcanada yeyote ??

Nadhani nyinyi watanganyika mjifunze kuwa huu si muungano ni uvamizi wa Tanganyika kwa Zanzibar.
Hebu tuambie waunguja na wapemba wangapi wamenajisiwa, kuchukuliwa mali zao, na kuuawa kwa risasi na watanganyika? Halafu niambie wangapi walifanyiwa yote hayo wakati wa Mapinduzi na chini ya utawala wa Hayati Karume? Aidha, niambie wakati hao watanganyika wanafanya huo unyama nani alikuwa Rais wa Zanzibar? Mwisho niambie mtanganyika yupi alifuta matokeo ya uchaguzi wenu mwaka 2015, na aliyeharibu uchaguzi wenu wa hivi karibuni.
Hampendani lakini kwa unafik wenu mnataka kutulaumu machogo kwa chuki zenu.

Amandla...
 
Wanabodi,

Wale wenye access na Plus TV, watch now kipindi cha Uso kwa Uso, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman asema uongo wa wazi wa mchana kweupe kuhusu muungano wetu.

Mhe. Masoud anadanganya u kuwa Tanganyika na Zanzibar tulipoungana, ile 1964, ni nchi moja tuu ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, ndio pekee iliyopoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Jamhuri ya Tanganyika, lakini Tanganyika haikupoteza sovereignity yake, bali Tanganyika ilibadili tuu jina kutoka Tanganyika kugeuka Tanzania with its sovereignity, kitu ambacho sii kweli!.

Kiukweli kabisa Tanzania bado tunahitaji sana civic éducation kuhusu huu muungano wetu, hata kwa baadhi ya Viongozi wetu, hawaujui vizuri huu muungano wetu hivyo wanapotosha bure watu wao na umma kwa ujumla.

Msingi mkuu wa muungano wetu ni dhima, kuwa sisi Watanzania ni ndugu moja, sisi ni wamoja, hivyo muungano ni kurudisha tuu asili yetu iliyotenganishwa na wakoloni. Dhima hiyo ndio ikatumiwa na Nyerere na Karume kuasisi huu muungano uliopo hadi leo. Hivyo anapoibuka kiongozi yeyote kutaka kuipotosha hii Dhima, Wazalendo tuliopo tunaoujua ukweli huu hatuwezi kunyamaza !.

Ukweli ni kuwa, tulipoungana ile 1964, nchi zote mbili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, nchi zote mbili zilipoteza sovereignity zake, kwa Zanzibar kupoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Tanzania, la Tanganyika pia sio tuu ikapoteza sovereignity yake, bali hadi jina lake la Tanganyika na kuikabidhi kwa Tanzania. Tukaunda taifa moja jipya la Tanzania lenye nchi mbili ndani yake na zote hazina sovereignity zake. Nchi iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ikawa haipo tena na nchi ya Jamhuri ya Tanganyika pia ikawa haipo, kilichopo ni nchi moja mpya ya JMT, ambayo ina sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Mimi sitatizwi na uongo wowote wa kawaida ambao hauna madhara, lakini uongo mkubwa kama huu, kuhusu muungano wetu adhimu, na kutoka kwa mtu mwenye cheo kikubwa kama hiki, aliyekuwa mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, huu ni uongo wenye madhara makubwa kwa mustakabali mwema wa muungano wetu. Uongo kama huu una kitu kinachoitwa "ill motives" kwenye "the reasons or motivés behind" Jee lengo la uongo huu ni nini?.

Wakati wa Bunge la Katiba, niliwahi kutoa angalizo hili kuhusu mtu huyu
na kweli Dr. Shein alimshughulikia.

Muungano wetu ni muungano wa nchi mbili zenye hadhi sawa sawa, hakuna mkubwa wala mdogo, ndani ya muungano Tanganyika na Zanzibar ziko sawa sawa na zote mbili zilipoteza sovereignity zake na kuikabidhi kwa serikali ya JMT.

