G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Unataka nianze kuchapa TANZIA ambazo nimeona zinanichosha kwa wingi wake? Unataka nianze kesho na mbunge wa CCM kisha kesho kutwa mihamie viongozi wa kitaifa? Nitafanya hivyo.Wasalaam,
Niende kwenye mada moja kwa moja
Kipindi kile serikali inatoa takwimu za maambukizi na vifo vya Covid-19 mara kwa mara huku kwenye mitandao ya
kijamii yaliibuka mengi ambayo kwa asilimia kubwa yaliaminika:
Wengi tulitilia shaka takwimu zilizotolewa na serikali hivyo mitandao ya jamii ilisheheni:-
Shuhuda za jinsi wapendwa wetu wanavyozikwa usiku na ndugu kupigwa mkwara wasisambaze taarifa
Wengine walikuja na taarifa za uwepo wa wagonjwa wengi mahospitalini.
Wengine walikuja na shuhuda za wapendwa wao kukosa huduma hospitali.
Tangu serikali isitishe kutoa takwimu na kusisitiza maambukizi yamepungua hayo yote hayapo tena kwenye mitandao
Kwasababu watu hawalalamiki kama zamani, hii ni indicator mojawapo kwamba yanayosemwa na serikali ni sahihi maana hakuna malalamiko tena huku mitandaoni.