Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,408
Nimewahi vuta Bangi mara moja....Kumbe haina madhara???
Tuvuteni bangi wana Jf
Kwako MziziMkavu umeona sasa hapo vifo vya sigara na alcohol.
========================
Bangi (pia: bhang, bhangi; kutoka Kihindi भांग, bhāṅg) ni maandalizi kutoka majani na maua (matumba) ya mmea wa kike wa Cannabis.
Ndani yake kuna dawa linalosababisha namna ya ulevi unaotegemea kiasi cha dawa linaloingia mwilini. Hutumiwa aidha kama kinywaji, kama kiungo ndani ya vyakula au huvutwa. Katika desturi asilia za Uhindi mavuno na maandalizi huja wakati wa maadhimisho ya Holi mwezini Machi na Vaisakhi mwezini Aprili, hivyo kuhusishwa na Bwana Shiva. Imekuwa sawa na Holi, mpaka kuvuta bangi wakati huo ni kitu cha kawaida.
Nta (wakati mwingine fuwele) hutenganishwa na majani na matumba ya Cannabis. Bangi inayochangamsha akili husaidia kueneza roho ya Holi, tamasha ambayo hailazimisha vikwazo vyovyote. Thandai,Pakoras na vadas,yote mapochopocho ya kitamaduni yenye bangi kama kiungo cha muhimu, huonjwa na kila mtu siku hiyo.
Bhang Ki Thandai(Kihindi) ni kinywaji maarufu katika maeneo mengi ya India ambacho hutengenezwa kwa kuchanganya bangi na Thandai, kinywaji baridi kitayarishwacho kwa karange,masala, maziwa na sukari. Matumizi ya bangi na vitu vya kuchangamsha akili kumekatazwa na baadhi ya madhehebu ya dini la kihindi kama vile Shikshapatri, na pia ni haramu katika Uislamu, ingawa si katika madhehebu yote.
Historia, Bangi mwanzoni ilitumika kama sehemu ya ibada ya Hindu nchini India kuzunguka mwaka wa 1000 KK na baadaye ikawa sehemu muhimu ya utamaduni wa Kihindi. Katika nakala ya zamani ya Atharvaveda, bangi inaelezewa kama mitishamba ya manufaa ambayo "humaliza wasiwasi". Maandalizi ya bangi yalikuwa takatifu kwa miungu, hasa Shiva. Moja wa sitiari za Shiva ni "Bwana wa Bangi" na inasemekana ni yeye aliyegundua tabia aali ya mchanganyiko.
Maandalizi
Katika kumuiga Shiva, wengi wa Wasadhu hutumia bangi kuongeza kutafakari na kufikia hali ya transcendental. Bangi au boza inajulikana pia ni maarufu miongoni mwa Wasufi kama msaada ecstasy kiroho.
Mila ya kutumia bangi wakati wa Holi ni wamba hasa Kaskazini mwa India ambapo Holi yenyewe huadhimishwa kwa pupa huku haijulikani mahali kwengine. Walakini bangi hutumiwa sana kule Varanasi au Chembada, nchi ya Shiva, ambapo bangi hutayarishiwa kwenye ngazi zake maarufu Popote kwenye ngazi, mtu anaweza kupata idadi kubwa ya wanaume wanaohusika katika mchakato wa kuandaa bangi.
Kutumia kinu na mchi, matumba na majani ya Cannabis husagwa na kuwa uji mzito wa kijani. Kwa mchanganyiko huu maziwa, siagi, na masala huongezwa. Wigo la bangi sasa ni tayari kufanywa kinywaji kinacho lewesha, Thandai, mbadala kwa pombe. Bangi pia huchanganywa na siagi na sukari kufanya uji wa kijani, na pia vipira vidogo vya kutafuna vinavyo washa, viitavyo 'golees' (ambayo kwa mantiki hii inamaanisha peremende au kidonge katika Kihindi).
Utamaduni.
Kwa vile ni ya kale, bangi imekuwa ni sehemu muhimu ya utamaduni wa India hata imekuwa kiashirio cha mambo mengi. Bangi huhusishwa na Bwana Shiva, kwani mmea wa Hampa hujulikana kama mtakatifu kwa Wahindu wa Kaskazini mwa India. Kuna hata imani kwamba kukutana na mtu liyebeba bangi ni ishara mbaya ya kufanikiwa. Na, kama hamu ya mmea wa hampa kunaashiria furaha, kuuona katika ndoto kunahakikisha mafanikio kwa mtu katika siku zijazo. Pia, kutembea juu ya jani takatifu la bangi hua minika kuashiria mabaya.
Watu wanaamini katika mali ya dawa ya mmea wa Hampa. Ikitumiwa kwa kiwango sahihi, inaaminika bangi kutibu homa, kuhara na sunstroke, kutoa kikohozi, kuharakisha kusagwa kwa chakula tumboni, hamu ya chakula, kutibu kasoro za kuongea na utata, kufanya mwili kuelewa yanayoendelea. [3] Wenyeji pia hudai kwamba bangi hutoa Kuwakwa Mchomo kwenye shingo ya nyuma.
Baadhi michoro ya mapenzi kutoka era ya Mughal ya India huonyesha wanandoa wakifanya ngono huku wakivuta bangi kuongeza mapenzi. Nchini Nepal, siku ya tamasha ya Wahindu ya Matta Shivaratri, bangi hutumiwa katika aina mbalimbali kama moshi, kuchanganywwa na pipi au kinywaji. Kutoa sadaka ya bangi kwa Bwana Shiva ni kawaida wakati wa tamasha hii.
Kalasinga Wanihang kutoka jadi wanapenda bangi sana, ambayo wanaiita Sukkha Prasad yaani "Apatianaye amani ". Katika Kisanskriti neno "Sukhi" humaanisha furaha na, "Prasad" ni sadaka kwa mungu ambayo ameionja na kuamua kugawana na kerende. Ilikuwa ikitumiwa kutuliza maumivu kabla na baada ya vita kwa vile wengi wa WaNihang wakirudi wangekuwa na majeraha makubwa. Kalasinga hufunzwa kuitumia kama dawa badala ya burudani.