Kuhusu hili la umeme TANESCO mnasemaje???

Mzee wa Rula

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
8,171
3,346
Daaaah ukweli hali ya umeme inatisha. Umeme tulioahidiwa hautakatika sasa imekuwa kama hadithi.

Hali ni mbaya sana kwa baadhi ya mikoa hasa Arusha ambako baadhi ya wadau wanasema hawataki hata kusikia jina la TANESCO.

Wadau sijui wewe hapo ulipo hali ya umeme ipoje?
 
Mzee wa Rula habari gani Best!

Bila shaka U mzm kama unavyosomeka jukwaani.
Kuhusu hili la umeme kwa kweli hili ni janga moja kubwa sana kwa Mkoa wetu na hata Taifa kwa ujumla.
Hapa mtaani ama area yote ya kwangu kwa kweli hata vijana wote kwa upande wa garage na hata useremala hakika wamekaa vijiweni wakiliongelea hili jambo tu la umeme na hata hivyo wamehamishia upande wa KISIASA zaidi na wakiishutumu serikali iliyoko madarakani ya kwamba haya mateso wanayowaletea kwa kweli sasa inaonekana kabisa ya kwmb ni kutokana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo kuongoza karibu kanda yote ya Kaskazini na wataendelea kuichagua mpaka waone mwisho wao.
Na kwa kweli hali hii ikiendelea hivi na ccm na serikali yake imejiweka pabaya sana na kwenye wakati mgumu kiuongozi.

Ila kwa ujumla hali si nzuri hapa A town kwa mgao huu wa umeme!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom