Kuhusu Miamala na Tozo: Naenda kufungua kesi mahakamani

mugah di matheo

JF-Expert Member
Jul 28, 2018
6,276
12,335
Ndugu zangu Wana JF natangaza kwenu kusudi langu la kufungua shauri mahakama kuu kanda ya Dodoma nikitaka yafuatayo:

1. Mahakama izuie utukaji wa tozo mpya kwenye simu hadi pale shauri litakaposikilizwa
2. Tozo hizo zifutwe kwani tayari tunalipa kodi mbili kwa kila mwamala
3. Wawalipe fidia ya shiling 10,000 kwa kila siku ambayo makato yalifanyika hii watalipwa mawakala ambao kipato chao kiliathirika
4. Kila Mwananchi arudishiwe pesa yake aliotapeliwa

5. walipe fidia kwa makampuni ya simu.

Katika kesi hii washitakiwa ni
1. Waziri wa fedha
2. Kamishina wa TRA
3. Makampuni ya simu

Naombeni ushauri zaidi.pia msisahau kuniombea wasinitike.

mama D Pascal Mayalla Sky Eclat Mwigulu Nchemba Zitto
 
1626382935489.png
 
Dah aisee watatuua

Alf nimeona kwenye law za m-pesa pesa ikikaa ndani ya miaka 5 nakuendelea wanaotaifisha hii inamaana tusifanye saving za muda mrefu kwenye simu zetu?

For amounts that remain in customer accounts unclaimed for more than 5 years, the money will be transferred to relevant authorities
in accordance with the laws of Tanzania
 
Mshahara makato, bidhaa makato, mafuta makato, huduma za afya mbovu, madawa hakuna. Inasikitisha mtanzania wa kipato cha chini ananyonywa kusipo na kifani, ila wabunge ambao haijulikani kama uongozi ni wito au maslai hawalipi kodi kwa chochote #shame.
 
Waziri Wa Fedha anatakiwa ashtakiwe kwa "UONGO (Misrepresentation/False Statement)". Alidanganya kwa makusudi kwamba wanaongeza tozo ya Sh 100/= katika vocha, ila wameongeza tozo zaidi ya hio Sh 100/= kwenye miamala ya kutuma pesa/kutoa na mawakala.

Mungu amlaani kwanza hata kabla ya kuburuzwa mahakamani huyu mdudu.

#KatibaMpya.
#MwiguluOUT.
 
KAMA KUPANDA KWA BEI YA MKATE HUKO KWA WENZETU KULIMWONDOA RAIS MADARAKANI,

WATANZANIA NI MABWEGE KIASI GANI TUNABAKI KUKALAMIKA TU KUHUSU HII TOZO?
Yaani hii nchi hata hatujali yaani ni kupelekwa tu.
 
Halafu utasikia waziri wa fedha anakuja kuomba na kugombea uraia wa JMT

Huyu Muheshimiwa tutamalizana nae juu kwa juu

Asante
 
Ndugu zangu Wana JF natangaza kwenu kusudi langu la kufungua shauri mahakama kuu kanda ya Dodoma nikitaka yafuatayo
1.Mahakama izuie utukaji wa tozo mpya kwenye simu hadi pale shauri litakaposikilizwa
2.Tozo hizo zifutwe kwani tayari tunalipa kodi mbili kwa kila mwamala
3.Wawalipe fidia ya shiling 10,000 kwa kila siku ambayo makato yalifanyika hii watalipwa mawakala ambao kipato chao kiliathirika
4 .Kila Mwananchi arudishiwe pesa yake aliotapeliwa

5.walipe fidia kwa makampuni ya simu

Katika kesi hii washitakiwa ni
1.Waziri wa fedha
2.Kamishina wa TRA
3.makampuni ya simu


Naombeni ushauri zaidi.pia msisahau kuniombea wasinitike




mama D Pascal Mayalla Sky Eclat Mwigulu Nchemba Zitto
tukushaur halaf uje utufanye fursa. We nenda tuuu
 
Back
Top Bottom