Ufafanuzi: Kuvunjwa Halmashauri ya Jiji la Dar kuipandisha hadhi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kuwa Jiji

Tangu Rais Dr. John Pombe Magufuli kuvunja Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na kuipandisha hadhi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kuwa Jiji la Dar es Salaam, kumekuwa na mijadala kemkem kuhusu jambo hilo runingani, redioni na hata mitandaoni. Mjadala hasa unajikita katika kuelewa kilichofanyika jana. Wapo wanaosema kuwa kwasasa Mamlaka tu ya lililokuwa Jiji la Dar es Salaam ndiyo yaliyowekwa chini ya Ilala na jiji liko vilevile na pale pale.

Wapo wanaosema kuwa kwasasa Ilala ndiyo jiji na wengine ni Manispaa ndani ya Jiji la Dar es Salaam. Katika kuelewa jambo hili kuna mambo ya kuyafahamu. Mosi, kabla ya jana, Dar es Salaam kama mkoa ulikuwa na Halmashauri za Manispaa tano: Ilala, Kinondoni, Ubungo, Temeke na Kigamboni. Halafu, kulikuwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambalo kinadharia lilijumuisha Manispaa zote hizo.

Pili, hadhi ya juu kabisa ya kihalmashauri ni Jiji. Tatu, jana likavunjwa lililokuwa Jiji la Dar es Salaam (kwa maaa ya kuondolewa kwa iliyokuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam). Zikabaki Halmashauri za Manispaa tano. Moja ya Manispaa hizo-ya Ilala ikapandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Jiji na 'kubatizwa' jina la Dar es Salaam. Sasa kuna Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo kimsingi ni iliyokuwa Hamlmashauri ya Manispaa ya Ilala.

Ndiyo kusema, Jiji la Dar es Salaam kwasasa ni sehemu yote ya Wilaya ya Ilala na si vinginevyo. Wilaya za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni si sehemu ya jiji la Dar es Salaam. Hizo zimebaki kuwa Halmashauri za Manispaa. Katika kueleweka zaidi, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ya sasa imepakana na Halmashauri za Manispaa za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni. Kwahiyo, mtu wa Ubungo, Temeke, Kinondoni na Kigamboni hayupo ndani ya Jiji la Dar es Salaam.
Na kwakuongezea Dar inabaki kuwa mkoa wenye halamshauri ulizotaja hapo lakini ilala ikiwandio makao makuu yake. Watu wengi imewachanganya .
 
Acha upotoshaji usio na Tija.
Rejea taratibu za majiji yote duniani.
Ndicho kilichofanyika.
Iliyokua halmashauri ya jiji la DSM, Haikua na eneo la mamlaka hivo haikua na chanzo cha mapato kwaio tulikua tunagharamia kuendesha kitu kisichokuwepo.
Maeneo yote ya Dar mathalani
Ubungo, kibamba, mbezi beach, Tegeta mbagala nk bado ni sehemu ya jiji la Dar
Over.
 
Tangu Rais Dr. John Pombe Magufuli kuvunja Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na kuipandisha hadhi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kuwa Jiji la Dar es Salaam, kumekuwa na mijadala kemkem kuhusu jambo hilo runingani, redioni na hata mitandaoni. Mjadala hasa unajikita katika kuelewa kilichofanyika jana. Wapo wanaosema kuwa kwasasa Mamlaka tu ya lililokuwa Jiji la Dar es Salaam ndiyo yaliyowekwa chini ya Ilala na jiji liko vilevile na pale pale.

Wapo wanaosema kuwa kwasasa Ilala ndiyo jiji na wengine ni Manispaa ndani ya Jiji la Dar es Salaam. Katika kuelewa jambo hili kuna mambo ya kuyafahamu. Mosi, kabla ya jana, Dar es Salaam kama mkoa ulikuwa na Halmashauri za Manispaa tano: Ilala, Kinondoni, Ubungo, Temeke na Kigamboni. Halafu, kulikuwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambalo kinadharia lilijumuisha Manispaa zote hizo.

Pili, hadhi ya juu kabisa ya kihalmashauri ni Jiji. Tatu, jana likavunjwa lililokuwa Jiji la Dar es Salaam (kwa maaa ya kuondolewa kwa iliyokuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam). Zikabaki Halmashauri za Manispaa tano. Moja ya Manispaa hizo-ya Ilala ikapandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Jiji na 'kubatizwa' jina la Dar es Salaam. Sasa kuna Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo kimsingi ni iliyokuwa Hamlmashauri ya Manispaa ya Ilala.

Ndiyo kusema, Jiji la Dar es Salaam kwasasa ni sehemu yote ya Wilaya ya Ilala na si vinginevyo. Wilaya za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni si sehemu ya jiji la Dar es Salaam. Hizo zimebaki kuwa Halmashauri za Manispaa. Katika kueleweka zaidi, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ya sasa imepakana na Halmashauri za Manispaa za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni. Kwahiyo, mtu wa Ubungo, Temeke, Kinondoni na Kigamboni hayupo ndani ya Jiji la Dar es Salaam.
Kwhyo wale walio nje ya Ilala tuwaite wamikoani!?
 
sasa ndo nmeelewa,
MFANO: ni sawa useme Moshi iwe jiji ila Mwanga, Same, na Rombo isiwe jiji. haiwezekani mkoa mzima wa Kilimanjaro uwe jiji ila Moshi pekee ndo inaweza ikawa jiji.

ni sawa Morogoro mjini iwe jiji ila Ifakara, Malinyi na Ulanga haziwezi kuwa jiji.

•Ni sawa Ilala kuwa jiji ila Temeke, Kinondoni na kigamboni haziwezi kuwa jiji.
kiufupi nmeelewa mkoa hauwezi kuwa jiji bali inayokuwa jiji ni manispaa au halmashauri, hivi ndivyo nlivyoelewa.
niko tayari kusahihishwa kama nmekosea
 
Tangu Rais Dr. John Pombe Magufuli kuvunja Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na kuipandisha hadhi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kuwa Jiji la Dar es Salaam, kumekuwa na mijadala kemkem kuhusu jambo hilo runingani, redioni na hata mitandaoni. Mjadala hasa unajikita katika kuelewa kilichofanyika jana. Wapo wanaosema kuwa kwasasa Mamlaka tu ya lililokuwa Jiji la Dar es Salaam ndiyo yaliyowekwa chini ya Ilala na jiji liko vilevile na pale pale.

Wapo wanaosema kuwa kwasasa Ilala ndiyo jiji na wengine ni Manispaa ndani ya Jiji la Dar es Salaam. Katika kuelewa jambo hili kuna mambo ya kuyafahamu. Mosi, kabla ya jana, Dar es Salaam kama mkoa ulikuwa na Halmashauri za Manispaa tano: Ilala, Kinondoni, Ubungo, Temeke na Kigamboni. Halafu, kulikuwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambalo kinadharia lilijumuisha Manispaa zote hizo.

Pili, hadhi ya juu kabisa ya kihalmashauri ni Jiji. Tatu, jana likavunjwa lililokuwa Jiji la Dar es Salaam (kwa maaa ya kuondolewa kwa iliyokuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam). Zikabaki Halmashauri za Manispaa tano. Moja ya Manispaa hizo-ya Ilala ikapandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Jiji na 'kubatizwa' jina la Dar es Salaam. Sasa kuna Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo kimsingi ni iliyokuwa Hamlmashauri ya Manispaa ya Ilala.