Muungano wetu ni aina ya muungano very unique duniani, kimataifa muungano wetu ni union wa nchi mbili zimeungana na kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, ni taifa moja, ni dola moja yenye rais mmoja, rais wa JMT ambaye ni Samia. Pia tuna Amiri Jeshi Mkuu mmoja tuu. Kimataifa Zanzibar sio nchi, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ndani ya muungano, muungano wetu ni muungano wa nchi mbili, yaani federation, hivyo ndani ya muungano, Zanzibar ni nchi, yenye rais wake, serikali yake, ina katiba yake, ambayo mabadiliko yaliyofanywa 2010 kuunda SUK, hayatambuliwi na katiba ya JMT. Kwa vile ndani ya muungano Zanzibar ina mamlaka yake huru bila kuingiliwa na serikali ya JMT, la katiba hiyo ni kwa ajili ya mambo yake ya ndani, japo katiba hiyo iko kinyume cha katiba ya JMT, lakini kwa vile ni ya ndani ya Zanzibar,

Kwa upande wa GNU au SUK,
ni serikali ya coalition. Kwenye coalition zote kuna the majority na a minority. A minority ndani ya coalition anatekeleza sera za à majority. Hivyo Viongozi wa ACT ndani ya serikali ya SUK ya Zanzibar, wanatekeza sera CCM.

Hivyo Viongozi wote wa ACT Wazalendo waliomo ndani ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar wanapaswa kuhubiri na kutekeleza sera za CCM, hivyo hata wanapoalikwa popote kwenye public, watatanguliza maslahi ya Zanzibar kwa mujibu wa sera za chama tawala.

Sasa mtu huyu ndio yuko ndani ya nyumba, yuko jikoni kabisa, asipothibitiwa, amini usiamini, amini nawaambieni akija tokea kufika kule juu kileleni, very soon, tutagawana fito!.

Paskali
Huu ni uchochezi wa kwango cha SGR.

Unapo mtaja makamu wa rais wa zanzibar pekee kuwa ni muongo wakati ndani ya ccm ndiyo kiwanda cha waongo.
 

Ni haki yake kuzungumza atakacho. Lakini kwa nini asubiri mpaka mtanganyika amvue koti badala ya kulivua mwenyewe wakati linambana kwa miaka 57? Mmo kwenye serikali ya Muungano ambayo mnasema imeumbwa kuidhibiti Zanzibar lakini mnaishia kuwaomba watanganyika wawape talaka? Mnadai mmepigwa, mmeuawa, mmedhulumiwa katika uchaguzi uliopita lakini hamkusita kujiunga na serikali iliyotokana na uchaguzi huo? Leo Chadema inapambana kudai Katiba Mpya ambayo itazungumzia hayo mnayolalamikia lakini mmekaa pembeni mnawaangalia!

Quebec, Scotland na Catalonia walipoona wanaonewa katika mfumo uliokuwepo waliweka wazi agenda ya kujitoa katika Muungano wao na wakapigania. Nyinyi mnashindwa nini? Hasa kwa sababu mnajua Muungano wenyewe hauna uhalali kwa sababu hamjau ratify? Acheni kupambana na machogo. Washikeni wanasiasa wenu ili waanze juhudi za kuvunja muungano ambao hauna faida kabisa kwenu.

Amandla...
 
Nisome vizuri. Sijasema Oman ni nchi maskini. Nimesema nchi kuwa na GDP per Capita kubwa haina maana wananchi wake wote wana maisha bora.
Kwa mantik yako, watanganyika wengi wanajuta kupata uhuru maana wangekuwa bado sehemu ya empire ya Uingereza maisha yao yangekuwa bora kwa sababu Uingereza ni nchi tajiri.

Mapinduzi yalifanyika kwa sababu ya dhulma ambayo baadhi ya wazanzibari ( pamoja na waarabu wa Umma) waliona watawala wao wenye damu ya kiomani walikuwa wanawatendea. Wanaosema kuwa maisha yalikuwa bora chini ya usultani ni wale tu waliofaidika nao na sio wale waliokuwa wanahesabiwa kama watwana.

Amandla...
GDP per Capita ni kipimo cha uchumi na ni kipimo kinachotumiwa hata na Benki ya dunia. Uchumi ambao unasema ni moja la jukumu la serikali ya JMT kusimamia halafu imeshindwa kutokana na umasikini uliopo.

