Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,427
'Mtu asilazimike kuwa na chama ili kuwa kiongozi'.
Tushawishi bunge waone umuhimu wa hili.
- Siasa za vyama vingi Tanzania zinachukua sura isiyopendeza sana,
- Vyama vimejanga hali ya wao na sisi,ambayo sio chanya,
- Watu wanabeba lawama au sifa zisizo zao bali kwa sababu ya vyama,
- Watu wanashindwa kuwa wakweli yanapokuja masuala ya vyama vyao,
- Vyama vilivyopo havisimamii tena misingi wala falsafa,bali misimamo ya viongozi wa vyama husika na vingine havina vinachosimamia kabisa,
- Kuna watu wenye mawazo mazuri ila wanabanwa na misimamo ya chama
- Kuna watu wanakosa nafasi za kuwa viongozi kwa sababu ya vyama Lakini ni watu wazuri tu,
- Kuna watu wasiokubaliana na yanayotendeka ndani ya vyama, n
- Kwa kuwa kuna watu hawana vyama lakini ni watu wazuri;
Umefika wakati wa kulishawishi bunge kufikiria umuhimu wa wagombea binafsi. Tunasema bunge kwa sababu suala hilo kwa sasa haliko kikatiba na kwa mujibu wa hukumu ya Mahakama ya rufaa ya mwaka 2010 kati ya Mtikila na AG ilishasema 'suala hilo ni la kisiasa na wenye uwezo wa kulishughulikia ni bunge' .Ni muhimu kulishauri bunge lione umuhimu wa suala hili na kufanya marekebisho madogo ya Katiba ili kuli 'accommodate'.
Faida zake itakuwa ni kama ifuatavyo;
1. Dhana ya sisi na wao itakufa,
2. Kila mtu atabeba lawama au sifa kulingana na matendo yake mwenyewe, hakuna atakayesulubiwa kwa makosa ya mwenzake, au kubebwa kwa sifa za wenzake,
3. Itakuwa rahisi kuwawajibisha wanaokosea au kuvunja sheria ,
4. Tutakuwa na bunge lenye watu mchanganyiko na walio huru,
5. Migogoro kwenye uchaguzi itapungua na haki itatawala,
6. Kutakuwa na mawazo ya aina mbalimbali na kwa kadiri kunavyokuwa na mawazo tofauti ndivyo uwezekano wa maendeleo unavyoongezeka.
7. Umoja wa kitaifa utaimarika
Hasara ni kama ifuatavyo;-
Kila lenye faida lina hasara pia, hasara watasaidia kuziainisha wengine.
Asanteni!
======
Hoja za wadau
Napenda sana maandiko yako. Yamejaa weledi na hoja nzuri. Nasikitika wana JF wengi huwa wanapenda maandiko mepesi mepesi, ya kusutana na kushambuliana. Nadhani mfupo wa elimu yetu una-play part kubwa. Tuna kizazi chenye ushabiki bila tafakari. Back kwenye mada: Moja ya ''hasara'' za kuwa na wagombea binafsi (kama inavyosema na wanasiasa) ni kuwa maadui wa Taifa watakuwa na urahisi wa ku-sponsor ''mwanasiasa kibaraka mzalendo'' na kumfanya awe mbunge kwa maslahi yao. Au watu matajiri wanaweza kutumia ufukara uliokithiri ''kununua'' eg ubunge kwa maslahi yao.
Mimi sikubalini nao. Hata mgombea mwakilishi wa Chama cha siasa anaweza kununuliwa tu. Leo nimekutana na habari kutoka BBC inayozungumzia jinsi Australia inavyoilamu China kwa kutaka kuingiza mbunge kibaraka kwenye bunge la Australia. (Habari yake iko hapa Australia probes alleged Chinese spy MP plot ). Kama Taifa kubwa kama Australia linachezewa huu mchezo, je haya mataifa yetu ya madongokuinama wamewekwa wangapi? Nikakumbuka jinsi Zitto alivyolivalia njuga suala la bandari ya Bagamoyo na mchina.