Ndiyo kusema, Jiji la Dar es Salaam kwasasa ni sehemu yote ya Wilaya ya Ilala na si vinginevyo. Wilaya za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni si sehemu ya jiji la Dar es Salaam. Hizo zimebaki kuwa Halmashauri za Manispaa. Katika kueleweka zaidi, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ya sasa imepakana na Halmashauri za Manispaa za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni. Kwahiyo, mtu wa Ubungo, Temeke, Kinondoni na Kigamboni hayupo ndani ya Jiji la Dar es Salaam.
Huu UJINGA utalast kwa miaka 5 tu. Ifikapo Jan 2026 Rais mpya atatudisha hadhi ya Jiji la Dar es Salaam kwa kurudisha kwanza makao makuu toka Dodoma, na kulifanya Jiji liwe Kama zamani.

Huyu mrundi hana mapenzi na nchi yetu, Ni mtu wa KUVURUGA TU
 
Acha upotoshaji usio na Tija.
Rejea taratibu za majiji yote duniani.
Ndicho kilichofanyika.
Iliyokua halmashauri ya jiji la DSM, Haikua na eneo la mamlaka hivo haikua na chanzo cha mapato kwaio tulikua tunagharamia kuendesha kitu kisichokuwepo.
Maeneo yote ya Dar mathalani
Ubungo, kibamba, mbezi beach, Tegeta mbagala nk bado ni sehemu ya jiji la Dar
Over.
Hapana, siyo upotoshaji. Ni mjadala tu na kila mtu ana haki ya kujadiliana na wenzake...

Ukisema hivyo, mwingine aweza kukuita hata wewe kuwa ni "mpotoshaji" kwa kuwa tu umetoa maoni yako kwa njia hii

Mimi kwa maoni yangu, DSM City Council iendelee kubaki kama chombo cha ku - oversee hizi mamlaka za manispaa zote tano...

Mapato ya uendeshaji yagharamiwe na hizi mamlaka tano...

Kama kuna changamoto, zitatuliwe kisheria na kimuundo kwa lengo la kuingozea kazi na mamlaka DCC...
 
Jiji litalazimika kuwa na special priority za kiujenzi ukivunja nyumba basi inayojengwa ni lazima iwe ya ghorofa nk nk
pia si jambo la kufurahia sana maana huenda ndani ya jiji hilo wanyonge wakashindwa kuishi humo due to living cost mfano unapoisikia new york city ogopa sana kila kitu ni ghalimpaka ilibidi tukimbilie harlem uswekeni kwa wahuni kupata cheap houses
 
Jiji litalazimika kuwa na special priority za kiujenzi ukivunja nyumba basi inayojengwa ni lazima iwe ya ghorofa nk nk
pia si jambo la kufurahia sana maana huenda ndani ya jiji hilo wanyonge wakashindwa kuishi humo due to living cost mfano unapoisikia new york city ogopa sana kila kitu ni ghalimpaka ilibidi tukimbilie harlem uswekeni kwa wahuni kupata cheap houses
Huu mfumo wa jiji huko huku Mwanza jiji tumeisha zoea ndo maana tunakimbilia kujenga manispaa ya Ilemela,Misungwi na manispaa mpya ya kisesa.Mwanza jiji(nyamagana manispaa) inasheria zake ukijenga nyumba ambayo sio gorofa ni nyundo tu.Ila ndo mabadiliko lazima tukubali.
 
Na kwa hivyo hatutakuwa na mkuu wa Wilaya ya Ilala? Maana wilaya sasa imefutwa... Au?
 
Tangu Rais Dr. John Pombe Magufuli kuvunja Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na kuipandisha hadhi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kuwa Jiji la Dar es Salaam, kumekuwa na mijadala kemkem kuhusu jambo hilo runingani, redioni na hata mitandaoni. Mjadala hasa unajikita katika kuelewa kilichofanyika jana. Wapo wanaosema kuwa kwasasa Mamlaka tu ya lililokuwa Jiji la Dar es Salaam ndiyo yaliyowekwa chini ya Ilala na jiji liko vilevile na pale pale.