Sababu za mapinduzi ziko nyingi, nyingine hizi hapa

 
Naona mazuzu mnapongezana
Ni vigumu kutambua idadi ya watu wenye mafaili kule hospitali ya Milembe waliopo hapa jukwaani. Lakini kwa kuwa visa vingi vya wangojwa hulipuka katika kipindi cha miezi ya Septemba na Octoba, sioni ajabu kwa mgonjwa wa kwanza kujitokeza hadharani na maoni kama haya.

Ugua pole mkuu, "wishing you quick recovery"
 
Ni vigumu kutambua idadi ya watu wenye mafaili kule hospitali ya Milembe waliopo hapa jukwaani. Lakini kwa kuwa visa vingi vya wangojwa hulipuka katika kipindi cha miezi ya Septemba na Octoba, sioni ajabu kwa mgonjwa wa kwanza kujitokeza hadharani na maoni kama haya.

Ugua pole mkuu, "wishing you quick recovery"
Hiyo habari za mirembe anazijua Ndugaye maana alishajitangaza kuwa anafaili.
 
NB: Kuna mambo ya muungano.

Tanganyika na Zanzibar tuliungana katika mambo hayo tu. Mengine yote nje ya mambo hayo, Zanzibar ni nchi na inajitegemea. Ila Tanganyika (kwa yale yasio ya Muungano) inategemea JMT.

To be honest, muungano wetu ni wa kulazimishana tu. Muundo wake ni wa hovyo (kwa maoni yangu).
 
Hebu tuambie waunguja na wapemba wangapi wamenajisiwa, kuchukuliwa mali zao, na kuuawa kwa risasi na watanganyika? Halafu niambie wangapi walifanyiwa yote hayo wakati wa Mapinduzi na chini ya utawala wa Hayati Karume? Aidha, niambie wakati hao watanganyika wanafanya huo unyama nani alikuwa Rais wa Zanzibar? Mwisho niambie mtanganyika yupi alifuta matokeo ya uchaguzi wenu mwaka 2015, na aliyeharibu uchaguzi wenu wa hivi karibuni.
Hampendani lakini kwa unafik wenu mnataka kutulaumu machogo kwa chuki zenu.

Amandla...
Tumekusikia ,Sasa jibu swali
Kuna MQuebec yupi aliwahi kuuliwa, kunajisiwa ,kuibiwa Na mKanada yeyote?
 
Tumekusikia ,Sasa jibu swali
Kuna MQuebec yupi aliwahi kuuliwa, kunajisiwa ,kuibiwa Na mKanada yeyote?
Mwaka 2019 waquebec 77 waliuawa. Idadi za walio najisiwa hazijulikani maana watu wengi wana ficha. Au unadhani Canada watu hawauawi, kunajisiwa au kuibiwa? Kuwa hayo yanatokea kwenu tu?

Amandla...
 
Asante sana, anayezungumza ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe
Othman Masoud Othman Sharrif sio Makamo wa Pili.

Naombeni sana mnisamehe kuwachanganya hawa Makamo wawili, hivyo vyeo vya Zanzibar ambayo havitambuliki ndani ya katiba ya JMT, vinatuchanganya sana sisi waumini wa supremacy ya Katiba. Kama katiba yetu ya JMT haiwatambui Makamo hawa, who M I nisiwachanganye ?

Mixing is highly regreted. Mode please do the needful.
P
Confusing vs Mixing. Hata hivo Asante kwa andiko murua
 
GDP per Capita ni kipimo cha uchumi na ni kipimo kinachotumiwa hata na Benki ya dunia. Uchumi ambao unasema ni moja la jukumu la serikali ya JMT kusimamia halafu imeshindwa kutokana na umasikini uliopo.

