Kuhusu Bima ya Afya: Naomba ufafanuzi katika hili jambo

faru john junior

JF-Expert Member
Dec 26, 2016
1,596
1,717
Habari za mchana wadau wa JamiiForums

Kama kichwa cha habri kinavyoeleza, ningependa kupatiwa ufafanuzi katika hili jambo. Leo asubuhi nimeenda hospital ya agakhan pale makao makuu karibu na bahari kwa wale wanaojua raman ya Dsm,na lengo ni kupata huduma ya matibabu nikitumia bima ya afya. Mimi ni mtumishi wa umma moja ya shirika kubwa hapa nchini .

Kilichonishangaza ni kwamba kadi yangu ya bima walikataa kunipatia huduma kwa madai kuwa kadi yangu haina nembo ya shirika ninalolitumikia kwani bima zote za serikali wanazopokea zina nembo au majina ya mashirika husika.

Kwanza nilshangaa kidgo kusikia hivyo kwani kadi yangu haikuwa na hyo nembo kama alivyodai mtoa huduma. Lakini hyo haikuwa shida sana ila nikaendelea kumuliza kuwa hawa wenye hizo kadi zenye nembo au majina ya taasisi husika kuna nini hasa tofauti na mm japo nilimweleza ni taasisi gani natoka.

Majibu niliyopewa ni kwamba hizo taasisi huwa zinatoa fedha ya nyongeza tofauti na ile ambayo wangekata kutoka kwenye mfuko wa bima ya afya. Alinitajia badhi ya taasisi ambazo hutoa fedha za ziada kwa watumishi wake kutibiwa pale ni kama bank kuu BoT, TRA.

Sasa swali langu ni kwamba je serikali haioni kuwa huu ni ubaguzi kwa watumishi wasio patiwa hyo nyongeza ya malipo? Watumishi wa umma na serikali ni sawa baba/mama na watoto wake je kuweka ubaguzi wa wazi kiasi hiki haoni kuwa ni kudidimiza huduma hasa upande usio pata hicho kipaumbele?

Je, hao TRA na BoT wataweza kufanya kazi vzri bila kumtegemea nesi, mwalim,polisi, nk?
Asante sana
 
No hiyo sio sawa,wapigie simu bima ya afya haraka,watawashughulikia hao aghakhan sasa hivi
 
Agha Khan Wana migogoro na nhif
Maana matibabu yao ni ghali mno
Ukiwa na bima ya nhif brown ndo kabisa hupati kitu labda zile za vip yaani green card
Nhif wameweka standard zao kitu ambacho agha Khan hawakubaliani nacho! Kuna muda serikali iliwaondoa kabisa agha Khan kuhuhudumia wagonjwa wenye nhif ila walidai tofauti zao na serikali zipo kwenye majadiliano! Agha kahan ya kibada wanatoa huduma vzr kwa bima za nhif
 
Sasa swali langu ni kwamba je serikali haioni kuwa huu ni ubaguzi kwa watumishi wasio patiwa hyo nyongeza ya malipo? Watumishi wa umma na serikali ni sawa baba/mama na watoto wake je kuweka ubaguzi wa wazi kiasi hiki haoni kuwa ni kudidimiza huduma hasa upande usio pata hicho kipaumbele?
Na ndiyo hapa panawafanya watu waichukie serikali, inaubaguzi mkubwa sana, huko BoT wamejaa watoto wa vigogo na ndiyo maana kuna upendeleo kama vile wao ndiyo walipakodi pekee.

Hili la ubaguzi ndilo lilikuwa linapigiwa kelele hata kwenye mishahara, watu wenye qualification sawa, wote ni watumishi wa serikali, tofauti yao ya mishahara ni kubwa mno, Mwendazake alianza kulifanyia kazi lakini halikufika mbali likazimwa.
 
Habari za mchana wadau wa JamiiForums

Kama kichwa cha habri kinavyoeleza, ningependa kupatiwa ufafanuzi katika hili jambo. Leo asubuhi nimeenda hospital ya agakhan pale makao makuu karibu na bahari kwa wale wanaojua raman ya Dsm,na lengo ni kupata huduma ya matibabu nikitumia bima ya afya. Mimi ni mtumishi wa umma moja ya shirika kubwa hapa nchini .

Kilichonishangaza ni kwamba kadi yangu ya bima walikataa kunipatia huduma kwa madai kuwa kadi yangu haina nembo ya shirika ninalolitumikia kwani bima zote za serikali wanazopokea zina nembo au majina ya mashirika husika.

Kwanza nilshangaa kidgo kusikia hivyo kwani kadi yangu haikuwa na hyo nembo kama alivyodai mtoa huduma. Lakini hyo haikuwa shida sana ila nikaendelea kumuliza kuwa hawa wenye hizo kadi zenye nembo au majina ya taasisi husika kuna nini hasa tofauti na mm japo nilimweleza ni taasisi gani natoka.

Majibu niliyopewa ni kwamba hizo taasisi huwa zinatoa fedha ya nyongeza tofauti na ile ambayo wangekata kutoka kwenye mfuko wa bima ya afya. Alinitajia badhi ya taasisi ambazo hutoa fedha za ziada kwa watumishi wake kutibiwa pale ni kama bank kuu BoT, TRA.

Sasa swali langu ni kwamba je serikali haioni kuwa huu ni ubaguzi kwa watumishi wasio patiwa hyo nyongeza ya malipo? Watumishi wa umma na serikali ni sawa baba/mama na watoto wake je kuweka ubaguzi wa wazi kiasi hiki haoni kuwa ni kudidimiza huduma hasa upande usio pata hicho kipaumbele?

Je, hao TRA na BoT wataweza kufanya kazi vzri bila kumtegemea nesi, mwalim,polisi, nk?
Asante sana
Nina ni janga, japo serikali inadai kuandaa mfumo wa bima kwa wote. Ulikataa bima ya afya mpaka ipite miezi 3 ndio unapata matibabu, nayo ndio ni kwenye baadhi ya hospitali, pengine unaambiwa bima yako ni ndogo, hatuihudumii. Serikali inadai matibabu watoto wachanga under 5 ni bure. Kichekesho mama mzazi mwenye bima akijifungua tu mtoto hatibiwi. Kwa nini serikali isiweke mipango wa mtoto atumie bima ya mama? Hawaoni kina mama watahamasika kukata bima? Ni wizi mtu kulipia bima kisha asubiri miezi 3.
 
Back
Top Bottom