Kuhusu Makusanyo ya Kila Mwezi: Serikali iseme Ukweli

Gamba la Nyoka

JF-Expert Member
May 1, 2007
7,022
9,285
Hadi hivi sasa taarifa za Makusanyo ya kila mwezi kwa mwezi November haijatolewa.

Na kwa jinsi tunavyoona serikali ikiendelea kujifunga mkanda yenyewe, wananchi tungependa kujua, Je hali ya Makusanyo iko shwari?.

Tumeona hapa serikali ikisitisha vibali vya ajira, hapo mwanzo ikasema inasubiri zoezi la uhakiki lipite, hata hivyo zoezi limeisha na Wafanyakazi hewa 17000 wameonekana na kuondolewa kwenye payroll, Je ni kama serikali imesevu pesa nyingi baada ya kuwaondoa wafanyakazi hewa kwa nini haikurasimisha ajira za wale waliokwishapewa barua za ajira?. Hapo ndipo tunapoiuliza serikali je Makusanyo ya kila mwezi yako shwari?.

Tumeona bodi ya mikopo, ikisitisha mkopo wa tiketi ya ndege kwa vijana wanaopata scholarship katika nchi rafiki, China ikiwa ndiyo rejea, hii haijawahi kutokea katika serikali zilizopita, Tunaomba serikali itueleze, Je makusanyo ya kila mwezi yako Shwari?

Majuzi nilipita sehemu nikawakuta watu wanapiga soga,nikajibanza sehemu nikawa nawasikiliza, miongoni mwa mazungumzo yao ilikuwa ni kushuka kwa ukusanyaji wa mapato ya TRA, nikasikia mmoja akisema kwa hali anayoiona ni dhahiri TRA hawakusanyi hata shilingi bilioni 650 kwa mwezi!. Mimi nikashtuka sana kwa hilo, Sasa tunaomba serikali itupe majibu juu ya hali ya Makusanyo kwa mwezi, Je hali iko shwari?
 
Hakuna mazingira rafiki kati ya kodi na watoa kodi, huwezi kuwa na ukusanyaji mzuri wa mapato.

KADA
 
Hii nchi mambo yake yote wanataka wafanye gizani na wananchi tunachotakiwa ni kuitikia tu NDIYO MZEEE........

Walianza kulipeleka gizani Bunge letu.

Baadaye vikafuata vyombo vya habari makini vinavyoripoti habari za kiuchunguzi kwa weledi.....

Hivi sasa wanainyemelea JF yetu nayo wanataka kuitia kitanzi......

Sijui hadi itakapofika 2020 hali itakuwaje?

Most likely, our country could become another North Korea.
 
Du ila kweli. mkuu miezi ya hapo mwnzo mamlaka zilikuwa zinatoa taarfa kila mwsho wa mwzi ila miez ya krbni cjasikia lolote
 
Hadi hivi sasa taarifa za Makusanyo ya kila mwezi kwa mwezi November haijatolewa.

Na kwa jinsi tunavyoona serikali ikiendelea kujifunga mkanda yenyewe, wananchi tungependa kujua, Je hali ya Makusanyo iko shwari?.

Tumeona hapa serikali ikisitisha vibali vya ajira, hapo mwanzo ikasema inasubiri zoezi la uhakiki lipite, hata hivyo zoezi limeisha na Wafanyakazi hewa 17000 wameonekana na kuondolewa kwenye payroll, Je ni kama serikali imesevu pesa nyingi baada ya kuwaondoa wafanyakazi hewa kwa nini haikurasimisha ajira za wale waliokwishapewa barua za ajira?. Hapo ndipo tunapoiuliza serikali je Makusanyo ya kila mwezi yako shwari?.

Tumeona bodi ya mikopo, ikisitisha mkopo wa tiketi ya ndege kwa vijana wanaopata scholarship katika nchi rafiki, China ikiwa ndiyo rejea, hii haijawahi kutokea katika serikali zilizopita, Tunaomba serikali itueleze, Je makusanyo ya kila mwezi yako Shwari?

Majuzi nilipita sehemu nikawakuta watu wanapiga soga,nikajibanza sehemu nikawa nawasikiliza, miongoni mwa mazungumzo yao ilikuwa ni kushuka kwa ukusanyaji wa mapato ya TRA, nikasikia mmoja akisema kwa hali anayoiona ni dhahiri TRA hawakusanyi hata shilingi bilioni 650 kwa mwezi!. Mimi nikashtuka sana kwa hilo, Sasa tunaomba serikali itupe majibu juu ya hali ya Makusanyo kwa mwezi, Je hali iko shwari?
Reports zitatolewa muda ukifika. Pressures za nini? Zamani huku nyuma zilikuwa zinatoka kama alivyofanya JPM au wivu na hasira za kukosa!
 
Tuwe na subira, japo sio kawaida maana mwezi huu nao ndio unaishia
 
Nikiona haya mambo nafurahi japo yanatuumiza wote!!! Ila ngoja tuumie tumeyataka wenyewe! Siku expect chochote kwahio siumii; tatizo ni Hao Makada! Juzi kaja Mama mmoja Niko mahali akaniomba at least nimnunulie hata soda Hahahaha nikamkumbusha tu kuwa nani alitundika Bendera za kijani pale mtaani!!!???? Dah kama vile nilimtonesha kidonda! Akamaindi akaondoka, nikafurahi saaaana
 
Reports zitatolewa muda ukifika. Pressures za nini? Zamani huku nyuma zilikuwa zinatoka kama alivyofanya JPM au wivu na hasira za kukosa!
Ulizowea kujitangaza kila siku au ndo unatangaza kwenye mlima ukiwa bonden unajificha
 
Ngoja Kwanza tumalizie kujenga airport chato, hizo scholarship walipe wazazi wao serikali haihusiki
 
Huku ukame wa mvua,kule upungufu wa chakula,hapa mapato yanapungua,kule watumishi wanafukuzwa kama mbwa,pale mtumishi anatukanwa

Hii nchi INA matukio
 
Hii nchi mambo yake yote wanataka wafanye gizani na wananchi tunachotakiwa ni kuitikia tu NDIYO MZEEE........

Walianza kulipeleka gizani Bunge letu. NDIYO MZEE!

Baadaye vikafuata vyombo vya habari makini vinavyoripoti habari za kiuchunguzi kwa weledi..... NDIYO MZEE!

Hivi sasa wanainyemelea JF yetu nayo wanataka kuitia kitanzi...... NDIYO MZEE!

Sijui hadi itakapofika 2020 hali itakuwaje? HATUJUI MZEE ILA TUNAPIGIKA MZEE!

Most likely, our country could become another North Korea.
KWELI MZEE!
 
Back
Top Bottom