Sababu za mapinduzi ziko nyingi, nyingine hizi hapa


Inakubalika kote kuwa GDP siyo kipimo kamilifu cha hali ya uchumi wa nchi. Kwa mfano mapato yanayotokana na dhahabu yetu yatahesabiwa katika GDP yetu wakati ukweli ni kuwa sehemu kubwa inahamishwa na kupelekwa katika nchi ambako Barrick wana makao yao makuu. Kwa upande mwingine, sehemu kubwa sana ya biashara katika nchi zinazoelendelea sio formal kwa hiyo haziwi reflected katika GDP yake. Kingine ni kuwa remittances ambazo zinaingia nchini kutoka kwa raia wake wanaoishi humo ni nadra kuonekana katika hesabu za GDP. Ndio maana wakaja na GNP ( Gross National Product) kama kipimo sahihi zaidi ya hali ya uchumi wa cnhi. Lakini pamoja na haya, wachumi wakasema takwimu hizi hazireflect ubora wa maisha ya wananchi wanaoishi humo kwa sababu haionyeshi tofauti ya kipato baina ya wakati. K.m. Equatorial Guinea ni zaidi ya dola 34,000.00 lakini sehemu kubwa ya GDP imehodhiwa na watu wachache na sehemu kubwa ya raia wake wana hali duni sana. Mfano kama huo unaonekana Gabon ( Usd 19,266). Raia wa Equatorial Guinea wengi hawana access ya maji safi wakati Rais na ndugu zake wana majumba ya kifahari Marekani na kwengine. GDP per capita imekosolewa kwa kuto reflect thamani ya pesa nchini. Kwa mfano, sarafu inayotumika ni dola lakini kuna tofauti kubwa baina ya nchi ya thamani ya dola moja (vitu na huduma zinazoweza kununuliwa na dola moja) ndio maana kipimo kinachotumika sasa ni GDP PPP ( Purchasing Power Parity). Kwa sababu hiyo dhana ya kusema GDP per Capita ndio kipimo sahihi cha hali ya uchumi katika nchi haikubaliki tena. Inatumika tuu kwa sababu ya urahisi wake na mazoea.

Mimi sikatai kuwa JMT ni masikini. Ninachokipinga ni pale mnapoilaumu JMT kwa umasikini wa pemba na Unguja.

Anachozungumza Bharwani ni kuwa waliopindua ni Afro Shirazi dhidi ya waarabu wa chama cha Hizbu. Hajaeleza kwa nini Afro Shirazi walikuwa na chuki na Hizbu. Anawalaumu Waingereza kwa kuto kutoa ulinzi kwa serikali yao. Hizi ndio chuki ninazozizungumzia. Waarabu mpaka leo hawajawasamehe Afro Shirazi na Afro Shirazi wanahofia makaburi kufufuliwa.. Zanzibar wanatakiwa kuwa na Truth and Reconciliation Commission kuzungumzia historia yao na kuombana msamaha wa dhati badala ya kushinda kuwalalamikia machogo. Bharwani anasema wafuasi wa Afro Shirazi walitumia mishale kuteka arsenal ambayo ilikuwa na silaha. Ninachojiuliza ni kuwa kama walikuwa na silaha kutoka Algeria zilizopitia Dar, kwa nini walitumia mishale?

Amandla...
 
Ni haki yake kuzungumza atakacho. Lakini kwa nini asubiri mpaka mtanganyika amvue koti badala ya kulivua mwenyewe wakati linambana kwa miaka 57? Mmo kwenye serikali ya Muungano ambayo mnasema imeumbwa kuidhibiti Zanzibar lakini mnaishia kuwaomba watanganyika wawape talaka? Mnadai mmepigwa, mmeuawa, mmedhulumiwa katika uchaguzi uliopita lakini hamkusita kujiunga na serikali iliyotokana na uchaguzi huo? Leo Chadema inapambana kudai Katiba Mpya ambayo itazungumzia hayo mnayolalamikia lakini mmekaa pembeni mnawaangalia!

Quebec, Scotland na Catalonia walipoona wanaonewa katika mfumo uliokuwepo waliweka wazi agenda ya kujitoa katika Muungano wao na wakapigania. Nyinyi mnashindwa nini? Hasa kwa sababu mnajua Muungano wenyewe hauna uhalali kwa sababu hamjau ratify? Acheni kupambana na machogo. Washikeni wanasiasa wenu ili waanze juhudi za kuvunja muungano ambao hauna faida kabisa kwenu.

Amandla...

Mwaka 2019 waquebec 77 waliuawa. Idadi za walio najisiwa hazijulikani maana watu wengi wana ficha. Au unadhani Canada watu hawauawi, kunajisiwa au kuibiwa? Kuwa hayo yanatokea kwenu tu?

Amandla...
Tuwekee ushahidi kuwa wa Quebec hao waliuliwa kwa kudai uhuru wao ?
 
Back
Top Bottom