Wapo wanaosema kuwa kwasasa Ilala ndiyo jiji na wengine ni Manispaa ndani ya Jiji la Dar es Salaam. Katika kuelewa jambo hili kuna mambo ya kuyafahamu. Mosi, kabla ya jana, Dar es Salaam kama mkoa ulikuwa na Halmashauri za Manispaa tano: Ilala, Kinondoni, Ubungo, Temeke na Kigamboni. Halafu, kulikuwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambalo kinadharia lilijumuisha Manispaa zote hizo.

Pili, hadhi ya juu kabisa ya kihalmashauri ni Jiji. Tatu, jana likavunjwa lililokuwa Jiji la Dar es Salaam (kwa maaa ya kuondolewa kwa iliyokuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam). Zikabaki Halmashauri za Manispaa tano. Moja ya Manispaa hizo-ya Ilala ikapandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Jiji na 'kubatizwa' jina la Dar es Salaam. Sasa kuna Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo kimsingi ni iliyokuwa Hamlmashauri ya Manispaa ya Ilala.

Ndiyo kusema, Jiji la Dar es Salaam kwasasa ni sehemu yote ya Wilaya ya Ilala na si vinginevyo. Wilaya za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni si sehemu ya jiji la Dar es Salaam. Hizo zimebaki kuwa Halmashauri za Manispaa. Katika kueleweka zaidi, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ya sasa imepakana na Halmashauri za Manispaa za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni. Kwahiyo, mtu wa Ubungo, Temeke, Kinondoni na Kigamboni hayupo ndani ya Jiji la Dar es Salaam.
KWAHIYO CHANIKA IPO JIJINI DAR ES SALAAM WAKATI MIKOCHENI IPO MANISPAA YA KINONDONI....DAH
 
Hili swala sio geni mfano jiji la Mwanza linaundwa manispaa tatu ilemela,Nyamagana na kisesa(mpya) lakini kiutalawa Nyamagana ndo jiji na inaeleweka vizuri ila ukija mgeni uwezi elewa mipaka ya jij .
Jiji la Dar es Salaam lilipata hadhi ya kuwa Jiji tarehe 9.12.1961 siku ya Uhuru na wakati huo Kaskazini likiishia Salendar Bridge, Magharibi Magomeni Mapipa na Kusini Temeke pembeni mwa Barabara ya Airport, eneo likiitwa Ilala wakati huo mpaka leo. Ilichukua miaka kama miwili au mtatu kuandaa Muundo wa Jiji na Mfumo wa Utawala, wakati huohuo Kinondoni na Temeke zikiendelea kukua na kuingizwa kwenye Muundo wa Jiji wenye Wilaya Tatu. Kwa sababu ya Barabara ya Morogoro, Ilala, ikakua haraka sana kuelekea Kimara na Kigamboni nayo ikiwa sehemu ya Temeke, siku za karibuni ikakua haraka sana ikalazimu Wilaya hizi mbili zigawanywe kupata Wilaya ya Ubungo na Kigamboni kufanya Jiji kuwa na Wilaya Tano. Jiji lilifanywa Mkoa wa Wilaya 5 na kuongoza shughuli zake kama Mikoa na Wilaya zingine nchini, Jiji nalo likawa na Muundo na Mfumo wake wa Utawala ambao ndo umefikisha Jiji kutambuliwa Kimataifa kuwa ni moja ya Majiji 10 yanayokua haraka sana. Kwa kifupi hayo ni mafanikio makubwa ya kupongeza siyo ya mtu mmoja kubeza na kufanya mabadiliko kwenye Jukwaa la kisiasa. Mabadiliko wakati mwingine ni lazima yafanyike ikibidi lakini lazima yalete matokeo chanya, ila mabadiliko yasipofanywa ikibidi kwa utashi wa mtu, yatakuja yenyewe yakileta matokeo hasi. Awamu ya Tano inaogopa mabadiliko, mafanikio yake ni maneno na sifa tu!
 
Back
Top Bottom