Kuhusu Corona: WHO wanasema mask haisaidii kujikinga kwa wasio na maambukizi

alphonce.NET

JF-Expert Member
Jul 19, 2013
1,637
5,795
Kadri hatari ya Corona inavyozidi kuongezeka inatubidi kutafuta kila taarifa za kitaalamu kujua namna sahihi tunavyoweza kujikinga

Binafsi kuanzia siku ya leo nimeshuhudia watu wameanza kutumia mask kuziba mdomo na pua, lakini katika hali ya kawaida nimetafakari sana kama kweli kufanya hivyo ndio inasaidia kujikinga au labda hata ndio inaongeza hatari ya maambukizi kwa sababu ya kama kuzuia mzunguko wa hewa ya kutosha

Katika kutafuta taarifa nimepitia WHO website kujua wao wanasemaje kuhusu hizi masks nikakuta taarifa hii, ambayo kwa kifupi tu inaeleza kuwa matumizi ya masks haisaidii kumkinga mtu asiambukizwe ila inatakiwa kutumiwa na wale ambao tayari wana maambukizi na wameshaona dalili za kuumwa

When and how to use masks
 
1584461938789.png
 
Kuna seem nilisoma maski zinasaidia kwa saabu wadudu wa korona ni wakubwa ukilinganisha na vitundu vya kwene maski. Ila lazma maski ivaliwe kiukamilifu.



Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu mask inazuia majimaji ya mdomon au puan wakat wa kukohoa au kupga chafya, na kuongea ambayo yanaweza kuwa na virus, yasimfikie mtu mwingine na kumuambukiza. Virus ni mdogo kias kwamba hata macho yetu hayawez kumuona ndo maana had utumie darubin ndo unamuona, udogo wake huwez linganisha na matundu ya mask ambayo hata ukichujia maji yanapita yote muda huohuo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna seem nilisoma maski zinasaidia kwa saabu wadudu wa korona ni wakubwa ukilinganisha na vitundu vya kwene maski. Ila lazma maski ivaliwe kiukamilifu.



Sent using Jamii Forums mobile app
Wadudu wakubwa!! Unadhani hao ni mende au mijusi. Bacteria/Virusi unawaonaje ukubwa wao.

Mask zinazuia majimaji kutoka kwa mgonjwa kuja kwako, maana mtu anapokohoa ama kupiga chafya anatoa majimaji. Hayo majimaji yenye kuwa na maambukizi ndiyo huzuiliwa yasikuingie katika mdomo wako au pua na hata macho.

Sasa ukisema wadudu wakubwa utadhani ni kumbikumbi sielewi huo ukubwa nani kauonesha.
 
Unavaa mask uzuie usipate korona unaenda ipata kwenye noti
Unavaa mask usipate korona unaenda ipata baada ya kushika bomba kwenye gari la abiria
 
Back
Top Bottom