Kuhusu maandamano na matamasha ya mkumpongeza.

singojr

JF-Expert Member
Oct 28, 2014
5,306
6,883
Siku za karibuni pamekuwa na matamasha, mikutano na maandamano ya kumpongeza mtu mmoja mzalendo kuliko wote Tanzania.

Je, viongozi wote waliopita yeye ndo kafanya jambo la muhimu kufanya kila siku watu wasifanye kazi na kubaki kumpongeza.

Je, kwa pongezi hizo hapata tokea ushauri wa kumuongezea muda wa kuongoza?

Tulisema hapa kazi tu. Je kazi ni kupongeza.
Huku kupongeza ni kudanganyana kama anajiamini aseme wanaompinga pia wajionyeshe wazi nahakika angehamaki
 
Siku za karibuni pamekuwa na matamasha, mikutano na maandamano ya kumpongeza mtu mmoja mzalendo kuliko wote Tanzania.
Je, viongozi wote waliopita yeye ndo kafanya jambo la muhimu kufanya kila siku watu wasifanye kazi na kubaki kumpongeza.
Je, kwa pongezi hizo hapata tokea ushauri wa kumuongezea muda wa kuongoza?
Tulisema hapa kazi tu. Je kazi ni kupongeza.
Huku kupongeza ni kudanganyana kama anajiamini aseme wanaompinga pia wajionyeshe wazi nahakika angehamaki

Umenena vyema,huu unafiki utaisha lini?
Upumbavu huu ataondokaje ktk nchi hii ya laana?
Naomba waruhusu watu wanaompinga waone barabara zitakavyo jaa
 
Wamepiga vita maandamano,kumbe yaliyopigwa vita ni ya kukosoa serikali!
Wanakwaya walipoandamana kwenda kutoa sauti zao Gwajima aliposhikiliwa kwa tuhuma za kughushi na za chuki za bashite,JPM alimshangaa IGP na kusema "i wish i could be IGP"!
Kazi kwenu Polisi mtakaoruhusu hayo maandamano,Rais hapendi maandamano!
 
Mambo ya ajabu sana haya..

Mimi naamini mtu anayefanya mazuri hana haja ya kuyatangaza,yataonekana tu!

Wale wanaopenda kuonwa wameshamjulia huyu bwana ni nini anapenda, wanamfurahisha!
 
Umenena vyema,huu unafiki utaisha lini?
Upumbavu huu ataondokaje ktk nchi hii ya laana?
Naomba waruhusu watu wanaompinga waone barabara zitakavyo jaa

Mtu mwingine anaweza fanya jambo akawa anapongezwa kumbe hata yeye mwenyewe hajui alilifanyaje fanyaje anakuwa kama aliotea tu
 
Rais Dr Magufuri anavikwa kiremba cha ukoka
 

Attachments

  • IMG-20170624-WA0020.jpg
    IMG-20170624-WA0020.jpg
    54.7 KB · Views: 29
hapo mwanzo wanaccm waliponda sana kuhusu maandamano ya wapinzani.leo ndo wanahamasisha. kwa kweli taifa letu kwa unafiki ni hatar

Halafu walikuwa wanasema kila siku kuandamana eti kazi mtafanya saa ngapi. Kweli Mungu hamfichi mnafiki. Yale yale bunge live hapana kisa watu wafanye kazi kwa kuwa bunge linafanyika muda wa kazi. Hivi leo hata tu kumuapisha mkuu wa mkoa ni live tena saa 4 asubuhi. Baada ya hapo ni hotuba ya vijembe dhidi ya Tundu Lissu.
 
Watu wanajitekenya na kucheka wenyewe.Tatizo la akili ndogo zinazoongozwa na tumbo.Sijaona cha maana cha kufanya watu wapongezane.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom